Naibu Waziri Nishati na Mbunge wa Viti Maalum Vijana Taifa, Mhe. Judith Kapinga amewahamasisha wananchi katika Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma kujitokeza kwa wingi katika zoezi  la kujiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ili waweze kuchagua viongozi watakaowaletea maendeleo. 

Mhe. Kapinga amesema hayo hivi karibuni wakati akifungua Mafunzo ya Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 kwa Viongozi, Watendaji na Wadau wa Wilaya ya Mbinga.

"Ni muhimu kila mmoja wetu akashiriki zoezi la kujiandikisha,  sio kujiandikisha wewe tu bali kuhamasisha na wengine kwenye eneo lako waweze kujiandikisha." Ameeleza Kapinga

Amesema ili wananchi waweze kuweka viongozi imara watakaofaa kwenye jamii, ni lazima kuwe na watu wengi wa kuwapigia kura, hivyo ni vyema wananchi wakahamasishana ili kwenda kwa wingi  kujisajili kwenye daftari la kudumu la wapiga kura.

Aidha, ametoa rai kwa wananchi kuchagua viongozi  watakaowatumikia  kwa weledi na kutatua changamoto mbalimbali pale zinapojitokeza.


TAASISI  ya Moyo ya (JKCI), imeanza  kambi ya siku nne ya kupima na kutibu maradhi ya moyo kuanzia kesho kwa wakazi wa Mkoa wa Arusha.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Dk. Peter Kisenge alisema wameandaa kambi hiyo kwa kushirikiana na Arusha Lutheran Medical Center (Selian ya Mjini).

Dk. Kisenge alisema pia wameshirikiana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda kuandaa kambi hiyo ambayo wanatarajia kuwafanyia uchunguzi watu wengi na kuwapa matibabu wale watakaobainika kuwa na matatizo ya moyo.

Alisema kambi hiyo itaendeshwa kuanzia Jumanne tarehe 15 mpaka 18 katika viwanja vya Arusha  Lutheran Medica Center na kwamba watakaohudumiwa ni pamoja na mikoa jirani na Arusha.

Aliwaomba wananchi wa Arusha na mikoa jirani kujitokeza kwa wingi kupima afya zao kwani watakaogundulika kuwa na matatizo ya moyo watapatiwa matibabu na wengine kupewa rufaa kwenda Dar es Salaam kutibiwa JKCI.

Alisema kwenye kambi hiyo wataalamu wa lishe watakuwepo kutoa elimu kuhusu namna ya kula vyakula ili kuepukana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza yakiwemo ya moyo.

“Watu wajitokeze watumie fursa hii kwasababu watakaobainika kuwa na matatizo ya moyo watapatiwa matibabu hapo hapo au kupewa rufaa kwenda JKCI Dar es Salaam,” alisema

Alisema jamii inapaswa kujenga utamaduni wa kupima afya ya moyo mara kwa mara kwani baadhi ya watu wamekuwa wakishi na maradhi hayo bila kujua lakini iwapo wangepima wangegundua na kupatiwa matibabu mapema.

Alisema wananchi wanapaswa pia kuzingatia ushauri wa wataalamu kuhusu lishe bora kwani wakizingatia lishe bora wataepuka maradhi mengi hasa yasiyo ya kuambukiza kama moyo.

“Wananchi wanapaswa kuzingatia lishe bora na kuwasikiliza wataalamu kuhusu ulaji unaofaa utakaowaepusha na maradhi mbalimbali yasiyo ya kuambukiza ambayo mengi yanatokana na ulaji usiofaa na wataalamu wa JKCI watakuwepo Arusha kuwapa elimu hiyo,” alisema Dk. Kisenge

Alisema JKCI imeendelea kujiimarisha kwa kuwa na vifaa tiba vya teknolojia ya kisasa na wataalamu bobezi wa moyo hali ambayo imepunguza utegemezi wa kupeleka wagonjwa wa moyo kwa matibabu nje ya nchi kwa zaidi ya asilimia 90.

Dk. Kisenge alimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwekeza kwenye taasisi hiyo ambayo sasa imekuwa kimbilio kwa mataifa mengi ya Afrika kutokana na kuwa na madaktari bingwa bobezi na vifaa vya kisasa kama vile vilivyoko nchi zilizoendelea.

