Na: OWM – TAMISEMI, Dodoma


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amewaasa viongozi katika Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kuepuka migogoro miongoni mwao na baina yao na watumishi wanaowaongoza, akisisitiza kuwa migogoro mahali pa kazi inakwamisha ufanisi na azma ya Serikali ya kuwapelekea wananchi huduma bora.

Prof. Shemdoe ametoa wito huo leo, Agosti 21, 2026, wakati akifunga Mkutano Mkuu wa 16 wa Mwaka wa Taasisi ya Maboresho katika Mamlaka za Serikali za Mitaa (TOA), uliofanyika kwa siku tatu kuanzia Agosti 19 hadi 21, 2026, katika Ukumbi wa Jiji  Mtumba, jijini Dodoma.

“Niwaase na kuwaomba sana muepuke migogoro miongoni mwenu; kati ya Mkurugenzi na Katibu Tawala, kati ya Mkurugenzi na Mkuu wa Wilaya, kati ya RAS na Mkuu  wa Mkoa, na kati ya kiongozi na watumishi unaowaongoza. Mahali penye migogoro hakuna ufanisi wa kazi na maendeleo,” amesema Prof. Shemdoe.

Amesema viongozi na watumishi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa wanapaswa kufanya kazi kwa kuheshimiana, akisisitiza kuwa hakuna sababu kwa Mkurugenzi wa Halmashauri kupambana na Mwenyekiti wa Halmashauri au Mstahiki Meya.

Prof. Shemdoe amesema uzoefu wake katika uongozi umemfundisha umuhimu wa ushirikiano na kuheshimiana, akieleza kuwa alipokuwa Mkurugenzi wa Halmashauri hakuwahi kugombana na Mwenyekiti wa Halmashauri, na alipokuwa Katibu Tawala wa Mkoa hakuwahi kupishana lugha na Mkuu wa Mkoa.

Aidha, Prof. Shemdoe amewataka viongozi hao kutumia maarifa, weledi na uzoefu wao katika kuwatumikia wananchi, akieleza kuwa Serikali za Mitaa ziko karibu zaidi na wananchi na hivyo ni kimbilio lao katika kupata huduma mbalimbali.

Amesema wananchi wanapopima mafanikio ya Serikali, kwa kiasi kikubwa huyapima kupitia huduma wanazozipata katika maeneo yao, zikiwemo huduma za afya ya msingi, elimu ya msingi, usafiri na usafirishaji.

Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe ametumia fursa hiyo kumshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuidhinisha na kuleta fedha kwa ajili ya uendeshaji wa Taasisi za Umma na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Amesema fedha hizo zinaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wananchi kufanya shughuli za kiuchumi na kujiingizia kipato kwa ajili ya kuendesha maisha yao.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Taasisi ya Maboresho katika Mamlaka za Serikali za Mitaa (TOA), Bw. Albert Gabriel Msovela, amemhakikishia Prof. Shemdoe kuwa wajumbe wa taasisi hiyo ni askari wake kiutendaji na kwamba TOA itaendelea kutekeleza majukumu yake ya msingi kwa mujibu wa Katiba.

Bw. Msovela amesema TOA itaendelea kushirikiana na Serikali katika kutekeleza malengo mbalimbali ya kitaifa, ikiwemo utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

“Mhe. Waziri, naomba nikuhakikishie kwamba kupitia Mkutano Mkuu huu wa 16 wa Mwaka wa TOA, tutatoka na mikakati, maazimio pamoja na mipango madhubuti ambayo tutakwenda kuwashirikisha wananchi katika utekelezaji wake kwa ajili ya kuwaletea wananchi maendeleo,” amesisitiza Bw. Msovela.

Mkutano Mkuu wa 16 wa Mwaka wa TOA uliowakutanisha Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na Makatibu Tawala wa Wilaya, umefanyika chini ya Kaulimbiu isemayo: “Ugatuzi wa Madaraka katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ni Nguzo Madhubuti ya Kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.”

