Meneja wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Mkoa wa Dodoma, QS Emmanuel Wambura,akizungumza kwenye banda la TBA  katika Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela, Nzuguni jijini Dodoma.

Na.Mwandishi Wetu

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) umefungua fursa mpya za uwekezaji katika sekta ya makazi, majengo ya biashara na maendeleo ya miji, hatua inayolenga kuboresha huduma kwa wananchi, kuvutia mitaji na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Meneja wa TBA Mkoa wa Dodoma, Qs. Emmanuel Wambura, amesema hayo katika Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela, Nzuguni, jijini Dodoma.

Amesema TBA imeendelea kutekeleza kwa ufanisi miradi mbalimbali ya Serikali katika sekta tofauti, ikiwemo ujenzi wa majengo ya Wizara ya Kilimo na taasisi zake, ofisi za Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), vituo vya afya pamoja na taasisi nyingine za umma.

Kwa mujibu wa Qs. Wambura, utekelezaji wa miradi hiyo unalenga kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma kwa wananchi na kuboresha mazingira ya kazi katika taasisi za Serikali.

“TBA inaendelea kutekeleza dhamana yake ya kuhakikisha Serikali inapata majengo bora, salama na ya kisasa. Miradi mingi ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji, huku mingine ikiwa katika hatua za mwisho kukamilika ili wananchi waanze kunufaika na huduma zinazotolewa kupitia miundombinu hiyo,” amesema Qs. Wambura.

Amesema mbali na miradi ya Serikali, TBA imeweka mkazo katika kuendeleza miradi ya makazi na miji ya kisasa, ikiwemo mradi wa ujenzi wa nyumba 3,500 katika eneo la Nzuguni jijini Dodoma, ambao unaendelea kutekelezwa.

Amebainisha kuwa wakala huo umefungua fursa za uwekezaji kupitia mfumo wa ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP), ambapo tayari baadhi ya wawekezaji, ikiwemo kampuni ya Fit Group kutoka Nigeria, wameonyesha nia ya kuwekeza katika mradi huo wa makazi.

Aidha, amesema TBA imeandaa maeneo yenye fursa kubwa za uwekezaji katika mikoa mbalimbali, ikiwemo Dodoma, Dar es Salaam, Mwanza na Arusha, ambapo wawekezaji wanakaribishwa kuwekeza katika nyumba za makazi, majengo ya biashara, hoteli, ofisi na maghala ya kisasa ya kuhifadhi mazao.

Qs. Wambura amefafanua kuwa Mkoa wa Dodoma pekee una eneo la takribani hekta 630 lililoandaliwa kwa ajili ya uwekezaji, likiwa na miundombinu muhimu na mazingira rafiki kwa shughuli za biashara.

“Taratibu za uwekezaji ni wazi na rahisi. Tunawakaribisha Watanzania na wawekezaji kutoka nje ya nchi kushirikiana nasi katika kuendeleza miradi yenye tija kwa uchumi wa Taifa. Tunahitaji wawekezaji wenye uwezo na wanaozingatia sheria za nchi ili kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa viwango vinavyotakiwa,” amesema.

Katika hatua nyingine, amesema TBA imepanua wigo wa shughuli zake hadi kusimamia miradi ya ujenzi na ukarabati wa majengo ya ubalozi wa Tanzania nje ya nchi kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Amesema hatua hiyo inaonesha kuendelea kuaminiwa kwa uwezo wa kitaalamu wa wakala huo katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi ndani na nje ya Tanzania.

Akizungumzia mchango wa TBA katika sekta ya kilimo, Qs. Wambura amesema wakala huo umeendelea kubuni na kusimamia ujenzi wa maghala ya kisasa ya kuhifadhi mazao, maabara za utafiti wa kilimo na miundombinu mingine muhimu inayosaidia kuongeza thamani ya mazao, kuimarisha usalama wa chakula na kukuza ushindani wa sekta hiyo.

Amewakaribisha wananchi, taasisi na wawekezaji kutembelea banda la TBA katika Maonesho ya Nanenane ili kupata taarifa kuhusu huduma zinazotolewa na wakala huo, ikiwemo usanifu wa majengo, ukadiriaji wa gharama za ujenzi, usimamizi wa miradi na fursa mbalimbali za uwekezaji.

