NA EMMANUEL MBATILO, DODOMA

TAASISI ya HakiElimu Tanzania inaendelea na juhudi mahsusi za kushirikisha wadau wa elimu nchini ili kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa mtoto wa kike, hatua inayolenga kukabiliana na ongezeko la wasichana wanaokatisha masomo kutokana na vikwazo vya kijinsia.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dkt. Maulid Maulid (wa pili kulia) na Bi. Bertha Mwaihojo (wa kwanza kulia) wakionesha Mkataba wa makubaliano ya kufanya kazi pamoja mbele ya Vyombo vya habari, katika Ukumbi wa Mikutano, hoteli ya Stella Maris. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania (TLSB) na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo cha Ukutubi na Uhifadhi Nyaraka (SLADS) Dkt. Mboni Ruzegea, wa pili kushoto ni Mgeni Rasmi wa Mahafali ya 31 ya SLADS Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Shaibu Ndemanga wakishuhudia tukio hilo.

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI anayeshughulikia Elimu, Mhe. Reuben Kwagilwa, amewatoa hofu wazazi na walezi nchini kuwa Serikali imejipanga kikamilifu  kuwapokea wanafunzi wa shule za msingi na sekondari kuanzia Januari 2026, kwani imeandaa  miundombinu ya kutosha itakayowahudumia wanafunzi wote watakaopokelewa.

Mhe. Kwagilwa ametoa kauli hiyo mkoani Lindi wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, ambapo alitembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Shule ya Msingi Likong’o, iliyopo katika Manispaa ya Lindi.

“Shule hii inakwenda kuongeza na kutimiza idadi ya shule 567 zilizojengwa nchini. Ukiacha shule hii, tayari zipo shule 566 zilizojengwa nchi nzima, na kwa hapa mkoa wa Lindi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameleta Shilingi Bilioni 114 kwa ajili ya kuimarisha sekta ya Elimu,” amesema Mhe. Kwagilwa.

Ujenzi wa Shule ya Msingi Likong’o ni sehemu ya miradi ya kijamii inayotekelezwa kupitia sera ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) chini ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), kwa kushirikiana na kampuni za Equinor na Shell, ambazo ni wadau wa maendeleo katika sekta ya mafuta na gesi.

Mhe. Kwagilwa amesema mradi huo umelenga kuboresha miundombinu ya elimu kwa watoto wa shule za msingi kwa kutoa mazingira salama, ya kisasa na bora ya kujifunzia, ikizingatiwa kuwa awali eneo hilo lilikuwa likikabiliwa na changamoto ya miundombinu ya elimu.

Ujenzi huo unahusisha vyumba vya madarasa na miundombinu ya kusaidia utoaji wa elimu bora kwa wanafunzi, ambapo thamani ya mradi huo inakadiriwa kufikia Shilingi Bilioni 1.2 za Kitanzania na Serikali imesisitiza kuwa hatua hii ni sehemu ya jitihada za kuwekeza katika elimu kwa maendeleo endelevu ya taifa.


WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa Kampasi ya Lindi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika eneo la Ngongo mkoani Lindi na kusema kwamba huo ni uthibitisho wa dhamira ya Serikali ya kupanua fursa za elimu ya juu nchini.

“Uwekezaji huu ni utekelezaji wa vitendo wa nguzo ya pili ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika kujenga uwezo wa watu kifikra, kiubunifu, kufanya uchambuzi, kutatua changamoto, pamoja na kuwa na utaalamu na umahiri katika nyanja mbalimbali za maisha,” amesema.

Akizungumza na viongozi na mamia ya wananchi wa mkoa wa Lindi waliofika kushuhudia uzinduzi huo leo (Jumamosi, Desemba 20, 2025), Waziri Mkuu amewapongeza viongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kuamua kutekeleza maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kupanua huduma za elimu ya juu katika maeneo ya kimkakati kama vile Mkoa wa Lindi.

