Maisha yangu kwa miaka mingi yalikuwa kama mduara usio na mwisho wa kufeli. Kila jambo jema nililojaribu kuanzisha liliporomoka dakika za mwisho. Kama ni biashara, ilikufa ghafla pindi tu nilipoweka Mtaji.TAZAMA VIDEO HAPA.

Kama ni mahusiano, yalivunjika bila sababu ya msingi; na hata nilipopata fedha, zilipotea bila kufanya la maana. Nilikabiliwa na mikosi mfululizo kiasi cha kuanza kuamini kuwa labda nilizaliwa chini ya nyota ya nuksi na bahati mbaya tu.

​Ndugu na marafiki walizoea kuniona kama mtu wa mikosi. Kila nilipoomba msaada au ushauri, nilionekana kama mzigo. Msongo wa mawazo ulinisonga sana, na matumaini ya kufanikiwa maishani yalianza kutoweka kabisa.
Kuwekeza akiba yangu yote kwenye duka la bidhaa za jumla ilikuwa hatua kubwa ya kimaisha. Hata hivyo, biashara hiyo iligeuka kuwa chanzo cha maumivu makubwa. Ndani ya miezi sita tu, wezi walivamia duka langu mara tatu mtawalia....TAZAMA VIDEO HAPA.

Kila mara walivunja kufuli na kubeba bidhaa za thamani kubwa pamoja meza ya fedha. Nilipata hasara ya mamilioni ya fedha, na ripoti za polisi hazikuzaa matunda yoyote.

​Nilishindwa kulala usiku kwa hofu na wasiwasi. Nilikopa fedha tena ili kujiweka sawa, lakini mawazo ya kuvamiwa tena yalinikosesha amani. Nilijua wazi kuwa uvamizi mwingine mmoja ungekuwa mwisho wa biashara yangu na mwanzo wa umaskini wa kutupwa. 

Tafadhali Zingatia: Ikiwa unasoma kwenye PHOENIX, tafadhali bofya kitufe cha “Soma Makala Asili” kilicho upande wa juu kulia ili kusoma makala kamili.



๐Ÿ“Œ Asema ucheleweshaji wa mradi hauendani na matarajio ya Serikali na wananchi.

๐Ÿ“Œ Amuagiza mkandarasi kuongeza kasi ya utekelezaji na kuzingatia masharti ya mkataba.

๐Ÿ“Œ Aelekeza hatua stahiki kuchukuliwa iwapo maendeleo ya mradi hayataboreshwa kabla ya Septemba 30, 2026.

๐Ÿ“Œ Mradi wa kV 220 utaiunganisha Mikoa ya Lindi na Mtwara kwenye Gridi ya Taifa na kuimarisha upatikanaji wa umeme Kusini mwa Tanzania.


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, ameonesha kutoridhishwa na kasi ya utekelezaji wa Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa msongo wa kilovoti 220 kutoka Songea hadi Masasi kupitia Tunduru na kuagiza mkandarasi kuongeza juhudi ili kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati uliopangwa.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa maendeleo ya mradi huo leo Julai 22, 2026, Mhe. Ndejembi amesema Serikali haitakuwa tayari kuona miradi ya kimkakati inayogusa maisha ya wananchi ikicheleweshwa bila sababu za msingi.

Amesema mradi huo ni miongoni mwa miradi muhimu ya Sekta ya Nishati inayopewa kipaumbele na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutokana na mchango wake katika kuimarisha upatikanaji wa umeme na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika ukanda wa Kusini.

“Maendeleo ya mradi huu hayaridhishi ukilinganisha na muda uliopita tangu utekelezaji wake uanze. Serikali inatarajia kuona kasi kubwa zaidi ya utekelezaji katika kipindi kilichobaki. Nimemuagiza Katibu Mkuu kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa maelekezo haya na kuhakikisha hatua stahiki zinachukuliwa iwapo hakutakuwa na maboresho yanayoonekana,” amesema Mhe. Ndejembi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Nyasa, Mhe. Boniface Magiri, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, amesema Mkoa utaendelea kushirikiana na Serikali Kuu katika kufuatilia utekelezaji wa mradi huo ili kuhakikisha unakamilika na kuanza kutoa huduma kwa wananchi kwa wakati.

