Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuleta neema ya maendeleo kwa wananchi wa mkoa wa Arusha kwa kuanza utekelezaji wa mradi wa kusambaza umeme katika vitongoji 127 kwa gharama ya shilingi bilioni 19.5.

Mradi huo unatekelezwa kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika awamu ya Pili B na unatarajiwa kuwanufaisha wateja 4,086 katika wilaya za Arusha DC, Meru, Karatu, Ngorongoro, Longido na Monduli.

Akizungumza Februari 4, 2026 mkoani Arusha wakati wa hafla ya kumtambulisha mkandarasi aliyeshinda zabuni, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Herini Mhina, amesema utekelezaji wa mradi huo ulianza rasmi Februari 2, 2026 na mkandarasi mzawa Kampuni ya NAKUROI Investment Co. Ltd.

“Tunamshukuru Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia utekelezaji wa mradi huu muhimu. Tumewaelekeza wakandarasi kuepuka rushwa, kutumia vibarua wa maeneo husika kwa kazi zisizo za kitaalamu na kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa ubora na kwa wakati,” amesema Mhandisi Mhina.

Mhandisi Mhina ameongeza kuwa hadi sasa vitongoji 368 kati ya 1,505 mkoani Arusha vimefikishiwa umeme, huku jitihada zikiendelea kufikisha nishati hiyo katika vitongoji vilivyobaki.

“Dhamira ya Serikali ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 vitongoji vyote nchini viwe vimefikishiwa umeme. REA imejipanga kikamilifu kutekeleza dhamira hiyo kupitia miradi mbalimbali ya kimkakati,” amefafanua Mhandisi Mhina.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. CPA Amos Makala, ameipongeza REA kwa kutekeleza kwa vitendo maelekezo na dira ya Rais Samia ya kuwaletea wananchi maendeleo.

“Ofisi ya Mkuu wa Mkoa itatoa ushirikiano wa kutosha kwa mkandarasi na REA kuhakikisha mradi huu unakamilika kwa mafanikio,” amesema Mhe. Makala.

Naye Meneja wa Mradi kutoka Kampuni ya NAKUROI Investment Co. Ltd, Mhandisi Selestine Egongo, ameishukuru Serikali kwa kuwaamini na kuahidi kutekeleza mradi kwa ufanisi kwa kushirikiana na viongozi na wananchi wa maeneo husika.

 


Serikali imetoa wito kwa wadau kutoka sekta ya fedha nchini kuanzisha huduma na bidhaa za kifedha zitakazowezesha ajenda ya nishati safi ya kupikia kusambaa zaidi, hususan kwa kuwawezesha wajasiriamali wadogo katika maeneo ya pembezoni na vijijini pamoja na wabunifu wa teknolojia za matumizi ya nishati hiyo.

Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba  tarehe 4 Februari 2026 wakati akimwakilisha Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi katika uzinduzi wa mradi wa nishati safi ya kupikia katika shule ya sekondari Bunge Wasichana iliyopo mkoani Dodoma.

"Tanzania imepiga hatua kubwa katika ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia, matumizi ya nishati hii yameongezeka kutoka asilimia 6.9 mwaka 2021 na kufikia asilimia 23.2 mwaka 2025. Hata hivyo, bado takribani asilimia 77 ya kaya nchini zinatumia nishati isiyo safi ya kupikia, hivyo natoa wito kwa sekta binafsi kuendelea kushirikiana na Serikali katika kusukuma ajenda hii kwa kuwezesha upatikanaji wa nishati mbalimbali safi za kupikia katika maeneo ya pembezoni na yale ya vijijini." Amesema Mhe. Salome

Aidha, Mhe. Salome amewasisitiza Wasambazaji wa gesi za mitungi kuongeza vituo vya usambazaji na ujazaji wa gesi za mitungi ili kurahisisha upatikanaji wake kwa watumiaji wengi zaidi, pia Wabunifu na vijana walioko vyuoni kufanya tafiti na kubuni nyenzo na teknolojia zitakazowezesha ajenda hii kusambaa na kuwafikia watu wengi. 

