Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imetangaza kuwa jumla ya walimu 3,153 wamejisajili kushiriki Shindano la Taifa la Nne la Stadi za Ufundishaji kwa Walimu wa Shule za Awali na Msingi pamoja na Shindano la Pili la Stadi za Ufundishaji kwa Walimu wa Shule za Sekondari Tanzania Bara,ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuendelea kuimarisha ubora wa ufundishaji na ujifunzaji nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 2, 2026, jijini Dodoma, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir, amesema kuwa hafla ya utoaji wa zawadi kwa washindi wa mashindano hayo itafanyika Juni 6, 2026 katika Ukumbi wa Maktaba Mpya wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Amesema mashindano hayo yanatoa fursa kwa walimu kuonesha umahiri wao wa kitaaluma, ubunifu na matumizi ya mbinu bora za ufundishaji darasani, huku yakitumika pia kama sehemu ya utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Mafunzo Endelevu ya Walimu Kazini (MEWAKA).

"Kati ya walimu 3,153 waliosajiliwa kupitia Mfumo wa National Teaching Skills Competition System (TSCS), walimu 1,263 walitimiza masharti yote ya ushiriki kwa kuwasilisha video za ufundishaji pamoja na maandalio ya masomo kwa ajili ya tathmini."amesema Mhe.Ameir

Amesema mchakato wa tathmini umekamilika na tayari orodha teule ya walimu watano bora imepatikana katika kila eneo la ushindani, huku mgeni rasmi katika hafla ya utoaji wa zawadi akitarajiwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe.

Mhe. Ameir ameeleza kuwa mshindi wa kwanza katika kila kundi atazawadiwa Shilingi milioni 2.5, cheti cha pongezi, cheti cha ushindi pamoja na kompyuta mpakato. Aidha, shule anayofundisha mshindi huyo itapatiwa projekta kwa ajili ya kuimarisha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji.

Katika hatua nyingine, amesema shule zitakazotoa washindi wa kwanza katika maeneo ya Kusoma kwa Darasa la Awali, Kiingereza kwa Darasa la Kwanza na Ufaraguzi wa Zana kwa Darasa la Pili zitapatiwa vibao vya kielektroniki 100 vyenye thamani ya Shilingi milioni tano.

Serikali inaendelea kutumia mashindano hayo kama nyenzo ya kuhamasisha ubunifu, kuongeza ari ya utendaji kwa walimu na kuibua mbinu bora za ufundishaji zitakazochangia kuinua viwango vya elimu nchini.

Kaulimbiu ya shindano la mwaka huu ni “UFUNDISHAJI BORA, TAIFA IMARA.

 
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Shirika la Viwango Tanzania limeandaa Jukwaa la Biashara la Viwango (Viwango Business Forum) litakalofanyika Juni 5, 2026 katika ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam, likiwa sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa shirika hilo mwaka 1975 na kuanza utekelezaji wake mwaka 1976.
Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, imewahukumu kifungo cha maisha jela Suleiman Thabit Ngulangwa na Farid Hamis Said baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la biashara haramu ya dawa za kulevya aina ya heroin yenye uzito wa kilo 15.19.
Na: OWM (KAM)

Tanzania imeshiriki kikao cha Kamati ya Utekelezaji wa Viwango vya Kazi kinachoendelea jijini Geneva, Uswisi, ikiwa ni sehemu ya Mkutano Mkuu wa 114 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO).
Nilipofikisha miaka 40, nilikuwa nimeanza kukubaliana na wazo kwamba huenda nisingeolewa tena. TAZAMA VIDEO/ SOMA ZAIDI.

Kwa miaka mingi nilikuwa nimeota kuwa na familia yangu mwenyewe. Niliona marafiki na ndugu wakifunga ndoa, wakijenga familia, na kuendelea na maisha yao.

