Wananchi wa wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro wamewaomba viongozi kuhakikisha tamasha la utalii la Same Utalii Festival linafanyika kila mwaka kutokana na mchango wake mkubwa katika kukuza uchumi wa jamii.

Wito huo umetolewa leo na kina mama lishe wakati wa joggin ya kuhamasisha tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika Aprili 10 hadi 12 mwaka huu, likiwa ni msimu wa tatu tangu kuanzishwa kwake.

Akizungumza katika joggin hiyo, Anna Mzava, ambaye ni mama lishe katika stendi ya mabasi wilayani Same, alisema tamasha hilo limekuwa msaada mkubwa kwao kiuchumi.

Alisema mbali na kuhamasisha utalii, tamasha hilo limeongeza kipato kwa wafanyabiashara wadogo kutokana na ongezeko la watu wanaohudhuria.

“Tunaomba tamasha hili liwe endelevu kwani sisi wananchi wa chini tunafaidika nalo. Biashara zetu zinaenda vizuri na tunapata fedha zaidi. Kwa mfano, badala ya kupika mchele kilo tatu, wakati wa tamasha napika hadi kilo 10 na zote zinaisha,” alisema Mzava.

Kwa upande wake, Jumanne Idd alisema tamasha hilo limekuwa chachu ya kutangaza utalii wa wilaya ya Same pamoja na vyakula vya asili vya kabila la Wapare.

Aliongeza kuwa tukio hilo limechangia kuitangaza wilaya hiyo kitaifa na kuchochea ukuaji wa shughuli za kiuchumi wakati wa msimu wa tamasha.

Akizungumza katika joggin hiyo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Same, Yusto Mapande, alisema wamejipanga kuhakikisha tamasha hilo linakuwa endelevu ili kuendelea kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo wilayani humo.

Alisema halmashauri itaendelea kubuni na kuibua vivutio vipya ili kuongeza fursa za kiuchumi kwa wananchi.

“Faida kubwa tunazotarajia ni za kiuchumi.Panapokusanyika watu wengi ni fursa, kwani wanahitaji huduma mbalimbali na hivyo kuongeza kipato kwa wananchi,” alisema Mapande.

 



Na Oscar Assenga,TANGA


MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Tanga imefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 406.17 katika kipindi cha miezi tisa kuanzia Julai 2025 hadi Machi 2026, ikilinganishwa na lengo la bilioni 296.3 ukiwa ni ufanisi wa asilimia 137.


Akizungumza kuhusu mafanikio hayo leo  Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga, Casto John, alisema kuwa matokeo hayo makubwa yametokana na mchango na ushirikiano mzuri wa wadau mbalimbali, ikiwemo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wakuu wa Wilaya, pamoja na vyombo vingine vya serikali ambavyo vimekuwa mstari wa mbele kuhakikisha ukusanyaji wa kodi unafanyika katika mazingira salama na tulivu.


Aidha, aliwashukuru walipa kodi wote kwa mchango wao mkubwa akisisitiza kuwa mafanikio hayo ni matokeo ya wananchi kujitokeza kwa hiari kulipa kodi zao  



Pia alipongeza ushirikiano kutoka kwa vyama vya wafanyabiashara kama JW na TCCIA, pamoja na taasisi za serikali na binafsi ambazo zimekuwa zikifanya kazi kwa pamoja kama timu.


Katika hatua nyingine, Meneja huyo alisisitiza umuhimu wa kipindi cha makadirio ya kodi (Januari hadi Machi) kwa wafanyabiashara kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi huku akiwashukuru walipa kodi waliojitokeza kukadiriwa na kulipa kodi zao.



 Hata hivyo, aliwataka wale ambao bado hawajafika kujitokeza haraka kwani ofisi za TRA ziko wazi kwa huduma hiyo.


Alionya kuwa kutakuwa na zoezi la kuwafuatilia wadaiwa wa kodi, likiwemo ukaguzi wa barabarani kwa magari na wafanyabiashara wasiolipa kodi, hivyo ni vyema wakazingatia sheria mapema.



Kuhusu matumizi ya mashine za kielektroniki za kutoa risiti (EFD), amesema bado kuna changamoto katika baadhi ya maeneo kutokana na baadhi ya wafanyabiashara kutokutoa hivyo niwatake 


Aliwataka wafanyabiashara kuhakikisha wanatoa risiti kwa kila huduma au bidhaa wanayouza, huku akiwahimiza wananchi kudai risiti wanaponunua bidhaa au kupata huduma.


Pia alibainisha kuwa changamoto zozote zinazohusiana na EFD zinapaswa kuripotiwa ili zipatiwe ufumbuzi.


Akizungumzia suala la magendo, alisema Mkoa wa Tanga unapakana na nchi jirani akionya baadhi ya wafanyabiashara wanaotumia njia zisizo rasmi kuingiza bidhaa nchini .huku akiwataka kutumia mipaka rasmi ili kuhakikisha bidhaa zinakaguliwa na taasisi husika kama TBS kwa ajili ya kulinda afya za wananchi.


