Gifted Nature NGO ni shirika lisilo la kiserikali la Tanzania lililoanzishwa mwaka 2021 na Dr. Sophia Mfaume Kizigo, linalojikita katika kuiwezesha jamii, kulinda mazingira pamoja na kutengeneza fursa kwa vijana ili waweze kuwa na maisha yenye tija na endelevu. Kupitia programu zinazolenga jamii, shirika linashughulikia changamoto za kijamii na kimazingira huku likihamasisha elimu, uongozi, ukuzaji wa ujuzi, uwajibikaji na ushiriki wa wananchi katika maendeleo.

Miongoni mwa mipango yake muhimu ni Mradi wa ‘Shujaa Path’ ulioanzishwa mwaka 2025, unaolenga hasa kuwawezesha wavulana na vijana wa kiume ambao mara nyingi hawapati uangalizi wa kutosha katika programu mbalimbali za maendeleo. Shujaa Path umeanzishwa kutokana na kutambua changamoto zinazowakabili wavulana, zikiwemo kuacha au kutoshiriki kikamilifu katika elimu, ukosefu wa malezi na ushauri wa kitaalamu, ukosefu wa ajira na fursa za kiuchumi, ushawishi hasi wa rika pamoja na ukosefu wa mazingira bora ya kukuza vipaji na uwezo wao.

Kupitia kaulimbiu “Every Boy, A Shujaa - Kila Kijana wa Kiume ni Shujaa,” Shujaa Path hailengi tu kutatua changamoto zinazowakabili wavulana, bali kuwasaidia kutambua thamani na uwezo wao, kujenga kujiamini, kuwa na maadili mema, kupata ujuzi wa maisha, ujasiriamali na ajira, pamoja na kuwa viongozi na raia wenye mchango chanya katika familia na jamii zao.

Gifted Nature NGO inaamini kuwa kumjenga kijana leo ni kuijenga jamii bora ya kesho. Kupitia ushirikiano na Serikali, shule, jamii, wadau wa maendeleo, sekta binafsi na vyombo vya habari, shirika linalenga kuendeleza na kupanua Shujaa Path ili kuwafikia wavulana na vijana wengi zaidi Tanzania.









Muonekano wa bweni la kisasa lililojengwa kupitia mradi wa elimu wa Barrick -Twiga
Muonekano wa sehemu ya madarasa ya kisasa yaliyojengwa kwa fedha kutoka Barrick
Muonekano wa sehemu ya madarasa ya kisasa yaliyojengwa kwa fedha kutoka Barrick
Viongozi wa CCM na Serikali na madiwani mkoani Njombe wakibadilishana mawazo baada ya kufanya ziara ya kikazi katika sekondari ya Ulayasi mkoani Njombe

Viongozi wa CCM na Serikali na madiwani mkoani Njombe wakibadilishana mawazo baada ya kufanya ziara ya kikazi katika sekondari ya Ulayasi mkoani Njombe
Wakikagua moja ya bweni lililojengwa kupitia mradi wa elimu wa Barrick-Twiga
Muonekano wa miundombinu ya bweni jipya lililojengwa kupitia mradi wa elimu wa Barrick -Twiga
Viongozi wakitembelea miundombinu ya vyoo vinavyoendelea kujengwa

Muonekano wa Madarasa ya zamani katika shule hiyo

👉Wanafunzi sekondari Ulayasi Njombe wasomea katika mazingira bora
Kusoma kwa bidii na kupata shahada au vyeti vya elimu ni hatua inayotoa matumaini ya kupata ajira nzuri na kujenga maisha ya baadaye.

Hata hivyo, pale unapotumia miaka kadhaa mtaani ukituma maombi ya kazi kila siku bila hata kuitwa kwenye usahili (interview), maisha huanza kuwa mzigo mzito mno.

Baada ya kumaliza masomo yangu ya chuo kikuu, nilituma barua na vifungashio vya maombi ya kazi (CV) zaidi ya mia moja kwenye makampuni, taasisi za serikali, na mashirika mbalimbali.

