Na Munir Shemweta, Dodoma
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imekutana leo tarehe 12 Agosti 2026 Bungeni jijini Dodoma kupokea na kujadili taarifa kuhusu utendaji wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya, ikiwa ni sehemu ya jukumu la Bunge la kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa majukumu ya Serikali katika sekta ya ardhi.
Katika kikao hicho, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeieleza Kamati hatua mbalimbali zilizochukuliwa katika kuboresha utendaji wa Mabaraza hayo, ambayo yako chini ya Wizara hiyo.
Miongoni mwa hatua zilizobainishwa ni kuongezeka kwa idadi ya Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya, kupungua kwa mashauri na malalamiko, kuimarishwa kwa matumizi ya mifumo ya kidijiti pamoja na kuboreshwa kwa mfumo wa uendeshaji wa shughuli za madalali.
Pamoja na mafanikio hayo, Kamati imeelezwa kuwa bado zipo changamoto kadhaa zinazoathiri utendaji wa Mabaraza hayo na kwamba Wizara inaendelea kuzifanyia kazi ili kuongeza ufanisi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kaspar Mmuya, amewaeleza wajumbe wa Kamati kuwa, Serikali inaendelea kushughulikia changamoto zinazoyakabili Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya, akieleza kuwa kutatuliwa kwa changamoto hizo kutasaidia kuyafanya Mabaraza kuwa bora zaidi na yenye manufaa makubwa kwa wananchi.
Awali, wajumbe wa Kamati wameitaka Wizara kuweka mkazo zaidi katika matumizi ya usuluhishi wakati wa kushughulikia migogoro ya ardhi badala ya kila shauri kulenga kupata mshindi na mshindwa.
Wamesema, usuluhishi unaweza kusaidia kupunguza migogoro, kuharakisha utatuzi wa mashauri na kujenga mahusiano mazuri miongoni mwa wananchi.
Wajumbe hao wameeleza kuwa, pamoja na mafanikio yanayoonekana katika utendaji wa Mabaraza, bado ipo haja ya Wizara kuchukua hatua za haraka kukabiliana na changamoto zilizopo ili Mabaraza hayo yaweze kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na kuendelea kujenga imani ya wananchi.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Timotheo Mzava, amesisitiza umuhimu wa Wizara kuongeza idadi ya wenyeviti wa Mabaraza, kupanua upatikanaji wa Mabaraza katika wilaya mbalimbali pamoja na kukamilisha mfumo wa kidijiti ili kuongeza ufanisi na kupunguza malalamiko kutoka kwa wananchi.
“Sisi kama Kamati tunaona umuhimu wa kuwa na Mabaraza kila Wilaya pamoja na kukamilika kwa mfumo wa kidijiti, kwa kuwa mtakapoboresha, kelele kuhusu Mabaraza zitapungua,” amesema Mhe. Mzava.
Kikao hicho kilichoongozwa na Mhe. Mzava pia kimehudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhandisi Anthony Sanga, Naibu Katibu Mkuu Bi. Lucy Kabyemera, pamoja na viongozi na watendaji wengine wa Wizara.
Nilitengwa na Kudharaulika kwa Kukosa Mtoto kwa Miaka Mingi, Mpaka Tiba ya Asili Iliponibariki Pacha
Baada ya kufunga ndoa na mume wangu, tulikuwa na hamu kubwa ya kupata mtoto wetu wa kwanza. Hata hivyo, miaka ilianza kupita mmoja baada ya mwingine bila dalili yoyote ya mimba.
Taratibu, furaha na amani zilianza kutoweka nyumbani kwetu, zikibadilishwa na maswali ya kejeli, maneno ya shombo, na dharau kutoka kwa ndugu na majirani waliotutenga na kuniona mimi kama mwanamke asiye na thamani.
Nilitumia fedha nyingi kutembelea hospitali mbalimbali kubwa na ndogo, nikifanyiwa vipimo vya kila aina na kutumia dawa za hospitali kwa miaka mingi bila mafanikio yoyote.