NAIBU Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Bw. Atupele Mwambene ametoa wito kwa walimu walioshiriki mafunzo ya somo la Elimu ya Biashara kuonesha ushirikiano kwa walimu wataowakuta katika vituo vyao vya kazi ili kuwasaidia watoto katika malezi pamoja na ujifunzaji.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu imeiomba Serikali kuongeza ruzuku kwa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), ili kuwezesha kuongeza kasi ya ujenzi wa nyumba za makazi ya watumishi wa umma nchini.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Selemani Kakoso, wakati wa ziara ya kukagua miradi ya nyumba za watumishi inayotekelezwa na TBA katika maeneo ya Kisasa na Nzuguni jijini Dodoma, ikiwa ni sehemu ya ziara ya kutathmini utekelezaji wa miradi ya miundombinu nchini.

Kakoso amesema Kamati imejiridhisha na juhudi zinazofanywa na Serikali pamoja na TBA katika kukabiliana na changamoto ya makazi kwa watumishi wa umma, huku akisisitiza umuhimu wa kuongeza kasi ya ujenzi kutokana na mahitaji makubwa ya nyumba nchini.

Amesema eneo la Nzuguni lenye takribani ekari 630 lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa makazi ni hatua muhimu katika kuendeleza mji mpya wa Serikali, kwa kuwa uwepo wa nyumba hizo utawasaidia watumishi, wakiwemo walio katika ngazi za chini, kupata makazi yaliyo karibu na maeneo yao ya kazi.

“Tunawapongeza Serikali kwa juhudi kubwa zilizofanyika na pia TBA kwa mipango mizuri ya kuandaa nyumba za makazi ya watumishi. Tumekagua eneo la Kisasa na tumeona maboresho makubwa katika nyumba zilizojengwa,” amesema Kakoso.

Hata hivyo, Kamati imeishauri Serikali kuharakisha upatikanaji wa wabia kupitia utaratibu wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP), ili kuongeza uwezo wa TBA kutekeleza miradi mikubwa ya nyumba kwa wakati na kukidhi mahitaji ya watumishi.

Kwa mujibu wa Kamati hiyo, ushirikishwaji wa sekta binafsi utawezesha kupatikana kwa mitaji na utaalamu zaidi, huku Serikali ikiendelea kusimamia miradi hiyo kuhakikisha inatoa huduma bora na nyumba zenye viwango vinavyokidhi mahitaji ya watumishi.

Kuhusu huduma ya maji, Kamati imepongeza TBA kwa kuanzisha mfumo wake wa maji bila kutegemea kikamilifu huduma kutoka Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA).

Hata hivyo, imeitaka TBA kuongeza juhudi za kuchimba visima na kuimarisha mifumo ya majitaka ili kukidhi mahitaji ya eneo hilo kwa muda mrefu.

Aidha, Kamati imeishauri TBA kuangalia uwezekano wa kutumia nishati ya jua kama chanzo mbadala cha umeme, hatua ambayo itasaidia kupunguza utegemezi wa mfumo wa kawaida wa umeme na kuhakikisha huduma zinaendelea kupatikana wakati changamoto za umeme zinapotokea.

Vilevile, Kamati imeitaka Wizara ya Ujenzi kushirikiana na Ofisi ya Rais-TAMISEMI, TANROADS, TARURA pamoja na TBA katika ujenzi wa miundombinu bora ya barabara katika maeneo hayo, hususan barabara za lami, ili kuongeza mvuto wa makazi hayo na kurahisisha usafiri.

Kamati imesisitiza kuwa ujenzi wa nyumba za watumishi ni uwekezaji wa muda mrefu unaopaswa kuzingatia thamani ya fedha, ubora wa majengo na mahitaji ya wananchi, ili miundombinu hiyo iwe na tija kwa Serikali na kizazi cha sasa na kijacho.

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Miliki wa TBA, Said Rajabu Mndeme, aliyemwakilisha Mtendaji Mkuu wa TBA, amesema mradi huo unatekelezwa katika eneo lenye takribani ekari 640, ambapo ujenzi wa nyumba 150 tayari umekamilika.