Mimi pia nilitamani furaha hiyo, lakini kila uhusiano niliouanzisha uliishia njiani. Kwa kweli iliniumiza sana. 

Kadri miaka ilivyopita, maswali kutoka kwa watu yaliongezeka. Kila sherehe ya familia ilikuja na swali lile lile: “Wewe lini?”

Wakati mwingine nilicheka mbele za watu, lakini moyoni nilikuwa na huzuni kubwa. Kilichoniumiza zaidi ni kuona matumaini yangu yakipungua mwaka baada ya mwaka.

Nilijaribu mahusiano mbalimbali, lakini hayakudumu. Baadhi yaliishia kwenye kuvunjika moyo, mengine yalikufa kabla hata hayajafika mbali.

Polepole nilianza kuamini kwamba ndoa haikuwa sehemu ya hatima yangu.
Hakuna kitu kinachoumiza mzazi kama kuona mtoto wake akijitahidi lakini matokeo yake yaendelee kuwa mabaya. Hivyo ndivyo nilivyokuwa nikihisi kuhusu mwanangu. TAZAMA VIDEO/ SOMA ZAIDI.

Kwa miaka kadhaa alikuwa akirudi nyumbani na matokeo ambayo hayakuwa mazuri. Walimu walikuwa wakisema hakuwa makini darasani, wengine wakisema hakupenda kusoma. Kadri muda ulivyopita, watoto wengine walikuwa wakimpita huku yeye akibaki nyuma.

Kwa kweli iliniumiza sana. Kilichoniumiza zaidi ni kusikia baadhi ya watu wakimuita mzembe. Mimi nilijua alikuwa mtoto mwenye akili, lakini nilikuwa nashindwa kuelewa kwa nini hakufanya vizuri kama wengine.

Matokeo yalipozidi kushuka, hali ikawa ngumu zaidi. Mtoto wangu alianza kupoteza confidence. Wakati mwingine alikuwa anakataa hata kuonyesha report form yake. Nilimuona akianza kuamini maneno mabaya aliyokuwa akiyasikia kutoka kwa watu.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo kila siku nilifungua biashara yangu bila kujua kama ningepata faida au hasara. TAZAMA VIDEO/ SOMA ZAIDI.

Nilikuwa nimewekeza fedha nyingi kwenye biashara yangu nikiamini ingeweza kubadilisha maisha yangu na ya familia yangu.

Mwanzoni mambo yalikuwa yanaenda vizuri, lakini baada ya muda hali ilianza kubadilika. Wateja walipungua.

Mauzo yakaanza kushuka mwezi baada ya mwezi. Nilijaribu matangazo mbalimbali, offers, na hata kupunguza bei za bidhaa zangu, lakini matokeo hayakuwa mazuri kama nilivyotarajia.

Kwa kweli nilianza kuchoka. Kilichoniumiza zaidi ni kuona madeni yakiongezeka huku mapato yakipungua.

Kulikuwa na wakati nilishindwa hata kulipa baadhi ya bili kwa wakati. Watu wa karibu walianza kuniambia nifunge biashara kabla sijapata hasara kubwa zaidi.
Sikuwahi kufikiria kwamba siku moja ningejikuta nikituhumiwa kwa kosa ambalo sikuwahi kulifanya. Nilikuwa nikiishi maisha ya kawaida kijijini kwetu.SOMA ZAIDI/TAZAMA VIDEO

Watu walinifahamu kama mtu mtulivu, mwenye bidii, na asiye na ugomvi na mtu yeyote. Nilikuwa na marafiki wengi na niliheshimika katika jamii.

Lakini siku moja kila kitu kilibadilika. Kulitokea tukio la wizi katika eneo letu, na ghafla jina langu likaanza kutajwa. 

Mwanzoni nilidhani ilikuwa ni tetesi za kawaida ambazo zingeisha haraka. Lakini kadri siku zilivyopita, watu wengi zaidi walianza kuamini kwamba mimi ndiye nilihusika.