“TBA ipo katika mikoa yote 26 ya Tanzania na itaendelea kushirikiana na sekta binafsi katika kujenga miundombinu ya kisasa, kuvutia uwekezaji na kuchangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050,” amesema Qs. Wambura.

Meneja wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Mkoa wa Dodoma, QS Emmanuel Wambura,akizungumza kwenye banda la TBA  katika Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela, Nzuguni jijini Dodoma.

Na. Mwandishi Wetu – Dar es Salaam

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt. Tausi Kida ameongoza kikao cha Makatibu Wakuu kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kikao hicho ambaye ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Dkt. Jim Yonazi kilicholenga kujadili utendaji wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka -BRT leo 04 Agosti, 2026 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu Jijini Dar es Salaam.

Serikali kupitia Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC) imewahakikishia wakulima nchini upatikanaji wa mbolea ya kutosha kwa msimu wa kilimo wa mwaka huu, ikitangaza kuanza kwa usambazaji wa tani 33,000 za mbolea ya kupandia aina ya DAP zilizowasili nchini kupitia Bandari ya Dar es Salaam.

Akizungumza leo Agosti 4,2026 katika Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea kitaifa katika viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Uendeshaji Biashara wa Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC), Lameck Borega, amesema kampuni hiyo imejipanga kuhakikisha wakulima wanapata mbolea kwa wakati, kwa bei nafuu na katika maeneo yote ya nchi.

Amesema TFC, ambayo ni kampuni inayomilikiwa kwa asilimia 100 na Serikali chini ya Wizara ya Kilimo, ina jukumu la kuhakikisha upatikanaji wa mbolea kwa wakulima wote ili kuongeza uzalishaji na kuimarisha usalama wa chakula nchini.

Bw.Borega amesema kwa msimu wa mwaka huu kampuni imepanga kusambaza takribani tani 200,000 za mbolea za aina mbalimbali, huku meli ya MV Aurora ikiwa tayari imewasili na tani 33,000 za mbolea ya DAP ambazo zimeanza kusafirishwa kwenda vituo vya TFC na kwa mawakala wake nchini kote.

"Mbolea hii imewasili kwa wakati muafaka wakati wakulima wengi wanaendelea kuandaa mashamba yao kwa ajili ya msimu mpya wa kilimo. Lengo letu ni kuhakikisha hakuna mkulima anayekosa mbolea kutokana na ucheleweshaji wa usambazaji," amesema Borega.

Aidha, amesema Serikali inaendelea kubeba sehemu kubwa ya gharama za mbolea kupitia mpango wa ruzuku ili kupunguza mzigo kwa wakulima. Alifafanua kuwa mfuko mmoja wa kilo 50 wa mbolea ya DAP ungegharimu karibu shilingi 200,000 bila ruzuku, lakini kutokana na msaada wa Serikali mkulima analipa karibu nusu ya gharama hiyo huku Serikali ikigharamia sehemu iliyobaki.

Amesema hatua hiyo ni sehemu ya dhamira ya Serikali ya kuongeza tija katika sekta ya kilimo kwa kuhakikisha pembejeo muhimu zinapatikana kwa gharama zinazomuduwa na wakulima.

Bw.Borega ameongeza kuwa baada ya kukamilika kwa usambazaji wa mbolea ya kupandia, Serikali inatarajia kuingiza nchini tani 40,000 za mbolea ya kukuzia aina ya Urea mwezi Septemba, hatua itakayowezesha wakulima kupata pembejeo zote muhimu katika kipindi sahihi cha uzalishaji.

"Niwaondoe wasiwasi wakulima wote nchini Serikali imejipanga kikamilifu kuhakikisha mbolea inapatikana kwa wakati na kwa mfumo wa ruzuku ili kila mkulima aweze kunufaika na kuongeza uzalishaji wa mazao," amesema 

Sambamba na hilo,Bw. Borega amewataka wakulima wanaotembelea Maonesho ya Nanenane kutembelea  banda la TFC ili kupata elimu ya matumizi sahihi ya mbolea, namna ya kunufaika na mfumo wa ruzuku na mahali pa kupata mbolea hizo.