Kuhusu mradi wa nishati safi ya kupikia aliouzindua Mhe. Salome amesema kuwa ni utekelezaji wa agizo la Serikali kwa taasisi zinazolisha watu zaidi ya 100 kutumia nishati safi ya kupikia ili kulinda afya za binadamu na kutunza mazingira.

Ameongeza kuwa mfumo huo  uliozinduliwa  utawezesha chakula kupikwa kwa usafi, kwa haraka, kwa ufanisi, kwa gharama nafuu na bila madhara ya moshi kwa wapishi na wanafunzi huku mazingira  yakiendelea kustawi.

Mhe. Salome ameeleza kuwa kuzinduliwa kwa mradi huo ni sehemu ya juhudi za kitaifa zinazoongozwa na Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha asilimia 80 ya watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo 2034 ambapo mpaka sasa tayari asilimia 23.2 ya wananchi wanatumia nishati safi ya kupikia huku taasisi 1,136 zinazolisha zaidi ya watu 100 kwa siku zikihamia katika matumizi ya nishati hiyo.

Akiwa katika shule hiyo ya Wasichana Bunge, Naibu Waziri amezindua pia Klabu ya Nishati Safi ya Kupikia  yaani Clean Cooking School Club ambayo ni ya kwanza kuzinduliwa kwa Tanzania ambayo itakuwa mfano wa kuigwa na shule nyingine nchini katika kueneza elimu ya Nishati Safi ya Kupikia.

Wanafunzi watakaojiunga na klabu hiyo watakuwa Vinara  wa Nishati Safi ya Kupikia (Clean Cooking Champions) na watashirikiana na Wizara ya Nishati na wadau wengine katika kutoa elimu mashuleni na katika jamii pamoja na kubuni teknolojia za nishati safi ya kupikia zitakazolinda afya na mazingira.

Awali Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Bunge Wasichana, Richard Msana  alisema shule hiyo yenye wanafunzi 555 imefanikiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa gharama za nishati ya kupikia baada ya kuachana na matumizi ya kuni na kuhamia katika gesi.

Amesema kuanzia Julai 2020 hadi Mei 2022, shule ilikuwa ikitumia takribani shilingi milioni 10.5 kwa kila miezi mitatu kununua kuni. Baadaye walipoanza kutumia mkaa mbadala, gharama zilishuka hadi kufikia shilingi milioni 2.7 na hivi sasa, kupitia mradi wa matumizi ya gesi, shule imenunua tani moja ya gesi iliyotumika kwa miezi miwili, ambapo matumizi ni wastani wa shilingi milioni 1.3 kwa mwezi, kiwango ambacho ni nafuu zaidi kiuchumi.








Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu Bi. Prisca Kayombo,akizungumza wakati wa kikao cha kumtambulisha rasmi Mkandarasi wa Mradi huo Burhani Engineers limited atakaye hudumia Vitongoji 415 vya Mkoani wa Simiyu kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anamringi Macha.

Na.Mwandishi Wetu-SIMIYU

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu Bi. Prisca Kayombo akimwakilisha Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Anamringi Macha ametoa rai kwa Wanachi Mkoani Simiyu kuchangamkia fursa ya umeme Vitongojini wenye thamani ya kiasi cha Shil Bil. 4.8 unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Bi. Kayombo pia amewataka wananchi kutokuhujumu miradi hio kwani lengo lake ni kukuza na kuinua uchumi wa mwananchi mmoja mmoja na Mkoa kwa ujumla.

Ameyasema hayo leo tarehe 04/02/2026 Ofisini kwake wakati wa kikao cha kumtambulisha rasmi Mkandarasi wa Mradi huo Burhani Engineers limited atakaye hudumia Vitongoji 415 vya Mkoani wa Simiyu.