Amesema nyumba nyingine 110 zipo katika hatua mbalimbali za ujenzi, zikiwemo nyumba 50 za chini zilizofikia hatua ya mwisho na zinatarajiwa kuanza kutumika. Aidha, majengo mawili ya ghorofa tano yako katika hatua ya msingi, ambapo kila jengo litakuwa na uwezo wa kuhudumia familia 30.

Kwa mujibu wa Mndeme, TBA imeanza kushirikisha sekta binafsi katika utekelezaji wa mradi huo baada ya eneo hilo kutangazwa na wadau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi kuwasilisha mapendekezo ya kushirikiana na Wakala.

Amesema mradi huo umepangwa kuwa na huduma muhimu zikiwemo shule za awali, shule mbili za msingi, maeneo ya biashara pamoja na vyuo.

Mndeme amesema mahitaji ya nyumba katika Jiji la Dodoma ni makubwa, akifichua kuwa wakati ujenzi wa nyumba 150 za awali ulipokuwa ukiendelea, TBA ilipokea zaidi ya maombi 1,000 kutoka kwa watumishi waliokuwa wakihitaji makazi.

Amesema hadi sasa, Meneja wa TBA Mkoa wa Dodoma ana maombi zaidi ya 8,000 ya nyumba kutoka kwa watumishi na wananchi, hali inayoonyesha ukubwa wa changamoto ya makazi katika jiji hilo.

Mndeme ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita na Wizara ya Ujenzi kwa kuendelea kuiwezesha TBA kupitia ruzuku, akisema mradi huo ulioanza mwaka 2021 umeendelea kutekelezwa kwa ufadhili wa Serikali.

Amesema TBA sasa inalenga kuongeza kasi ya ushirikishwaji wa sekta binafsi ili kuharakisha ukamilishaji wa mpango wa ujenzi wa nyumba 3,500 na hivyo kupunguza changamoto ya makazi katika Jiji la Dodoma.

 


Na Oscar Assenga, TANGA

Programu ya Tanga Yetu imeendelea kuwa chachu ya maendeleo kwa vijana na watoto wa Jiji la Tanga, kupitia miradi inayolenga kuimarisha elimu, ujuzi, teknolojia na ubunifu kwa ajili ya kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii.

Akizungumza katika Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu, Afisa Mawasiliano wa Programu ya Tanga Yetu, Cliford Sangai, alisema programu hiyo inayofadhiliwa na Foundation Botnar na kutekelezwa na Kampuni ya Innovate kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji la Tanga, imeshiriki maonyesho hayo kuonyesha matokeo ya miradi mbalimbali inayotekelezwa jijini humo.

Alisema Tanga Yetu inatekeleza zaidi ya miradi 15 katika maeneo ya elimu, teknolojia na ubunifu, ikiwa na lengo la kuhakikisha watoto na vijana wanapata fursa za kukuza uwezo wao na kutumia maarifa kutatua changamoto zinazowakabili.

“Tumekuja kwenye wiki hii kuonyesha namna ambavyo Tanga Yetu imekuwa ikifadhili miradi mbalimbali katika elimu, ujuzi na ubunifu, pamoja na kuonyesha bidhaa na suluhisho zinazotokana na mawazo ya vijana wa Tanga,” alisema Sangai.

Kwa mujibu wa Sangai, baadhi ya miradi inayotekelezwa inalenga kukabiliana na changamoto ya watoto katika kujifunza kusoma na kuandika, huku matokeo ya mradi huo yakitumika katika kutengeneza mpango wa Kitaifa wa KKK.

Alisema programu hiyo pia imejikita katika kuwawezesha vijana kutumia vipaji na ujuzi wao katika teknolojia na ubunifu, akisisitiza kuwa vijana wa Tanga wana uwezo wa kubuni na kutengeneza bidhaa zinazoweza kutatua changamoto za jamii na hata kufikia soko la kitaifa.

