Habari za kushangaza zimeibuka kuhusu mwanamke mmoja kutoka Arusha aliyeacha madaktari wakiwa midomo wazi baada ya kupona ugonjwa ambao awali waliamini hauna tiba. Tukio hilo limezua mjadala mkubwa mitandaoni huku wengi wakijiuliza ni nini hasa kilichomfanya arudie afya yake kwa kasi ya ajabu kiasi hicho.

Kwa miaka mitatu, nilipitia mateso yasiyoelezeka. Nilikuwa nikisumbuliwa na ugonjwa wa tumbo uliosababisha maumivu makali kila siku. Nilishindwa kula vizuri, kulala kwa amani, na hata kutabasamu. Nilihisi kama maisha yangu yalikuwa yanafika mwisho. Nilihangaika kutoka hospitali moja hadi nyingine, kila daktari akinipa matumaini mapya ambayo yangepotea wiki chache baadaye. Hatimaye, nilisikia maneno yaliyokata tamaa kabisa: “Hali yako haiwezi kutibika.”

Nilitoka hospitalini nikiwa nalia. Nilijiona kama mzigo kwa familia yangu. Nilijifungia chumbani, nikiamini huu ndio ulikuwa mwisho wangu. Rafiki zangu walijitahidi kunitia moyo, lakini kila siku nilihisi mwili wangu ukizidi kudhoofika. Nilianza hata kuandaa mawazo ya kuandika ujumbe wa mwisho kwa wapendwa wangu. Lakini Mungu alikuwa bado hajamaliza na mimi.

Siku moja, dada yangu alinitembelea akiwa na tabasamu la matumaini. Aliniambia amesikia habari za mganga mwenye dawa za mitishamba ambaye amesaidia watu wengi waliokuwa wamekata tamaa kama mimi. Nilimwangalia kwa macho ya mashaka, nikijiuliza kama kweli dawa za miti zinaweza kufanya kile madaktari walishindwa. Baada ya kusitasita kwa siku kadhaa, nilikubali kujaribu. Soma zaidi hapa 

 

NA Mwandishi wetu

MAMLAKA ya Masoko ya Mitaji na dhamana Tanzania (CMSA) imeeleza kuwa mfuko wa pamoja wa uwekezaji Vertex International Securities Exchange Traded Fund (Vertex ETF)” ni wa kuigwa.

Afisa Mtendaji Mkuu wa CMSA, Nicodemus Mkama, ameyasema hayo leo wakati wa tukio la kihistoria katika Soko la Hisa La Dar es Salaam (DSE) baada ya kuorodheshwa kwa mfuko huo kwenye soko hilo.

Amesema mafanikio hayo makubwa ni kutokana na mamlaka ya masoko (CMSA) kushusha kiwango cha ushiriki kutoka sh 1,000,000 hadi sh 20,000 ambapo imewezesha wawekezaji wengi mmoja mmoja kuweza kushiriki.

"Siku muhimu ya kihistoria katika soko la mitaji, mfuko wa kwanza kuuza hisa ya vipande kuorodheshwa katika soko la hisa jambo jema ambalo linawapa nafasi kubwa wawekezaji kuwekeza, na pia tunazitaka kampuni nyingine kuiga mfano wa Vertex kuja na bidhaa bunifu kama hizi,"amesema Mkama.

"Ni furaha kubwa kujumuika nanyi leo hii kushuhudia tukio hili la kihistoria ambalo lina mchango mkubwa katika maendeleo na ustawi wa masoko ya mitaji na uchumi kwa ujumla hapa nchini,"

Aidha Mkama amesema kwa namna watu walivyoudhuria ni uthibitisho kwamba sekta ya masoko ya mitaji nchini ina wadau wengi wanaounga mkono utekelezaji wa mikakati inayosimamiwa na (CMSA) ya kuanzisha bidhaa mpya na bunifu zinazotoa wigo mpana kwa wawekezaji wa ndani na wa kimataifa kushiriki katika uwekezaji kwenye masoko ya mitaji hapa nchini.