Naye Mhe. Sikudhani Chikambo kwa niaba ya wabunge wa Mkoa wa Ruvuma, viongozi hao wameishukuru Serikali kwa kuendelea kuwekeza katika miundombinu ya umeme ambayo itachochea ukuaji wa uchumi, uwekezaji na kuboresha huduma za kijamii katika maeneo ya Kusini mwa Tanzania.

Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa msongo wa kilovoti 220 kutoka Songea kupitia Tunduru hadi Masasi unatekelezwa na Mkandarasi Kalpataru Power kutoka India. Mradi huo unatarajiwa kuiunganisha Mikoa ya Lindi na Mtwara kwenye Gridi ya Taifa pamoja na kuimarisha upatikanaji wa umeme katika Wilaya ya Tunduru na maeneo jirani.












 


๐Ÿ“ŒNi baada ya kukamilika kwa njia ya kusafirisha umeme ya kilovoti 33 Masasi - Mtwara

๐Ÿ“ŒMradi umeimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa wananchi wa Wilaya ya Newala na maeneo jirani.

๐Ÿ“ŒMD Twange asema thamani ya mradi ni takribani shilingi bilioni 4.65


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amezindua rasmi mradi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 33 kutoka Masasi hadi Newala, akieleza kuwa mradi huo ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa wananchi na kuweka mazingira wezeshi kwa ukuaji wa shughuli za kiuchumi katika Wilaya ya Newala.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa njia hiyo, Mhe. Ndejembi amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaendelea kuwekeza katika miradi ya kimkakati ya umeme ili kuhakikisha huduma ya nishati inawafikia wananchi wengi zaidi na kuwa chachu ya maendeleo.

"Njia hii ya umeme ni msingi wa kukuza uchumi, kuongeza uzalishaji, kuvutia uwekezaji na kuboresha upatikanaji wa umeme kwa Wilaya ya Newala," amesema Mhe. Ndejembi.

Aidha, Waziri Ndejembi amesema Serikali itaendelea kuhakikisha Mikoa ya Lindi na Mtwara inapata umeme wa uhakika ikiwa ni pamoja na kuiunganisha Mikoa hiyo na umeme wa gridi ya Taifa.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Donald Msengi amesema miradi mbalimbali imeendelea kutekelezwa Mkoa wa Mtwara.

"Mheshimiwa Waziri niipongeze Serikali kwani Vijiji vyote vya Mkoa wa Mtwara 785 vinapata huduma ya umeme". Amesema Kanali Msengi.

Ameongeza kuwa katika kuboresha huduma kwa wateja mkoa wa Mtwara umepokea vitendea kazi yakiwemo magari kumi na moja, bajaji nne na pikipiki tisa.

Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi Mramba amesema Serikali imekuwa ikiboresha uwekezaji na upatikanaji wa umeme Mikoa ya  Mtwara na Lindi.

"Mahitaji ya Lindi na Mtwara yameendelea kuongezeka na Serikali imewekeza kwenye uzalishaji na hivi sasa Mkoa wa Mtwara tunazalisha zaidi ya megawati 50". Amesema Mha. Mramba.

Awali akitoa taarifa za utekelezaji wa mradi Mkurugenzi Mtendaji TANESCO, Bw. Lazaro Twange amesema ujenzi wa njia hiyo umetekelezwa kwa shilingi bilioni 4.56 kwa umbali wa Kilometa 76 kutoka Masasi hadi Newala.

"Mheshimiwa mgeni rasmi kabla ya mradi huu kutekelezwa Wilaya ya Newala ilikuwa ikipata umeme kutokea Mtwara kupitia Nanyumbu umbali wa kilometa 170, hali iliyochangia tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara". Amesema Bw. Twange.