“Vitu ambavyo tunaona vinafanyika katika miji mingine vinafanyika pia Tanga. Vijana wetu wamekuja na bidhaa walizobuni na kuzitengeneza wenyewe, jambo linaloonyesha uwezo mkubwa walionao,” alisema.

Sangai alisema katika eneo la ujuzi, Tanga Yetu imekuwa ikiwawezesha vijana kupata mafunzo mbalimbali yanayowaongezea uwezo wa kujiajiri na kuzalisha kipato kupitia teknolojia.

Alitaja baadhi ya mafunzo hayo kuwa ni Graphic Design, uchapishaji wa mabango na T-shirt, utengenezaji wa maudhui ya kidijitali (Content Creation), usimamizi wa mitandao ya kijamii (Social Media Management) pamoja na ujuzi mwingine wa kidijitali.

Alisema vijana wanaotembelea banda la Tanga Yetu katika maonyesho hayo wanaweza kuona miradi mbalimbali inayotekelezwa katika maeneo ya elimu, ujuzi na ubunifu, pamoja na namna inavyowasaidia vijana wa Tanga kujenga uwezo na kutengeneza fursa.

Sangai alisema Tanga Yetu pia imeanzisha Mfuko wa Ubunifu wa Tanga Yetu, ambao umewezesha vijana wanane kupata ufadhili wa kujaribu mawazo yao ya kibunifu yenye lengo la kutatua changamoto zinazoikabili jamii ya Jiji la Tanga.

Alisema miongoni mwa miradi hiyo ni mfumo unaolenga kuwasaidia wavuvi kufahamu maeneo yenye samaki pamoja na kufuatilia usalama wa vyombo vyao wanapokuwa baharini.

“Tumeshazoea wavuvi kuamka usiku na kwenda kuvua bila kujua samaki wapo wapi. Vijana wamekuja na mfumo unaoweza kumsaidia mvuvi kufahamu eneo ambalo samaki wapo na kwenda kuvua kwa ufanisi zaidi,” alisema.

Aliongeza kuwa mfumo huo pia unafuatilia mwenendo wa chombo cha uvuvi, hivyo iwapo kunapotokea  ajali baharini, watu waliopo nchi kavu wanaweza kufahamu eneo ambalo chombo hicho kimepata tatizo na kuchukua hatua kwa haraka.

Sangai alisema hatua hiyo inaonyesha namna ubunifu unavyoweza kutumika kama nyenzo ya kutatua changamoto zinazolikabili Jiji la Tanga na Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake, Zainabu Msuya, mnufaika wa Mradi wa Kidijitali unaosimamiwa na Swahili Digital chini ya Programu ya Tanga Yetu, alisema amepata fursa ya kujifunza ujuzi mbalimbali wa teknolojia na sasa anaweza kutumia maarifa hayo kujiajiri na kuwawezesha vijana wengine.

Alisema mradi huo unatoa mafunzo katika maeneo ya Graphic Design, Artificial Intelligence (AI), Content Creation, Social Media Management na ujuzi wa kidijitali kwa ujumla.

Msuya alisema yeye ni mmoja wa wanufaika wa awamu ya kwanza ya mafunzo hayo na baadaye alipata nafasi ya kuwa mmoja wa wasimamizi katika awamu zilizofuata.

“Mradi huu umeweza kuwawezesha vijana wengi. Kwa awamu zilizofuata tulihusisha vijana 100 kwa kila awamu, na kwa ujumla vijana 300 wamepata mafunzo kupitia programu hii,” alisema.

Alisema mafunzo hayo yamewasaidia vijana kuongeza uelewa wa teknolojia na kupata uwezo wa kutumia mitandao ya kijamii kama sehemu ya kujenga fursa za kiuchumi.

Naye Swahibu Bilal, msimamizi wa mradi wa kidijitali, alisema programu hiyo imekuwa ikiwafundisha vijana namna ya kutumia mitandao ya kijamii kwa ufanisi na kuitumia kama nyenzo ya kutengeneza kipato.