​Hata hivyo, miaka ilipita bila majibu yoyote ya maana. Kila mara nilipoona fursa za kazi na kutuma maombi, majina yangu yalirukwa au barua zangu zilitupwa jalani.

Nilibaki nikitazama wenzangu tuliosoma nao na hata wengine waliokuwa na ufaulu mdogo kuliko wangu wakipata kazi nzuri na kupiga hatua kimaisha.

Nilianza kuishi kwa kutegemea wazazi na ndugu, nikipatwa na msongo mkubwa wa mawazo, unyonge, na aibu kila nilipokutana na watu mtaani waliokuwa wakiniuliza kuhusu shughuli ninayofanya. SOMA ZAIDI.

 


Na. Farida Ramadhani na Saidina Msangi, WF, Dodoma.

Serikali imewaagiza wataalamu wanaosimamia mipango na bajeti katika wizara na taasisi mbalimbali nchini kuzingatia nidhamu ya matumizi ya fedha za umma ili kuboresha utekelezaji na usimamizi wa bajeti ya Serikali.

Hayo yalibainishwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Nsubili Joshua, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba, wakati akifungua kikao kazi cha Tathmini ya Uandaaji na Utekelezaji wa Bajeti kwa watalaam kutoka wizara, idara zinazojitegemea, wakala za Serikali na Sekretarieti za mikoa na Mamlaka ya Serikali za Mitaa, kinachofanyika katika ukumbi wa Kambarage, Treasury Square, Dodoma.

Alisema ni muhimu kwa wataalamu hao kuwa na vikao vya kamati za bajeti kwa ajili ya kupanga, kuweka vipaumbele na kugawana rasilimali fedha za mafungu yao, akisisitiza utekelezaji wa majukumu ya taasisi kwa mujibu wa bajeti iliyoidhinishwa.

‘‘Nasisitiza muandae na kuhuisha mipango mikakati ya taasisi zenu kwa kuwianisha na Dira  ya Maendeleo ya Taifa 2050 na Mpango wa Nne wa  Maendeleo wa Miaka 5 (FYDP IV), na mipango mingine ya sekta’’, alisema Bw. Joshua.

Aliongeza kuwa ni muhimu kwa wataalamu hao  kuandaa mipango na bajeti za mafungu yao kwa kuzingatia mipango ya kisekta ili kufaidika na ushirikiano wa pamoja.

Aliwahimiza wataalamu hao kushiriki kikamilifu na kutoa maoni yatakayosaidia kuboresha na kuongeza ufanisi katika utekelezaji na usimamizi wa bajeti ya Serikali pamoja na kuboresha Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Serikali wa mwaka 2027/28-2029/30.

Bw. Jishua alisema ushiriki wao katika kikao hicho unaashiria kujitolea kwa pamoja katika kuboresha utekelezaji na usimamizi wa bajeti ya Serikali, kuongeza ufanisi katika mchakato wa bajeti na kuhakikisha vipaumbele vya Serikali vinatekelezwa ipasavyo.

Alibainisha kuwa kikao hicho lilikuwa jukwaa muhimu la kutafakari na kujadili kwa kina kuhusu mafanikio na changamoto zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2025/26 na Maandalizi ya Bajeti ya Serikali wa mwaka 2026/27 ili kubaini maeneo yanayohitaji maboresho kwa lengo la kupata maoni na kuweka mikakati itakayotusaidia kuboresha uandaaji wa mipango na bajeti kwa mwaka 2027/28-2029/30.
 
Aidha, aliwafahamisha kuwa mchakato wa maandalizi ya Mwongozo wa Mpango na Bajeti ya mwaka 2027/28-2029/30 umeanza na kubainisha kuwa Mwongozo huo ni nyenzo muhimu katika maandalizi ya Mipango na Bajeti za mafungu yao.

“Ushauri na mapendekezo yatakayotokana na kikao hiki yatasaidia katika kuboresha maandalizi ya Mwongozo huu. Nichukue fursa hii kuwaasa washiriki wote, kutumia fursa hii vizuri ili tuweze kupata Mwongozo wa maandalizi ya bajeti na bajeti ya Serikali nzuri na inayotekeleza kwa mwaka 2027/28-2029/30 ”, alisema Bw.Joshua.