Alisema baadhi ya mataifa ya Afrika yamekuwa yakiwaomba madaktari wa JKCI kwenda kutoa mafunzo ya utaalamu wa kibingwa wa matibabu ya moyo kwenye nchi zao na kuongeza kuwa hivi karibuni watalaamu wake walikuwa nchini Zambia kwa kazi kama hiyo.

Dk Kisenge alisema JKCI ilikuwa ikitoa matibabu kwenye maonyesho ya madini mkoani Geita kwa kushirikiana na hospitali ya kanda ya Chato.

Alisema taasisi hiyo itaendelea kushirikiana na hospitali zote nchini kuhakikisha wanatimiza ndoto za Rais Samia Suluhu Hassan kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba.

“Kwenda Arusha ni mwendelezo wa kile tulichokuwa tukikifanya kwenye maonyesho ya madini tukishirikiana na hospitali ya kanda ya Chato,” alisema 

Naye Profesa Mohamed Janabi ambaye ni Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), alishukuru jitihada na ubunifu wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda kwa kushirikiana na hospitali za mkoa huo kuhakikisha Tanzania inakuwa kitovu cha utalii tiba.

Mkuu wa wilaya ya Ilala Edward Mpogolo amewataka vijana kuwa wazalendo  ili kuendelea kumuenzi Baba wa Taifa hayati  Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika kudumisha Demokrasia na kushiriki katika chaguzi kwa kupiga kura kwenye chaguzi za mitaa, vijiji na vitongoji. 

Amesema Mwalimu Nyerere amekua kiongozi wa kuonesha mfano mzuri wa Demokrasia hata kukubali uanzishwaji wa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992  nchini na kukubali kung'atuka katika madaraka  jambo ambalo si lakawaida kwa viongozi waliopigania uhuru wa nchi zao. 

Mpogolo ameyasema hayo katika mahojiano maalum juu ya maadhimisho ya miaka 25 ya kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Amesma ili kumuenzi Nyerere na kuendelea kumkumbuka ni vema vijana wa Tanzania kudumisha amani, umoja, mshikamano na kuwa wazalendo kwa Taifa lao.

Ameongeza kuwa miaka 25 ya kumbukizi ya kifo cha Mwalimu Nyerere kilichotokea tarehe 14 ya mwezi 10 mwaka 1999 katika hospitali ya mtakatifu thomas nchini uingereza alikokua anapatiwa matibabu ya maradhi yaliyokua yanamsumbua ni majonzi kwa Taifa.

Ameeleza miaka 25 ya kifo cha Mwalimu vijana wanatakiwa kujifunza maisha ya mwalimu Nyerere aliyependa Utu, kujifunza na kutosheka katika madaraka hali iliyomjengea heshima ya kisiasa nchini, barani Afrika na duniani kwa ujumla.

Amesisitiza kitendo cha mwalimu Nyerere kuaminiwa na wazee na chama cha Tanu kuongoza Watanganyika kutafuta Uhuru ni kutokana na heshima, busara na unyenyekevu licha ya elimu yake alikubali kutumwa kusaidia nchi yake. 

Mpogolo amesema Hayati Mwalimu Nyerere amekua na mchango mkubwa kuhakikisha muungano wa Tanganyika na Zanzibar unafanikiwa kwa kushirikiana na aliyekua Rais wa Zanzibar Hayati Shekhe Abeid Amani Karume, muungano ambao hadi sasa unaendelea kudumishwa.

 Licha  ya ndoto yake ya kutamani Bara lote la Afrika linaungana bado Watanzania wanaona mchango wake wa kuunda umoja wa nchi za Afrika mashariki unaendelezwa. 


Mpogolo ameeleza alama aliyoacha Mwalimu Nyerere ni kubwa maeneo mbalimbali nje ya Tanzania kwa nchi zilizosaidiwa na Mwalimu Nyerere kupata uhuru ikiwemo  Msumbiji, Afrika Kusini,  Angola na Namibia.

Amebainisha kumbukizi ya miaka 25 ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere watanzania bado wanashuhudia Marais wa awamu zote wakiendelea kulinda tunu za Taifa la Tanzania toka kifo chake kilipotokea kipindi cha awamu ya tatu chini ya hayati Benjamin Mkapa, awamu ya nne ya Jakaya Kikwete, awamu ya tano ya Hayati John Magufuli hadi sasa awamu ya sita ya Rais Samia Suluhu Hassan. 