Kwa kweli nilivunjika moyo. Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu ambao walikuwa wakinisalimia kila siku wakianza kuniepuka. 

Baadhi yao walikuwa wakininyoshea vidole kwa siri, huku wengine wakizungumza kunihusu nyuma yangu.

Nilijaribu kueleza ukweli. Lakini ilionekana kama hakuna aliyekuwa tayari kunisikiliza. Watu walikuwa tayari wameunda maoni yao kuhusu mimi. Hata baadhi ya ndugu zangu walionekana kuwa na mashaka.

Kulikuwa na usiku nilikosa usingizi. Nilikuwa nikijiuliza ni kwa nini jambo lile lilikuwa limenitokea. Nilihofia kupoteza kabisa heshima niliyokuwa nimeijenga kwa miaka mingi. Kulikuwa na wakati nilitaka kuondoka kijijini.
Miaka saba ni muda mrefu sana kumkosa mtu unayempenda. Lakini ndivyo ilivyokuwa kwetu baada ya kaka yangu kutoweka ghafla bila kuaga wala kuacha maelezo yoyote. Mwanzoni tuliamini angerudi baada ya siku chache. TAZAMA VIDEO/ SOMA ZAIDI.

Tulidhani labda alikuwa amesafiri au alikuwa na matatizo aliyohitaji kuyatatua peke yake. Lakini siku zikageuka wiki. Wiki zikageuka miezi. Na miezi ikageuka miaka. Kwa kweli ilikuwa kipindi kigumu sana kwa familia yetu.

Mama yangu alikuwa akikesha akiomba na kutamani kusikia sauti yake tena. Kila simu iliyopigwa kutoka namba ngeni ilitupa matumaini kwamba huenda alikuwa amepatikana. Lakini mara nyingi tulibaki na maswali kuliko majibu.

Tulijaribu kutafuta taarifa kupitia marafiki zake, watu aliokuwa akifanya nao kazi, na hata ndugu wa mbali. Wakati mwingine tulipata taarifa zilizotupa matumaini, lakini zilikuja kuonekana si za kweli.

Kadri miaka ilivyopita, maumivu hayakuondoka. 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu amesema Serikali itaendelea kushirikiana na Taasisi za Dini nchini kuimarisha maadili kwa jamii na kukuza maemdeleo.

Mhe. Sangu amesema hayo alipomwakilisha Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba katika hafla ya kumsimika uaskofu mchungaji Daniely Liyaseke wa Kanisa la The Charismatic Episcopal Church of Tanzania, Dayosisi mpya ya Ukanda wa Tanzanite One, iliyofanyika Mei 31, 2026 Kijiji cha Terat, Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Sangu amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango wa makanisa katika kuimarisha maadili, mshikamano wa kijamii na maendeleo ya Taifa na itaendeleza ushirikiano huo. Ameongeza kuwa kauli mbiu ya kanisa hilo “Kwa neema ya Mungu, tunajenga Huduma kwa vizazi vya sasa na vijavyo” inaakisi dhamira ya kuwekeza kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Vile vile, Mhe. Sangu alisisitiza mambo matatu muhimu kwa Taasisi za dini ziendelee kuombea amani, mshikamano na afya njema kwa viongozi wakuu wa nchi akiwemo Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kadhalika, amesema Serikali itaendelea kushirikiana na tasasisi za dini katika malezi ya vijana ili kujenga Taifa lenye maadili, upendo na uwajibikaji, pia kuendeleza ushirikiano katika utoaji wa elimu na huduma za kijamii kwa kizazi chenye uzalendo na uwajibikaji.

Aidha, Mhe. Sangu aliongoza harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa, Ofisi na ununuzi wa gari, ambapo katika harambee hiyo Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amechangia Shilingi Milioni 15 na Waziri Sangu amechangia Shilingi Milioni 5.