Ameongeza kuwa kukamilika kwa ujenzi wa njia hiyo ya umeme kumeimarisha upatikanaji wa umeme na kuondoa changamoto ya kukatika kwa umeme kwa Wilaya hiyo.

Aidha, Serikali kupitia TANESCO imetenga takribani shilingi bilioni 5.27 kwa ajili ya kujenga kituo cha kubadilishia umeme (Switching Station) kitakacho saidia kuboresha upatikanaji wa umeme na kukidhi mahitaji ya sasa na ya badaye ya wananchi na wawekezaji wa Wilaya ya Newala. 

Mbunge wa Newala Vijijini Dkt. Yahaya Nawanda kwa niaba ya Wabunge wa Mkoa wa Mtwara ameipongeza Serikali kwa kuendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme Mkoa wa Mtwara.













.




NA DENIS CHAMBI TANGA.


MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt.Batilda Burian amewasisitiza watumishi wa umma, watendaji wa taasisi pamoja na wakurugenzi wa halmashauri zote mkoani humo kutambua thamani ya fedha zinazoteolewa na serikali kwaajili utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa kuhakikisha kuwa wanazuia ubadhilifu fedha na mianya yote ya rushwa ambayo inaweza kuwa kikwazo katika utoaji wa huduma kwa wananchi.


Akitoa rai hiyo kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Tanga, mkuu wa wilaya ya Handeni Salum Nyamwese katika warsha ya wadau wa usimamizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo mkoa wa Tanga iliyoandaliwa na taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU amewataka kuonyesha uzalendo uwajibikaji pamoja na kutokuwa sababu ya kuzuia maendeleo kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa mkoani humo.


"Rushwa ni adui mkubwa wa maendeleo ya Taifa lolote, kuhujumu matumizi sahihi ya rasilimali za umma, kudhoofisha ubora wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kupunguza ufanisi wa utoaji wa huduma kwa wananchi na kuondoa imani kwa wananchi , taasisi za serikali serikali kwa ujumla"


"Hatuwezi kufikia malengo ya maendeleo ambayo tumejiwekea kufikia kwenye dira ya maendeleo ya mwaka 2050 ikiwa tutaruhusu rushwa, ubadhilifu , ufisadi na ukiukwaji wa taratibu kuendelea" amesema Nyamwese


"Mapambano dhidi ya rushwa sio jukumu la TAKUKURU pekee mapambano haya ni ya kwetu sisi sote ambao tuna wajibu Kila kiongozi na Kila mtishi kwenye eneo lake kushiriki katika mapambano dhidi ya rushwa na hii inaakisi kaulimbiu ya kuzuia rushwa ni jukumu lako na langu tutimize wajibu wetu" amesisitiza.

Amesema serikali inautazama mkoa wa Tanga kama kitomvu cha biashara na utakaowavutia wawekezaji mbalimbali kutoka nje ya nchi kupitia miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo bomba la mafuta , ujenzi wa barabara inayotoka Tanga Hadi Dar es salaam pamoja na uboreshaji wa bandari ambapo kupitia fedha zilizoletwa ndani ya miaka mitano takribani Trillion 3.17 hazitokuwa na maana kama watendaji wa wasimamizi wa miradi hiyo hawatawajibika kikamilifu kwenye nafasi zao.


"Rais ametuamini na kutukabidhi dhamana ya kusimamia rasilimali za umma kwa niaba ya wananchi, hizo fedha zinazokuja na kupelekwa kwenye miradi hatuna budi kuonyesha kwamba imani hiyo hajaiweka mahali pasipo sahihi Kila moja wetu awajinike kikamilifu katika kufanya kazi kwa weledi ubadhilifu na uzalendo wa hali ya juu sisi kama watendaji kazi kubwa tuliyonayo ni kidaiwa matokeo" ameongeza Nyamwese.


Awali akizungumza mkuu wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa mkoa wa Tanga 'TAKUKURU' Ramadhani Ndwatah amesema kuwa wamefanikiwa kufanya tahmini na kupitia miradi yote inayotekelezwa ndani ya mkoa ambapo wamebaini baadhi ya changamoto zilizochangiwa na usimamizi mbovu, ucheleweshwaji wa miradi na matumizi yasiyosahihi ya fedha zilizotolewa kwenye miradi husika ambapo iliweza kuchukua hatua kisheria .