Jambo ambalo Watanzania wataendelea kumkumbuka Mwalimu Julius Nyerere ni kuwacha katika misingi ya umoja, amani, upendo na mshikamano pamoja na kukemea suala la udini, ukabila na ukanda katika Taifa.

  MBUNGE wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu,akizungumza katika mahafali ya Kidato cha Nne shule ta sekondari Mwau iliyopo Kata ya Manginyi



MBUNGE wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu ameshiriki mahafali ya Kidato cha Nne shule ta sekondari Mwau iliyopo Kata ya Manginyi na kutoa msaada wa mashine ya kudurufu na Sh.Milioni tatu ya kukarabati ofisi ya Walimu na ununuzi wa samani ili kutatua changamoto walizonazo.

Changamoto ni miongoni mwa changamoto walizozitaja kwenye risala na taarifa iliyosomwa na Mkuu wa shule Mwalimu Robert Simon.

Akizungumza katika mahafali hayo Mtaturu amewapongeza wazazi na walimu kwa kuwasimamia watoto kupata elimu iliyo bora na kuhakikisha wanafunzi wanapata lishe shuleni.

Ametumia nafasi hiyo kuwahakikishia kuwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan itaendelea kuboresha miundombinu ya shule ili kuweka mazingira mazuri ya kujifunzia.

"Kฤบatika miaka mitatu serikali ilileta jumla ya Sh Milioni 245 kwa ajili ya kujenga madarasa matano mapya,maabara za sayansi,vyumba viwili na matundu sita ya vyoo,na tukumbuke kabla ya Mwaka 2020 shule ilikuwa na changamoto kubwa ya vyumba vya madarasa,hivyo Rais wetu amesaidia kutatua changamoto hii,"amesema.

Akieleza mabadiliko mengine ya maendeleo yanayoonekana ni umeme,miradi ya maji,barabara katika Kata ya Mang'onyi.

Akisoma taarifa Mkuu wa Shule hiyo Simon ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt Samia kwa kuwaletea fedha za miradi shuleni hapo na hivyo kuondoa changamoto iliyokuwepo awali na kuboresha mazingira ya kujifunzia.

Amempongeza Mbunge Mtaturu kuwa sauti ya wananchi Bungeni kuomba fedha hatimaye changomoto zimetatuliwa.

Pia amemshukuru kwa kuwapelekea kompyuta mbili na printa moja inayosaidia shughuli za kielimu hapo shuleni.

Changamoto alizoziwasilisha ni uhaba wa nyumba za walimu,kutokuwa na mwalimu wa kike,ukosefu wa mashine ya kudurufu ,ukosefu wa jengo la utawala na samani za ofisi.

Akijibu risala hiyo Mtaturu ameahidi atika kujibu kuzipeleka kunakohusika ili zipatiwe ufumbuzi.

Katika kuhamasiaha ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha nne shuleni hapo aliahidi kumtunuku kila mwanafunzi atakayepata ufaulu wa daraja la kwanza Sh.laki moja na upande wa Walimu zikipatikana daraja la kwanza 10 atawatunuku milion moja.

Amewakumbusha kushiriki zoezi la uandikishaji wa daftari la mpiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27,2024.

Mwenyekiti wa bodi amemshukuru Mbunge Mtaturu kwa kuendelea kuwa sauti ya wananchi na kulibadilisha jimbo la Singida Mashariki kimaendeleo kwani kila mahali kuna miradi ya kutosha na hivyo kuahidi kuendelea kumuunga mkono.

#SingidaMashariki#MaendeleoYanayoonekana#TuliahidiTumetekelezaTumewafikia#         

 


Dada mmoja aitwaye Khadija kazi yake ilikuwa rahisi tu, kazi hiyo ilimbidi tu kujifanya kama anauza mkufu wa dhahabu kwa bei ya kutupa kisha kuwavuta wateja hadi eneo fulani la uchochoni karibu na Old Town, halafu hapo wanaume kadhaa watajitokeza na kumpora mwanaume huyo.

Alikuwa na sehemu tatu tofauti za kufanya uhalifu huo ambao uliongozwa na wanaume wenye bunduki moja, visu kadhaa na pingu zilizonunuliwa kutoka kwa afisa polisi ambaye anaunga mkono uhalifu.