Kila mwezi ulipopita bila matokeo, nilijikuta nikitumbukia kwenye msongo mkubwa wa mawazo na vilio vya usiku kucha.
Mume wangu alianza kubadilika na kupata shinikizo kubwa kutoka kwa familia yake wakimtaka anifukuze au aoe mke mwingine wa kumzalia watoto.
Nilibaki kwenye maumivu makali, nikihofia ndoa yangu kuvunjika na kuachwa peke yangu nikiwa na aibu na simanzi tele. SOMA ZAIDI.
KKwa miaka kadhaa, maisha ya familia yangu yaliingia kwenye misosagano na dhiki kubwa baada ya majirani zetu kuanza kuonyesha wazi chuki zao punde tu tulipoanza kuboresha nyumba yetu, kuanzisha biashara ndogo, na kununua vitu vya maendeleo.
Wivu wao ulikuwa wa wazi kabisa ilianza na maneno ya shombo na majungu mtaani, kisha ikageuka kuwa fitna za waziwazi zilizolenga kutugombanisha na viongozi wa mtaa na wenye nyumba.
Hali ilipozidi kuwa mbaya, fitna hizo zilianza kuvuka mipaka ya kawaida na kuingia kwenye mazingara ya giza na ushirikina.
Tulianza kuona vitu vya ajabu vikitupwa ndani ya kiwanja chetu usiku, watoto walianza kuugua magonjwa yasiyoeleweka kila mara, na biashara yetu iliyoanza vizuri ilianza kupoteza wateja ghafla bila sababu.
Kila tulipojaribu kufanya jambo lolote la maendeleo, majirani hao walifanya kila njia kutukosesha amani, kutuchongea, na kuweka mikosi ili turudi nyuma na kuwa maskini kama zamani.
Hofu na msongo wa mawazo vilitutawala, na tulifikiria hata kuama eneo hilo kwa aibu.SOMA ZAIDI.
Kwa miaka kadhaa, nilitokea kumpenda sana msichana mmoja mtaani kwetu. Kila nilipomwona au kupishana naye, moyo wangu ulikuwa ukidunda kwa nguvu, lakini kila nilipojaribu kumsogelea au kumweleza hisia zangu, alinipuuza kabisa na kunichukulia kama mtu asiyekuwa na thamani yoyote mbele yake.
Hali hii ilininyima sana amani ya nafsi. Nilijaribu kutumia mbinu mbalimbali za kumvutia, ikiwa ni pamoja na kumharibia zawadi, kumtumia ujumbe wa mahaba, na hata kujitahidi kuvaa vizuri kila mara nilipojua nitakutana naye, lakini hakuna kilichobadilika.
Alibaki akinitazama kwa jicho la dharau na wakati mwingine kuniepuka kabisa. Nilibaki nikiumia moyoni, nikitazama watu wengine wakipata wapenzi wanaowapenda kwa dhati, wakati mimi nikibaki peke yangu na maumivu ya kupenda bila kupendwa. SOMA ZAIDI.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Siuluhu Hassan, akizungumza alipotembelea banda la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kwenye Maonesho ya Tamasha la Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar Agosti 12, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan (kulia), akimsikiliza Meneja wa Ofisi ya Zanzibar ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bi. Mariam Saleh, alipotembelea banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya Tamasha la Kizimkazi 2026 (Kizimkazi Festival 2026) Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar Agosti 12, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan (kushoto), akimsikiliza Meneja wa Ofisi ya Zanzibar ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bi. Mariam Saleh, alipotembelea banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya Tamasha la Kizimkazi 2026 (Kizimkazi Festival 2026) Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar Agosti 12, 2026.
Zanzibar, Agosti 12, 2026
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametembelea banda la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) katika Maonesho yanayoambatana na Tamasha la 10 la Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.