"Mfuko wa Vertex ETF una tofauti na mifuko mingine ya uwekezaji wa pamoja iliyoidhinishwa na CMSA, kwani Mfuko huo unaorodheshwa kwenye soko la hisa; na kutoa fursa kwa wawekezaji kuuza na kununua vipande vya mfuko ambao unawekeza kwenye kampuni zilizoorodheshwa kwenye soko la hisa.

Mkama amesema "mfuko huu umebuniwa kimkakati kwa lengo mahsusi la kuwekeza kwenye kampuni zenye utendaji mzuri zaidi, na hivyo kuongeza ukwasi katika soko la hisa na kupanua ushiriki wa wawekezaji katika masoko ya mitaji.


Amesema Mfuko wa Vertex ETF utawekeza kwenye hisa za kampuni zilizoorodheshwa Soko la Hisa la Dar es Salaam, ambazo zina utendaji mzuri zaidi.

"Uwekezaji utaanza kwenye hisa za Benki ya CRDB, Benki ya NMB, Kampuni ya Uwekezaji ya NICO - National Investment Company Limited (NICO), Dar es Salaam Stock Exchange PLC (DSE) na Kampuni ya AFRIPRISE. Lengo la uwekezaji wa aina hii ni kuufanya mfuko huu kuwa na ukwasi wa kutosha kukidhi mahitaji ya fedha kwa wawekezaji pindi yanapotokea".

Amesema (CMSA) ina jukumu la kuendeleza na kusimamia masoko ya mitaji hapa nchini, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kwamba shughuli katika masoko ya mitaji zinafanyika kwa kufuata sheria, taratibu na miongozo ili kuleta uwazi na haki kwa washiriki wote.

"Kama tulivyoshuhudia mauzo ya vipande vya mfuko wa Vertex ETF yamepata mafanikio ya asilimia 136, ambapo kiasi cha sh billioni 6.8 kimepatikana, ikilinganishwa na lengo la sh.bilioni 5.

Aidha, asilimia 82.2 ya mauzo ya vipande imetoka kwa wawekezaji mmoja mmoja na asilimia 17.8 imetoka kwa Kampuni na taasisi.

Naye Mtendaji Mkuu wa Vertex International Securities, Mateja Mgeta, amesema wakati wanaanza kuuza vipande hivyo lengo ilikuwa kupata bilioni tano kwani kipande kimoja cha mfuko kilikuwa kinauzwa sh. 200, hadi zoezi la mauzo ya awali linakamilika waliweza kupata bilioni 6.8 Sawa na asilimia 136 na kuvuka lengo

Mgeta amesema mfuko wa ETF umeweza kupata idadi ya wawekezaji zaidi ya 6,300 na katika hao kuna wawekezaji wapya hali inayoenda sambambamba na Serikali katika masuala ya uchumi jumuishi.

"Vertex inapenda kutoa ahadi kwa Watanzania na wawekezaji wote kwa ujumla kwamba itasimamia huu mfuko kwa weledi ili kuhakikisha wawekezaji wanafaidika na matunda ya uwekezaji wao na kuendelea kuleta bidhaa bunifu sokoni zitakazokidhi mahitaji ya masoko ya mitaji na dhamana nchini.

Mgeta amesema ETF imevuka lengo na kuanzia sasa itapatikana katika soko la hisa.

Mecklaud Edson, Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Soko la Hisa la Dar es Salaam, akimwakilisha Afisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam, Peter Nalitolela amesema zaidi ya miaka 20 toka kuanzishwa kwa soka la hisa hawakuwahi kuwa na bidhaa kama hii ya Vertex.

"Tunawasihi Watanzania waje soko la hisla Dar es Salaam wataipata bidhaa hii nzuri kabisa ambayo imeorodheshwa katika soko la hisa,".






 

 



‎Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), imekamilisha ujenzi wa barabara ya Dodoma - Iringa eneo la Fufu kwa kunyanyua tuta la barabara lenye urefu wa kilomita 4 na kujenga makalvati makubwa manne uliogharimu kiasi cha Shilingi Bilioni 8.7.