Siku moja Khadija alisimulia hadithi yake ya jinsi yalivyoweza kuachana na genge hilo na kuanza maisha yake mapya huko Kiembeni, Mombasa nchini Kenya.

Basi kuna siku ilianza kama kawaida, yeye na genge lake walipata bahati ya kuwaiba watalii wawili kutoka Uholanzi. Wawili hao walikuwa na kama Euro 3,000, fedha hiyo kwao ilimaanisha mwanzo mzuri wa biashara yao ya uporaji kwa siku hiyo.

Anasema kwa kipindi hicho walikuwa wanatengeneza haribia Ksh5,000 wa siku kutokana na shughuli zao za uporaji, kwa hakika ilikuwa ni kazi haramu iliyowalipa zaidi.

Sasa siku hiyo Mzee mmoja mwenye umri wa miaka 62 hivi, alipita eneo lake na mara moja Khadija alimchangamkia na kutaka kumuuzia vito ili kumuibia mzee huyo ambaye alikuwa na begi lenye kiasi cha Ksh200,000.

Kama ilivyo kawaida yake, Khadija alifanikiwa kumuongoza moja kwa moja hadi kwenye genge lake ambalo walimpora Mzee huyo fedha zote alizokuwa nazo.

Kutokana na umri wake, hakuweza kukimbia, hivyo wakamsukuma tu na kuanza kuhesabu pesa hizo ambazo ziliwachanganya sana.

"Mzee alipiga simu, na kale kasimu kadogo tulichomuachia, na baada ya muda mchache, mambo yakaharibika. Tulishtuka baada ya kuona kuwa wote tumepoteza uwezo wa kutembea. Tulibaki kama sanamu na tusijue la kufanya," alisema.

Mzee huyo alirudi akiwa na mkusanyiko mdogo wa wanafamilia na marafiki zake na kuwakuta wakiwa bado wameganda katika eneo lile kama sanamu, na punde tu walipokea kipigo ambacho Khadija anasema hatakisahau maishani mwake.

Khadija anasema kwamba Mzee huyo aliwasiliana na Dr Bokko ambaye ni mtaalamu wa mitishamba na akamueleza jinsi alivyoporwa fedha zake Ksh200,000 na ndipo walipomfanyia matambiko yao ya kurejesha mali zake.

Hii inatoa somo kwa wengi, iwapo una mali zake ziliporwa, basi unaweza kuwasilina na Dr Bokko kwa namba +255618536050 na kupata usaidizi ndani ya muda mfupi tu.



Naibu Waziri Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga amesema kuwa matumizi ya nishati safi ya kupikia yanaenda kuwaokoa  watu wenye mahitaji maalum na kadhia zinazotokana na matumizi ya nishati isiyo safi ya kupikia ikiwemo kuni na mkaa.

 Amesema kadhia hizo wanazipata nyakati za utafutaji na utumiaji wa nishati hizo zisizo safi za kupikia ambazo hutoa moshi mwingi unaoleta pia athari kwenye mfumo wa upumuaji.

Nderiananga ameyasema hayo jijini Dodoma wakati alipokuwa akihamasisha wananchi kupika kisasa kwa kutumia nishati safi ya kupikia kupitia programu ya Pika Kisasa inayoendeshwa na Wizara ya Nishati.

"Natoa rai kwa jamii kuwa na mtazamo chanya juu ya nishati safi ya kupikia ili kuongeza kasi ya matumizi ya nishati hii nchini." Amesema Nderiananga

Ameongeza kuwa, Viongozi katika ngazi mbalimbali nchini wataendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa vitendo na hii inajumuisha Wabunge wanawake  nchini kuwa na programu maalum ya kuelimisha jamii majimboni.

Akizungumzia mazingira amesema faida mojawapo ya nishati safi ya kupikia ni uhifadhi wa mazingira utakaopelekea mvua kupatikana kwa wakati.

Ametaja faida  nyingine ya matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kuwa ni jamii kuondokana na magonjwa yanayotokana na matumizi ya nishati isiyo safi  ikiwemo athari katika  mapafu  inayopelekea tatizo la upumuaji.