Alisema awali vijana wengi hawakuwa na uelewa wa kutosha kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii kibiashara, lakini kupitia mafunzo hayo wameweza kujifunza namna ya kusimamia akaunti, kutengeneza maudhui na kutumia majukwaa hayo kukuza shughuli zao.

“Vijana wengi awali walikuwa hawaelewi namna ya kutumia mitandao ya kijamii kutengeneza kipato, lakini kupitia mafunzo haya sasa wanaweza kufanya mambo mbalimbali na kutumia ujuzi huo kujenga fursa zao,” alisema Bilal.

Programu ya Tanga Yetu inaendelea kushirikisha vijana katika elimu, ujuzi, teknolojia na ubunifu, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuwaandaa kutumia maarifa na vipaji vyao katika kutatua changamoto za jamii na kuchangia maendeleo ya Jiji la Tanga na Taifa kwa ujumla.



Na Mwandishi Wetu - DAR ES SALAAM


Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki, ametoa maelekezo manne kwa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), akitaka Awamu ya Pili ya Mradi wa Faiba Mlangoni Kwako (FTTH) iwanufaishe wananchi kupitia huduma yenye ubora, uhakika na gharama nafuu.

Mhe. Kairuki alitoa maelekezo hayo wakati akizindua rasmi utekelezaji wa awamu hiyo katika Ukumbi wa Johari Rotana, Dar es Salaam, akisisitiza kuwa mafanikio ya mradi hayapaswi kupimwa kwa idadi ya Home Pass pekee, bali kwa idadi ya wananchi wanaounganishwa, ubora wa huduma, kasi ya intaneti na kiwango cha kuridhika kwa wateja.

Ametaka TTCL kupanua huduma ya faiba hadi maeneo yenye makazi yanayokua, masoko, maeneo ya biashara, viwanda, shule, vyuo, vituo vya afya na ofisi za Serikali Tanzania Bara na Zanzibar.

Pia ameagiza Shirika kudumisha ubora wa huduma na kuimarisha huduma kwa wateja, ikiwemo kushughulikia malalamiko kwa haraka na kwa ufanisi.

Waziri huyo amelitaka TTCL kuhakikisha huduma inapatikana kwa gharama nafuu kwa kuandaa vifurushi vinavyokidhi mahitaji ya familia, wanafunzi, vijana na wafanyabiashara wadogo na wa kati.

Katika agizo la nne, amesisitiza uwajibikaji na nidhamu ya kibiashara katika usimamizi wa mradi, akitaka wazabuni na wakandarasi wasimamiwe kwa ufanisi ili kazi zikamilike kwa wakati, kwa ubora na kwa kuzingatia thamani ya fedha.

Amesema Faiba Mlangoni Kwako si mradi wa kujenga miundombinu ya mawasiliano pekee, bali ni hatua ya kimkakati ya kufungua fursa za elimu, biashara, ajira na ubunifu na kuchochea uchumi wa kidijitali.


Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TTCL, CPA Moremi Marwa, amesema Awamu ya Pili ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Biashara wa Miaka 10 wa Shirika wa 2025/26–2034/35.

Marwa amesema Awamu ya Kwanza imewezesha TTCL kujenga zaidi ya Home Pass 280,000 na kufikisha karibu 300,000 maungio ya huduma ya nyuzi za macho nchini.

Amesema katika Awamu ya Pili TTCL inalenga kuongeza zaidi ya Home Pass 400,000, huku ikiendelea kutumia teknolojia ya Gigabit Passive Optical Network (GPON) ili kuongeza ufanisi, kupunguza gharama za uendeshaji na kuboresha ubora wa huduma.

Ameongeza kuwa utekelezaji unafanyika kwa ushirikiano na makandarasi wa ndani na wa kimataifa, wakiwemo Huawei, ZTT na Visoll.