Amesema TFC pia inaendelea kushiriki maonesho ya Nanenane katika kanda mbalimbali nchini ikiwemo Mbeya, Arusha, Mwanza, Simiyu, Iringa na Morogoro, ambako wakulima wanaendelea kupewa elimu ya kitaalamu kuhusu matumizi bora ya mbolea na njia rahisi za kuzipata kupitia mtandao wa vituo na mawakala wa kampuni hiyo.

Hata hivyo amesisitiza kuwa matumizi sahihi ya mbolea ni nguzo muhimu ya kuongeza tija ya kilimo, hivyo akawataka wakulima kutumia fursa ya maonesho hayo kupata elimu itakayowawezesha kuongeza uzalishaji na kuinua kipato chao.




RAIS SAMIA KUFUNGUA MKUTANO WA UMOJA WA MABUNGE DUNIANI (IPU) JIJINI ARUSHA

Zaidi ya washiriki 2,000 kutoka nchi mbalimbali duniani wanatarajiwa kuhudhuria Mkutano wa 153 wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) utakaofanyika Oktoba 5-9, 2026 jijini Arusha.

Taarifa hiyo imetolewa na Spika wa Bunge, Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 4, 2026 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (AICC) Jijini Arusha kuhusu utayari wa Bunge kuwa mwenyeji wa mkutano huo.

Mheshimiwa Spika amesema miongoni mwa watakaoshiriki mkutano huo ni Maspika wa Bunge, Wabunge, maafisa wa Bunge, wawakilishi wa mashirika ya kimataifa na kikanda, wanadiplomasia, washirika wa maendeleo, mashirika ya kiraia, taasisi za Elimu ya juu pamoja na vyombo vya habari.

Ameitaja Kauli Mbiu ya Mkutano kuwa “Kuimarisha Utawala Bora na Kuiwezesha Jamii kupitia Ushirikishwaji, Imani na Fursa kwa Wote" na kwamba ufunguzi rasmi utafanywa na Rais, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan 05 Oktoba, 2026.

Amesema Bunge la Tanzania lipo tayari kikamilifu kuwa mwenyeji wa mkutano huo wa kihistoria na kwamba ni heshima kubwa kwa nchi na ni uthibitisho wa imani ambayo jumuiya ya kimataifa ya mabunge inayo kwa Tanzania.

"Hii inathibitisha dhamira yetu ya muda mrefu katika kudumisha demokrasia, amani, ushirikiano wa kimataifa na diplomasia ya kibunge" amesema Mheshimiwa Spika.

Mheshimiwa Spika amesema ana imani mkutano huo utaleta mchango mkubwa katika kutatua changamoto zinazokabili dunia kwa sasa ikiwemo Mabadiliko ya Tabianchi, migogoro ya kimataifa na ugumu wa maisha.

 Mbali na ratiba rasmi, amesema mkutano huo utaimarisha ushirikiano wa Kimataifa, kukuza ushirikiano wa kimkakati na kutoa fursa adhimu kwa sekta za utalii, usafirishaji na huduma nchini.

“Pia utatoa fursa ya kuionesha dunia utajiri wa utamaduni wa Tanzania, fursa za uwekezaji na vivutio vya utalii vinavyotambulika duniani,” amesema

Awali akizungumza baada ya kukagua Ukumbi wa AICC, Mheshimiwa Zungu amesema mandaliziyanaendelea vizuri kupitia ushirikiano wa karibu kati ya Bunge, Serikali, Sekretarieti ya IPU na wadau wengine.

Amewakaribisha washiriki wote Jijini Arusha katika mkutano huo.
Urafiki wa kweli ulipata nafasi ya kuadhimishwa kwa namna ya kipekee wakati wanawake kutoka maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam walipokutana katika hafla ya Girlfriends Circle, iliyoandaliwa na kampuni ya Eventfully kwa kushirikiana na Serengeti Premium Apple.

 


Na Saidina Msangi, WF, Dar es Salaam.

 

Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Africa50 Bw. Alain Ebobisse, amebainisha kuwa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Taasisi ya Africa50 (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM) pamoja na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Infra for Africa Forum), ni fursa ya kuonesha mafanikio ambayo Tanzania imeyapata katika sekta ya miundombinu, kutangaza fursa zinazopatikana ikiwa ni ushahidi kuwa uwekezaji katika miundombinu ya Afrika una tija, unalipa na unaweza kufadhiliwa.