Mfanyakazi wa GPF ORGANICS LTD akiwa amebeba zao la Mdalasini tayari kwa hatua ya uchakataji.
Zoezi la uchakataji wa mazao ya viungo likiendelea  GPF ORGANICS LTD   kazi kubwa ya uchakataji inafanywa na wanawake ambapo asilimia 95 ya  waajiriwa wa  kampuni hiyo ni wanawake.
Zoezi la uchakataji wa mazao ya viungo likiendelea  GPF ORGANICS LTD   kazi kubwa ya uchakataji inafanywa na wanawake ambapo asilimia 95 ya  waajiriwa wa  kampuni hiyo ni wanawake.


Na Tukuswiga Mwaisumbe,Muheza Tanga


Ni habari zenye simulizi ya mafanikio kwa wanawake na wananchi wa shoroba ya Amani Nilo juu ya kilimo cha mazao ya viungo,  Bi Esther John Nzalia kutoka kijiji cha Antakae  kata ya Kwezitu ni mwanamke wa mfano ambaye analima na kuchajata mazao haya ya viungo.


Kabla ya ujio wa mradi wa USAID tuhifadhi maliasili anasema katika kijiji chao walilima na kuuza mazao kwa  mazoea yasiyo na tija, baada ya ujio wa mradi  wamepewa miche na elimu bure wameitumia  soko limepaa.


Serikali ni msimamizi wa umma dhidi ya wawekezaji katika Maendeleo ya kilimo,  Marekebisho ya kiuchumi yamesababisha kufunguka kwa sekta hiyo kwa uwekezaji binafsi katika uzalishaji na usindikaji  na masoko ya kilimo.


Ingawa Ushoroba huu una maeneo mazuri ya uzalishaji,  Bi Magreth David  ( GPF ORGANICS LTD) anasema uzalishaji na uuzaji wa mazao haya ya viungo bado ni wa chini, anasema  kuna ukuaji mkubwa wa mahitaji ya mazao ya viungo duniani ikiwa uzalishaji utakuwa na ubora hasa kilimo kisichotumia mbolea za viwandani.


Uwepo wa wadau hawa wa GPF ORGANICS LTD  ni fursa kwa wakazi wa shoroba hii ya Amani Nilo kiweza kupata soko la nje na kuweza kuuza mazao yao kwa bei nzuri na kulima mazao yenye ubora  unaozingatia kilimo HAI.

#USAID tuhifadhi maliasili

KATIKA kuadhimisha kumbukizi ya miaka 25 ya kifo cha Baba wa Taifa mwalimu julias kambalage Nyerere  watumishi wa shirika la umeme Tร nesco MKoa wa Lindi wametembelea na kutoa mahitaji maalumu katika kituo cha kulelea watoto cha loving heart.
KATIKA kuadhimisha kumbukizi ya miaka 25 ya kifo cha Baba wa Taifa mwalimu julias kambalage Nyerere  watumishi wa shirika la umeme Tร nesco MKoa wa Lindi wametembelea na kutoa mahitaji maalumu katika kituo cha kulelea watoto cha loving heart.


KATIKA kuadhimisha kumbukizi ya miaka 25 ya kifo cha Baba wa Taifa mwalimu julias kambalage Nyerere  watumishi wa shirika la umeme Tร nesco MKoa wa Lindi wametembelea na kutoa mahitaji maalumu katika kituo cha kulelea watoto cha loving heart.

Msaada uliotolewa kituoni hapo ni pamoja na unga , mchele, mafuta ya kupikia, sabuni juice,Sukari,  sufulia pamoja na jiko janja la kupikia la umeme.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo Meneja wa Tร nesco MKoa wa Lindi Athumani Jumbe  amesema wameamua kutembelea kituo hicho ili kuwapa faraja watoto wanaoishi Katika kituo hicho pamoja na walezi wao.


Afisa mahusiano na huduma kwa wateja wa shirika hilo MKoa wa Lindi Robert Fred amesema wameona kuwakabudhi jiko janja la umeme ili kuwarahisishia shughuli zao za mapishi ikiwa sambamba na kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais Samia za kuhamasisha matumizi ya nishati Safi.



Joyce Makajula ni malezi wa kituo hicho cha loving  heart amelishukuru Shirika hilo la Tร nesco kwa kukukumbuka kituo hicho na kwamba jiko walilolitoa litawasaidia kurahisisha shughuli zao za upishi .