Kwa upande wake, Kaimu Kamishna wa Idara ya Bajeti, Wizara ya Fedha, Bw. Raymond Kwohelera, alieleza kuwa kikao hicho hufanyika kila mwaka kwa ajili ya kutoa fursa kwa wataalamu na wadau kujadili kwa kina changamoto zinazojitokeza katika mchakato wa bajeti, pamoja na kutoa mapendekezo ya namna ya kuzitatua.

Alibainisha kuwa katika hatua hiyo wamehusishwa wataalamu kutoka wizara, sekta na taasisi mbalimbali, ambao wanatarajiwa kushirikiana katika kupitia utekelezaji wa bajeti, kubaini maeneo yenye changamoto na kuweka mikakati ya kuboresha mchakato huo

Kutafuta fedha na kuweka akiba kwa miaka mingi ni kazi inayotaka uvumilivu na jasho kubwa, lakini pale unapokutana na matapeli wakora wanaokupora na kukutapeli kila kitu ndani ya dakika chache, dunia yote huonekana kugeuka giza.

Kwa zaidi ya miaka kumi, nilikuwa nikifanya kazi kwa bidii na kuwekeza fedha zangu kwenye benki kwa ajili ya kununua kiwanja na kujenga nyumba ya familia.

Hata hivyo, nilikutana na kikundi cha matapeli waliojifanya ni wauzaji wa viwanja na madalali waaminifu waliokuwa na nyaraka zote za serikali zilizochorwa vizuri.

​Kwa kutumia maneno ya kuaminika na ushawishi mkubwa, walinishawishi kuwahamishia akiba yangu yote ya maisha ili kukamilisha malipo ya eneo hilo.

Lakini siku chache tu baada ya kuwakabidhi fedha hizo, simu zao zote zilianza kupatikana zikiwa zimezimwa, na nilipofuatilia eneo la kiwanja niligundua nilikuwa nimetapeliwa vibaya mno na eneo hilo lilikuwa la mtu mwingine kabisa.

Nilibaki nikiwa nimechanganyikiwa, nikilia kwa uchungu na kupatwa na msongo mkubwa wa mawazo. Nilikwenda polisi na kutoa taarifa, lakini matapeli hao walikuwa wametoweka bila kuacha alama yoyote, wakiniacha nikiwa mfilisi, masikini wa kutupwa, na nikiwa na aibu kubwa mbele ya mke na watoto wangu. SOMA ZAIDI.
Kujituma na kufanya kazi kwa uaminifu ni nguzo inayokupa heshima kwenye jamii, lakini pale maadui na watu wenye husuda wanapokutengenezea kesi ya uongo ya jinai ili kukufunga gerezani, maisha yote hugeuka kuwa jinamizi.

Kwa zaidi ya miaka miwili, nilipitia mateso mazito ya kisheria na kisaikolojia baada ya aliyekuwa bosi wangu wa zamani na washirika wake kunisingizia kesi kubwa ya wizi wa mamilioni ya fedha mahakamani.

Walitengeneza nyaraka za uongo, wakawapanga mashahidi wa uongo, na kutumia fedha zao na ushawishi wao mkubwa kuhakikisha ninahukumiwa kifungo cha miaka mingi gerezani.

​Hali hii iliniletea msongo mkubwa wa mawazo na unyonge mwingi. Kila nilipokwenda mahakamani kusikiliza kesi hiyo, niliona wazi jinsi haki yangu ilivyokuwa ikikandamizwa.

Nilitumia fedha zangu zote za akiba kulipia mawakili na gharama za kesi, lakini bado ushahidi wa uongo uliowekwa dhidi yangu ulionekana kunibana vibaya mno.

Nilibaki nikitazama familia yangu ikilia kwa hofu ya kunipoteza, huku mimi mwenyewe nikikosa usingizi na kutetemeka kila tarehe ya hukumu ilipokuwa ikikaribia, nikijua wazi kuwa maisha yangu yote yalikwenda kuangamia gerezani kwa kosa nisilolijua. SOMA ZAIDI.