Katika ziara hiyo, Mhe. Rais Samia amepongeza PSSSF kwa kushiriki katika maonesho hayo na kutoa huduma pamoja na elimu kwa wanachama na wananchi wanaotembelea banda la Mfuko.
Mhe. Rais Samia alipokelewa na Meneja wa PSSSF Ofisi ya Zanzibar, Bi. Mariam Saleh, ambaye alimueleza kuhusu huduma zinazotolewa na Mfuko, pamoja na namna wanachama na wananchi wanavyonufaika na huduma hizo kupitia banda hilo.
Mhe. Rais Samia ameupongeza Mfuko kwa utoaji wa huduma na kusisitiza umuhimu wa kusikiliza na kushughulikia kwa wakati changamoto zinazowasilishwa na wananchi na wanachama.
“Nawapongeza sana kwa huduma nzuri. Kama kuna malalamiko, yakusanyeni na muyafanyie kazi,” ameagiza Mhe. Rais Samia.
Ushiriki wa PSSSF katika Tamasha la Kizimkazi unalenga kuendelea kuwafikia wanachama na wananchi kwa kuwapatia elimu kuhusu hifadhi ya jamii, huduma zinazotolewa na Mfuko pamoja na kuwawezesha kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali yanayohusu mafao na huduma za PSSSF.
Mwisho
Na Mwandishi Wetu
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa, ameanza ziara ya kikazi mkoani Mwanza kwa lengo la kuimarisha udhibiti wa bidhaa bandia na kukuza ushindani wa haki katika soko.
Katika ziara hiyo, iliyofanyika leo Agosti 12, 2026, Bi. Ngasongwa amekutana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Ndugu Balandya Elikana, ambapo wamejadili umuhimu wa kuimarisha ushirikiano katika kudhibiti uingizaji, uzalishaji na usambazaji wa bidhaa bandia.
Akizungumza katika kikao hicho, Balandya amesema udhibiti wa bidhaa bandia ni muhimu katika kuhakikisha bidhaa halali zinapata fursa sawa ya kushindana katika soko, hatua ambayo itasaidia kuchochea shughuli za kiuchumi na kuongeza kasi ya maendeleo ya Taifa.
"Kuimarisha udhibiti wa bidhaa bandia kutasaidia kuwalinda wafanyabiashara wanaofuata sheria, kuongeza imani ya wananchi kwa bidhaa zinazouzwa sokoni na kuchochea ukuaji wa uchumi."amesema Balandya
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, amesema Tume itaendelea kuchukua hatua dhidi ya uingizaji, uzalishaji na usambazaji wa bidhaa bandia ili kuhakikisha bidhaa halali zinapata mazingira bora ya ushindani katika soko.
Bi.Ngasongwa amesema kuwa hatua hizo ni sehemu ya jitihada za FCC za kulinda ushindani wa haki, kuwalinda wafanyabiashara wanaozingatia sheria na kuhakikisha shughuli za kibiashara zinafanyika kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa.




Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Asha-Rose Migiro, amefungua rasmi Tawi la CCM Kibuteni, Wilaya ya Kusini, Mkoa wa Kusini Unguja, leo tarehe 12 Agosti 2026.
Tawi hili lina historia kubwa tangu nyakati za ASP na TANU, na ni jambo la kujivunia kuona sasa lina sura mpya inayokwenda sambamba na mahitaji na hadhi ya Chama.
Dkt. Migiro amewahimiza viongozi na wanachama kuhakikisha Tawi hilo linakuwa kituo cha uhai wa Chama, mshikamano, mafunzo, vikao na utekelezaji wa shughuli za Chama.
Pia, Katibu Mkuu amewashukuru wana-CCM wa Kibuteni kwa mapokezi mazuri, upendo na zawadi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akimkabidhi Meneja wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Zanzibar, Bi. Mariam Saleh Tuzo ya shukran kutokana na mchango wa Mfuko huo kuwa miongoni mwa Taasisi zilizofanikisha kufanyika kwa Kongamano hilo ambalo ni sehemu ya Tamasha la 10 la Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar usiku wa kuamkia leo Agosti 12, 2026.
Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja na Wawakilishi wa Taasisi zilizopatiwa tuzo
Rais wa Zaznibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi (Kushoto) na mkewe Mama Mariam Mwinyi (mwenye raba nyekundu), wakitembelea mabanda ya Maonesho baada ya kuzindua Tamasha la Kizimkazi Agosti 12, 2026

Meneja wa PSSSF Zanzibar, Bi. Mariam Saleh, akiwa na Tuzo ya shukrani baada ya kukabidhiwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan baada ya kukabidhiwa
Zanzibar, Agosti 12, 2026
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameutunuku Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) tuzo ya kutambua mchango wake katika kuwezesha kufanyika kwa Mdahalo wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, uliofanyika Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, usiku wa kuamkia leo, Agosti 12, 2026.
Tuzo hiyo imekabidhiwa kwa Meneja wa PSSSF Zanzibar, Bi. Mariam Saleh, kwa niaba ya Mfuko, ikiwa ni sehemu ya utambuzi kwa taasisi na wadau walioshiriki katika kuwezesha mdahalo huo, uliofuatiwa na Maonesho ya Picha za Tamasha la Kizimkazi.
Mdahalo huo umefanyika sambamba na Tamasha la 10 la Kizimkazi (Kizimkazi Festival 2026), linalofanyika Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, ambapo tamasha hilo limeanza rasmi leo kwa matembezi pamoja na uzinduzi uliofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi.
Ushiriki wa PSSSF katika mdahalo huo unaakisi dhamira ya Mfuko ya kushirikiana na Serikali, taasisi na wadau mbalimbali katika kuunga mkono mijadala yenye umuhimu kwa jamii, mazingira na maendeleo endelevu.
Aidha, PSSSF inawakaribisha wanachama na wananchi kutembelea banda la Mfuko katika Maonesho ya Tamasha la Kizimkazi yanayoanza leo, Agosti 12, 2026, kwa ajili ya kupata elimu na huduma mbalimbali zinazotolewa na Mfuko, amesema Afisa Uhusiano Mkuu wa PSSSF, Bi. Fatma Elhady.
📌Asema wajibu wa kila Mtanzania ni kuhakikisha mafanikio yanakuwa endelevu
Naibu Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Mhe. Dkt. Doto Biteko, amesema Tanzania imepiga hatua kubwa katika utekelezaji wa Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia, huku akisisitiza kuwa ni wajibu wa kila Mtanzania kuhakikisha mafanikio yaliyopatikana yanaendelea kuwa endelevu.
Dkt. Biteko amesema hayo wakati akishiriki mjadala kuhusu “Uongozi wa Kimkakati wa Tanzania katika Kuharakisha Mabadiliko ya Nishati Endelevu na Jumuishi”, uliofanyika katika Mdahalo wa Nishati Safi ulioandaliwa na Taasisi ya Mwanamke Initiative Foundation (MIF), Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.
Amesema uwepo wa Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia ni sehemu ya jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ameendelea kuipa msukumo ajenda hiyo katika ngazi mbalimbali za uongozi wake na kuifikisha hadi katika majukwaa ya kimataifa.
Dkt. Biteko amesema umuhimu wa kuendelea kuipa kipaumbele ajenda hiyo unatokana na ukubwa wa athari za matumizi ya nishati isiyo safi ya kupikia, ikiwemo uharibifu wa mazingira unaosababishwa na matumizi ya kuni na mkaa, ambapo takribani hekta 470,000 za misitu hupotea kila mwaka nchini.
Aidha, amesema zaidi ya watu 33,000 hupoteza maisha kila mwaka kutokana na magonjwa yanayohusishwa na uchafuzi wa hewa wakati wa kupika, hali inayoonesha umuhimu wa kuongeza kasi ya mpito kuelekea matumizi ya nishati safi.