" Licha ya mafanikio yaliyopatikana kwenye miradi ya maendeleo lakini bado kuna changamoto ya udhaifu katika utekelezaji wa miradi ucheleweshwaji wa miradi kwa baadhi ya wadau wenye dhamana, kuongeza gharama zisizo za lazima na kupunguza manufaa yanahotarajiwa kwa wananchi"


"Kutokana na changamoto hizo zilizojitoleza tumeona ni vyema kukaa na wadau wa usimamizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili tuweze kukumbuahana kuhusu wajibu wao katika usimamizi na utekelezaji wa programu na miradi inayotekelezwa katika maeneo yetu" amesema Ndwatah.


Amewataka wadau wote wenye dhamana ya usimamizi wa miradi mbalimbali inayotekelezwa kushirikiana kikamilifu na TAKUKURU ili kuweza kutimiza adhima ya serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo kupitia miradi inayotekelezwa kwenye maendeleo mbalimbali.


Akizungumza katika warsha hiyo mkurugenzi wa Halmashauri ya jiji la Tanga mhandishi Juma Hamsini ameiomba serikali kupitia mamlaka za serikali tawala za mikoa na serikali za mitaa 'TAMUSEMI' mara wanapopeleka BOQ za ujenzi wa miradi mbalimbali ikiwemo madarasa kuzingatia thamani halisi ya vifaa vinavyotumika kwenye miradi husika.











Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), Ndugu Rabia Abdalla Hamid , ameshiriki Mkutano Mkuu wa Chama cha Botswana National Front (BNF) unaofanyika mjini Jwaneng, Botswana, akiwakilisha Chama Cha Mapinduzi.




Akizungumza katika mkutano huo, Ndugu Rabia amesisitiza kuwa kila chama tawala kina wajibu wa kuwatumikia wananchi kwa uadilifu, kuimarisha misingi ya utawala bora, na kuendelea kutoa huduma zinazokidhi mahitaji ya wananchi bila kuchoka.




Aidha, amekisii Chama cha BNF kuendelea kuzingatia maslahi ya wananchi katika utekelezaji wa sera na maamuzi yake, pamoja na kuhakikisha kuwa hakuna mwananchi anayebaki nyuma katika mchakato wa maendeleo ya taifa.


Aidha,Ndg. Rabia amempongeza Rais wa Chama cha Botswana National Front (BNF) na Rais wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Duma Gideon Boko kwa ushindi wa Chama chake na kuchaguliwa kwake kuwa Rais wa Jamhuri ya Botswana.

Ameeleza kuwa kuchaguliwa kwa Rais Boko na Chama cha BNF ni kielelezo cha imani waliyopewa na wananchi wa Botswana na amewatakia mafanikio katika kuwaletea maendeleo na ustawi wao.
Mbunge wa Jimbo la Kwela ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Deus Sangu akipata Maelezo kutoka kwa msimamizi wa mradi wa ujenzi wa madarasa Noble Helium ambayo Inafanya shughuli za utafiti na uchimbaji wa gesi ya helium Christian Temba (20 Julai 2026) alipokuwa akikagua miradi ya Maendeleo katika Kijiji cha Kinambo Kata ya Milepa Wilaya ya Sumbawanga.



Mbunge wa Jimbo la Kwela na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi,Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu akizungumza na wananchi wa kijiji cha Lwanji Tarafa ya Kipeta Sumbawanga ambapo amewasihi kuendelea kuunga mkono juhudi za maendeleo jana. Kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Ephraim Konta
( Picha na OWM- KAM)


Na: OWM (KAM), Sumbawanga

Mbunge wa Jimbo la Kwela ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Deus Sangu amewataka vijana wa Mkoa wa Rukwa kujitokeza kwa wingi kuchangamkia fursa za ajira zinazozalishwa na mradi wa kimkakati wa uchimbaji wa gesi ya helium katika Bonde la Ziwa Rukwa.