Waziri Kairuki amewataka wananchi kutumia huduma hiyo katika kujifunza, kufanya biashara, kuongeza uzalishaji, kubuni ajira na kupata huduma za Serikali kidijitali, huku akiwataka pia kulinda miundombinu ya mawasiliano dhidi ya uharibifu na wizi.








Mameneja wa Kanda na Mikoa wa Taasisi za Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Tume ya Ushindani (FCC) pamoja na Wakala wa Vipimo Tanzania (WMA) wameagizwa kuhakikisha hakuna bidhaa bandia na duni katika maeneo yao wanayoyasimamia kiutendaji.
Kariakoo, 20 Agosti, 2026

‎ Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi Kariakoo imeimarisha ushirikiano na uongozi wa Mabalozi Jengo kwa lengo la kuwafikia walipakodi na wadau mbalimbali kwa ufanisi zaidi.
Amani ya akili na usingizi mwanana usiku ni haki ya kila binadamu, lakini pale usiku unapogeuka kuwa uwanja wa mateso na ndoto za kutisha, maisha yote hugeuka kuwa jinamizi. Kwa zaidi ya miaka miwili, nilikuwa nikiteseka sana kila nilipoweka kichwa changu kitandani.

Nilikuwa nikoota ndoto za kufukuzwa na wanyama wakali, kuogelea kwenye maji machafu, kula chakula usiku, au kukabiliwa na watu waliokufa zamani waliokuwa wakinitisha na kuninyonga.

​Kila nilipoamka asubuhi, nilijikuta nikiwa na uchovu mwingi mwilini, maumivu ya viungo, na hofu kuu iliyoniletea msongo wa mawazo. Hali hii haikuishia kwenye usingizi tu; ndoto hizo zilianza kuniletea nuksi na mikosi kwenye maisha yangu ya kila siku.

Biashara zangu zilianza kufilisika, mahusiano yangu yakavunjika, na afya yangu ikaanza kudorora bila madaktari hospitali kuona ugonjwa wowote. Nilibaki nikihofu kufika usiku, nikiteseka kwa kukosa usingizi na kuona maisha yangu yakiangamia polepole. SOMA ZAIDI.
Kushirikiana vyema na majirani zako wa karibu ni msingi mkuu wa amani na usalama nyumbani, lakini pale unapozungukwa na majirani wenye chuki, maneno ya shombo, na fitna zisizo na msingi, nyumba yako hugeuka kuwa uwanja wa mateso.

Kwa zaidi ya miaka miwili, nilipitia maisha ya ubaguzi na kelele zisizokwisha kutoka kwa majirani zangu wa mtaani. Kila nilipofanya maendeleo madogo iwe ni kukarabati nyumba, kununua chombo kipya, au hata watoto wangu kufanya vizuri shuleni vilizua chuki na maneno ya ushirikina dhidi yangu na familia yangu.

​Ugomvi ulitengenezwa bila sababu yoyote; walitupa taka mlangoni kwangu, wakatusingizia kashfa mbaya mtaani, na kunifanyia matusi ya wazi kila nilipopita mbele zao.

Nilitumia njia zote za kiustaarabu kwa kwenda kulalamika kwa wajumbe wa mtaa, wazee wa eneo hilo, na hata polisi, lakini kila walipoonywa, chuki yao iliongezeka na kuanza kutishia usalama wa watoto wangu.

Nilibaki nikinaikwa na msongo mkubwa wa mawazo, nikipoteza kabisa amani ya kukaa kwenye nyumba yangu mwenyewe na kufikiria kuiweka sokoni ili nikimbie mateso hayo ya maneno. SOMA ZAIDI.

Kinshasa, 17 Agosti 2026: Airtel Africa imeandika historia baada ya kuwa kampuni ya kwanza ya mawasiliano barani Afrika kuzindua kibiashara intaneti ya satelaiti kwa simu nchini Jamhuriya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ikifungua ukurasa mpya katika upatikanaji wa mawasilianokatika maeneo yasiyofikiwa na minara ya kawaida ya simu.