Ameongeza kuwa matumizi ya nishati isiyo safi yana athari za kijinsia, hususan kwa wanawake ambao hutumia muda mwingi kutafuta kuni badala ya kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji na maendeleo ya kiuchumi.
Amesema athari hizo pia zinawagusa watoto, ambapo baadhi yao hukosa muda wa kutosha wa kuhudhuria masomo kutokana na kulazimika kusaidia familia zao kutafuta kuni kwa ajili ya kupikia.
Katika mjadala huo, Dkt. Biteko amesisitiza umuhimu wa kufanya tathmini za mara kwa mara ili kubaini kiwango cha uendelevu wa matumizi ya nishati safi ya kupikia, hususan baada ya wananchi kuwezeshwa kupata teknolojia na miundombinu husika.
Amesema tathmini hizo zitasaidia Serikali na wadau kubaini changamoto zilizopo, kupima matokeo yaliyofikiwa na kuweka mikakati madhubuti zaidi ya kuendeleza matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.
Pia, Dkt. Biteko ameipongeza Taasisi ya Mwanamke Initiative Foundation (MIF) kwa kuwa miongoni mwa taasisi zinazochangia utekelezaji wa Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia kupitia shughuli mbalimbali, ikiwemo kusaidia upatikanaji wa miundombinu pamoja na kuendesha midahalo inayowakutanisha wadau kujadili namna bora ya kuharakisha matumizi ya nishati safi, salama na endelevu nchini.
MIAKA 40 YA COSTECH: MKURUGENZI MKUU AKAGUA MIRADI YA UTAFITI KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI
Kwa muda mrefu, nilikuwa napitia changamoto ya kukosa hamu ya tendo la ndoa na kuwa mkavu kiasi kwamba nikawa naogopa kumuona mume wangu akirudi nyumbani.
Ili kukwepa unyumba, nilianza tabia ya kujifanya nimevamiwa na “pepo la usingizi”, nikifika tu chumbani, najilaza sakafuni au kitandani na kuanza kukoroma kwa nguvu hata kama sijalala, ili tu mume wangu asiniguse.
Mume wangu alianza kuchoka na tabia yangu. Alisema, “Elizabeth, mbona kila nikirudi unakuwa umechoka kiasi hiki? Unafanya kazi gani Dodoma nzima mpaka ukorome kama trekta?”. Nilianza kukosa amani maana nilijua mume wangu anaweza kuanza kutafuta mwanamke mwingine nje, na hali hiyo ingeharibu sifa yetu kama familia ya kiongozi.
Nilienda kwa madaktari bingwa hapa Dodoma wakaniambia nina upungufu wa damu, lakini dawa walizonipa hazikurudisha hamu wala kuondoa ukavu uliokuwa unanichoma kama moto wakati wa tendo. SOMA ZAIDI.
Mume wangu ni mfanyabiashara mkubwa wa vito vya thamani kama Tanzanite, hivyo maisha yetu yalikuwa ni ya anasa, lakini ndani ya chumba chetu cha kulala, kulikuwa na “jangwa” la kutisha.
Kwa takriban miaka minne, nilipoteza kabisa hamu ya tendo la ndoa na mwili wangu ukawa mkavu kiasi cha kutisha. Kila mume wangu alipojaribu kunigusa, nilihisi maumivu makali kama ninasuguliwa na msasa butu.
Katika hali ya kukata tamaa na kuogopa mume wangu asije kunitupa nje, nilianza kufanya kitendo cha hatari. Nilikuwa naiba mafuta ya kulainisha mashine (lubricants) kutoka kwenye gereji ya mume wangu na kuyaweka kwenye kopo la ‘lotion’ ili tu kumlainisha mume wangu wakati wa tendo.