Sangu alitoa wito huo Julai 20, 2026 alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Kinambo Kata ya Milepa Wilaya ya Sumbawanga akisema mradi huo una nafasi kubwa ya kuongeza ajira na kuinua uchumi wa wananchi hususan vijana wa maeneo yanayouzunguka.

Alisema Serikali imeingia makubaliano na kampuni ya Marekani ya Noble Helium kufanya shughuli za utafiti na uchimbaji wa gesi ya helium katika ukanda wa Bonde la Ziwa Rukwa, ambapo shughuli hizo tayari zimeanza na kuendelea kuzalisha nafasi mbalimbali za ajira.

Waziri Sangu ambaye ndiye mwenye dhamana na masuala ya ajira nchini alisema tayari amefanya mazungumzo na viongozi wa kampuni hiyo ili kuhakikisha vijana wa Kijiji cha Kinambo kilicho jirani na mradi huo wa gesi na Mkoa wa Rukwa wanapewa kipaumbele katika nafasi za ajira zinazopatikana kupitia mradi huo.

“Fursa za ajira katika mradi huu ni nyingi. Lengo letu ni kuona vijana wa maeneo haya wananufaika moja kwa moja kwa kupata ajira zitakazowaongezea kipato na kuboresha maisha yao,” alisema.

Mbali na kutoa ajira kampuni ya Noble Helium imeanza kutekeleza shughuli za uwajibikaji kwa jamii kwa kujenga madarasa mawili katika Shule ya Msingi Kinambo hatua inayolenga kuboresha mazingira ya elimu kwa watoto wa eneo hilo.
Akizungumza kwa niaba ya kampuni hiyo msimamizi wa mradi wa ujenzi wa madarasa Christian Temba alisema ujenzi huo ni sehemu ya mchango wa kampuni katika kuunga mkono jitihada za maendeleo zinazofanywa na wananchi na Serikali katika sekta ya elimu.

Katika ziara hiyo Sangu pia alikabidhi madawati 20 kwa Shule ya Msingi Msia iliyopo Kata ya Milepa. Madawati hayo yametolewa kwa ufadhili wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) na yanatarajiwa kunufaisha wanafunzi zaidi ya 60 kwa kuboresha mazingira ya kujifunzia.

Aidha, aliwahakikishia wananchi wa Jimbo la Kwela kuwa ataendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kutafuta misaada na rasilimali za kuchangia utekelezaji wa miradi ya maendeleo, akisisitiza kuwa utekelezaji wa ahadi zake za uchaguzi wa mwaka 2025 unaendelea kwa vitendo.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Ephraim Konta, alimpongeza Waziri Sangu kwa mchango wake katika miradi ya maendeleo akisema msaada wake wa vifaa vya ujenzi umechangia kukamilika kwa ujenzi wa madarasa katika Shule za Msingi Lwanji na Kanyala hatua iliyotoa unafuu kwa wananchi wengi.





Jumuiya ya Afya ya Nchi za Afrika Mashariki, Kati na Kusini (ECSA-HC), kwa kushirikiana na Wizara ya Afya Tanzania na wadau mbalimbali, imeandaa kambi maalum ya huduma za madaktari bingwa na bobezi iliyoanza Julai 20 hadi 30 mwaka huu katika Hospitali ya Rufaa ya Arusha Mount Meru na Hospitali ya Kanda ya Kusini ya Mtwara.


Akizungumza Jijini Arusha kuhusu kambi hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa ECSA-HC, Dkt. Ntuli Kapologwe, amesema kambi hizo zinalenga kuwahudumia wananchi wenye mahitaji mbalimbali ya upasuaji na huduma za kitabibu, huku ECSA ikitoa shilingi milioni 211 kufanikisha zoezi hilo.


Amesema kati ya fedha hizo, shilingi milioni 52 zitatumika kununua vifaa tiba, dawa na mahitaji mengine muhimu, huku shilingi milioni 158 zikielekezwa kugharamia wataalamu pamoja na madaktari bingwa na bobezi watakaotoa huduma kwa takribani siku 10.