“Maono haya ni ya kwake mwenyewe Mheshimiwa Rais. Zilipotolewa fedha za mradi huu kwa vyuo vikuu kama vya Dar es Salaam na Mzumbe, alisema ujenzi uelekezwe katika kupeleka kampasi za vyuo vikuu kwenye mikoa yote ambayo haikuwa na vyuo vikuu.”

Amesema Mkoa wa Lindi, kama ilivyo kwa mikoa mingine ya Kusini mwa Tanzania una ardhi yenye rutuba, rasilimali watu na mazingira rafiki kwa kilimo cha kisasa na biashara ya mazao.

“Kampasi hii ya kilimo itasogeza huduma ya elimu karibu na wananchi wa Kanda ya Kusini na kuendeleza utafiti na ubunifu katika sekta ya kilimo ambayo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wa Taifa letu. Uwekezaji huu utachangia kwa kiasi kikubwa katika kuimarisha sekta ya kilimo kupitia maarifa, teknolojia na tafiti za kisasa zitakazojibu changamoto halisi za wakulima wetu,” amesisitiza.

Dkt. Mwigulu amesema ujenzi wa Kampasi ya Kilimo ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mkoani Lindi ni ushahidi mwingine wa dhamira ya dhati ya Serikali ya kuifanya elimu ya juu kuwa chombo cha mageuzi ya kiuchumi na kijamii. “Kupitia Kampasi hii, Serikali inalenga kuandaa wataalamu wabobezi wa kilimo, utafiti na biashara ya kilimo watakaosaidia kuongeza uzalishaji, thamani ya mazao, ajira kwa vijana na mapato ya wakulima.”

Sambamba na ujenzi wa chuo hicho, Waziri Mkuu amesema katika kipindi cha miaka mitano ijayo ya utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2025, Serikali itahakikisha inafanya ukarabati wa barabara katika maeneo ya Nane Nane (Ngongo), ujenzi wa barabara zenye urefu wa km. sita kwa kiwango cha lami katika Kampasi za Chuo Kikuu (Ngongo na Ruangwa); ujenzi wa barabara za lami za Kilambo (km 1.5); Mtange – Kinengene - Kibaoni na barabara ya Mahakama – Mitwero (km 1.2).

Mapema, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Rais mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete alimpongeza Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba kwa sababu yeye ni zao la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. “Shahada zako zote tatu umezipatia pale chuo kikuu. Tunajivunia kwani wewe ni miongoni mwa mabalozi wema wa chuo chetu,” alisema. 

Akielezea uwekaji wa jiwe la msingi la Kampasi ya Lindi, Dkt. Kikwete alisema anaamini iko siku kampasi ya Lindi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam nayo pia itakuwa chuo kikuu kamili.

Alisema chuo hicho kinatarajiwa kuanza kupokea wanafunzi wa kwanza ifikapo Oktoba, mwakani. “Mwaka ujao wa masomo utakaoanza Oktoba, 2026 Chuo Kikuu cha Dar es Salaam - Kampasi ya Lindi kitapokea wanafunzi wa kwanza; vivyo hivyo kwa kampasi za Bukoba na kule Zanzibar,” alisema.

Alitumia fursa hiyo kumshukuru Waziri Mkuu mstaafu, Kassim Majaliwa kwa kusaidia upatikanaji wa ardhi wilayani Ruangwa ambako Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimejenga tayari kituo cha utafiti wa kilimo.

Naye, Naibu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam anayesimamia Fedha, Utawala na Mipango, Prof. Bernadeta Killian alisema ujenzi wa chuo hicho unafuata masterplan ya miaka 20 (2025-2045) kutegemea na uwezo wa Serikali na uwepo wa bajeti. “Mradi wote utagharimu sh. bilioni 14.8 na kati ya hizo, sh. bilioni 13.7 ni za mkandarasi ambaye tayari amelipwa sh. bilioni 5.9. Shilingi bilioni moja ni za kumlipa mshauri mwelekezi.” 