Kulea mtoto na kutamani kumwona akikua akiwa na maadili mema, heshima, na mwelekeo mzuri wa maisha ni ndoto ya kila mzazi.

Hata hivyo, pale mtoto wako wa kumzaa anapogeuka kuwa kero ya mtaa, anapojihusisha na wizi, uraibu wa dawa za kulevya, na tabia za kihuni, furaha yote ya uzazi hutoweka na kubaki maumivu makubwa.

Kwa zaidi ya miaka mitatu, nilipitia mateso mazito kutokana na tabia za mwanangu wa kiume. Alianza kwa kuiba vitu vidogo nyumbani kama pesa na simu, lakini baadae tabia hiyo ilikua na kuanza kuvunja nyumba za majirani na kuiba mali za watu mtaani.

​Kila wiki nilikuwa nikipokea wageni wa usiku wakija kulalamika, kutishia kumfikisha polisi, au hata kutaka kumpiga nondo na kumchoma moto kwa hasira.

Nilitumia fedha nyingi kulipa fidia za vitu alivyoiba ili kuokoa maisha yake, nikampeleka kwenye viapo vya dini, na hata kujaribu kumfunga kamba na kumfundisha kwa vipigo, lakini hakuna kilichobadilika.

Kila alipowekwa huru, alirudi kwenye michezo hiyo hiyo kwa kasi zaidi. Nilibaki nikilia kwa aibu na unyonge, mtaa mzima ukitutenga na kuninyoshea vidole kama mzazi niliyefeli malezi, huku kila siku nikiishi kwa hofu ya kupokea taarifa za kifo chake. SOMA ZAIDI.
Afya bora ndiyo msingi mkuu wa kila utafutaji wa riziki, lakini pale mwili unapofungwa na kuteseka kwa magonjwa ya ajabu, maisha yote husimama ghafla. Kwa zaidi ya miaka miwili, nilikabiliwa na mtihani mzito uliotishia kukatisha kabisa ndoto zangu.

Yalianza kama maumivu ya kawaida ya viungo na mgongo, lakini ndani ya muda mfupi, hali ilibadilika na kuwa mbaya zaidi miguu na mikono yangu ilipooza kabisa, na kuacha mwili wangu ukiwa hauna nguvu wala uwezo wa kujitikisa.

​Nilitumia fedha zote za akiba na hata kuuza baadhi ya mali zangu ili kupata matibabu kwenye hospitali kubwa na kwa madaktari bingwa.

Hata hivyo, kila vipimo vya MRI, CT scan, na vipimo vya damu vilipofanyika, majibu yalikuja yakionyesha kuwa sina ugonjwa wowote unaoonekana kisayansi.

Nilibaki kitandani nikihudumiwa kila kitu kama mtoto mchanga, nikiteseka na maumivu makali ya ndani kwa ndani usiku kucha.

Nilianza kuona aibu na unyonge mkubwa, nikitazama familia yangu ikiteseka kwa kuniuza na kunisikitikia, huku nikipoteza kabisa matumaini ya kuwahi kusimama tena kwa miguu yangu. SOMA ZAIDI.
Kusafiri nje ya nchi kwa ajili ya masomo, kazi, au fursa za kimaisha ni ndoto ya kila kijana anayetaka kubadilisha mfumo wa maisha yake na wa familia yake.

Kwa zaidi ya miaka mitatu, nilikabiliwa na kizingiti kizito na cha ajabu sana kila nilipojaribu kukamilisha mchakato wa kusafiri kwenda ng’ambo.

Nilitumia fedha nyingi sana kulipia ada za maombi ya Visa, mawakili wa usafiri, na vipimo vya afya, lakini kila nilipofika hatua ya mwisho ya usahili (interview) au kupokea majibu kutoka ubalozi, nilipokea barua za kukataliwa.

​Mara ya kwanza nilijiambia ni bahati mbaya, lakini baada ya kukataliwa Visa mara ya nne mtawalia hata kwa safari ambazo nilikuwa na nyaraka zote halali na mwaliko rasmi ndipo nilipoanza kutambua kuna kitu kisichokuwa cha kawaida.

