Naibu Katibu Mkuu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM- TAMISEMI) anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila, amewataka wakandarasi wanaotekeleza miradi mbalimbali chini ya Mradi wa TACTIC kuzingatia viwango vya ubora vilivyoainishwa katika mikataba yao.

Mhandisi Mativila ametoa agizo hilo Mei 29,2026 wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi ya miundombinu inayotekelezwa na TACTIC katika mkoa wa Mara, ambapo amesisitiza kuwa ubora wa kazi ni jambo lisilopaswa kufanyiwa mzaha.

“Katika ziara hii, moja ya mambo muhimu tunayoyaangalia ni ubora wa miradi kwa kuzingatia maelezo yaliyopo kwenye mikataba, hivyo wakandarasi wote mnapaswa kuhakikisha mnatekeleza kazi kwa viwango vilivyokubaliwa,” amesema Mhandisi Mativila.

Ameeleza kuwa wakandarasi wanaposaini mikataba ya utekelezaji wa miradi, wanakuwa wamekubali kutekeleza kazi kwa ubora unaotakiwa, hivyo ni wajibu wao kujisimamia na kuhakikisha wanazingatia masharti yote ya mikataba bila kushurutishwa.

Aidha, Mhandisi Mativila amesema kuwa utekelezaji wa miradi kwa ubora ni sehemu ya kutekeleza maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye amekuwa akisisitiza umuhimu wa kujenga miradi yenye viwango bora ili iweze kudumu kwa muda mrefu na kutoa huduma stahiki kwa wananchi.

Katika ziara hiyo, Mhandisi Mativila amekagua miradi mbalimbali inayotekelezwa chini ya Mradi wa TACTIC, ikiwemo ujenzi wa soko, jengo la Ofisi ya TARURA pamoja na Stendi ya Bweli iliyopo mkoani humo.

Serikali imeahidi kuendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini ili kuipa nafasi pana sekta binafsi kushiriki katika ukuaji wa uchumi na uzalishaji wa ajira kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga, ameagiza Menejimenti ya Kiwanda cha Kuzalisha Bidhaa za Kibaolojia Tanzania (TBPL) kinachomilikiwa na Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) kuongeza uzalishaji na kuimarisha mikakati ya masoko ili kunufaika na mahitaji makubwa yaliyopo sokoni, kuhakikisha kiwanda kinaendelea kujiendesha kwa ufanisi wa kibiashara


Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amesema Serikali itaendelea kuweka kipaumbele katika ustawi wa wazee na uwezeshaji wa vijana kupitia utekelezaji wa programu mbalimbali zinazolenga kuboresha maisha yao na kuongeza ushiriki wao katika shughuli za maendeleo ya taifa.

Mhe. Mahundi ameyasema hayo tarehe 30 Mei, 2026 wakati akizungumza na wageni kutoka Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Maryprisca Women Foundation wakiongozana na Machifu kutoka Mkoa wa Mbeya waliowasili mkoani Dodoma kwa ziara ya mafunzo na kujionea maendeleo yaliyofikiwa katika Mji wa Serikali Mtumba pamoja na shughuli zinazotekelezwa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum.

Amesema Serikali inaendelea kuhakikisha wazee wanapata huduma stahiki ikiwemo bima ya afya na kuishi katika mazingira salama na bora, huku ikiimarisha mikakati ya kuwawezesha vijana kiuchumi kupitia fursa za mikopo, mafunzo ya ujasiriamali na programu mbalimbali za maendeleo.

Katika ziara hiyo, wageni hao walipata fursa ya kutembelea Mji wa Serikali Mtumba na kujionea majengo ya kisasa ya Wizara na Taasisi mbalimbali yaliyojengwa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mMhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, hatua ambayo imeendelea kuifanya Dodoma kuwa kitovu cha shughuli za Serikali.

Aidha, walijifunza kuhusu majukumu na huduma zinazotolewa na Wizara katika kuimarisha ustawi wa jamii, hususan kwa makundi maalum yakiwemo wazee, wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.


Kwa upande wao, baadhi ya machifu walioshiriki ziara hiyo wameipongeza Serikali kwa mafanikio makubwa yaliyofikiwa katika ujenzi wa Mji wa Serikali Mtumba na kwa kuendelea kutoa kipaumbele katika masuala ya maendeleo ya jamii. 