Aidha, Bi. Kayombo amewasisitiza wananchi wa Mkoa huo kutoa ushirikiano kwasababu mradi huo unakwenda kupelekea Maendeleo ya kiuchumi katika Mkoa huo.

"Mradi huu utakwenda kusaidia uendeshaji wa viwanda vidogo, Umeme utakwenda kurahisisha uchimbaji wa Dhahabu na kusaidia katika viwanda vya uchakataji wa zao la Pamba na mafuta ya kupikia ya Alizeti.

“Hii Miradi ni Miradi ya Maendeleo hivyo Wananchi mtoe ushirikiano kwa asilimia kubwa. Lakini sisi pia ni wakulima wazuri wa zao la alizeti na pamba, nahakika umeme huu utasaidia katika viwanda vitakavyo tengeneza mafuta yakupikia yatokanayo na alizeti” amesisitiza Bi. Kayombo.

Kwa upande wake, Mhandisi Seif Abduli, Mhandisi wa Miradi kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA) amesema kwa Mkoa wa Simiyu Jumla ya Vitongoji 415 vitaanza kufikishiwa Umeme huku taratibu zingine zikiendelea ili kabla ya 2030 Vitongoji Vilivyo bakia 1026 vinafikiwa na Umeme

Mhandisi Seif ameeleza kuwa Vitongoji hivyo Vitahusisha kuunga Wateja 13292 na Mradi utatekelezwa kwa Muda wa Miaka Mitatu hivyo ametoa wito kwa Wananchi kuhakikisha kwamba wanachangamkia Fursa ya kuanzisha viwanda vidogo vidogo vitongojini kwani transformer zitakazo fungwa zitakuwa na uwezo wa kukidhi mahitaji ya viwanda.

Mhandisi Seif amesema kuwa Serikali inatumia gharama kubwa ya kufikisha huduma ya umeme kwa wananchi wake, hivyo akawataka kila mwananchi awe mlinzi wa miundombinu hiyo ili malengo ya kuwainua wananchi vijijini kiuchumi na kijamii yaweze fikiwa.

 

Maisha yangu nyumbani yalikuwa hatari. Kila usiku, nilihisi kama kuna mtu anakuja. Hatua zisizoelezeka zilisikika nje ya mlango wangu. Wakati mwingine, niliona kivuli kisichoelezeka karibu na dirisha.

Familia yangu ilikuwa katika hofu. Hatukuwa na njia ya kujua ni lini hatari ingeibuka. Nilijaribu kuziba milango, kuacha kufanya kelele, na hata kulala na tahadhari. Lakini kila kitu kilionekana kushindwa.

Usiku ulikuwa mzito, na mawazo mabaya yalikuwa sehemu ya kila siku yangu. Nilihisi kama hatimaye maisha yangu yatakuwa hatarini.Soma Zaidi.
Baada ya harusi yangu, nilikuwa na furaha kubwa. Ndoa ilikuwa mpya, maisha yalionekana kuanza upya, na kila mtu alinitakia heri. Lakini baada ya wiki chache, kitu cha ajabu kilianza kutokea.

Nilianza kuota ndoto ileile mara kwa mara. Kila wiki, ndoto hiyo ilirudi bila kubadilika mandhari ileile, hisia ileile, na hofu ileile. Mwanzoni nilipuuzia.

Nilijiambia labda ni mawazo mengi au uchovu wa maandalizi ya harusi. Lakini ndoto zilipoendelea, nilianza kuona athari zake hata nikiwa macho.

Nilikuwa mchovu kila siku, moyo haukuwa na amani, na ndoa yangu ilianza kuingia ukimya usio wa kawaida. Hakukuwa na ugomvi mkubwa, lakini furaha ile ya mwanzo ilianza kupotea polepole.

Nilipomweleza mume wangu, alicheka na kusema ni kawaida. Lakini moyoni nilijua kuna kitu hakiko sawa. Ndipo nikaanza kutafuta ushauri wa busara.Soma Zaidi.
Nilikuwa kwenye ndoa ambayo kwa nje ilionekana ya kawaida. Hakukuwa na ugomvi mkubwa, hakukuwa na kelele. Lakini kulikuwa na tatizo moja lililonisumbua kimya kimya kila aliponikaribia, mwili wangu ulikataa kabisa.