Akitoa maelezo ya ujenzi huo mbele ya Waziri Mkuu, Prof. Killian ambaye pia ni msimamizi wa mradi wa kuendeleza elimu ya juu kwa mageuzi ya kiuchumi (HEET) alisema majengo mengi yanaendelea yakiwemo ya utawala, vyumba vya mikutano, madarasa sita yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 60 kila moja, karakana ya mafunzo na maabara yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 125 kwa wakati mmoja.

Alisema kampasi hiyo pia ina mabweni mawili yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 200 lakini kuna nafasi ya kuongeza ghorofa tatu kila moja na hivyo kuweza kuchukua wanafunzi 800.

 



Mbunge wa Jimbo la Mtumba Mh. Anthony Mavunde ametoa rai kwa jamii kuwajali na kuwakumbuka yatima na wajane katika utatuzi wa changamoto zao mbalimbali na kuwapa faraja.

Mh. Mavunde ameyasema hayo leo wakati wa hafla fupi iliyoandaliwa na Taasisi ya Joy of Giving ya kugawa mahitaji kwa wajane na yatima ikiwemo vyakula na mahitaji ya shule kwa watoto.

“Nawapongeza Joy of Giving Foundation kwa kuwajali na kuwakimbilia wahitaji mara zote.

Mmekuwa mfano mzuri kwenye jamii na hivyo mnatuma ujumbe kwa Jamii nzima juu ya kuwajali na kuwakumbuka wajane na yatima huku tukijua kwamba hii ni ibada kubwa.

Nitaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuwahudumia wajane na yatima na kwasasa tunatarajia kuwa na Tamasha kubwa la wahitaji la kila mwaka ili kutengeneza msingi wa utatuzi wa changamoto zao”Alisema Mavunde

Naye Mkurugenzi wa Taasisi ya Joy of Giving Bi. Jackline Nitwa Machoke amesema Taasisi yake imejipanga kufanya tukio la mara moja kila mwaka la kuwahusu wajane na yatima na kutoa rai kwa wadau kuiwezesha Taasisi hiyo ili kuweza kutimiza malengo yake hasa katika huduma za kila siku za kuwahudumia watu wenye ugonjwa mbalimbali na upatikanaji wa bima ya Afya kwa wananchi wanaoishi katika mazingira magumu.

Hafla hiyo imehusisha watoto yatima na wajane takribani 200 ambao wote wamepatiwa mahitaji mbalimbali kutoka kwa Mbunge Mavunde na Taasisi ya Joy of Giving.







 


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Mwigulu Nchemba amepongeza Wizara ya Nishati kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kwa ujenzi wa shule bora ya Awali na Msingi katika Kijiji cha Likong'o mkoani Lindi inayojengwa kupitia mradi wa uzalishaji na usindikaji wa Gesi Asilia kuwa kimiminika ( LNG). .

Waziri Mkuu ametoa pongezi hizo tarehe 20 Desemba 2025 wakati akikagua ujenzi wa shule hiyo itakayokuwa na uwezo wa kuhudumia wanafunzi 400 katika Kijiji cha Likong'o, Kata ya Mbanja, Halmashauri ya Manispaa ya Lindi.


" Nawapongeza TPDC kwa hatua hii ya kutekeleza shughuli za uwajibikaji kwa jamii (CSR) kupitia mradi huu wa LNG, shule hii ni bora ya kisasa na imezingatia mahitaji mbalimbali ikiwemo kuwa na miundombinu inayokidhi watu wenye mahitaji maalum na watoto wa kike." Amesema Mhe. Nchemba

Katika hatua nyingine Dkt. Nchemba ametoa msisitizo kwa Wizara ya Nishati kuhakikisha kuwa shule hiyo inafungwa miundombinu ya Nishati Safi ya Kupikia kuunga mkono utekelezaji wa Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia ambayo kinara wake ni Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kutokana na uwepo wa shule hiyo, Waziri Mkuu amewaasa wananchi kuchangamkia fursa kwa kuwasomesha watoto wao na hivyo kuunga mkono jitihada anazofanya Rais Rais Samia za ujenzi shule katika maeneo mbalimbali nchini ili kuwawezesha watoto wote kupata elimu.