Pia wamempongeza Mhe. Mahundi kwa juhudi zake katika kusimamia utekelezaji wa mipango inayolenga kuboresha maisha ya wananchi, hususan makundi maalum.


MWISHO


Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.Mwigulu Nchemba amepongeza kiwanda darasa cha kubangua korosho kilichoanzishwa na kituo cha zana za kilimo na teknolojia vijijini (CAMARTEC) wilayani manyoni mkoani singida na kuitaka sekta binafsi kuchangamkia fursa ya kuanzisha viwanda vipya vya kubangua korosho ili kuwawezesha wakulima kupata bei nzuri na kuongeza fursa za ajira kwa vijana.

Akizungumza mara baada ya kutembelea Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho kilichoanzishwa na CAMARTEC ambapo amejionea shughuli za ubanguaji wa korosho.Dr.Mwigulu Nchemba amesema kiwanda hicho ni utekelezaji wa Ilani ya CCM pamoja na Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050 hivyo ameitaka sekta binafsi kuanzisha viwanda vya kubangua korosho.

Kaimu mkurugenzi Mkuu wa CAMARTEC Mhandisi Godifrey Mwinama amesema iwapo korosho zitabanguliwa nchini zaidi ya ajira 36000 zitazalishwa na pia ameipongeza serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dr.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za ujenzi wa kiwanda darasa hicho kwa ajili ya kuwasaidia wakulima wa korosho na wananchi kwa ujumla.

kwa upande wake mbunge wa jimbo la manyoni Dr.Pius Chaya ameitaka serikali kuanzidha kongani ya viwanda huku meneja wa bodi ya korosho tawi la manyoni wanaeleza hali ya uzalishaji ilivyo









 



Waziri wa Madini, Mheshimiwa Anthony Mavunde ameielekeza Timu ya Majadiliano ya Serikali kwenye Sekta ya Madini (GNT) kuwaita na kufanya nao majadiliano wamiliki wote wa leseni za uchimbaji madini kinywe nchini Tanzania kujadiliana kuhusu ubia wa serikali katika Kampuni hizo na kuwataka kuanza utekelezaji wa uchimbaji kwa mujibu wa masharti ya leseni na Sheria ya Madini Sura ya 123.

Ameyasema hayo leo tarehe 30 Mei, 2026 Wilayani Ruangwa aliposhiriki zoezi la utiaji saini na Kampuni za Grafica Resources na Eminent Minerals Limited zenye ubia wa uwekezaji wa hisa asilimia 83 na Serikali asilimia 17 kwa kila kampuni. 

"Sisi sekta ya madini tunamshukuru kwa dhati Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyotupa maelekezo na kutuwezesha kusimamia sekta kikamilifu kwa maendeleo ya Taifa letu"

"Na ndiyo maana Kampuni zote ambazo hazijaanza uzalishaji kwa mujibu wa masharti ya leseni zao tumeziandikia hati ya makosa (Default Notice) kwa mujibu wa Sheria ya Madini Sura ya 123. Kusaini kwetu mikataba siku ya leo, hakutoi unafuu kwa wawekezaji hawa kutotekeleza uwekezaji wao kwa mujibu wa Sheria yetu ya madini" amesisitiza Mhe. Mavunde.

Waziri Mavunde amesema hatua ya Timu ya GNT kuwaita na kuwataka wamiliki wa leseni za uchimbaji madini kinywe kufuata masharti ya Sheria na kuanza uzalishaji kutapelekea ufikiaji wa lengo la kuifanya Tanzania kuwa mzalishaji wa kwanza duniani wa madini kinywe ifikapo mwaka 2030.

Vilevile, Waziri Mavunde ametoa wito kwa wawekezaji wa miradi hiyo kutoa fursa ya kipaumbele cha ajira kwa watanzania hususan wanaozunguka miradi hiyo. Kwa kufanya hivyo kutachochea uchumi wa Vijiji, Wilaya ya Ruangwa hususan kupitia wajibu wa uwekezaji kwa jamii (CSR) na kupelekea maendeleo ya uchumi wa Nchi yetu.

Aidha, Waziri Mavunde amebainisha kuwa miradi hiyo itakapoanza kuzalisha kikamilifu, itakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 101,048 za kinywe kila mwaka kwa upande wa mradi wa Grafica na tani 15,930 za kinywe kila mwaka kwa upande wa mradi wa Eminent mtawalia, hali inayoifanya Ruangwa sasa kuwa sehemu ya mnyororo wa thamani wa teknolojia za kisasa duniani.