Naye, Askofu Daniely Liyaseke aliwashukuru viongozi wa Serikali, viongozi wa dini na waumini kwa mshikamano na ushirikiano, akisisitiza kuwa “ukiona kobe yupo juu ya mti, ujue kuna aliyempandisha.”

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. James Millya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mhe. Fakih Lulandala, walipongeza uongozi wa Askofu Liyaseke na kusisitiza kuwa uwepo wa Dayosisi hiyo ni nguzo ya mshikamano wa kijamii na maendeleo ya kiroho.

MBUNGE wa Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akichangia  hotuba ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum leo Juni 1,2026 bungeni jijini Dodoma.

MBUNGE wa Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akichangia  hotuba ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum leo Juni 1,2026 bungeni jijini Dodoma.

......

MBUNGE wa Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, ameitaka Serikali kuboresha mazingira ya kazi kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii nchini ikiwemo kuwapatia magari ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.

Akichangia hotuba ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum bungeni, Dkt. Jafo amesema maafisa hao ni nguzo muhimu katika kusukuma maendeleo ya jamii na wanastahili kuwezeshwa kwa vitendea kazi vinavyokidhi mahitaji ya kazi zao.

Amesema Maafisa Maendeleo ya Jamii ni mawakala wa mabadiliko katika jamii kwa kuwa karibu kila programu ya maendeleo inayotekelezwa nchini inahitaji ushiriki wao wa moja kwa moja, hivyo ni muhimu kupewa heshima na mazingira bora ya kufanyia kazi.

Dkt. Jafo ameeleza kuwa pamoja na magari, maafisa hao wanapaswa kuwa na ofisi zenye hadhi na rasilimali za kutosha zitakazowawezesha kuwafikia wananchi kwa urahisi na kutoa huduma stahiki.

Aidha, ameishauri Serikali kuanzisha vitengo vya Maendeleo ya Jamii katika wizara zote na taasisi za umma zaidi ya 325 ili kuhakikisha masuala ya maendeleo ya jamii yanapewa kipaumbele na kuratibiwa kwa ufanisi katika sekta mbalimbali.

Pia amependekeza kuanzishwa kwa Kitengo cha Uratibu wa Sekta ndani ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii kitakachosaidia kuunganisha taarifa za maendeleo kutoka wizara na taasisi mbalimbali, hatua ambayo alisema itaiwezesha nchi kuwa na mfumo imara wa kufuatilia maendeleo ya wananchi na taifa kwa ujumla.

 


Na OWM - TAMISEMI, Dar es Salaam


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amesema jumla ya wanafunzi 246,197 wakiwemo wasichana 114,102 na wavulana 132,095 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano mwaka 2026 wanatakiwa kuripoti shuleni kuanzia Julai 04, 2026 hadi Julai 31, 2026 kwakuwa muhula wa kwanza wa masomo utaanza Julai 06, 2026. 

Prof. Shemdoe amesema hayo leo Juni 01, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi Ndogo ya Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI Magogoni Jijini Dar es Salaam, wakati akitoa taarifa kwa umma kuhusu wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya elimu ya ufundi kwa mwaka 2026.

“Wanafunzi 172,114 sawa na asilimia 69.9 wakiwemo wasichana 85,987 na wavulana 86,127 wenye sifa wamechaguliwa kujiunga na kidato cha tano katika shule  za sekondari za Serikali 856 zikiwemo shule za bweni 825, kutwa 25 na kutwa na bweni sita (06),” amefafanua Prof. Shemdoe.

Aidha, Prof. Shemdoe amesema jumla ya wanafunzi 74,083 sawa na asilimia 30.1  wakiwemo wasichana 28,115 na wavulana 45,968 wamechaguliwa kujiunga na vyuo vya Ufundi.