Kwa upande wake Mhe. Salome Makamba ambaye ni Naibu Waziri wa Nishati, amesema mradi wa ujenzi wa Shule ya Msingi Likong'o unatekelezwa kama sehemu ya kurudisha fadhila kwa wananchi waliotoa ardhi kwa ajili ya utekelezaji mradi wa LNG.

Ameeleza kuwa ujenzi wa Shule hiyo ambao umefikia asilimia 70 unaonesha jinsi kaulimbiu ya kazi na utu inavyotekelezwa kwa vitendo na Serikali ya Awamu ya Sita.

Katika hatua nyingine, Mhe. Salome ameeleza kuwa agizo la Waziri Mkuu la shule hiyo kuwekewa miundombinu ya nishati safi ya kupikia litatekelezwa na kuongeza kuwa ndani ya siku 100 za uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan taasisi 52 zitasambaziwa miundombinu ya nishati safi ya kupikia.

Naye, Mbunge wa Lindi, Mohamed Utaly amemshukuru Rais Samia kwa uwekezaji huo wa mradi wa LNG ambao amesema unaleta chachu ya elimu mkoani Lindi.

Amepongeza pia TPDC kwa kuhakikisha kuwa miradi ya uwajibikaji kwa jamii imeanza kutekelezwa mapema kupitia mradi huo wa LNG.

Awali, Mhandisi Msimamizi wa mradi wa shule ya Awali na Msingi Likong'o, Upendo Mahavanu kutoka TPDC alisema mradi huo unagharimu Sh .bilioni 1.27 ambapo shule itakuwa na Madarasa 9; saba yakiwa ni ya shule msingi na mawili ni ya awali. Pia kutakuwa na ofisi na nyumba za walimu.

Utekelezaji wa mradi wa LNG unatarajiwa kuwa na manufaa mbalimbali nchini ikiwemo mapato ya Serikali yatakayotokana na uuzaji wa LNG kwenye soko la kimataifa, fursa za ajira, fursa kwa wazawa kuuza bidhaa, uhaulishaji wa teknolojia mbalimbali ili kuwajengea uwezo wataalam wa ndani n.k

 -Washukuru kufikishiwa majiko banifu kwa bei ya ruzuku


Wananchi wa Kijiji cha Mtakuja Kata ya Kapalala katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi wameipongeza Serikali kwa kuweka ruzuku kwenye majiko banifu hatua ambayo wamesema inawezesha mwananchi wa kipato chochote kutumia Nishati Safi ya Kupikia

Wametoa pongezi hizo kwa nyakati tofauti Desemba 19, 2025 wakati wa zoezi la usambazaji wa majiko banifu yanayouzwa kwa bei ya ruzuku kijijini hapo unaotekelezwa na Kampuni ya Tango Energy Limited chini ya uratibu na usimamizi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

“Tunaipongeza na kuishukuru Serikali kwa kuweka ruzuku katika bidhaa za nishati safi ya kupikia ikiwemo haya majiko banifu; mpango huu utamfikia kila mwananchi hata yule wa kipato kidogo; Serikali imeamua kutusapoti nasi tumejitoa kama watanzania kuunga jitihada hizi za Serikali,” alisema Felix Milwano Mkazi wa Kijiji cha Kapalala

Kwa upande wake Nelia Fungameza alisema jiko banifu litampunguzia gharama za maisha kwani hapo awali alikuwa akitumia gunia moja la mkaa ndani ya mwezi mmoja lakini kutokana na ufanisi wa majiko hayo kama alivyoelezwa na wataalam ataweza kutumia gunia moja kwa zaidi ya miezi miwili.