Dkt. Kapologwe ametoa shukrani kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na viongozi wa Wizara ya Afya wakiongozwa na Waziri Mohammed Mchengerwa na Katibu Mkuu Dkt. Grace Maghembe kwa ushirikiano mkubwa walioutoa katika maandalizi ya zoezi hilo na  wadau mbalimbali, wakiwemo mabenki, kwa michango yao iliyowezesha kufanikisha utekelezaji wa kambi hizo.


Amesema mbali na kupunguza maumivu na kuwasaidia wananchi wenye uhitaji wa huduma za kibingwa, lengo kuu la mpango huo ni kuwawezesha wagonjwa kurejea katika hali yao ya kawaida ili waendelee kushiriki katika shughuli za uzalishaji na kuchangia maendeleo pamoja na pato la Taifa.


Ameongeza kuwa zoezi hilo ni sehemu ya programu ya ECSA inayotekelezwa katika nchi mbalimbali, baada ya kufanyika Lesotho na Uganda, huku Tanzania na Malawi zikitekeleza kambi hizo kwa kipindi na tarehe zinazofanana.


Halikadhalika, Dkt. Kapologwe amewataka wananchi wenye uhitaji wa huduma za upasuaji kujitokeza kwa wingi kupata huduma hizo ili warejee katika  katika afya njema na maisha yao ya kawaida.

Siku ya harusi yangu ilitakiwa kuwa siku ya furaha zaidi maishani mwangu. Ukumbi ulikuwa umepambwa kwa maua meupe ya kuvutia, wageni waalikwa walikuwa wamekaa, na keki ya ghorofa tano ilikuwa tayari.

Nikiwa nimevalia shela langu la harusi, nikisubiri kuingia kanisani, mlango wa chumba changu ulifunguka kwa nguvu. Alikuwa ni bwana harusi mtarajiwa, akiwa na uso wa baridi, na kuniambia maneno yaliyosimamisha moyo wangu: “Siwezi kufanya hivi. Harusi imefutwa.”

​Saa moja tu kabla ya kiapo, aliondoka na kuniacha nikiwa nimechanganyikiwa, nikilia kwa uchungu na aibu kubwa mbele ya wazazi wangu. Ndoto yangu ya miaka minne ilisambaratika kwa sekunde chache.

Ndugu walibaki wameduwaa, na sherehe iligeuka kuwa msiba wa kihisia. Nilihisi sitaweza kamwe kuinua uso wangu mbele ya jamii tena. SOMA ZAIDI.

Kuhitimu masomo yangu ya chuo kikuu kwa kiwango cha juu ilikuwa fahari kubwa kwa familia yangu. Tuliamini kuwa elimu hiyo ingekuwa ufunguo wa kuondoa umaskini nyumbani.

Hata hivyo, ukweli wa mitaani ulikuwa tofauti kabisa. Miaka minne ilipita nikiwa nazurura na bahasha ya vyeti chini ya jua kali, nikituma maombi ya kazi kila kona bila mafanikio yoyote.

​Kila usaili niliompata uliishia kwa kuambiwa “tutakutafuta,” maneno ambayo yalikuwa ishara ya kukataliwa. 

Nilishuhudia wadogo zangu na marafiki zangu wakipata kazi nzuri, huku mimi nikibaki kuwa mzigo kwa wazazi wangu. Nilikata tamaa, nikapoteza kujiamini, na nilianza kuhisi kuwa labda nyota yangu ilikuwa imefifia kabisa.SOMA ZAIDI.
Ndoa yangu iliononekana kuwa ya mfano wa kuigwa katika jamii. Mume wangu alikuwa mtu mwenye upendo, mkarimu, na aliyetujali sana mimi na watoto wetu. Hata hivyo, kwa miaka mitatu ya mwisho, nilianza kuhisi mabadiliko ya chini kwa chini.