“Wanafunzi 3,144 wakiwemo wasichana 1,170 na wavulana 1,974 wamechaguliwa kujiunga na fani mbalimbali katika vyuo 04 vya elimu ya ufundi, vyuo hivyo ni Chuo cha Ufundi cha Arusha (ATC), Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST) na Chuo cha Maendeleo ya Maji (WMDI),” ameeleza Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe amesisitiza kwamba, uchaguzi wa wanafunzi wa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya elimu ya ufundi umefanyika kwa kuzingatia ufaulu na nafasi zilizopo katika shule; hivyo, hakutakuwa na fursa ya kufanya mabadiliko yoyote ya Shule kutokana na ukosefu wa nafasi.  

Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi zilizotumika kujenga miundombinu bora ya shule za kidato cha tano na vyuo vya kati ambayo itatumika kuwahudumia wanafunzi 246,197 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya elimu ya ufundi mwaka 2026.




>Yalenga Kuimarisha Ufanisi wa Chama

Na Oscar Assenga,TANGA

Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga kimeongeza kasi ya utekelezaji wa mradi wake wa ujenzi wa nyumba 36 za watumishi baada ya Mwenyekiti wa chama hicho mkoani humo, Rajab Abdulrahman, kukabidhi shilingi milioni 500 kwa ajili ya kukamilisha mradi huo unaotekelezwa katika wilaya tisa za mkoa huo.

Fedha hizo zilikabidhiwa  kwa Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga, Mfaume Kizigo, katika hatua inayodhihirisha dhamira ya chama ya kuboresha mazingira ya kazi na makazi kwa viongozi wake wa ngazi za wilaya.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Rajab alisema mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba mwaka huu na kwamba utakuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha utendaji wa watumishi pamoja na shughuli za chama katika maeneo mbalimbali ya mkoa.

Alieleza kuwa mradi huo una thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 2.5, huku fedha zote zinazohitajika kwa ajili ya utekelezaji wake zikiwa tayari zimepatikana kupitia michango ya wanachama, viongozi na wadau mbalimbali wa chama.

"Mradi huu unagharimu jumla ya shilingi bilioni 2, milioni 500 na laki 250. Fedha hizi zimepatikana kupitia michango mbalimbali ikiwemo milioni 56 zilizotolewa awali, milioni 10 kutoka kwa MNEC pamoja na michango iliyokusanywa kutoka wilaya zote za mkoa," alisema Rajab.

Mwenyekiti huyo alibainisha kuwa kukamilika kwa nyumba hizo kutasaidia kutatua changamoto za makazi kwa baadhi ya viongozi wa chama katika ngazi ya wilaya, jambo litakaloongeza utulivu wa kazi, uwajibikaji na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Alisema nyumba hizo si tu kwamba zitakuwa makazi ya viongozi, bali pia ni uwekezaji wa muda mrefu wa chama katika kujenga taasisi imara yenye uwezo wa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kuendelea kuwahudumia wanachama wake.

"Tunajenga misingi ya chama kwa vizazi vya sasa na vijavyo. Viongozi wanaweza kubadilika, lakini miundombinu tunayojenga leo itaendelea kulitumikia chama kwa miaka mingi ijayo," alisisitiza.

Rajab aliongeza kuwa ujenzi wa chama ni jukumu endelevu linalohitaji mshikamano wa wanachama wote, akisisitiza kuwa maendeleo ya chama hayawezi kupatikana bila ushiriki wa pamoja wa wanachama wake.

Kutokana na hilo, aliwataka wana-CCM wa Mkoa wa Tanga kuendelea kuchangia kwa hali na mali, kutumia elimu na uzoefu wao pamoja na nguvu kazi katika kukiimarisha chama.

Kwa upande wake, Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga, Mfaume Kizigo, alisema mradi huo ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa chama wa kuimarisha utendaji wake katika ngazi za wilaya kwa kuhakikisha viongozi wanapata mazingira bora ya kazi na makazi.

Alifafanua kuwa kila wilaya imepangiwa kujenga nyumba nne ambazo zitatumika na viongozi muhimu wa chama na jumuiya zake.