Mbali na kupunguza gharama, Fungameza aliishukuru Serikali kwa dhamira yake ya kuboresha afya za wananchi wake kwani kwa kutumia majiko banifu alisema kwa namna alivyoshuhudia likifanya kazi halitoi moshi kama majiko mengine waliokuwa wakitumia hapo kabla.

“Haya majiko banifu mimi sifa zake nilielezwa na rafiki yangu yeye yupo Dar es Salaam, alinieleza ubora na ufanisi wake namna ambavyo yanafanya kazi na namna ambavyo yanaokoa gharama, leo nafarijika yamefika kwetu tena kwa bei ya ruzuku kwa hili naipongeza Serikali,” alisema Maiko Maseki.

Akizungumza wakati wa zoezi la uuzaji wa majiko hayo kwa bei ya ruzuku, Mtaalam wa Nishati na Jinsia kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Dkt. Joseph Sambali alipongeza mwitikio wa wananchi na aliwasisitiza kuwa mabalozi kwa wananchi wengine ambao hawakupata fursa ya kujipatia majiko hayo.

Alisema kuwa mwitikio huo mkubwa wa wananchi wa kujipatia majiko banifu kwa bei ya ruzuku kunadhihirisha kuwa uelewa kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia katika kulinda afya na kuhifadhi mazingira umeongezeka miongoni mwa wananchi.

“Zoezi hili la uuzaji wa majiko Mkoani Katavi kwa bei ya ruzuku ya shilingi 7,500 linaendelea, nawasihi wananchi waendelee kujitokeza kwa wingi waendelee kuchangamkia fursa hii kwani bei ya soko kwa jiko moja yaani bila ruzuku jiko hili huuzwa kwa shilingi 59,000,” alifafanua Dkt. Sambali.

Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Tango Energy Ltd, Musa Msofe alitoa wito kwa wananchi wanaofika kujipatia majiko banifu kwa bei ya ruzuku kuhakikisha wanakuwa na vitambulisho vya Taifa (NIDA) ili kuepuka usumbufu na kushindwa kupata huduma.

“Mwananchi anayefika hapa kujipatia jiko ahakikishe anakuja na kadi yake ya NIDA na huu ndio utaratibu nje ya hapo hatoweza kuhudumiwa; tumeanza rasmi uuzaji wa majiko hapa Nsimbo na tutakuwa na tutakuwa na vituo vitano vya uuzaji na tutatangaza ili kila mwananchi aelewe ratiba yetu,” alisema Msofe.

Alisema wamejipanga vyema kuhakikisha zoezi la uuzaji wa majiko hayo linakwenda kama ilivyoelekezwa na Serikali na kwamba kabla ya kuuza wanatoa elimu kuonyesha namna ambavyo majiko hayo yanafanya kazi sambamba na kumuonyesha mwananchi faida za kutumia majiko banifu.








 


Na Magesa Magesa,Arusha

WATANZANIA wametakiwa kujenga utamaduni wa kuwathamini na kuwajali madaktari na wauguzi hapa nchini kwani wao ndio wamekuwa wakitoa upanyaji kwa wanadamu kwa kupitia kwa Mungu.

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania(KKKT),Dayosisi ya Kaskazini Kati(DKAK)Dk.Godson Abel Mollel ameyasema hayoleo alipokuwa akizungumza na watoa huduma hao wa afya wakati wa kukabidhiwa zawadi kwa kutambua mchango wao.

Zawadi hizo zilitolewa na Mfanyabiashara Nathan Kimaro,alipokuwa akiwapongeza wahudumu hao wa afya wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Arusha,Mount Meru, ikiwa ni kumbukumbu ya kuzaliwa kwake miaka 27 iliyopita katika hospitali hiyo.

Askofu Mollel amesema kwamba watoa huduma ya afya ni watu muhimu sana katika jamii kwani wao ndio wamekuwa wakiwahudumia wagonjwa wa hali mbalimbali katika mazingira mbalimbali bila kujali changamoto wanazokutana nazo.