‎Barabara hiyo imefunguliwa rasmi kuanza kutumika leo tarehe 16 Oktoba 2025 na Meneja wa TANROADS wa Mkoa wa Dodoma, Mhandisi Zuhura Amani ambapo ameeleza kuwa ujenzi wa mradi huo wa dharura umezingatia viwango vya ubora ili kuondoa changamoto iliyokuwepo hapo awali ya kujaa maji na kusababisha adha kwa wasafiri na wasafirishaji.

‎“Tumekamilisha ujenzi wa barabara ya kipande cha fufu kilichokuwa kinajaa sana maji, na makalvati yalikuwa madogo ambayo yalikuwa yanashindwa kupitisha maji na kusababisha adha kwa watumiaji wa barabara ambao walikuwa wanasubiri Kwa saa kadhaa ili waweze kupita”, ameeleza Mhandisi Zuhura.

‎Mhandisi Zuhura ameeleza kuwa barabara hiyo imejengwa na Mkandarasi Mzawa kampuni ya GNSM Contractors Limited Kwa mkataba wa mwaka mmoja na mpaka sasa imekamilika kwa asilimia 97 na kazi zilizobakia ni uwekaji wa alama za barabarani pamoja na kingo za barabara.

‎Aidha, Mhandisi Zuhura ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuona umuhimu wa kutoa fedha kwa ajili ya miradi ya dharura ambapo kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2023/24 kiasi cha Shilingi Bilioni 35.6 zilitengwa.

‎Kwa upande wa wananchi wa kijiji cha Fufu wameipongeza Serikali Kwa kukamilisha ujenzi wa mradi huo ambao utachochea biashara na pia wameomba kuwekewa kivuko cha kuvusha mifugo pamoja na kujenga mitaro ili kuruhusu maji yaweze kupita kwa urahisi, hadi kwenye Makalvati mapya yakiyojengwa na kutosababisha uharibu tena wa maji katika kijiji cha Geza Ulole.

‎Naye, Dereva wa magari makubwa anayetumia Barabara hiyo Bw. Juli Daudi ameishukuru Serikali kwa ukarabati wa barabara hiyo na kuondokana na adha ya kupita kwa muda mrefu katika barabara ya changarawe ya mchepuo ambapo walikuwa wakitumia dakika 35 hadi 40 na sasa hivi watatumia dakika 5 hadi 10.







  \

Kwa muda mrefu nilikuwa nimepoteza amani ndani ya ndoa yangu. Mume wangu alianza kubadilika kimapenzi, akawa anakaa kimya, akirudi nyumbani akiwa amechoka kila mara. Nilijua tatizo halikuwa kazi wala msongo wa mawazo, bali mimi mwenyewe. 

Mwili wangu hakuwa sawa na tayari, hivyo kila jaribio la kuungana lilikuwa mateso zaidi ya raha, na hilo lilianza kuniumiza zaidi kiakili kuliko kimwili.

Nilianza kujihisi kama nimezeeka kabla ya wakati wangu. Marafiki wangu walikuwa wakijisifia jinsi wanavyofurahia ndoa zao, lakini mimi nilikuwa na siri nzito moyoni.

Mume wangu alianza kulala sebuleni, akitoa visingizio vya kazi nyingi. Nilijua mapenzi yalikuwa yanatoweka polepole. Nililia mara nyingi usiku, nikijiuliza ni wapi nilikosea. Nilihisi kama kila kitu kilikuwa kimeharibika kabisa. Soma zaidi hapa 

Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Samwel M. Maneno, amesema serikali imejipanga kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi zake za kisheria ili kuongeza ufanisi wa utendaji na kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa.

  


Jina langu ni Sharon kutoka Nakuru. Kwa muda mrefu nilikuwa natamani sana kuolewa, lakini kila uhusiano niliouanzisha haukudumu. Wanaume walianza kwa upendo mwingi, kisha ghafla wananiacha bila sababu ya kueleweka. Nilijaribu kuomba ushauri kwa marafiki na hata kwa wachungaji, lakini hali iliendelea kuwa ile ile. Kila nilipoona rafiki yangu akiolewa, nilijikuta nalia usiku kucha nikijiuliza ni kwa nini bahati haikunichekea mimi.