Waziri Mavunde pia ameeleza kuwa bado Tanzania ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri katika uzalishaji wa madini mbalimbali duniani, na ndiyo maana tunaendelea kuweka mkazo kwenye ufanyaji wa utafiti wa kina ili kubaini mashapo zaidi yatakayoongeza uchimbaji hususan kupitia wachimbaji wadogo wenye mchango mkubwa katika uchumi wetu.

Awali, akieleza mchakato wa kufikia makubaliano hayo, Mwenyekiti wa Timu ya Majadiliano ya Serikali kwenye sekta ya Madini, Prof. Sifuni Mchome amebainisha kuwa, majadiliano hayo yalifanyika kwa kuzingatia maslahi mapana ya nchi yetu na hayakuwa na lengo la kutafuta mshindi, hali iliyopelekea Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupata hisa zisizofifishwa za asilimia 17 kwenye kila mradi wa ubia.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kampuni ya Grafica Resources, Bw. Vikas Bardiya ameeleza kuwa kampuni yao inaishukuru Serikali kwa ushirikiano iliyowapa mpaka kufikia makubaliano ya kuwekeza na kuahidi kwamba watahakikisha wanatekeleza uwekezaji huo kwa mujibu wa mkataba ili uweze kuleta manufaa kwa wananchi wa Ruangwa na Taifa kwa ujumla.

Pia, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Eminent Minerals Limited, Bw. Shafiqali Khaki ameeleza kufarijika kwao kuwa kampuni ya kizawa kuingia ubia na Serikali katika uwekezaji kwenye mradi huo wa uchimbaji madini kinywe na kwamba wao kama wazawa watahakikisha sehemu kubwa ya zaidi ya ajira 250 zitakazozalishwa katika uwekezaji huo zinachukuliwa na watanzania ili kuinua uchumi wa Taifa letu. 

Naye Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mheshimiwa Zainab Telack alimshukuru Mhe. Rais kwa kuwa kiongozi mahiri katika kusimamia uchumi na kuhakikisha rasilimali zetu zinanufaisha watanzania.

 Aidha, alisisitiza kuwa Serikali ya Mkoa wa Lindi itaendelea kuwapa ushirikiano wawekezaji hao ili waweze kuendesha shughuli zao kwa kasi na kunufaisha wananchi wa Lindi na Taifa kwa ujumla.
Jumla ya wafugaji wadogo 92,831 na wadau wa mnyororo wa thamani wa maziwawa Tanzania Bara na Visiwani-Zanzibar wamenufaika na Mradi Shirikishi waWasindikaji na Wazalishaji wa Maziwa (TI3P) tangu ulipoanzishwa mwezi Machi mwaka 2022, ambapo asilimia 30 ya wanufaika hao ni wanawake.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo nilihisi biashara yangu ilikuwa karibu kufungwa kabisa. 

Nilikuwa nimejenga biashara yangu kwa miaka ya juhudi na kujituma. Mwanzoni mambo yalikuwa mazuri.

Wateja walikuwa wanakuja kila siku, mauzo yalikuwa yanaenda vizuri, na nilianza kuona matumaini ya maisha bora kupitia biashara ile. Lakini ghafla mambo yakaanza kubadilika.

Nilianza kuona wateja wangu wa kawaida wakipungua mmoja baada ya mwingine. Mwanzoni nilidhani ni hali ya kawaida ya biashara, lakini kadri wiki zilivyopita, hali ilizidi kuwa mbaya.

Kilichoniumiza zaidi ni kuona wengi wakihamia kwa competitor aliyekuwa karibu. Mara kwa mara nilikuwa nasikia watu wakisema huko kulikuwa na huduma nzuri zaidi au offers ambazo zilikuwa zinawavutia. SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na kipindi ambacho nilianza kuhisi kama uhusiano wangu ulikuwa unabadilika polepole. Mwanzoni mimi na mpenzi wangu tulikuwa karibu sana. 

Tulizungumza kila siku, tulicheka pamoja, na kila kitu kilionekana kwenda vizuri. Nilikuwa naamini tulikuwa tunaelekea kwenye maisha mazuri pamoja.

Lakini ghafla mambo yakaanza kubadilika. Mpenzi wangu alianza kuwa tofauti. Alianza kurudi akiwa kimya, mazungumzo yetu yakapungua, na mara nyingi alikuwa anashika simu yake kwa siri. Wakati mwingine nilipomuuliza nini kinaendelea, alikuwa anakasirika au kubadilisha mada.