Alisisitiza kuwa magendo yana madhara makubwa kwa uchumi wa nchi, kwani husababisha kukosekana kwa takwimu sahihi za biashara, kupunguza mapato ya serikali, na kuathiri wafanyabiashara halali pamoja na wananchi kwa ujumla.


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Uvuvi Prof. Mohammed Sheikh,akizungumza leo Aprili 8,2026 wakati akizindua mafunzo ya siku tano kwa maafisa wakaguzi wa mazao ya uvuvi 25 yaliyoandaliwa na Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kwa kushirikiana na Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO).

.....

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Uvuvi Prof. Mohammed Sheikh amewataka wakaguzi wa mazao ya uvuvi kufanya kazi zao kwa ubora ili kulisaidia Taifa kuongeza kiwango cha mazao ya uvuvi yanayosafirishwa nje ya nchi.

Prof Sheikh ametoa kauli hiyo 8 April, 2026 wakati akizindua mafunzo ya siku tano kwa maafisa wakaguzi wa mazao ya uvuvi 25 yaliyoandaliwa na Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kwa kushirikiana na Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO).

"Takwimu zinaonesha kwasasa tunasafirisha tani 60,000 pekee za samaki kwenda nje ya nchi hivyo uwepo wa mafunzo haya uwe chachu ya kuongeza ubora utakaosaidia Taifa kuongeza kiasi cha samaki kinachopelekwa nje ya nchi" Amesema Prof. Sheikh

Kwa uoande wake Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Dkt Semvua Mzighani amesema Mafunzo haya yamelenga kuwajengea uwezo maafisa ukaguzi wa mazao ya uvuvi juu ya taratibu za ukaguzi wa mazao ya uvuvi pamoja na viwango vya ubora vya kitaifa,kikanda na kimataifa.

Pia amewasihi washiriki wa mafunzo kuzingatia mafunzo watakayopatiwa na elimu watakayoipata kupitia mafunzo hayo ikawasaidie wananchi katika maeneo yao.

Awali Mratibu wa mafunzo hayo Mkufunzi Anold Mbunda amesema hii ni awamu ya kwanza ya mafunzo ambapo imejumuisha washiriki toka ukanda wa pwani, awamu ya pili ya mafunzo haya itafanyika mkoani Kigoma ambapo itahusisha washiriki kutoka kanda ya ziwa.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Uvuvi Prof. Mohammed Sheikh,akizungumza leo Aprili 8,2026 wakati akizindua mafunzo ya siku tano kwa maafisa wakaguzi wa mazao ya uvuvi 25 yaliyoandaliwa na Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kwa kushirikiana na Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO).

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Dkt Semvua Mzighani,akizungumza  wakati wa mafunzo ya siku tano kwa maafisa wakaguzi wa mazao ya uvuvi 25 yaliyoandaliwa na Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kwa kushirikiana na Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO).

Sehemu ya washiriki wakifatilia hotuba ya Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Uvuvi Prof. Mohammed Sheikh (hayupo pichani) ,wakati akizindua mafunzo ya siku tano kwa maafisa wakaguzi wa mazao ya uvuvi 25 yaliyoandaliwa na Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kwa kushirikiana na Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO). 

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Uvuvi Prof. Mohammed Sheikh,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzindua  mafunzo ya siku tano kwa maafisa wakaguzi wa mazao ya uvuvi 25 yaliyoandaliwa na Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kwa kushirikiana na Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO).



Na Munir Shemweta, Nairobi

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Leonard Akwilapo, anatarajiwa kuongoza ujumbe wa Tanzania kushiriki Kongamano la Pili la Jukwaa la Miji Afrika (2nd African Urban Forum) litakalofanyika kuanzia tarehe 8 hadi 10 Aprili 2026 katika jiji la Nairobi nchini Kenya.

Kongamano hilo linaongozwa na kauli mbiu isemayo “Adequate Housing for All: Advancing Socio-Economic and Environmental Transformation Towards the Realization of Agenda 2063,” linalenga kuhamasisha mijadala itakayotoa fursa kwa washiriki kutoka nchi mbalimbali za Afrika kubadilishana uzoefu na suluhisho bunifu katika kukabiliana na changamoto za maendeleo ya miji na makazi.

Kupitia kongamano hilo, Tanzania inatarajiwa kutoa tamko la nchi litakaloeleza jitihada za Serikali katika kuchochea maendeleo endelevu ya miji na makazi, ikiwa ni pamoja na sera, mipango na mikakati inayotekelezwa kuboresha makazi na upangaji wa miji.

Aidha, Mhe. Dkt Akwilapo atashiriki katika mijadala ya ngazi ya juu itakayowahusisha mawaziri, mameya na wataalamu mbalimbali, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kimataifa katika sekta ya maendeleo ya miji.