Simu yake ilianza kuwekwa nenosiri (password) kali, safari za kikazi za ghafla zilipishana, na upendo wake kwangu ulianza kupoa. Kila nilipomuuliza, alinituhumu kwa kuwa na wivu usio na msingi. Niliumia moyoni na kukosa amani ya nafsi.

​Kilele cha sintofahamu hii kilikuja kudhihirika siku tuliyofanya sherehe kubwa ya kifamilia nyumbani kwetu, tukiwa tumewaalika ndugu, jamaa, na marafiki zetu wa karibu.

Katikati ya vicheko na furaha ya wageni wetu, siri nzito iliyokuwa imefichwa kwa miaka mitatu ililipuka kama bomu mbele ya kila mtu.SOMA ZAIDI.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (kulia) akimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge mara baada ya kuwasili mkoani humo kwa ajili ya ziara ya kikazi ambayo anatarajia kuifanya kuanzia leo Julai 20,2026.
Mbunge wa Jimbo la Kwela ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akizungumza na Viongozi na Wananchi mara baada ya kukagua mradi wa Shule ya Msingi Mfinga iliyopo Sumbawanga, Mkoani Rukwa tarehe 19 Julai, 2026.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, akizungumza na wafanyabiashara wa mifugo na mazao yake wakati wa kikao kilichoandaliwa na Umoja wa Wafanyabiashara wa Mifugo na Mazao Yake Temeke (UWAMIMATE), kilichofanyika Julai 19, 2026 katika Ukumbi wa Wakala wa Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) Temeke, Dar es Salaam. Katika kikao hicho, wafanyabiashara waliwasilisha changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya biashara ya mifugo na mazao yake, huku Waziri akiahidi kuzifanyia kazi kwa kushirikiana na wizara na taasisi husika
 

Na.Mwandishi Wetu

Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela ( NM- AIST) inatumia mbio za marathon kama moja ya mikakati ya kupata fedha za kutoa ufadhili wa masomo kwa wanawake na wasichana ili kuongeza ushiriki wao katika masomo ya Sayansi, Teknolojia, Hisabati na Ubunifu (STEM).

Hayo yamebainishwa Julai 19, 2026 Jijini Arusha wakati wa Maadhimisho ya Mbio za Taasisi hiyo na Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Dkt. Toba Nguvila ambapo amesema kuwawezesha wanawake na wasichana katika masuala ya Sayansi si hisani bali ni uwekezaji wa kimkakati wa Maendeleo ya Taifa

Dkt. Nguvila ameeleza kuwa Dira ya Taifa 2050 inalenga kujenga uchumi wa maarifa unaotegemea ujuzi, utafiti na teknolojia hivyo ametoa wito kwa Taasisi za Elimu ya Juu hususan NM- AIST kuhakikisha tafiti zinazofanyika katika Taasisi hiyoziwe ni zile zizotatua changamoto za wananachi katika sekta za Kilimo, mifugo, madini na viwanda.

​Akizungumza awali katika tukio hilo Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Prof. Maulilio Kipanyula amesema kuwa mbio hizo zilianzishwa mwaka 2024 kuhamasisha wasichana kusoma masomo ya sayansi na kutimiza ndoto zao za kuwa madaktari, wahandisi na watafiti.

"​Kwa sasa, Mbio za Mandela zimekuwa alama ya mkoa wa Arusha kwa kuchangia ukuaji wa sekta za michezo, elimu, sayansi, afya na utalii. Tukio hili limeweka msingi imara wa kujenga taifa lenye ujumuishi, mshikamano, na kuandaa kizazi kipya cha wanasayansi na wabunifu wasichana na wanawake," amesema Prof Kipanyula

Mbio hizo zilizohusisha umbali wa kilomita 2.5, 5 10 na 21 zimevuta ushiriki mkubwa wa jamii kutoka ndani na nje ya nchi, na kufanya azma ya kuifanya Arusha kitovu cha sayansi na ubunifu barani Afrika kuwezekana.

Mbio za NM- AIST za Mwaka 2026 zina kauli mbiu isemayo Jitihada kwa Sayansi Hatua kwa Mafanikio.