Sikuwa najifanya, wala sikuwa namchukia. Ilikuwa ni kama mwili wangu na moyo wangu havikuelewana tena. Nilitembea hospitali kadhaa. Vipimo vikafanywa, majibu yakarudi yale yale: uko sawa.

Lakini nilijua ndani yangu kuna kitu hakiko sawa. Nilihisi hatia, huzuni, na hofu kuwa ndoa yangu ingeangamia kwa jambo ambalo sikuweza kulieleza vizuri hata kwa maneno.

Kadri siku zilivyopita, ukimya ukaingia kati yangu na mume wangu. Nilijitenga, nikajilaumu, na wakati mwingine nikajikuta nikilia peke yangu usiku. Madaktari walikuwa wamesema niko sawa, lakini kwa nini basi mwili wangu ulikataa?

Ndipo nilipopata ushauri wa kumtafuta mtu anayeelewa mahusiano, nafsi, na mizizi ya matatizo ya ndani.Soma Zaidi.
Maumivu ya mgongo na misuli yalikuwa sehemu ya kila siku yangu. Kila asubuhi niliamka nikiwa nimechoka, na kila hatua ilinichosha. Nilijaribu dawa za maduka, lakini matokeo yalikuwa madogo.

Nilihisi kama hakuna suluhisho lolote, na kila siku ilikuwa ni vita mpya ya kuhimili maumivu. Nilijaribu mazoezi madogo na kupumzika mara kwa mara. Lakini maumivu hayakupungua.

Nilihisi kama mwili wangu ulikuwa unanikataa. Hisia za hofu na wasiwasi zilikuwepo kila wakati. Nilijua lazima nifate suluhisho ambalo lingefanya mabadiliko ya kweli.Soma Zaidi.
Nilihisi moyo wangu umevunjika. Aliondoka ghafla, bila kueleza sababu yoyote. Kila siku niliamka nikihisi huzuni na upweke. 

Nilijaribu kuwasiliana, kumwambia maneno mazuri, na kujaribu kurekebisha mahusiano.

Lakini kila jaribio lilishindikana. Nilihisi tamaa na kuhisi kuwa upendo wangu ulikosa nguvu. Nilijaribu kufanya kila kitu ili kumfanya arudi: zawadi, maneno mazuri, na hata kujaribu kubadilisha tabia yangu.

Lakini hakuonekana. Nilihisi kuwa na shida kubwa zaidi kuliko nilivyoweza kushughulikia peke yangu. Nilihitaji msaada wa kweli, suluhisho lililo na nguvu na linaloweza kurejesha upendo wa kweli.Soma Zaidi.

 


Na OWM - TAMISEMI, Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(OWM- TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amekutana na uwakilishi wa Benki ya NMB na kujadili namna wanavyoweza kufanya maboresho katika mchakato wa kutoa fedha za mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi kupitia taasisi hiyo ya kifedha.

Prof. Shemdoe amekutana na ujumbe huo leo Februari 03, 2026 ofisini kwake jijini Dodoma, ikiwa ni mwendelezo wa Serikali kutafuta namna bora ya kurahisisha utolewaji wa mikopo hiyo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha makundi yote lengwa ya Wanawake, Vijana na wenye Ulemavu yananufaika na mikopo hiyo.

Msisitizo wa Prof. Shemdoe kwa ujumbe huo ulioongozwa na Mkuu wa Biashara ya Serikali wa Benki ya NMB, Bi. Vicky Bishubo umekuwa ni kuhakikisha vikundi vya wanufaika vyenye sifa stahiki vinapata mikopo hiyo kwa wakati.