Kila mara nilipokaa mbele ya afisa wa ubalozi, nilipatwa na woga wa ajabu, ulimi ulikuwa mzito kujieleza, na sura yangu ilionekana kama ya mtu asiye na uaminifu mbele yao.

Nilibaki nikitazama marafiki zangu waliokuwa na nyaraka dhaifu kuliko zangu wakipata Visa kwa urahisi na kuondoka, huku mimi nikibaki nikiwa nimefilisika kwa gharama za safari zisizopatikana na kuchekwa na watu wa mtaani. SOMA ZAIDI.
Msiba wa wazazi ni pigo kubwa linalomuachia kila mtoto simanzi na ukiwa, lakini inapojitokeza hali ambapo ndugu wa damu wanatumia fursa hiyo kukudhulumu na kukupora urithi wako, maumivu yake huwa mazito mno kuvumilika.

Baada ya kuondokewa na wazazi wangu waliotutoka kwa pamoja, nilibaki mimi kama mtoto wa pekee nikiwa na matumaini ya kuendeleza mali zao ikiwemo nyumba ya familia na shamba kubwa la kilimo.

Hata hivyo, kabla hata ya siku arobaini kumalizika, mijomba na mashangazi zangu waligeuka ghafla. Walikaa kikao cha familia bila kunishirikisha, wakatengeneza nyaraka za uongo, na hatimaye walinifukuza kwenye nyumba na kupora shamba lote.

​Nilibaki mtaani nikiwa sina mbele wala nyuma, nikilia kwa uchungu na unyonge. Nilitafuta msaada kwa viongozi wa mtaa na hata kujaribu kwenda polisi, lakini ndugu hao walitumia fedha na ushawishi wao kuziba pengo kila mahali.

Nilipojaribu kuwasogelea na kuwaomba wanihurumie, walinitishia kunifanyia vitendo vya kishirikina au hata kuniondoa duniani kama nitaendelea kufuatilia mali hizo.

Nilibaki nikiishi maisha ya uombaomba, nikiwa nimekonda kwa mawazo, huku nikitazama mali za wazazi wangu zikitumiwa na watu waliokosa huruma wala woga wa Mungu. SOMA ZAIDI.
 

Na.Mwandishi Wetu

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu imeendelea kuonyesha mafanikio makubwa, ambapo tangu kuanzishwa kwake Watanzania 27 wamefanikiwa kushinda katika nyanja mbalimbali za uandishi bunifu.

Amesema mafanikio hayo yanaonyesha namna tuzo hiyo inavyoibua na kutambua vipaji vya waandishi bunifu nchini, huku idadi ya washiriki ikiongezeka kila mwaka kutoka ndani na nje ya Tanzania.

Prof. Mkenda amebainisha kuwa Serikali imewekeza takribani Shilingi milioni 800 kwa ajili ya kuchapisha vitabu vilivyoshinda tuzo hizo na kuvisambaza katika shule za Tanzania Bara na Zanzibar, hatua inayolenga kuwafikia wasomaji wengi zaidi na kuhamasisha utamaduni wa kusoma.

Aidha, Waziri Mkenda amesema tuzo hizo zimeendelea kukua na kuvutia washiriki kutoka mataifa mbalimbali, jambo linaloonyesha kuongezeka kwa hadhi yake na umuhimu wa uandishi bunifu katika kukuza fasihi na lugha ya Kiswahili.

Ameongeza kuwa tuzo hizo zimekuwa jukwaa la kuwahamasisha vijana na waandishi kutumia vipaji vyao katika kutengeneza kazi zenye ubunifu na maudhui yanayoweza kuelimisha na kujenga jamii.

“Tuzo hii sasa imeingizwa rasmi katika orodha ya tuzo za uandishi bunifu duniani, ukiitafuta mtandaoni utaona tarehe 13 Aprili ni siku ya kutoa Tuzo ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu,” amesema Prof. Mkenda.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu, Prof. Penina Mlama, amesema dirisha la kuwasilisha miswada ya kazi za ubunifu limefunguliwa rasmi leo, Agosti 19, 2026, na litafungwa Novemba 30, mwaka huu.