Awali Dkt Akwilapo aliongoza kikao cha maandalizi kwa ujumbe wa Tanzania utakaoshiriki kongamano hilo katika ubalozi wa Tanzania nchini Kenya tarehe 7 April, 2026 ambapo masuala mbalimbali ya uwakilishi wa nchi yalijadiliwa.

Dkt Akwilapo ameambatana na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Makazi Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bw. Deogratias Kalimenze, Mkurugenzi Msaidizi Uzingatiaji Mipango ya Matumizi ya Ardhi kutoka Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi Bi. Rehema Kishoa, Maafisa kutoka Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi pamoja na taasisi binafsi.











Mkuu wa wilaya ya Ilala, Mheshimiwa Edward Mpogolo, ambaye amemuwakilisha Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Albert Chalamila, amepongeza na kuwashukuru viongozi wa dini kwa mchango wao mkubwa wa kuimarisha na kudumisha amani lengo kuleta maendeleo katika jamii.

Akizungumza katika maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 19 ya kanisa la WRC Kivule tarehe,6 April, DC Mpogolo alisema licha ya changamoto mbalimbali viongozi wa dini wameendelea kujitoa na kushirikiana na serikali pale wanapohitajika.

Aidha alimpongeza mgeni rasmi, Deus Sangu, Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu kazi na ajira , ambaye alimuwakilisha makamu wa raisi Mheshimiwa Emmanuel Nchimbi kwa kushiriki katika maadhimisho hayo.

DC Mpongolo ameipongeza serikali chini ya Mheshimiwa raisi Dkt Samia Suluhu Hassan kwa juhudi zake za kuleta maendeleo kwa utoaji wa fedha katika mkoa huo na kusisitiza kuwa mafanikio hayo yasingewezekana bila uwepo wa amani, maadili na mchango wa viongozi wa dini.

Aliongeza kuwa viongozi wa dini wamekuwa nguzo muhimu katika kuleta amani, utulivu, upendo na mshikamano miongoni mwa wananchi na kujenga jamii kupitia hofu ya Mungu hali inayochangia kwa kiasi kikubwa utekelezaji wa malengo ya serikali.

“Mgeni rasmi kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam tufikishie salamu kwa raisi wetu amekuwa na mafanikio makubwa lakini mafanikio haya ni kutokana na maombi ya viongozi wetu na waumini”

Mheshimiwa Mpogolo aliwataka waumini na wananchi kwa ujumla kuendelea kumuombea Rais pamoja na kudumisha amani, akibainisha kuwa mafanikio ya Taifa yanatokana na ushirikiano wa viongozi wa dini na wananchi kwa ujumla.













 



Na Oscar Assenga, Tanga

Askofu Mkuu wa Kanisa la (FPCT) Tanzania, Stevie Mulenga, amewataka viongozi wa dini nchini, wakiwemo maaskofu, kutumia majukwaa ya kidini kuhubiri amani badala ya ujumbe unaoweza kuleta uchonganishi.

Askofu Mulenga alitoa wito huo leo wakati wa ibada ya Sikukuu ya Pasaka iliyofanyika katika kanisa hilo. Alisisitiza kuwa Yesu Kristo hakukuja kuleta uchonganishi, bali alikuja kuleta amani, hasa kupitia kufufuka kwake.

Alieleza kuwa viongozi wa dini wanapaswa kuhubiri amani, upendo, uvumilivu na mshikamano miongoni mwa jamii, ili watu waweze kuishi kwa utulivu. Alisema huo ndio ushauri wake mkubwa kwa viongozi hao katika kipindi hiki cha Sikukuu ya Pasaka.

“Tunamshukuru Mungu kwa sababu haki ya kuabudu inaendelea kuheshimiwa nchini. Ingawa serikali haina dini, wananchi wake wana dini, na wanaendelea kuabudu bila kuvunja sheria. Wana uhuru mkubwa wa kuabudu mchana na usiku,” alisema Askofu Mulenga.

Aidha, aliwataka wananchi kulinda amani iliyopo na kuepuka vitendo vinavyoweza kusababisha fitina au vurugu. Alisisitiza kuwa ibada zinapaswa kuwa sehemu ya kufundisha neno la Mungu, siyo majukwaa ya kuchochea chuki au upendeleo kwa watu fulani.

Kwa upande mwingine, Askofu Mulenga alisema chanzo kikubwa cha mmomonyoko wa maadili ni tamaa  binafsi, ambazo husababisha matukio mbalimbali yanayoshangaza hata jamii ya kimataifa.

Aliongeza kuwa viongozi wa dini wanapaswa kuwaelimisha waumini wao juu ya kuepuka ukatili wa kijinsia, huku wakisisitiza umuhimu wa kuishi kwa amani, utulivu na kufuata matendo mema.