Sanjali na hilo, Prof. Shemdoe ameipongeza na kuishukuru Benki ya NMB kwa kuiunga mkono Serikali katika uboreshaji wa miundombinu ya afya msingi na elimu msingi pamoja na kurahisisha utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa walengwa. 

Akitoa ufafanuzi kuhusu hoja ya walengwa kutakiwa kuweka dhamana ili kupata mikopo ya asilimia 10, Bi. Bishubo amesema kuwa, hoja hiyo si ya kweli kwani mikopo hiyo ni nafuu na inatolewa bila dhamana yoyote, hivyo amewataka walengwa kuchangamkia fursa hiyo ya mikopo. 

Katika hatua nyingine, uwakilishi huo wa Benki ya NMB umekutana na Naibu Waziri OWM- TAMISEMI, anayeshughulikia Elimu, Mhe. Reuben Kwagilwa, pamoja na Naibu Waziri, OWM - TAMISEMI, anayeshughulikia Afya, Mhe. Dkt. Jafal Seif kama sehemu ya Kuimarisha mahusiano baina ya Benki hiyo na OWM- TAMISEMI.



Na Mwandishi Wetu - DODOMA


Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji ( EWURA) imetangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta aina ya petroli zitakazotumika hapa nchini kwa mwezi kuanzia tarehe 4 Februari 2026, zikionesha kushuka maradufu kwa bei ya dizeli kwa mafuta yaliyopokelewa bandari za Dar es Salaam, Tanga na Mtwara.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Mwainyekule, leo 4 Februari 2026, imebainisha kuwa, bei ya rejareja ya petroli dizeli imepungua kwa shilingi 90 kwa mafuta yaliyopokelewa Dar es Salaam, 25 kwa Tanga na shilingi 24 kwa bandari ya Mtwara. Aidha, bei ya mafuta ya taa nayo imepungua kwa shilingi 17, 14 na 93 kwa mafuta yaliyopokelewa Dar es Salaam, Tanga na Mtwara mtawalia ikilinganishwa na bei za mwezi Januari 2026.

Hivyo basi, bei za reja reja za bidhaa za mafuta kwa mwezi huu, zitakuwa shilingi 2,788, 2,849 na 2881 kwa Dar es Salaam, Tanga na Mtwara mtawalia. Na bei ya dizeli, Dar es Salaam ni shilingi 2,701, Tanga 2,762 na Mtwara 2,807 huku bei ya mafuta ya taa kwa Dar es Salaam ikiwa ni shilingi 2,881, Tanga 2794 na Mtwara 2,838.

Aidha, kwa mwezi Februari 2026, gharama za kuagiza mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam ziliongezeka kwa wastani 1.88% kwa mafuta ya petroli na 1.65% kwa mafuta ya taa na kupungua kwa wastani wa 5.10% kwa mafuta
ya dizeli. Kwa bandari ya Tanga zimepungua kwa 1.62% kwa petroli na dizeli; huku bandari ya Mtwara zikipungu kwa 9.24% kwa mafuta ya petroli. Vilevile, wastani wa gharama za kubadilisha fedha za kigeni umeongezeka kwa 1.86%.

EWURA inawahimiza wauzaji wa mafuta nchini kutoa stakabadhi za mauzo kwa wanunuzi zinazoonesha jina la kituo, tarehe, aina ya mafuta yaliyonunuliwa na bei kwa lita.

Aidha,vituo vyote vya mafuta nchini vichapishe bei za bidhaa za mafuta katika mabango yanayoonekana bayana kwani kutokufanya hivyo ni kosa na atakayekiuka atapata adhabu kali kwa mujibu wa sheria.





 

Na Mwandishi Wetu, Tabora

NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara,John Mongella, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, ameshiriki katika ibada ya mazishi ya aliyekuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa mstaafu, Ndugu Nassor Hamdani.

Mazishi hayo yamefanyika leo Februari  3,2026 katika makaburi ya Mihogoni, Kata ya Mbugani, Manispaa ya Tabora mkoani Tabora. 