Mwisho

 


Jina lagu Abigail, nilikutana na mchumba wangu akiwa hana kazi, mimi nilikuwa na kazi kwa hiyo nikawa namsaidia kifedha huku tukitafuta ramani za yeye kupata chochote cha kufanya kupata kipato na kuendesha maisha yetu.

Nilijaribu kumuombea kazi ofisini kwetu lakini hakufanikiwa na kila sehemu alikokuwa anapeleka barua hakufanikiwa. Ilifika kipindi hadi alipokuwa anaishi kwa ndugu zake ikawa shida maana alionekana kama mzingo.

Isingekuwa rahisi kipindi kile kukubali aje kuishi na mimi maana hatukuwa tumeoana. Hivyo familia yangu lazima ingeleta shida maana imekuwa yenye kufuata maadili kwa sana.

Ili kuepuka kukaa bila kazi ilibidi nianzishe mradi wa kufuga kuku wa mayai nje ya mji, na vyeti vyake akawa msimamizi. Ndani ya miaka mitatu, pesa iliyoingia kwenye kuku ni zaidi ya mshahara wangu.

Hata hivyo, ukweli ni kwamba mafanikio haya hajakuja kwa bahati mbaya, nasema hivyo kwa sababu kabla ya kuingia katika ufugaji wa kuku niliamua kwenda kwa Dr Bokko ambaye walinifanyia dawa za kukuza biashara na kuilinda.

Tangu wakati huo mambo yakawa yanaenda kama tulivyopanga na mpenzi wangu. Kuku wakawa wanazaliana kwa wingi, na hata wateja wakawa ni wengi sana kiasi kwamba hadi tukawa tunashindwa kuwatimizia mahitaji yao.

Kutokana na mafanikio ya biashara hii, mimi na mpenzi wangu tumeoana na tunaendesha familia yetu vizuri bila ya tabu yoyote ile. Kusema kweli namshukuru sana Dr Bokko kwa usaidizi wake.

Dr Bokko anayejulikana kwa uwezo wao wa kuongeza na kupunguza nguvu ya kufanya tendo la ndoa, alikuwa amerejesha tena maelewano kwenye ndoa ya jamaa huyo na mambo kuwa mazuri.

Utaalam wao unavuka mipaka ya kijiografia, kutoa uponyaji hata kwa wale waliombali wanaohitaji msaada yao. Kabla ya kutoa dawa, hufanya mashauriano na uchunguzi wa kina kisha kutoa matibabu yao.

Vilevile Dr Bokko ana uzoefu wa miongo kadhaa ya kutibu kwa kutumia dawa kali za mitishamba kuponya magonjwa kama shinikizo la damu, kisukari, vidonda vya tumbo, kisonono, kaswende, TB, miguu kuvimba au kuwaka moto n.k.

Hushughulikia matatizo ya jumla kuanzia kushinda kesi za mahakama, kushinda bahati nasibu, ulinzi wa familia na mali na hutabiri kwa usahihi nyota.

Ukiona mambo hayaendi kama unavyotaka, basi usisite kuwasiliana na Dr Bokko kwa namba +255618536050, mtaalamu huyo amesaidia watu wengi ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka, amekuwa mgeni rasmi katika ibada ya kumsimika Msaidizi wa Askofu Mteule, Mchungaji Dkt. Johnson Lunanilo Gudaga, wa KKKT Dayosisi ya Kusini. Ibada hiyo imefanyika tarehe 13 Oktoba 2024, ikiwa ni tukio muhimu kwa kanisa na jamii nzima ya Kusini.

Rc Mtaka ametoa salamu za serikali na kumpongeza Mchungaji Gudaga kwa uteuzi huo. Alisema, "Ninakupongeza kwa kuaminiwa na kuchaguliwa kuwa Msaidizi wa Askofu. Uteuzi huu ni ishara ya imani kubwa iliyowekwa juu yako katika kulitumikia kanisa na jamii kwa ujumla." Ujumbe huu ulikuwa na uzito mkubwa kwa kanisa, ukiashiria matumaini na wajibu mpya kwa mteuliwa huyo.