Kwa kweli iliniumiza sana. Kilichoniumiza zaidi ni kuona mtu ambaye zamani alikuwa karibu sana nami akianza kuwa distant. 

Nilianza kujiuliza kama kuna kitu nilikuwa nimekosea au kama kulikuwa na mtu mwingine kwenye maisha yake.

Kulikuwa na usiku nilikosa usingizi. Nilikuwa na mawazo mengi sana kuhusu future ya relationship yetu. Wakati mwingine nilijikuta nikilia kimya kwa sababu sikuwa nataka kupoteza mtu niliyempenda sana.

Lakini sikutaka kufanya maamuzi ya haraka. Nilijaribu kuzungumza naye kwa utulivu mara kadhaa, lakini ilikuwa ngumu kupata maelezo ya wazi. Polepole nilianza kupoteza furaha na confidence yangu. SOMA ZAIDI.
Kulikuwa na kipindi ambacho nilianza kuishi na wasiwasi mkubwa kuhusu maendeleo ya mtoto wangu. Nilikuwa namwangalia akikua vizuri kwenye mambo mengi, lakini kulikuwa na jambo moja lililoniumiza moyo.

Wakati watoto wa rika lake walikuwa wanaanza kusema maneno mengi na kuwasiliana vizuri, wangu alikuwa bado anapata ugumu wa kujieleza. Mwanzoni nilijipa moyo.

Nilijua watoto hukua kwa tofauti, hivyo niliamini labda muda wake ulikuwa bado. Lakini kadri miezi ilivyopita, nilianza kupata pressure kutoka kwa watu wa karibu.

Wengine walikuwa wakiuliza kwa nini bado haongei vizuri, jambo lililonifanya nizidi kuwa na mawazo. Kwa kweli nilihuzunika sana. Kilichoniumiza zaidi ni kuona mtoto wangu akijaribu kueleza kitu lakini ashindwe.

Wakati mwingine alikuwa anakasirika au kulia kwa sababu hatukuelewa alichotaka kusema. Nilianza kutafuta msaada. 

Nilizungumza na walimu na nikatafuta ushauri wa kitaalamu ili kuelewa kama kulikuwa na changamoto ya maendeleo ya lugha au kitu kingine kilichohitaji attention mapema. SOMA ZAIDI.
Kwa muda mrefu nilikuwa nikihangaika kukuza biashara yangu bila mafanikio makubwa. Nilikuwa nauza bidhaa mtandaoni na wakati mwingine dukani, lakini ukweli ni kwamba mambo hayakuwa rahisi.

Nilikuwa napost bidhaa kila siku, nikijitahidi kutangaza kwa watu, lakini wateja walikuwa wachache sana. Kulikuwa na siku nilikaa bila kuuza kitu chochote. Kwa kweli nilianza kukata tamaa.

Kilichoniumiza zaidi ni kuona biashara nyingine zikikua kupitia social media huku yangu ikionekana kusimama sehemu moja. 

Nilikuwa najitahidi kurecord videos, kupost picha, na hata kufanya offers, lakini hakuna kilichokuwa kinabadilika sana. SOMA ZAIDI.
Kwa muda mrefu nilikuwa na ndoto ya kufanya kazi Gulf ili nibadilishe maisha yangu na kusaidia familia yangu. Nilikuwa nikiona watu wakirudi kutoka nje wakiwa wamejenga nyumba, kuanzisha biashara, na kusaidia familia zao.

Moyoni nilijua na mimi nilitaka nafasi kama hiyo. Lakini safari yangu haikuwa rahisi hata kidogo. Nilianza kutuma applications kupitia agencies mbalimbali.

Mwanzoni nilikuwa na matumaini makubwa. Nilihakikisha documents zangu zimekamilika, nikafanya interviews, na hata mara nyingine nikatoa pesa za process nikiamini safari yangu ilikuwa karibu.

Lakini kila mara kulikuwa na disappointment. Mara application inakataliwa, mara nafasi inaenda kwa mtu mwingine, mara naambiwa nisubiri bila majibu ya kueleweka. 

Kadri muda ulivyopita, madeni yalianza kuniongezea pressure kwa sababu nilikuwa nimetumia pesa nyingi kufuatilia process ile.