Akizungumza katika ibada hiyo,Mongella amewasilisha salamu za rambirambi kutoka Chama Cha Mapinduzi, akimuelezea marehemu ndugu Nassor Hamdani kuwa alikuwa mshauri mwema wa Chama kwa kipindi chote cha uhai wake, sambamba na mchango wake mkubwa wa kujitolea kwa jamii.

Amesema CCM itaendelea kumkumbuka marehemu kwa uadilifu, hekima na mchango wake katika kukijenga Chama pamoja na ustawi wa jamii kwa ujumla.












 Veronica Simba - WMA 

Wakala wa Vipimo (WMA) umesimika mtambo wa kisasa wa kidijitali wa kuhakiki dira za maji katika jengo la makao yake makuu lililopo jijini Dodoma.

Meneja Uhakiki wa Vipimo na Viwango wa WMA Makao Makuu, Magesa Biyani amesema usimikaji mtambo huo uliogharimu takribani shilingi milioni 400, utawezesha uidhinishaji na uhakiki wa dira za maji kwa muda mfupi na kwa usahihi zaidi kupitia miradi mingi ya maji inayoendelea kutekelezwa nchini ikiwemo Mkoa wa Dodoma na mikoa mingine jirani.

Akizungumza na wanahabari wa WMA Februari 3, 2026, Biyani amesema kuwa “Mtambo huu umekuja kwa wakati mwafaka kuwezesha wafanyabiashara pamoja na Mamlaka za Maji kuzingatia kwamba dira za maji zote ambazo wanawafungia wateja katika maeneo yao ziwe zimehakikiwa na WMA ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma kulingana na thamani ya fedha wanazolipa.”

Akifafanua zaidi, amesema kuwa mtambo huo una uwezo wa kuhakiki dira za maji nyingi zaidi kwa wakati mmoja kwa kutumia muda mfupi zaidi tofauti na mitambo ya awali ambayo ni ya ki-makenikali (Mechanical Test Bench) yenye uwezo wa kuhakiki dira za maji 10 kwa wakati mmoja ikitumia dakika 20 hadi 30.

Amesema kuwa mtambo huo pamoja na mingine miwili ya aina hiyo iliyoko katika Kituo cha Uhakiki Vipimo, Misugusugu mkoani Pwani, kwa pamoja imeleta faida kubwa ikiwemo kupima dira za maji nyingi zaidi, kwa usahihi zaidi na kwa muda mfupi tofauti na awali kabla ya uwepo wake.

Akitoa mfano, Biyani amesema mathalani kwa Kituo cha Misugusugu ambako mitambo ya aina hiyo ilitangulia kusimikwa kabla ya Dodoma, dira za maji kati ya laki mbili hadi laki tatu zimekuwa zikipimwa kwa mwaka kutegemea na uhitaji kutokana na kuongezeka kwa miradi ya kimkakati.

“Kwahiyo imeleta faida kubwa sana na kusaidia thamani ya fedha iweze kuonekana kwa wateja/wananchi, Mamlaka za Maji na wafanyabiashara na hata kwa uchumi wa nchi,” ameeleza Biyani.

 Akidadavua zaidi namna WMA inavyohusika katika uidhinishaji na uhakiki wa dira za maji, ameeleza kuwa hilo ni mojawapo ya majukumu yake ya uhakiki wa vipimo vya aina mbalimbali nchini kwa lengo la kumlinda mlaji.

Amesema kuwa, WMA huidhinisha na kuhakiki vipimo kwa niaba ya Serikali ambapo kwa upande wa dira za maji, mfanyabiashara yeyote binafsi au kampuni kabla ya kuagiza au kuzalisha bidhaa hizo anatakiwa awasilishe sampuli yake WMA ili kuhakiki muundo wake na baada ya kuidhinishwa anatakiwa kuziwasilisha bidhaa zote alizoagiza au kuzalisha ili zihakikiwe kwa kila moja kujiridhisha kuhusu usahihi wake.