Ameeleza kuwa waandishi bunifu wanatakiwa kutumia kipindi cha takribani miezi mitatu kuwasilisha miswada yao, huku matangazo yenye vigezo na taratibu za kushiriki yakitolewa kupitia mitandao ya kijamii ya tuzo hiyo pamoja na mitandao ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Taasisi ya Elimu Tanzania.

Prof. Mlama amesema mshiriki anatakiwa kuwa raia wa Tanzania, kazi iwe imeandikwa kwa Kiswahili na kila mwandishi anaruhusiwa kuwasilisha andiko moja tu katika nyanja atakayochagua. Aidha, mswada unaowasilishwa unatakiwa kuwa haujawahi kuchapishwa popote.

Amefafanua kuwa miswada iliyowahi kushika nafasi ya kwanza hadi ya 10 katika miaka iliyopita haitaruhusiwa kuwasilishwa tena, ingawa waandishi waliowahi kushika nafasi hizo wanaweza kushiriki kwa kuwasilisha miswada mipya. Pia, miswada iliyowahi kushinda tuzo nyingine haitazingatiwa katika ushindani wa mwaka huu.

Kwa upande wa vigezo mahususi, tamthilia ya jukwaani inapaswa kutumia vionjo vya sanaa za maonyesho za Tanzania, iwe na muda wa dakika 40–60, isiwe na maonyesho zaidi ya sita na wahusika wasiozidi sita. Ushairi unatakiwa kuwa na mashairi yasiyopungua 50 wala kuzidi 60, huku kila shairi likiwa na beti zisizozidi 15.

Kwa riwaya, urefu unatakiwa kuwa kati ya maneno 60,000 na 100,000, wakati hadithi za watoto zinatakiwa kuwa na kati ya maneno 250 na 500 kwa hadithi moja. Prof. Mlama amesisitiza kuwa kazi zinazowasilishwa zinapaswa kuwa na mawazo asilia ya mwandishi na kujikita katika masuala muhimu ya jamii.



Na Mwandishi Wetu - Tanga


Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) inaendelea kushiriki katika Maonesho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayofanyika katika Viwanja vya Usagara jijini Tanga, ikitumia jukwaa hilo kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi salama ya mionzi na fursa zinazotokana na teknolojia ya nyuklia katika kuchochea maendeleo ya Taifa.

Maonesho hayo, yanayoratibiwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, yanawakutanisha taasisi za Serikali, taasisi za elimu na utafiti, wabunifu, wanafunzi, wataalamu pamoja na wadau mbalimbali wa sekta ya elimu, sayansi na teknolojia.

Katika banda la TAEC, wananchi, wanafunzi na wadau mbalimbali wanaendelea kupata elimu kuhusu jukumu la Tume la kusimamia na kudhibiti matumizi salama ya mionzi nchini, pamoja na mchango wa teknolojia ya nyuklia katika sekta mbalimbali zikiwemo afya, kilimo, mifugo, maji, viwanda, migodi, utafiti na nishati.

Ushiriki wa TAEC katika maonesho hayo pia unatoa fursa kwa wanafunzi na vijana kufahamu taaluma mbalimbali zinazohusiana na teknolojia ya nyuklia na umuhimu wa kujikita katika masomo ya sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati (STEM) ili kujenga kizazi cha wataalamu kitakachosaidia Taifa kutumia kikamilifu fursa zinazotokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Akifungua rasmi maonesho hayo Agosti 18, 2026, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, alisisitiza umuhimu wa elimu, ujuzi, sayansi, teknolojia na ubunifu katika kujenga uchumi wa kisasa na kuongeza uwezo wa Taifa kutumia maarifa na teknolojia katika kutatua changamoto mbalimbali za maendeleo.