Kwa kweli nilianza kuchoka. Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu nilioanza nao process wakifanikiwa kusafiri huku mimi nikibaki nyuma. Watu wengine walianza kuniambia labda safari ile haikuwa ya kwangu.SOMA ZAIDI.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu leo ameongoza watumishi, mawakili na wananchi kumuaga aliyekuwa mtumishi wa Ofisi hiyo, marehemu Wakili Msomi Charles Boaz Swai aliyefariki jana jijini Dodoma.






Na Mwandishi Wetu


DAR ES SALAAM — Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema uhuru wa uhariri ni nguzo muhimu katika taaluma ya habari na unapaswa kulindwa ili vyombo vya habari viweze kutekeleza majukumu yake kwa weledi, uwajibikaji na kwa maslahi ya umma.


Akizungumza Mei 26, 2026 katika mahojiano maalum yaliyofanyika katika Ofisi za JAB jijini Dar es Salaam, Wakili Kipangula alisema hakuna mtu anayepaswa kuingilia maamuzi ya uhariri wa chombo cha habari, awe ni chanzo cha taarifa, mmiliki wa chombo, mwanasiasa au mtu mwingine yeyote mwenye maslahi binafsi.


Alisema uhuru huo unapaswa kuendana sambamba na uwajibikaji wa kitaaluma, huku akisisitiza kuwa maadili ya taaluma ya habari yanamtaka mwandishi kufanya kazi kwa uadilifu, bila upendeleo na kuhakikisha taarifa zote zinathibitishwa kabla ya kuchapishwa au kurushwa.


“Ukweli ndio mlinzi wa taaluma ya habari. Mwandishi anatakiwa kutoa taarifa ambazo amezithibitisha na ana uhakika nazo kwa sababu jamii inategemea kupata taarifa sahihi na kwa wakati ili iweze kufanya maamuzi sahihi kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo,” amesema Wakili Kipangula.


Aidha, alisema waandishi wa habari wana nafasi kubwa katika kujenga jamii yenye uelewa, mshikamano na maendeleo, hivyo ni muhimu kutumia uhuru wa habari kwa kuzingatia sheria, maadili ya taaluma pamoja na kuheshimu haki na uhuru wa wengine kwa mujibu wa Katiba na sheria za nchi.


Kwa upande wake, Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Jamhuri, Bw. Deodatus Balile, alisema uhuru wa vyombo vya habari utakuwa na maana halisi pale vyombo hivyo vitakapokuwa na uwezo wa kiuchumi wa kujiendesha bila kutegemea ushawishi wa nje.


“Uhuru wa vyombo vya habari utakuwa uhuru wa kweli pale vyombo vya habari vitakapokuwa na nguvu ya kiuchumi,” amesema Balile.

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeendelea kuonesha nafasi yake katika kuchochea maendeleo ya viwanda na kukuza ubunifu wa vijana kwa kutoa elimu ya viwango na ubora wa bidhaa katika Maonesho ya Fursa za Kazi na Ubunifu kwa Vijana (Career Fair 2026), hatua inayolenga kuwajengea vijana uwezo wa kuzalisha bidhaa zenye ushindani katika soko la ndani na kimataifa.

 


Katibu Mtendaji wa NACTVET Dkt.Mwajuma Lingwanda akizungumza na Waandishi wa habari kuhusiana na kufunguliwa kwa udahili wa wanafunzi katika mwaka wa masomo 2026/2027.




Baadhi ya matukio katika picha wakati wa kutangazwa kwa dirisha la udahili mwaka wa masomo 2026/2027.

Na Mwandishi Wetu
BARAZA la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) limefungua dirisha la Udahili wa wanafunzi kwa mwaka wa masomo 2026/2027 kwa ngazi ya Astashahada na Stashahada katika kozi zote zinazosimamiwa na NACTVET.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma Katibu Mtendaji wa NACTVET Dkt.Mwajuma Lingwanda amesema dirisha Hilo limefunguliwa rasmi Mei 28 2026.

Amesema maombi ya udahili kwa kozi za Afya na Sayansi Shirikishi -Tanzania Bara, yatafanyika kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) unaopatikana katika tovuti ya Baraza (www.nactvet.go.tz).

Dkt.Mwajuma amesema udahili umeanza Mei 28 hadi Julai 10 2026 kwa awamu ya kwanza.