Biyani amefafanua zaidi kuwa zoezi hilo hulenga kuzilinda pande zote mbili yaani mteja na muuzaji ili yeyote kati yao asipunjwe. Dira za maji zilizohakikiwa humuwezesha mteja kulipia kiwango stahiki kulingana na matumizi yake ilhali kwa upande wa muuzaji humwezesha kupata malipo stahiki kulingana na huduma anayotoa.

Akijibu swali la mwandishi kuhusu mipango ya WMA kufikisha huduma hiyo nchi nzima, Biyani ameeleza kuwa Mpango Mkakati wa Wakala wa miaka mitano ijayo kuanzia mwaka huu wa 2026 ni kusimika mitambo ya aina hiyo katika Kanda zote zilizosalia nchini ambazo amezitaja kuwa ni Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Ziwa, Kanda ya Magharibi pamoja na Kanda ya Kusini.

Hata hivyo, ameweka bayana kuwa kutokuwepo kwa mitambo ya kisasa katika Kanda tajwa haimaanishi kuwa kazi hiyo haifanyiki katika maeneo hayo, la hasha, inafanyika kwa kutumia mitambo ya ki-makenikali pamoja na ile midogo inayobebeka (Portable Test Kit) ambayo amesema Maafisa Vipimo kote nchini huibeba mikononi na kwenda nayo katika maeneo mbalimbali kuhakiki dira za maji.

Katika hatua nyingine, Biyani ametoa hamasa kwa wadau wa vipimo mkoani Dodoma na mikoa ya jirani hususani katika sekta ya maji kutumia fursa ya uwepo wa mtambo huo wa kisasa kupeleka dira za maji WMA zikahakikiwe na kuidhinishwa.

Biyani ameonya kwamba ni kosa kisheria kwa mtu yeyote kufunga na/au kutumia dira ya maji ambayo haijahakikiwa na Wakala wa Vipimo huku akibainisha kuwa adhabu yake huanzia kutozwa faini ya shilingi laki moja hadi milioni 20 kwa kosa la kwanza na shilingi milioni 20 hadi milioni 50 kwa kosa la pili kutegemea na aina ya kosa.

Ametaja gharama za kuhakiki dira za maji kwa mujibu wa sheria kuwa ni shilingi elfu kumi tu kwa kila moja na kwa uidhinishaji wa muundo ni shilingi elfu hamsini.

Sheria ya Vipimo, Sura Namba 340 kupitia kanuni zake mbalimbali inaielekeza WMA kuhakiki dira za maji walau mara moja kila mwaka lakini pia Wakala hufanya kaguzi mbalimbali za kushtukiza ili kubaini endapo kuna udanganyifu na kuchukua hatua.

Wakala imeendelea kutoa elimu kwa wadau wa vipimo na umma kwa ujumla katika maeneo mbalimbali ikiwemo namna ya kutambua kipimo ambacho kimehakikiwa ambapo kwa upande wa dira za maji, utambuzi kuwa dira husika imehakikiwa ni kwa kuona lakiri iliyofungwa pamoja na muhuri wa WMA ukionesha tarehe, mwezi na muda ambao kifaa hicho kimehakikiwa. Dira yoyote ambayo haina lakiri na muhuri wa WMA inamaanisha kuwa haijahakikiwa.

Mtambo wa kisasa unaotumika kuhakiki dira za maji. Mtambo huu wa kidijitali umefungwa katika Jengo la Makao Makuu ya Wakala wa Vipimo (WMA), Dodoma.
Sehemu ya Mtambo wa kisasa unaotumika kuhakiki dira za maji. Mtambo huu wa kidijitali umefungwa katika Jengo la Makao Makuu ya Wakala wa Vipimo (WMA), Dodoma.
Jengo lenye mitambo ya kuhakiki dira za maji, lililopo katika Kituo cha Uhakiki Vipimo Misugusugu, Mkoa wa Pwani.

Afisa Vipimo kutoka Wakala wa Vipimo (WMA), akihakiki dira za maji.