Mbali na pongezi hizo, Mhe. Mtaka alitumia fursa hiyo kuhamasisha wananchi wa Njombe kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa. Aliwaambia wananchi, "Ni muhimu kila mwananchi ajitokeze kwa wingi kujiandikisha ili tushiriki kwa pamoja kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, maana ndiyo sauti yetu kama wananchi katika maendeleo yetu."

Mwisho wa hotuba yake, Mhe. Mtaka alisisitiza umuhimu wa kushirikiana katika maendeleo, akihimiza uongozi wa kanisa na serikali kuendelea kuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha wananchi kuhusu umuhimu wa kushiriki kwenye michakato ya kisiasa na kijamii.












 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia  Hassan ameipongeza wizara ya madini kwa usimamizi mzuri na  madhubuti wa sekta ya madini unaopelekea ukuaji wa haraka na kuwa kinara katika  kuchangia kwenye Pato la Taifa.

Hayo yameelezwa leo Oktoba 13, 2024 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan wakati akifunga maonesho ya Saba ya Teknolojia ya Madini mkoani Geita.

Aidha Mh Rais Samia ameeleza katika mikakati ya kuimarisha uchumi wa nchi na upatikanaji wa fedha za kigeni Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imetenga kiasi cha shilingi Trilioni moja kwa ajili ya ununuzi wa dhahabu  kutoka kwa wachimbaji.

Rais, Dkt. Samia amesema kwamba  sekta ya madini imekuwa na mchango mkubwa katika kuliingizia taifa fedha za kigeni ambapo kwa mwaka wa fedha 2022\/2023 ilichangia asilimia 56 ya fedha za kigeni.

Sambamba na hapo Rais , Dkt.Samia amesema kiasi cha shilingi 250 zimetengwa kama dhamana ya mikopo zitakazo wawezesha wanunuzi wa dhahabu kupata mtaji.

Rais Dkt. Samia amesema kuwa kwa mwaka wa 2023 mauzo ya madini yenye thamani ya zaidi ya shilingi trilioni mbili yaliuzwa katika masoko 44 na vituo mbalimbali vya uuzaji madini  vilivyopo sehemu mbalimbali nchini.

Akielezea kuhusu mwenendo wa biashara ya madini nchini kuanzia mwaka 2019 mpaka septemba 2024 , Dkt.Samia amesema kwa kipindi husika kiasi cha tani 20.8 za dhahabu zenye gharama ya shilingi trilioni 5.2 zimenunuliwa kutoka kwa wachimbaji na wafanyabiashara ya madini nchini.

Dkt.Samia ameeleza serikali inatambua mchango wa asilimia 40 kutoka kwa wachimbaji wadogo nchini, ambapo ametoa leseni 21 kwa vikundi vya Vijana na wanawake  vikiwemo vikundi vya GEWOMA , Ushirika Madirisha na TEWOMA vinavyojihusisha na uchimbaji mdogo.








 


Kamishna wa Uhifadhi TFS, Prof. Dos Santos Silayo, akionesha tuzo aliyokabidhiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Pindi Chana (kushoto), kwa kutambua juhudi kubwa za uhifadhi zinazofanywa na TFS na kuimarisha sekta ya utalii nchini. Tuzo hiyo ilikabidhiwa leo kwenye hafla ya kuhitimisha Onesho la Swahili International Tourism Expo (S!TE) mwaka 2024 jijini Dar es Salaam.

Onesho la Swahili International Tourism Expo (S!TE) mwaka 2024 limehitimishwa rasmi leo jijini Dar es Salaam, likiteka hisia za wengi kwa mafanikio makubwa ya kuingiza takribani wanunuzi 120 wa kimataifa wa bidhaa za utalii.

Katika hafla ya kufunga onesho hilo kwenye ukumbi wa Mlimani City, Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Dkt. Pindi Chana, alieleza kuwa mwitikio wa washiriki umeongezeka, akitaja filamu maarufu ya "The Royal Tour" aliyotengeneza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kama kichocheo muhimu.

"Utalii unachangia kwa kiasi kikubwa pato la taifa, kuanzia pale mtalii anaposhuka uwanja wa ndege, hadi anapohudumiwa na hoteli na kufanya shughuli mbalimbali," alisema Dkt. Chana.

Waziri alisisitiza kwamba ulinzi wa rasilimali za nchi, hususan misitu na mbuga za wanyama, ni muhimu kwa ustawi wa uchumi wa taifa. 