"Kila wilaya imepangiwa kujenga nyumba nne ambazo ni nyumba ya Katibu wa CCM wa Wilaya, nyumba ya Katibu wa Jumuiya ya Vijana, nyumba ya Katibu wa Jumuiya ya Wazazi pamoja na nyumba ya Katibu wa UWT," alisema Kizigo.

Alieleza kuwa uwepo wa nyumba hizo utasaidia kupunguza gharama za upangaji wa makazi, kuimarisha upatikanaji wa viongozi katika maeneo yao ya kazi na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa shughuli za chama na jumuiya zake.

Kwa mujibu wa Kizigo, kukamilika kwa mradi huo kutakuwa hatua muhimu katika kuijengea CCM Mkoa wa Tanga miundombinu imara itakayosaidia kuendeleza shughuli zake za kisiasa, kiutawala na kijamii kwa ufanisi zaidi katika miaka ijayo.

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Benezeth Lutege, akizungumza wakati wa ufunguzi wa Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agness K. Meena. Warsha hiyo imefanyika leo Juni 1, 2026, katika Ukumbi wa Masailand Hall jijini Arusha.

Mkurugenzi Msaidizi wa Epidemiolojia na Magonjwa ya Mifugo Yanayovuka Mipaka (TADs) akitoa mchango wake katika majadiliano ya Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, iliyofanyika leo Juni 1, 2026, jijini Arusha.

Afisa Habari II wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Chiku Makwai, akitoa mchango wake katika majadiliano ya Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, iliyofanyika leo Juni 1, 2026, jijini Arusha.

Afisa Sheria I wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bw. Denis Ukaka, akitoa mchango wake katika majadiliano ya Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, iliyofanyika leo Juni 1, 2026, jijini Arusha.

Na Chiku Makwai – ARUSHA

Shirika la Afya ya Wanyama Duniani (WOAH), kwa kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, limeanza mchakato wa kuandaa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, hatua inayolenga kuimarisha uwezo wa nchi katika kuzuia, kudhibiti na kukabiliana na milipuko ya magonjwa ya mifugo.

Warsha ya kuandaa rasimu hiyo imefunguliwa leo, Juni 1, 2026, katika Ukumbi wa Masailand Hall jijini Arusha na Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo, Dkt. Benezeth Lutege, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Agness K. Meena.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo, Dkt. Lutege amesema mawasiliano yenye ufanisi ni nyenzo muhimu katika kudhibiti na kukabili milipuko ya magonjwa ya mifugo kwa kuwa huwezesha utoaji wa taarifa sahihi kwa wakati kwa wadau wote wanaohusika.

Amesema Serikali inaendelea kuimarisha mifumo ya tahadhari na mwitikio wa haraka ili kuhakikisha magonjwa ya mifugo yanagunduliwa na kudhibitiwa mapema kabla hayajasababisha athari kubwa kwa uzalishaji, biashara ya mifugo na afya ya jamii.

“Mkakati huu utaweka msingi wa kuwa na mfumo mmoja wa kitaifa wa mawasiliano ya dharura utakaoongoza utoaji wa taarifa, ushirikishwaji wa wadau na usimamizi wa mawasiliano wakati wa matukio ya milipuko ya magonjwa ya mifugo,” amesema Dkt. Lutege.

Aidha, amebainisha kuwa magonjwa mbalimbali ya mifugo, ikiwemo Homa ya Bonde la Ufa (Rift Valley Fever), yanahitaji uratibu madhubuti wa mawasiliano ili kuhakikisha wananchi na wadau wanapata taarifa sahihi zitakazowawezesha kuchukua hatua stahiki kwa wakati.