Kuna wakati nilifikiria labda tatizo ni mimi, nikabadilisha kila kitu kuhusu maisha yangu. Nilijaribu mavazi tofauti, kujipamba zaidi, hata kujiunga na vikundi vya kina dada ili nijue “mambo ya ndoa.” Lakini bado wanaume walinishirikisha hadi pale mambo yalipokuwa makubwa, kisha wakapotea. Wengine waliniahidi pete, lakini waligeuka dakika za mwisho. Nilihisi nimechoka na nikaamua sitapenda tena, maana moyo wangu ulikuwa umejaa maumivu na mashaka.

Kama haitoshi, watu waliokuwa karibu nami walianza kunitania. Wengine walisema nimerogwa, wengine wakasema labda nililaaniwa tangu utotoni. Hata wazazi wangu walionekana kukata tamaa. Nilihisi dunia imenigeuka. Nilikuwa nikiomba kila siku Mungu anipe tu mtu wa kunipenda kwa dhati, lakini majibu hayakuja. Nilijaribu kila njia, hadi nikaanza kukosa imani na mapenzi. Soma zaidi hapa 

 

Serikali kupitia Wizara ya Nishati imeeleza kuridhishwa kwake na kasi ya utekelezaji wa mradi mkubwa wa kitaifa wa kuzalisha umeme jua (150MW)  katika Wilaya ya Kishapu, mkoani Shinyanga ambao hadi sasa umefikia asilimia 80.4 ya ujenzi.

Baada ya kukagua maendeleo ya mradi huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba, amesema Serikali inaridhishwa na hatua zilizofikiwa na mkandarasi, akibainisha kuwa mradi huo ni sehemu ya utekelezaji wa malengo ya kitaifa na kimataifa ya upatikanaji wa nishati endelevu.

Mhandisi Mramba ameeleza kuwa mradi huo wa megawati 150  unatekelezwa kwa awamu mbili kwa gharama ya Shilingi bilioni 323.

 Amesema kuwa awamu ya kwanza ya mradi huo itakamilika desemba 2025 kwa kuanza kuzalisha megawati 50 huku Kampuni ya Sinohydro kutoka China ikiwa ndiyo mkandarasi mkuu wa mradi

“ Mradi huu ni sehemu ya jitihada za Serikali chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye anaendelea kuhakikisha kwamba Watanzania wote wanapata huduma ya nishati safi, salama na nafuu." Amesisitiza Mhandisi Mramba

Ameongeza kuwa, kukamilika kwa mradi wa umeme jua wa Kishapu kutazidi kutengemaza  upatikanaji wa umeme mijini na vijijini na kupunguza utegemezi wa vyanzo vya nishati visivyo rafiki kwa mazingira.

Kwa upande wake, Mhandisi Msimamizi wa Mradi,  Emmanuel Anderson amesema kasi ya ujenzi ni nzuri na wanatarajia mradi utakamilika katika muda uliopangwa.

Naye Meneja wa Kampuni ya Sinohydro, Eng. Daniel Xu, amesema dhamira ya kampuni yake ni kukamilisha mradi kwa viwango vya juu  ndani ya muda uliowekwa.

“Tumeongeza nguvu kazi na vifaa kuhakikisha tunamaliza kazi kwa wakati. Tunathamini ushirikiano mzuri kutoka serikalini na wananchi wa Kishapu, tunaahidi kukamilisha mradi huu kwa ubora unaostahili." Amesema Eng. Xu

Kukamilika kwa mradi wa umeme jua Kishapu kunatarajiwa kuongeza uwezo wa nchi kuzalisha umeme wa nishati jadidifu, kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa taasisi, viwanda na wananchi, pamoja na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika Mkoa wa Shinyanga na taifa kwa ujumla.

 


Kuanzishwa kwa Kampasi ya Njombe ya Chuo Kikuu cha Dodoma kupitia Mradi wa HEET kumeanza kutaleta mabadiliko makubwa katika sekta ya elimu, ajira na uchumi wa mkoa wa Njombe. Mradi huu unalenga kuongeza fursa za elimu ya juu kwa vijana wa Kusini na kuchochea maendeleo ya miundombinu ya kisasa.