 

Bw. Ebobisse alisema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Balozi, Khamis Mussa Omar (MB), katika kikao cha pamoja cha maandalizi kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam.

 

Bw. Ebobisse alibainisha kuwa ajenda kuu ya mkutano huo itakuwa ni ujenzi wa uchumi wa viwanda barani Afrika kupitia uongezaji thamani wa rasilimali za ndani, jambo linalotegemea kwa kiasi kikubwa uwepo wa nishati ya uhakika huku akipongeza dira ya uongozi wa Tanzania katika kuvutia mtaji wa sekta binafsi.

 

"Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ana maono makubwa ya kuvutia uwekezaji wa sekta binafsi katika sekta ya miundombinu nchini Tanzania. Sisi Africa50 ni mojawapo ya nyenzo zinazosaidia kutekeleza maono hayo kwa kushirikiana katika utekelezaji wa miradi, ambapo miundombinu mbalimbali ikiwemo nishati ni muhimu katika maendeleo ya viwanda na kutuma ujumbe kuwa Afrika iko tayari kwa uwekezaji," alisema Bw. Ebobisse.

 

Bw. Ebobisse aliongeza kuwa Africa50 imeweka kipaumbele kikubwa katika miundombinu ya gesi asilia ikiwemo mabomba na mitambo ya uchakataji ili kuelekeza gesi zaidi kwenye maeneo ya viwanda nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla ili kuongeza thamani ya rasilimali na kuimarisha uchumi wa Afrika.

 

Alisisitiza kuwa licha ya uwepo wa kundi kubwa la wawekezaji tayari wenye hamasa ya kushiriki, huo ulikuwa wakati muafaka wa kutuma ujumbe kwa Tanzania, Afrika na dunia nzima kwamba Bara la Afrika liko tayari na ni eneo salama na la kimkakati kwa uwekezaji wa miundombinu.

 

Naye Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Balozi, Khamis Mussa Omar (MB), alisema kuwa Serikali imekamilisha maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Jukwaa la Miundombinu Afrika unaolenga kuhamasisha uwekezaji wa sekta binafsi katika miundombinu ya kimkakati, ikiwemo gesi asilia, umeme na viwanda barani Afrika.

 

Alisema Tanzania itakuwa mwenyeji wa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Taasisi ya Africa50 (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM) pamoja na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Infra for Africa Forum), utakaofanyika tarehe 5 na 6 Agosti, 2026 katika Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC), Dar es Salaam unatarajiwa kufunguliwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

 

"Tunatarajia kusaini hati tatu za mashirikiano katika afya hasa usafishaji wa damu (dialysis), tumefanya tathmini ya maendeleo ya miradi ya kimkakati ikiwemo mradi wa gesi asilia, miundombinu ya usafirishaji wa nishati, pamoja na masuala mengine ya nishati yanayolenga kuharakisha maendeleo ya uchumi wa viwanda, " alisema Mhe. Balozi Omar.

 

Balozi Omar alithibitisha kuwa Serikali imejiridhisha kuwa maandalizi yote muhimu ya mkutano huo unaotarajiwa kukutanisha viongozi wa kitaifa, marais wa taasisi za kifedha, na wawekezaji wakubwa wa kimataifa yako tayari ili kuhakikisha mkutano huo wa siku mbili unapata mafanikio makubwa na kufikia malengo yaliyokusudiwa.

 Waswahili husema nyumba njema haikosi wageni na hii imedhihirika leo tarehe 4 Agosti, 2026 baada ya Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar mhe Zubeir Ali Maulid kutembelea eneo la Hifadhi ya Ngorongoro.

Akiwa katika geti la Loduare Spika Maulid alipata taarifa ya vivutio vya eneo hilo iliiyotolewa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Mariam Kobelo ambapo alielezwa kuendelea kuimarika kwa shughuli za uhifadhi,utalii na maendeleo ya jamii.

Aidha, haitoshi Spika Zubeir alielezwa kuhusiana na maajabu ya mchanga unaohama uliopo eneo la Olduvai ambapo mamia ya watu ambao mapenzi yao yamelega lega humiminika katika eneo hilo kuimarisha mapenzi.

Kwa mujibu wa simulizi za kihistoria kutokana na mchanga huo kuwa na asili ya sumaku wapendao wakifika mahali hapo penzi huwa motomoto na kuimarika.