“Wakati umefika watanzania tuamke tuhakikishe kuwa tunawajali watoa huduma za afya kwani wao wamekuwa wakitibu na watu kupata kuponywa kupitia kwao kwa uwezo wa Mungu kwani hata Yesu katika wanafunzi wake, Luka alikuwa ni tabibu na yesu alikuwa mponyaji”alisema Askofu huyo.

Kwa upande wake Mfanyabiashara Nathan Mollel aliwashukuru watoa huduma hao wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Arusha kwa kutimiza kikamilifu majukumu yao ya kuwahudumia wagonjwa na kuwataka kuendelea na moyo huo huo.

Alisema kuwa udaktari na uuguzi ni kazi ya wito hivyo hawana budi kufanya kazi zao kwa kuzingatia maadili na weledi kama wanavyofanya lakini wahakikishe kuwa wanamtanguliza Mungu kwani yeye ndiye muweza wa kila jambo.

Kahalika mfanyabiashara hyo aliutaka uongozi wa hospitali hiyo kumpatia eneo lolote lile ambalo atajenga bustani kubwa nay a kisasa itakayokuwa na maua na miti ya aina mbalimbali ambayo itakuwa ikisaidia kuwapa matumani na faraja wagonjwa pindi wanapopumzika katika bustani hiyo.

Katika kusherekea siku yake ya kuzaliwa Nathani Kimaro aliwapatia watumishi wa hospitali hiyovyakula na vifaa mbalimbali ikiwemo,mchele,mafuta,sabuni,sukari,maziwa na kadhalika kama shukrani na kusema kuwa huo ni mwanzo.

Kwa upande wake Kaimu mganga mfawidhi wa hospitali hiyo,Dkt.Abel Ndago alimshukuru mfanyabiashara hyo wa zawadi hizo kwao ikiwemo ahadi yake ya kujenga bustani ya kisasa katika hospitali hiyo

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe.Mshamu Munde,akimkabidhi tuzo Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha FCC, Bi. Roberta Feruzi kwa niaba ya Waziri wa Fedha tuzo hiyo imetolewa kwa Tume ya  Ushindani (FCC)  kutambua mchango wake katika maendeleo ya Sekta ya Manunuzi na Ugavi nchini.Hafla ya utoaji wa tuzo hiyo ilifanyika katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi,lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB)   jijini Arusha.

....

TUME ya Ushindani (FCC) imetunukiwa tuzo maalum ya kutambua mchango wake katika maendeleo ya Sekta ya Manunuzi na Ugavi nchini.

Tuzo hiyo imekabidhiwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mshamu Munde, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, na kupokelewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha FCC, Bi. Roberta Feruzi.

Hafla ya utoaji wa tuzo hiyo ilifanyika katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi, lililofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), jijini Arusha lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB).

FCC imeshiriki kongamano hilo kama mdau muhimu wa sekta ya manunuzi na ugavi, ambapo iliwasilisha mada kuhusu umuhimu wa ushindani wa haki katika masuala ya manunuzi na ugavi, hususan katika kulinda mnyororo wa thamani.

Kupitia kongamano hilo, Tume pia ilitoa elimu kwa wadau mbalimbali kuhusu majukumu na kazi zake, ikisisitiza nafasi yake katika kuhakikisha mazingira ya ushindani yanayochochea uwazi, ufanisi na maendeleo endelevu ya sekta ya manunuzi na ugavi nchini.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe.Mshamu Munde,akimkabidhi tuzo Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha FCC, Bi. Roberta Feruzi kwa niaba ya Waziri wa Fedha tuzo hiyo imetolewa kwa Tume ya  Ushindani (FCC)  kutambua mchango wake katika maendeleo ya Sekta ya Manunuzi na Ugavi nchini.Hafla ya utoaji wa tuzo hiyo ilifanyika katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi,lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB)  jijini Arusha.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe.Mshamu Munde,akimkabidhi tuzo Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha FCC, Bi. Roberta Feruzi kwa niaba ya Waziri wa Fedha tuzo hiyo imetolewa kwa Tume ya  Ushindani (FCC)  kutambua mchango wake katika maendeleo ya Sekta ya Manunuzi na Ugavi nchini.Hafla ya utoaji wa tuzo hiyo ilifanyika katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi,lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB)   jijini Arusha.