Hayo yameelezwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, alipokutana na viongozi wa Mkoa wa Njombe akiwemo Mkuu wa Mkoa, Katibu Tawala na Kamati ya Ulinzi na Usalama. Alisema Njombe imepata fursa ya kipekee kwa kuwa na matawi ya vyuo vikuu zaidi ya kimoja.

Prof. Nombo alieleza kuwa uwepo wa kampasi hiyo utachochea shughuli za kiuchumi katika maeneo jirani. Alisisitiza umuhimu wa kujenga nyumba za makazi, hosteli za wanafunzi, na vituo vya huduma kama maduka na migahawa  ili kuandaa mazingira rafiki kwa wanafunzi na watumishi wa kampasi hiyo.

Aliongeza kuwa ongezeko la wanafunzi litahitaji huduma bora za afya, usafi wa mazingira, Miundombinu ya  TEHAMA. Alitoa wito kwa taasisi husika kuhakikisha huduma hizo zinapatikana kwa wakati katika eneo la Mradi kabla ya kuanza Kwa udahili wa Wanafunzi hasa kwa kuzingatia mfumo wa “blended learning” unaotegemea miundombinu ya intaneti ya uhakika.

Prof. Nombo aliipongeza Njombe kwa ushirikiano wake katika utekelezaji wa miradi ya elimu. Aliahidi kuwa Wizara itaendelea kushirikiana na mkoa huo kuhakikisha mradi wa Kampasi ya Njombe unakamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.




Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba, ametoa wito kwa watendaji wa Tume ya Madini nchini kuhamasisha ujenzi wa viwanda vya uongezaji thamani ya madini ili kuongeza ajira, kukuza fursa za kiuchumi na kuimarisha mchango wa Sekta ya Madini katika Pato la Taifa.


Akizungumza leo, Oktoba 15, 2025, jijini Tanga katika kikao cha menejimenti ya Tume ya Madini kilichoshirikisha Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Dkt. Janet Lekashingo, Makamishna wa Tume ya Madini Mhandisi Theonestina Mwasha na Dkt. Theresia Numbi, Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Ramadhani Lwamo, Wakurugenzi, Mameneja na Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa, Mhandisi Samamba amesema kuwa Sekta ya Madini ina nafasi kubwa katika kukuza uchumi endapo uongezaji thamani utawekewa kipaumbele.


“Mnapoweka mazingira rafiki ya uwekezaji kama vile kurahisisha upatikanaji wa vibali na miundombinu, wawekezaji wanaongezeka, ajira zinapatikana, mapato ya Serikali yanaongezeka na uchumi unakua,” amesema Mhandisi Samamba.


Amesisitiza Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa kushirikiana na viongozi wa mikoa na taasisi nyingine za Serikali kuhakikisha mazingira ya uwekezaji kwenye viwanda vya uongezaji thamani wa madini yanakuwa wezeshi, ili kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.

Katika hatua nyingine, Mhandisi Samamba amewataka Maafisa hao kuendelea kuwajengea uwezo wachimbaji wadogo kwa kuwapatia elimu ya Sekta ya Madini, taarifa za kijiolojia kupitia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), kuwaunganisha na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) pamoja na taasisi za kifedha ili kuongeza tija na mapato yao.


“Ninaamini tukiwasaidia wachimbaji wadogo wataongeza ajira, kukuza mzunguko wa fedha na kuiwezesha Serikali kukusanya kodi zaidi kwa ajili ya kuboresha huduma za kijamii kama elimu, afya, barabara na maji,” amesisitiza.


Aidha, ameitaka Tume ya Madini kuendelea kutoa elimu kwa Chama cha Watoa Huduma kwenye Migodi (TAMISA) ili kuongeza ushiriki wa Watanzania katika Sekta ya Madini kupitia mpango wa Local Content.


Vilevile, amewataka Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa kuhakikisha usalama kwenye shughuli za uchimbaji wa madini kwa kufanya ukaguzi wa mara kwa mara na kutoa elimu ili kuepuka ajali na uharibifu wa mazingira. Pia amesisitiza umuhimu wa kusimamia haki katika utatuzi wa migogoro ya wachimbaji wadogo.