Aidha amesema maombi ya kozi zisizo za Afya na Sayansi Shirikishi, na kozi za Afya na Sayansi Shirikishi zitolewazo katika vyuo vilivyoko Zanzibar yatumwe moja kwa moja kwenye vyuo husika kuanzia Mei 28 Mei hadi Julai 10 mwaka Hui kwa awamu ya kwanza.

Hata hivyo Baraza limetoa orodha ya kozi zote na vyuo vinavyotoa kozi hizo, inapatikana katika Kitabu cha Mwongozo wa Udahili kwa Mwaka wa Masomo 2026/2027 kinachopatikana katika tovuti ya Baraza (www.nactvet.go.tz).

Baraza hilo limesema kila mwombaji kuhusika mwenyewe katika zoezi zima la kuomba kudahiliwa, kuandika taarifa zake kwa usahihi na umakini, na kutunza kumbukumbu atakazopatiwa na Baraza kupitia namba yake ya simu, bila kumpatia mtu mwingine yeyote ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza katika zoezi zima la maombi ya kujiunga na kozi katika vyuo mbalimbali.

Mambo ya Kuzingatia kwa Wanaoomba Kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (Central Admission System – CAS) ni Mwombaji anaweza kuomba chuo zaidi ya kimoja na Kuchaguliwa katika chuo alichoomba kutategemea ushindani utakaokuwepo katika chuo hicho.

Aidha amesema mwombaji akishachaguliwa, atapokea ujumbe kutoka NACTVET kupitia namba yake ya simu aliyoweka kwenye mfumo wakati wa kufanya maombi ujumbe utamjulisha kuwa amechaguliwa kujiunga na chuo husika na utakuwa na msimbo (code) ambao atatakiwa kuutunza na kuuwasilisha kwa chuo alichochaguliwa siku atakapowasili chuoni kwa ajili ya kuanza masomo.

Dkt. Mwajuma amesema baada ya kuwasilisha msimbo huo chuoni, atasajiliwa na chuo, kisha atapokea ujumbe kutoka NACTVET ukimweleza kuwa amesajiliwa. Baada ya kusajiliwa, mwanafunzi aingie katika tovuti ya NACTVET (www.nactvet.go.tz), kisha ajiridhishe kuwa amesajiliwa kwa kuhakiki taarifa zake kwa kubonyeza “link” inayosomeka “student’s information verification”.

 


Na Benny Mwaipaja, Congo Brazzaville

Tanzania imeelezea msimamo wake wa kuunga mkono mbinu za fedha za mseto (blended finance) zitakazosaidia kuimarisha sekta za usafiri wa anga na afya barani Afrika, akieleza kwamba hakuna chanzo kimoja kitakachoweza kuziba mapungufu ya miundombinu ya bara hilo.

Akizungumza kama Gavana Mbadala wa Tanzania kwenye mkutano ulioandaliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kuhusu “Platform solutions to Africa’s Transformation: De‑risking Aviation and Health systems through Innovative Financing”, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba alisema suluhisho linalopendekezwa ni la vitendo, nafuu na linaendana na vipaumbele vya kitaifa vya Tanzania.

“Tunasisitiza matumizi ya rasilimali za umma na binafsi pamoja na dhamana na msaada kutoka kwa washirika. Hatuwezi kutegemea chanzo kimoja pekee,” alisema Dkt. Mwamba, akiongeza kuwa ni muhimu kuzingatia udhibiti wa deni linalozidi kukua katika nchi za Afrika.

Katika Mkutano huo, Dkt. Mwamba alisisitiza kuwa usafiri wa anga ni kichocheo cha biashara, utalii, uwekezaji na ukuaji wa kikanda na kwamba Tanzania inakaribisha uwekezaji wa ubunifu kwa ajili ya uboreshaji wa viwanja vya ndege, uimarishaji wa usalama, utengenezaji wa mifumo ya usafirishaji na kuunganisha safari za kikanda kwa ufanisi. Lengo ni kuifanya Tanzania kuwa kituo cha usafiri kwa Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika.

 

Vilevile, kuhusu huduma za afya, Dkt. Mwamba alibainisha kuwa mifumo thabiti ya afya ni nguzo ya uzalishaji, raslimali watu na ustahimilivu wa kiuchumi inayohitaji fedha za kuaminika na nafuu kwa ajili ya dawa muhimu, vifaa vya kisasa na miundombinu ya afya inayoweza kustahimili mabadiliko ya tabianchi na mazingira.