Akizungumza baada ya ziara hiyo Spika Zubeir ametoa wito kwa watanzania kujenga utamaduni wa kutembelea vivutio vya utalii ili kujifunza na kupata utulivu.

Spika Zubeir ameipongeza Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa kufanya kazi usiku na mchana katika kulinda uhifadhi, kusimamia utalii na maendeleo ya jamii.








Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Hamad Yussuf Masauni pamoja na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith Kapinga(katikati) wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi wakati wa Mkutano wa Wadau Kuhusu Udhibiti wa Taka za Plastiki Nchini, kilichofanyika Ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam, Agosti 4, 2026.
 

Na Mwandishi Wetu, Dodoma Mfumo wa Supervisory Control and Data Acquisition (SCADA) yameimarisha udhibiti wa upotevu wa mafuta wakati wa shughuli za ushushaji kutoka melini kwenda kwenye maghala ya kuhifadhia.

Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea jijini Dodoma, Mhandisi wa PBPA, Bi. Elvira Muganga, alisema mfumo huo unaiwezesha Serikali kufuatilia kwa wakati halisi kiwango cha mafuta kinachopokelewa nchini.

Alisema SCADA hukusanya taarifa kutoka kwenye mita za Serikali zilizowekwa katika maeneo ya kupokelea mafuta na kuziwezesha kulinganishwa na taarifa za mita zilizopo kwenye maghala ya kuhifadhia mafuta.

“Ulinganishaji huu unasaidia kubaini tofauti zinazoweza kujitokeza wakati wa ushushaji na kuhakikisha kiasi cha mafuta kilichopokelewa kinarekodiwa kwa usahihi,” alisema Bi. Muganga.

Alieleza kuwa kabla ya matumizi ya teknolojia hiyo, ufuatiliaji wa shughuli za ushushaji wa mafuta ulikuwa unategemea zaidi taarifa zilizokusanywa kwa njia zisizo za moja kwa moja. Mfumo wa SCADA sasa umeongeza uwezo wa Serikali kupata taarifa sahihi kwa wakati na kusimamia operesheni hizo kwa karibu.

Kwa mujibu wa Muganga, udhibiti huo umeongeza uwazi na usalama katika mapokezi ya mafuta pamoja na kuimarisha usahihi wa taarifa zinazotumika katika ukokotoaji wa mapato ya Serikali.

Aidha, alisema matumizi ya mfumo huo yameifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zinazotumia teknolojia ya kidijitali kusimamia mapokezi ya bidhaa za mafuta na kudhibiti upotevu unaoweza kutokea wakati wa ushushaji.

Muganga alisema PBPA inatumia Maonesho ya Nanenane kutoa elimu kwa wananchi kuhusu utendaji wa mfumo huo na mchango wake katika kuhakikisha mafuta yanayoingia nchini yanasimamiwa kwa uwazi na ufanisi.

Aliwahimiza wananchi na wadau wa sekta ya nishati kutembelea banda la PBPA ili kufahamu zaidi kuhusu mfumo wa SCADA, Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja na majukumu mengine ya Wakala.

 
Viongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii leo, Agosti 4, 2026, wamehitimisha Mkutano wao wa Kimkakati (Retreat) kwa kufanya ziara maalumu ya kutembelea vivutio vya utalii ndani ya Hifadhi ya Taifa Nyerere kupitia Game Drive na utalii wa boti, wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Hassan Abbasi.


 


Katibu wa NEC, Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kitaifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Rabia Abdalla Hamid, leo Agosti 4, 2026, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Kitengo cha Siasa kutoka Ubalozi wa Marekani nchini, Ndugu Garvey Pierre, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM Lumumba, Dar es Salaam.

Mazungumzo hayo ni sehemu ya kuendeleza ushirikiano na kubadilishana mawazo kuhusu masuala mbalimbali ya kisiasa na uhusiano wa kimataifa.
Afya njema ndiyo msingi wa kila mafanikio na furaha maishani. Hata hivyo, kwa zaidi ya miaka mitatu, maisha yangu yaligeuka kuwa mfululizo wa maumivu makali yasiyovumilika.

Kila siku nilitawaliwa na maumivu makali ya miguu na mgongo yaliyokuwa yakinichoma kama sindano za moto au kuniunguza kwa ndani. Nilibaki siwezi kukaa kwa muda mrefu, siwezi kutembea umbali mfupi, wala siwezi kulala kwa amani kitandani.