Warsha hiyo imewakutanisha wataalamu wa mifugo, afya ya wanyama, mawasiliano na wadau wengine kutoka taasisi za Serikali pamoja na mashirika ya kimataifa kwa lengo la kujadili mbinu bora za mawasiliano ya hatari, usimamizi wa taarifa za dharura na mikakati ya kuimarisha mwitikio wakati wa milipuko ya magonjwa.

Washiriki pia wanatarajiwa kujadili matumizi ya teknolojia za kisasa katika utoaji wa taarifa pamoja na namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya sekta ya afya ya wanyama na afya ya binadamu kwa kuzingatia dhana ya Afya Moja (One Health).

Kupitia warsha hiyo, Tanzania inatarajia kuwa na mkakati madhubuti wa mawasiliano ya dharura utakaosaidia kuimarisha mifumo ya tahadhari ya mapema, kuongeza mwitikio wa haraka wakati wa matukio ya dharura na kulinda ustawi wa mifugo sambamba na kuchangia maendeleo ya uchumi wa taifa.

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Dunia la Haki Miliki (WIPO) kwa kushirikiana na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) pamoja na Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, wamezindua mradi wa miezi 12 utakaotumia teknolojia zilizopo kwenye kanzidata za kimataifa za hakimiliki kuongeza thamani ya mazao, kupunguza gharama za uzalishaji na kuimarisha sekta za kilimo na ufugaji nchini.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilikuwa sijitambui tena. Mwanzoni nilikuwa mtu mwenye furaha, confidence, na aliyependa kujitokeza mbele za watu. 

Nilipenda kuvaa vizuri, kuzungumza kwa uhuru, na kujiamini kwenye kila sehemu niliyokuwa.

Lakini kadri muda ulivyopita, mambo yalianza kubadilika. Nilipitia maumivu mengi ya mahusiano. Nilivunjwa moyo mara kadhaa na watu niliowaamini sana. 

Kila relationship ilipoisha vibaya, nilianza kupoteza sehemu ya confidence yangu. Polepole nilianza kuamini labda mimi ndiye nilikuwa tatizo.

Kwa kweli iliniumiza sana. Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu wengine wakionekana wenye furaha kwenye mahusiano huku mimi nikijihisi kama sipendwi au sioni bahati kabisa. Wakati mwingine hata nikitaka kuzungumza na mtu mpya, nilikuwa najihisi sina mvuto wa kutosha.

Kulikuwa na siku nilijifungia ndani. SOMA ZAIDI.
Kwa miezi 18 maisha yangu yalizunguka jambo moja tu kutafuta kazi. Kila asubuhi nilikuwa naamka mapema, kufungua simu au laptop yangu, na kutafuta matangazo mapya ya ajira.

Nilikuwa na ndoto ya kupata kazi nje ya nchi ili niweze kubadilisha maisha yangu na kusaidia familia yangu. Niliamini elimu na uzoefu wangu vingefungua milango mingi. Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia.

Nilituma CV kwa kampuni nyingi sana. Kila nilipoona tangazo jipya, nilihakikisha nimetuma maombi yangu kwa wakati. Wakati mwingine nilikuwa natumia saa nyingi kurekebisha CV na cover letter ili ziendane na nafasi husika.

Kilichoniumiza zaidi ni kutopata majibu. Wiki zikageuka miezi. Nilikuwa naangalia email kila siku nikitarajia mwaliko wa interview, lakini hakuna kilichokuwa kinatokea. Wakati mwingine nilipokea ujumbe wa kukataliwa, na mara nyingi sikupata jibu lolote.

Kwa kweli nilianza kukata tamaa. Nilianza kujiuliza kama kulikuwa na tatizo kwenye qualifications zangu au kama ndoto yangu ilikuwa kubwa sana. Watu wengine walinishauri niache kufikiria kazi za nje na nijikite kwenye nafasi za karibu. SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilifikiri nimepoteza pesa zangu milele. Nilikuwa nimeweka akiba kwa muda mrefu nikitarajia kuanzisha biashara ambayo ingebadilisha maisha yangu. Nilitumia miezi mingi kujinyima mambo mengi ili kukusanya mtaji huo.