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC) Bi. Khadija Ngasongwa,akizungumza katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi, lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB)   jijini Arusha.

Meneja Huduma za Sheria FCC Bw. Josephat Mkizungo, akitoa mada katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi,lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB)   jijini Arusha.

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC) Bi. Khadija Ngasongwa,akifuatilia mada mbalimbali wakati wa Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi,lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB)   jijini Arusha.

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC) Bi. Khadija Ngasongwa (kushoto),akifuatilia mada mbalimbali wakati wa Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi, lililofanyika  jijini Arusha .Katikati ni Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Bw. Godfrey Nyaisa na Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi Bw. John Paul Wanga.lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) .

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe.Mshamu Munde,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukabidhi tuzo kwa  Tume ya  Ushindani (FCC) ya kutambua mchango wake katika maendeleo ya Sekta ya Manunuzi na Ugavi nchini.Hafla  ilifanyika katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi, lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB)   jijini Arusha.

 

Na Mwandishi Wetu, Handeni TC

Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, amesema wilaya hiyo imejipanga kikamilifu kuhakikisha wananchi wanahamasika kujiunga na Bima ya Afya kwa Wote ili kuwa na uhakika wa kupata huduma bora za matibabu.

Akizungumza mjini Handeni, Mhe. Nyamwese amesema kuwa katika wilaya hiyo yenye Halmashauri ya Mji Handeni na Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, Serikali imewekeza kwa kiasi kikubwa katika ujenzi wa miundombinu ya kisasa ya kutolea huduma za afya.

Amesema kuwa katika kuhakikisha wananchi wananufaika na bima ya afya kwa wote, wilaya imejiandaa kikamilifu kwa kuweka mazingira wezeshi ya utoaji huduma ikiwemo upatikanaji wa vituo vya afya, vifaa tiba, dawa pamoja na rasilimali watu.

“Wilaya yetu tumejipanga na tuna mikakati madhubuti ya kuhakikisha tunamsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, kutimiza ahadi yake kwa Watanzania ya kuhakikisha wanapata huduma bora za afya kupitia bima ya afya kwa wote,” amesema Mhe. Nyamwese.

Amebainisha kuwa ndani ya wilaya ya Handeni kuna jumla ya vituo 84 vya kutolea huduma za afya ambavyo vimepatiwa vifaa tiba kulingana na ngazi ya utoaji huduma.

Aidha amesema huduma za kibingwa zinatolewa katika hospitali za wilaya kwa kushirikiana na wataalamu kutoka hospitali za rufaa za kikanda, hatua inayolenga kuhakikisha wananchi wanapata huduma karibu na maeneo yao.

Kuhusu upatikanaji wa dawa, Mkuu wa Wilaya amesema kuwa kwa sasa hali ni nzuri kwani zaidi ya asilimia 90 ya dawa zinapatikana katika hospitali zote za wilaya.

Ameongeza kuwa wilaya inatarajia kupokea wataalamu zaidi wa afya ili kuimarisha utoaji wa huduma, kutokana na Serikali tayari kuwekeza katika miundombinu na vitendea kazi.

“Nitoe wito kwa wananchi kutumia fursa ya bima ya afya kwa wote. Tusiiache itupite. Tutatangaziwa utaratibu wa kujiunga nayo na ni muhimu sisi wananchi kuwa mstari wa mbele kunufaika na fursa hii, kwani ina faida kubwa katika kupanua wigo wa upatikanaji wa huduma za afya,” amesisitiza Mhe. Nyamwese.