​Tulitembea kwenye hospitali kubwa na za kisasa zaidi nchini. Nilifanyiwa vipimo vya kila aina kuanzia MRI, X-ray, hadi vipimo vya damu kwa madaktari bingwa wa mifupa na neva.

Hata hivyo, kila vipimo viliporudi, majibu yalikuwa yale yale ya kushangaza: vipimo vilionyesha kuwa mimi niko salama kabisa na sina tatizo lolote linaloweza kusababisha maumivu hayo! Nilipewa dawa kenda za kutuliza maumivu (painkillers), lakini hazikusaidia kitu zaidi ya kuniongezea kizunguzungu.

Akiba yangu yote ilisha kwa kulipa bili za hospitali, huku kazi na biashara zangu zikiwa zimesimama kabisa na kunifanya nionekane kama mtu aliyepooza na aliyetengwa na ulimwengu. SOMA ZAIDI.

 ​

Usingizi ni zawadi ya pekee inayomwezesha mwanadamu kupumzika na kupata nguvu mpya baada ya mahangaiko na uchovu wa mchana. 

Hata hivyo, kwa zaidi ya miaka miwili, kwangu mimi usiku ulikuwa ni wakati wa hofu, mateso, na jinamizi lisiloelezeka.

Kila mara nilipoweka kichwa changu kitandani na kufumba macho, badala ya kupata mapumziko, nilitawaliwa na ndoto mbaya na za kutisha sana. ​

Nilitawaliwa na ndoto za kufukuzwa na wanyama wa ajabu niliokuwa sijawahi kuwaona sura zao zilikuwa za kutisha, zenye macho ya moto na pembe zisizo za kawaida.

Katika ndoto hizo, nilikuwa nikikimbia kwa kasi kubwa huku nikipiga yowe bila sauti kutoka, nikijikwaa na kuanguka huku wanyama hao wakiniingia na kunitishia maisha.

Nilikuwa niamka katikati ya usiku nikiwa nimeloa jasho mwili mzima, moyo ukienda mbio kama unataka kutoka kifuani, na mwili mzima ukiwa umechoka kana kwamba nilikuwa nikikimbia kweli barabarani.

Nilianza kuogopa hata kulala, nikibaki macho usiku kucha huku afya yangu ya mwili na akili ikizorota kwa kasi. SOMA ZAIDI.

 

Kutafuta fedha ni kazi ngumu inayohitaji jasho, muda, na akili nyingi, lakini hakuna maumivu makubwa kama kuona matunda ya kazi yako yakitoweka mikononi mwako kama moshi.

Kwa miaka kadhaa, nilikuwa nikifanya kazi kwa bidii na kupata mshahara pamoja na faida nzuri kwenye biashara zangu ndogo ndogo. Hata hivyo, maisha yangu ya kifedha yaligeuka kuwa fumbo la kutisha.

Kila pesa iliyoingia kwenye mikono yangu au akaunti yangu ya benki ilikuwa ikipotea kihasara na kwa njia za ajabu sana bila mimi kufanya la maana.

​Nikipokea fedha leo, kesho yake zingeibuka dharura zisizoelezeka simu au kifaa cha gharama kinaharibika ghafla, ugonjwa usiotarajiwa unaingia nyumbani, au kosa dogo linalogharimu fedha nyingi.

Hata pale nilipojaribu kuficha pesa taslimu kwenye kabati au pochi, nilikuta zimepungua bila mtu yeyote kugusa! Nilikuwa nikikaa na kuhesabu fedha zangu jioni, lakini kufika asubuhi nakuta kiasi kikubwa kimetoweka.

Nilibaki nikiwa na madeni yasiyotibika, nikikopa hapa na kurejesha pale, huku wenzangu niliowaingiza kwenye biashara wakipiga hatua na kujenga maisha yao. SOMA ZAIDI.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), amekutana na kuagana na Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Christine Grau, kufuatia kukamilika kwa muda wake wa uwakilishi nchini.



Na Oscar Assenga, TANGA

KATIBU Tawala wa Mkoa wa Tanga Rashid Mchatta amefungua kikao kazi cha Wakurugenzi na Mameneja wa Huduma kwa Wateja wa Mamlaka za Maji nchini huku akisisitiza matumizi teknolojia ya kisasa katika kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi ili kuongeza ufanisi katika utendaji wao.