Katika muktadha huo, ushiriki wa TAEC unaunga mkono juhudi za Serikali za kuhakikisha sayansi na teknolojia zinatumika moja kwa moja katika kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Teknolojia ya nyuklia ina matumizi mapana yenye manufaa kwa wananchi, ikiwemo katika uchunguzi na tiba ya magonjwa, kuongeza tija katika kilimo na mifugo, usimamizi wa rasilimali za maji, shughuli za viwandani na migodini, utafiti wa kisayansi pamoja na sekta ya nishati.

Wananchi wanaotembelea banda la TAEC pia wanapata nafasi ya kuzungumza moja kwa moja na wataalamu, kuuliza maswali na kupata ufafanuzi kuhusu usalama wa mionzi, udhibiti wa vyanzo vya mionzi na matumizi ya teknolojia ya nyuklia kwa madhumuni ya amani na maendeleo.

TAEC itaendelea kutoa elimu na kuhamasisha matumizi salama ya mionzi na teknolojia ya nyuklia kwa maendeleo endelevu ya Taifa.

“Mionzi kwa Matumizi Salama na Teknolojia ya Nyuklia kwa Maendeleo ya Taifa.”







SERIKALI imeonya kuwa mtu au taasisi itakayobainika kuharibu au kutenda kosa dhidi ya Miundombinu Muhimu ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (CII) atakabiliwa na adhabu kali kwa mujibu wa Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015.

Kaimu Mkurugenzi wa Udhibiti wa Bidhaa Bandia wa Tume ya Ushindani (FCC), Bw.Salvatory Chuwa, akiwasilisha mada  wakati wa Mkutano wa   Maafisa Biashara katika Kikao cha Tatu cha Wizara ya Viwanda na Biashara na Maafisa Biashara, kilichofanyika kwa siku mbili  jijini Dodoma.

Na Mwandishi Wetu

Tume ya Ushindani (FCC) imetoa elimu  kwa Maafisa Biashara kwa lengo la kuwaongezea uelewa kuhusu masuala ya ushindani katika biashara, udhibiti wa bidhaa bandia pamoja na umuhimu wa kumlinda mlaji dhidi ya bidhaa na huduma zisizokidhi viwango.

Semina hiyo imelenga kuwajengea uwezo Maafisa Biashara ambao wana nafasi muhimu katika kusimamia shughuli za biashara katika maeneo yao, ili waweze kutambua changamoto zinazohusiana na ushindani usio wa haki, bidhaa bandia na vitendo vinavyoweza kuwaathiri walaji.

Akitoa mada kuhusu udhibiti wa bidhaa bandia, wakati wa Mkutano wa  Maafisa Biashara nchini katika Kikao cha Tatu cha Wizara ya Viwanda na Biashara na Maafisa Biashara, kilichofanyika kwa siku mbili  jijini Dodoma.

Kaimu Mkurugenzi wa Udhibiti wa Bidhaa Bandia wa FCC, Bw. Salvatory Chuwa, ameeleza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya FCC na Maafisa Biashara katika kukabiliana na biashara ya bidhaa bandia.

"Bidhaa bandia zina madhara makubwa kwa uchumi, wafanyabiashara wanaofuata sheria na walaji, hivyo ni muhimu kwa Maafisa Biashara kuwa na uelewa wa kutosha kuhusu namna ya kubaini na kutoa taarifa kuhusu bidhaa zinazodhaniwa kuwa bandia."amesema Bw.Chuwa

Amesisitiza kuwa udhibiti wa bidhaa bandia unahitaji ushirikiano wa karibu kati ya taasisi za Serikali, wafanyabiashara na wananchi, huku akiwataka Maafisa Biashara kutumia nafasi zao kuelimisha wafanyabiashara na walaji kuhusu madhara ya bidhaa bandia.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Tafiti, Miungano ya Makampuni na Uraghibishi wa FCC, Bi. Zaytun Kikula, ametoa mada kuhusu masuala ya ushindani, akieleza umuhimu wa kuwepo kwa mazingira ya biashara yenye ushindani wa haki kwa ajili ya kukuza uchumi na kuwapa wafanyabiashara fursa sawa katika soko.

Bi.Kikula amebainisha kuwa ushindani wenye tija husaidia kuongeza ubunifu, kuboresha ubora wa bidhaa na huduma pamoja na kuwapa walaji fursa ya kupata bidhaa bora kwa bei shindani.