"Kila mmoja wetu anawajibika katika kuhifadhi na kutunza mazingira ili kuhakikisha maendeleo endelevu ya utalii," aliongeza.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii Tanzania, Balozi Dr. Ramadhan Dau, alionyesha matumaini makubwa kwa mafanikio yaliyopatikana mwaka huu, akisisitiza kuwa ni alama ya mafanikio ya maandalizi ya onesho lijalo, ambalo limefanyika kwa mara ya nane tangu kuanzishwa kwake mwaka 2014.

Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wa Misitu (TFS), Prof. Dos Santos Silayo, alisisitiza umuhimu wa utalii ikolojia, akisema, "Utalii wetu unategemea mazingira safi na yenye kuvutia, ambapo watalii wanapata fursa ya kutembea kwenye misitu, kupanda milima, na kushiriki katika michezo mbalimbali." 

Aliongeza kuwa, ikiwa fursa hizi zitatumika vizuri, zitaongeza muda wa kukaa kwa watalii nchini na hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa pato la taifa.

Prof. Silayo pia alihimiza Watanzania wote kushiriki katika uhifadhi wa maliasili, akitaja umuhimu wa misitu katika kutoa hewa safi na kulinda mazingira. 

"Ni jukumu letu sote kuhakikisha kuwa tunatunza mazingira yetu, si tu kwa faida yetu lakini pia kwa vizazi vijavyo," alisisitiza.









 


Na Benny Mwaipaja, Dar es Salaam

Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na Benki ya Dunia (World Bank Group), zimeitangaza Tanzania kuwa nchi ya pili, baada ya Madagascar, kunufaika na Mfumo wa Ushirikiano wa Kuimarisha Hali ya Hewa kwa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na athari mbaya za uharibifu wa mazingira.

Kupitia Mfumo huo, IMF na WBG watafanya kazi kwa karibu na washirika wengine wa maendeleo, kuratibu juhudi zao za kuunga mkono ajenda ya mageuzi ya sera ya Tanzania ili kukabiliana na vihatarishi na changamoto zinazohusiana na mabadiliko hayo ya tabianchi na kuimarisha ustahimilivu wa uchumi wa Tanzania.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam, Kiongozi wa Timu ya Wataalam kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa, Bw. Charalambos Tsangarides, alisema kuwa kupitia mpango huo, IMF itaunga mkono kuanzishwa kwa kanuni za uwekezaji wa umma zinazohimili mabadiliko ya tabianchi na utoaji taarifa, huku Benki ya Dunia itajikita katika kusaidia kutekeleza miradi katika sekta zitakazoimarisha uwezo wa Tanzania kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kama vile nishati, maji, hifadhi ya jamii na kilimo.

Taasisi hizo mbili pia zitasaidia uboreshaji na utekelezaji wa sera  ya Tanzania ya usimamizi wa hatari za maafa, ikiwa ni pamoja na kufadhili mfumo wa kukabiliana na hatari hizo na uimarishaji wa mtandao wa usalama wa kijamii ili kukabiliana na majanga ya hali ya hewa.

IMF na Benki ya Dunia pia zitasaidia sera za kuboresha usimamizi wa rasilimali za maji, kupanua upangaji na usimamizi wa matumizi bora ya ardhi ya vijiji, kusimamia vihatarishi vya hali ya hewa katika uchumi na fedha na kutoa msaada wa kiufundi na kifedha kwa kuishirikisha pia sekta binafsi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia, Bw. Nathan Belete, akizungumza kwa njia ya mtandao kutoka Washington D.C, nchini Marekani, alisema kuwa Tanzania itanufaika na msaada wa kiufundi na kifedha kutoka taasisi hizo mbili katika kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa miundombinu itakayokuza uzalishaji, kuhifadhi mazingira na kuwa na mchango mkubwa katika kuinua uchumi wa nchi.

Kwa upande wake, Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amezishukuru Taasisi hizo kubwa za Fedha Duniani (IMF na Benki ya Dunia) kwa kuiteua Tanzania kuwa nchi za mwanzo duniani, zitakazo nufaika na mpango huo kwa kuunga mkono juhudi za Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye ni kinara wa mapambano ya kukabiliana na athari mbaya za mabadiliko ya tabianchi.