Wito huo umetolewa jijini Tanga na Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga, Rashid Mchatta, aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, wakati akifungua kikao kazi cha Wakurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Sekta ya Maji nchini.

Kikao hicho kinafanyika chini ya kaulimbiu “Huduma Janja: Matumizi ya Teknolojia kwa Huduma Bora kwa Wateja”, kikilenga kuwawezesha wakurugenzi na mameneja hao kubadilishana uzoefu na kujadili mbinu mbalimbali za kuboresha huduma kwa wananchi.

Mchatta aliipongeza Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiamini na kuiwezesha Wizara ya Maji kutekeleza miradi na programu mbalimbali zinazolenga kuboresha upatikanaji wa maji safi na huduma za usafi wa mazingira nchini.

Pia aliipongeza uongozi wa Wizara ya Maji unaoongozwa na Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, Naibu Waziri, Mhandisi Mathew Kundo, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu, Rose Ambrose, kwa juhudi wanazofanya katika kusimamia utekelezaji wa majukumu ya wizara hiyo.

Alisema mafanikio yanayoonekana katika sekta ya maji, kuanzia utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati hadi uboreshaji wa huduma kwa wananchi, yanaonesha kuwa uongozi wa wizara hiyo umejikita katika kuhakikisha huduma zinaboreshwa kila siku.

“Viongozi hawa wameonesha weledi, uzoefu na uthubutu katika kusimamia sekta ya maji. Ushirikiano wao umeendelea kuleta mafanikio yanayoonekana na wananchi wanaendelea kushuhudia mabadiliko katika huduma za maji na usafi wa mazingira,” alisema Mchatta.

Alisema kikao hicho ni fursa muhimu kwa wakurugenzi na mameneja wa huduma kwa wateja kujifunza, kubadilishana uzoefu na kutafuta suluhisho la changamoto zinazojitokeza katika utoaji wa huduma.

Kwa mujibu wa Mchatta, mafunzo hayo pia yanahusu ufanisi wa biashara katika mamlaka za maji pamoja na mbinu za uwekezaji binafsi, ambapo wataalamu kutoka UTT-AMIS wanashiriki kutoa elimu kwa washiriki.

Aliwataka washiriki kutumia kikamilifu fursa hiyo kujifunza mbinu mpya, kubadilishana uzoefu na kujadili changamoto zinazowakabili katika utoaji wa huduma kwa wateja.

“Ninaamini mafunzo haya yatakuwa chachu ya kuboresha ufanisi mtakaporudi katika vituo vyenu vya kazi na hivyo kuongeza ubora wa huduma mnazozitoa kwa wananchi,” alisema.


JUKWAA LA WAKURUGENZI LAZIDI KUKUA

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Wakurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Mamlaka za Maji nchini, Alawi Ahmad, alisema jukwaa hilo ni sehemu muhimu ya uongozi katika sekta ya maji, kwa kuwa linawapa nafasi wakurugenzi na mameneja kukutana, kujadiliana na kutafuta suluhisho la changamoto zinazowakabili katika utoaji wa huduma.

Alisema jukwaa hilo limekuwa likifanya vikao kila mwaka na kwa sasa lina takribani miaka 10 tangu kuanzishwa kwake.

“Jukwaa hili limekuwa likitusaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika utoaji wa huduma kwa wateja na pia limetumika kama sauti ya pamoja ya wakurugenzi wa huduma kwa wateja katika sekta ya maji,” alisema Ahmad.

Naye Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Abbas Muslim Pyarali alisema kikao hicho kinawakutanisha wakurugenzi wa mamlaka za maji wanaojikita katika utoaji wa huduma kwa wateja.

Abbas ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi wa Usafi wa Mazingira kutoka Wizara ya Maji alisema kikao hicho kitakachodumu kwa siku tatu kitawapa washiriki nafasi ya kupata mafunzo maalumu na kubadilishana uzoefu kuhusu namna bora ya utoaji wa huduma kwa wananchi.

Alisema hatua hiyo ni sehemu ya juhudi za Wizara ya Maji za kuhakikisha huduma za maji safi na usafi wa mazingira zinaendelea kuboreshwa nchini.