Ndiyo maana siku nilipopata nafasi iliyoonekana kuwa nzuri mtandaoni, niliona kama ndoto yangu ilikuwa karibu kutimia. Mwanzoni kila kitu kilionekana cha kawaida.

Mtu niliyekuwa nikizungumza naye alionekana mtaalamu na mwenye kuelewa biashara. Alikuwa na maelezo mazuri, ahadi za faida, na alijibu maswali yangu kwa kujiamini. Kadri mazungumzo yalivyoendelea, nilianza kumuamini.

Hatimaye nilituma pesa. Baada ya kufanya malipo, mambo yakaanza kubadilika. Simu zilianza kutopokelewa, ujumbe haukujibiwa kwa wakati, na maelezo yalikuwa yanabadilika kila siku. Hapo ndipo nilianza kutambua kuwa huenda nilikuwa nimetapeliwa.

Kwa kweli niliumia sana. Kilichoniumiza zaidi ni kujua kuwa sehemu kubwa ya akiba yangu ilikuwa imeenda kwa muda mfupi sana. 

Nilihisi hasira, huzuni, na aibu kwa wakati mmoja. Kulikuwa na usiku nilikosa usingizi nikifikiria jinsi ningeeleza familia yangu kilichotokea. SOMA ZAIDI.
Nilipoanzisha biashara yangu, nilikuwa na matumaini makubwa sana. Nilikuwa naamini kwamba bidhaa zangu zingepata soko haraka na maisha yangu yangeanza kubadilika. 

Nilitumia akiba yangu kununua bidhaa, nikafungua ukurasa wa Facebook, na kuanza kutangaza kila siku.

Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia. Kila nilipopost bidhaa zangu, watu walikuwa wanapenda picha na wakati mwingine kuacha comments, lakini hakuna aliyekuwa akinunua. Siku zikageuka wiki, wiki zikageuka miezi, na bado mauzo yalikuwa karibu sifuri.

Kwa kweli nilivunjika moyo. Kilichoniumiza zaidi ni kuona biashara nyingine zikikua kupitia Facebook huku mimi nikihangaika kupata hata mteja mmoja wa kweli. Wakati mwingine nilikuwa natumia pesa kutangaza posts lakini matokeo yalikuwa madogo sana.

Nilianza kujiuliza kama nilifanya makosa kuanzisha bibiashara. Kulikuwa na siku nilifikiria kuacha kabisa na kuuza bidhaa nilizokuwa nimebaki nazo. SOMA ZAIDI.
Siku ambayo nilipokea taarifa kwamba harusi yetu haitafanyika ndiyo siku niliyohisi moyo wangu ukivunjika zaidi kuliko wakati mwingine wowote maishani mwangu.

Mimi na mpenzi wangu tulikuwa tumepanga harusi kwa miezi mingi. Familia zote mbili zilikuwa zimejiandaa, wageni walikuwa wamealikwa, na mipango mingi ilikuwa imekamilika. Nilikuwa nikihesabu siku zilizobaki kabla ya kuanza maisha mapya ya ndoa.

Lakini wiki mbili kabla ya harusi, kila kitu kilibadilika. Mpenzi wangu aliniambia kuwa alihitaji kusitisha harusi. Nilihisi kama dunia ilisimama kwa sekunde chache. 

Sikuelewa kilichokuwa kinaendelea. Nilijaribu kuuliza maswali mengi, lakini majibu hayakuwa wazi vya kutosha kunipa amani.

Kwa kweli iliniumiza sana. Kilichoniumiza zaidi ni kuwaeleza ndugu, marafiki, na watu waliokuwa tayari wamepanga kuhudhuria harusi. Nilihisi aibu, huzuni, na kuchanganyikiwa kwa wakati mmoja. SOMA ZAIDI.