 

Dkt. Mwamba alieleza mahitaji ya Tanzania kwa AfDB: kuendeleza msaada kwa ajili ya maandalizi ya miradi ili kuibua miradi inayoweza kuvutia wawekezaji, hususan kutoka sekta binafsi, upatikanaji wa dhamana na kuwa na masharti nafuu zaidi ya mikopo kutoka Taasisi za Fedha, ikiwemo AfDB.

 

“Tanzania iko tayari kushirikiana na AfDB na wadau wote kwa uwekezaji wa matokeo dhahiri kwa wananchi wetu,” alisema Gavana huyo.

 

Mkutano huo uliofunguliwa na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dkt. Sidi Ould Tah, uliwaleta pamoja Wadau wa maendeleo, Mawaziri wa Fedha, Magavana wa Benki Kuu, wawekezaji na viongozi wa Serikali kuzungumza kuhusu njia za kuondoa vikwazo vinavyoweka hatari kwa wawekezaji na kuleta mbinu za upatikanaji wa fedha zenye tija kwa miradi ya usafiri na afya barani Afrika.

 


Na. Peter Haule na Jordan Mbwambo, WF, Dodoma

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Bw. Nsubili Joshua amewataka watumishi wa Wizara hiyo kudumisha mshikamano, nidhamu, weledi na uzalendo katika kutekeleza majukumu ya kila siku ili kuwezesha kufikia malengo ya Wizara na Taifa kwa ujumla.

Rai hiyo imetolewa jijini Dodoma wakati akifunga kikao cha 39 cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Fedha kilichofanyika kwa muda wa siku mbili kuanzia tarehe 28 hadi 29 Mei 2026.

Alisema kuwa wajumbe wa Baraza hilo wanatakiwa kuwa mabalozi wazuri katika kuhakikisha maazimio na mapendekezo yote yaliyotokana na mijadala iliyokuwepo inazingatiwa kikamilifu na kufanyiwa kazi kwa wakati ili kuendelea kuimarisha ufanisi, uwajibikaji na mazingira bora ya kazi kwa watumishi wote wa Wizara.

Aidha, amewapongeza wajumbe wa Baraza hilo kwa mijadala yenye tija, maoni ya kujenga na michango yenye hekima, busara na mtizamo wa kuboresha utendaji wa wizara.

Alisema mada zote zilizowasilishwa zimegusa maeneo muhimu yanayohusu utendaji wa Wizara, ustawi wa watumishi pamoja na utekelezaji wa majukumu ya msingi ya kusimamia uchumi na fedha za umma.

Kwa upande mwingine Afisa Habari wa Wizara hiyo, Bw. Joseph Mahumi, amewataka wajumbe wa Baraza kutumia akaunti rasmi za mitandao ya kijamii ya Wizara ili kupata taarifa mbalimbali kuhusu mafanikio na mikakati mbalimbali ya Wizara, Sera na masuala ya uchumi na fedha.

“Kwa upande wa Akaunti ya LinkedIn Wizara imefanya vizuri si tu kwa Wizara na Taasisi za Serikali lakini pia kwa taasizi binafsi zikiwemo Benki na mashirika binafsi, jambo ambalo si la kubeza”, alisema Bw. Mahumi.

Amesema pia Wizara inafanya vizuri katika mitandao ya Instagram (urtmof), Facebook (MofURT), Youtube (Hazina TV), LinkedIn (Ministry of Finance Tanzania), Whatsapp Channel (Wizara ya Fedha Tanzania) na Threads (urtMof).

Amewataka watanzania kwa ujumla kufuatilia kwa karibu mitandao hiyo ili kupata taarifa muhimu za masuala ya Sera, fedha na programu mbalimbali zitakazowasaidia kufanya maamuzi sahihi katika kukuza maendeleo binafsi na ya Taifa kwa Ujumla.

WAZIRI wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu(Sera,Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Profesa Palamagamba Kabudi ameta taarifa ya hali ya dawa za kulevya kwa mwaka 2025 ambapo inaonesha namna Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ilivyowekeza na kuweka nguvu kubwa katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya.
UWEKEZAJI wa ndani umeendelea kupewa msukumo nchini kufuatia juhudi za Serikali za kuboresha mazingira ya biashara, huku uzinduzi wa kituo cha mafuta cha Orxy Karatu ukitajwa kuwa sehemu ya utekelezaji wa maono ya kukuza uchumi jumuishi chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.