Aidha, amewataka Maafisa Biashara kushirikiana na FCC katika kutoa elimu kwa wafanyabiashara kuhusu sheria za ushindani na kuhakikisha kuwa vitendo vinavyoweza kuzuia au kupotosha ushindani vinatambuliwa na kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

Semina hiyo ni sehemu ya jitihada za FCC za kuimarisha uelewa wa wadau kuhusu wajibu wa kulinda ushindani katika soko, kudhibiti bidhaa bandia na kuhakikisha haki za walaji zinalindwa.

FCC imeendelea kusisitiza kuwa ushirikiano wa wadau mbalimbali, hususan Maafisa Biashara, ni muhimu katika kujenga soko lenye ushindani wa haki, bidhaa salama na mazingira bora ya biashara kwa manufaa ya wafanyabiashara, walaji na uchumi kwa ujumla.

Kaimu Mkurugenzi wa Udhibiti wa Bidhaa Bandia wa Tume ya Ushindani (FCC), Bw.Salvatory Chuwa, akiwasilisha mada  wakati wa Mkutano wa   Maafisa Biashara katika Kikao cha Tatu cha Wizara ya Viwanda na Biashara na Maafisa Biashara, kilichofanyika kwa siku mbili  jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Tafiti, Miungano ya Makampuni na Uraghibishi wa FCC, Bi. Zaytun Kikula, akiwasilisha mada  wakati wa Mkutano wa   Maafisa Biashara katika Kikao cha Tatu cha Wizara ya Viwanda na Biashara na Maafisa Biashara, kilichofanyika kwa siku mbili  jijini Dodoma.

 Maafisa Biashara nchini wakifatilia mada mbalimbali kutoka kwa wataalamu wa Tume ya Ushindani (FCC) katika Kikao cha Tatu cha Wizara ya Viwanda na Biashara na Maafisa Biashara, kilichofanyika kwa siku mbili  jijini Dodoma.

 Maafisa Biashara nchini wakifatilia mada mbalimbali kutoka kwa wataalamu wa Tume ya Ushindani (FCC) katika Kikao cha Tatu cha Wizara ya Viwanda na Biashara na Maafisa Biashara, kilichofanyika kwa siku mbili  jijini Dodoma.

 



✅YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWA SAUDI ARABIA


Shirika la Madini la Taifa( STAMICO) limefanya mazungumzo na ujumbe wa wafanyabiashara kutoka Serikali ya Saudi Arabia kuelezea fursa za uwekezaji zilizopo katika mnyororo wa rasilimali madini kwa manufaa ya watanzania.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO Dkt. Venance Mwasse katika Mkutano uliofanyika Agosti 18 2026 jijini Dar es Salam

Dkt Mwasse, amesema STAMICO inaendelea kufungua milango kwa wawekezaji kulingana na Sheria na taratibu za Serikali ili kuhakikisha inaleta manufaa kwa wote.

Amesema Shirika linazingatia misingi ya kujiendesha kibiashara na kwa uwazi ili kuzuia mianya ya urasimu na kuhakikisha inatoa matokeo yenye tija kwa haraka.

STAMICO, ni Shirika sahihi kuingia nalo ubia kwa kuwa lina wataalam wenye ujuzi na uzoefu wa kutosha, ushirika mzuri na jamii inayozunguka miradi na uwezo wa kushirikiana na taasisi zingine.

Naye, Abdulrahman Al Thobaity Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyabiashara wa Saudia Tanzania, ameshukuru kwa taarifa za fursa za uwekezaji na ushirikiano waliopata kutoka STAMICO.

Kwa upande wa wataalam meneja wa Utafiti Bw Frederick Mangasini Ametumia nafasi hiyo kuonesha fursa za uwekezaji katika miradi mbalimbali ikiwemo ya dhahabu, makaa ya mawe, shaba (copper) na uendelezaji wa wachimbaji wadogo

STAMICO inaendelea kujiimarisha na kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji kwa maslahi ya taifa.