Mhandisi Samamba amehitimisha kwa kuwataka watumishi wote wa Tume ya Madini kushiriki kikamilifu katika zoezi la uchaguzi litakalofanyika Oktoba 29, 2025, nchi nzima.


Kwa upande wao, Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Dkt. Janet Lekashingo na Katibu Mtendaji, Mhandisi Ramadhani Lwamo, wameishukuru Wizara ya Madini kwa kuendelea kuiwezesha Tume kupitia vitendea kazi ikiwemo magari, pikipiki, fedha na rasilimaliwatu, hali iliyochangia ongezeko la makusanyo ya maduhuli mwaka hadi mwaka.


Wamesema katika robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2025/2026 (Julai–Septemba), Tume ya Madini imekusanya Shilingi Bilioni 315.4 sawa na asilimia 105.13 ya lengo la Shilingi Bilioni 299.99, na kuwataka Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa kuongeza ubunifu na juhudi ili kufikia na kuvuka lengo la Shilingi Trilioni 1.2 kwa mwaka wa fedha 2025/2026.








Mchezo kati ya timu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na Sixers ukiendelea
Mchezo kati ya timu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na Sixers ukiendelea
Wachezaji timu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na Sixers wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya mchezo

***
Mgodi wa Barrick Bulyanhulu uliopo katika halmashauri ya wilaya ya Msalala mkoani Shinyanga, umeendelea kujenga uhusiano mzuri na jamii za maeneo yanaozunguka mgodi kupitia jukwaa la michezo ambapo Oktoba 14,2025 timu ya mpira wa kikapu inayoundwa na wafanyakazi wa mgodi iliikaribisha timu ya Sixers kutoka Kahama katika mechi ya kirafiki ambapo Bulyanhulu imeibuka na ushindi wa vikapu 33-30.

  

Na Mwandishi Wetu, JAB

Vitambulisho vipya vya kidijitali vinavyoendelea kutolewa na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) vimepokelewa kwa furaha na matumaini makubwa na waandishi wa habari nchini. Hatua hii imeelezwa kuwa ni mwanzo wa mwelekeo mpya wa tasnia ya habari nchini Tanzania.

Waandishi wengi wa habari wamepongeza hatua hiyo, wakieleza kuwa utoaji wa vitambulisho hivyo unarejesha heshima ya taaluma na kuongeza thamani ya elimu pamoja na juhudi walizowekeza ili kufikia viwango vya elimu vinavyohitajika kisheria.

Mhariri wa Gazeti Mwananchi Lilian Timbuka amesema kuwa hatua hiyo inaleta matumaini mapya katika tasnia ya habari.

“Tunayo matumaini kwamba sasa tasnia yetu itaonekana kwa jicho jipya. Heshima itakuwepo, maslahi yataongezeka, na jamii itaona thamani ya kazi tunayoifanya,” amesema Lilian.

Amefafanua kuwa kwa miaka ya nyuma, kazi ya uandishi wa habari ilizoeleka kufanywa na watu waliokuwa wamemaliza elimu ya sekondari bila ufaulu mzuri, au wale wenye vipaji vya kuzungumza na kupanga maneno, bila kujali vigezo vya kitaaluma.

Hata hivyo, ujio wa Bodi ya Ithibati umeweka mwelekeo mpya ambapo mtu atakayefanya kazi za kihabari na utangazaji ni yule mwenye kiwango cha elimu kisichopungua Stashahada (Diploma) katika fani ya Uandishi wa Habari au Mawasiliano kwa Umma.
Absalom Kibanda ni miongoni mwa waandishi wa habari wakongwe wanaounga mkono matakwa ya kisheria yanayomtaka mwandishi wa habari kuwa na kiwango cha elimu kisichopungua Stashahada (Diploma), ili kuipa taaluma hiyo heshima na hadhi inayostahili.

Wakili Patrick Kipangula, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Wanahabari (JAB), amesema kuwa wakati Sheria ya Huduma za Habari ilipotungwa mwaka 2016, Waziri mwenye dhamana alitoa kipindi cha mpito cha miaka mitano kwa wale waliokuwa na elimu chini ya Stashahada, au ambao hawakuwa na elimu rasmi ya uandishi, kurudi shuleni na kusomea taaluma hiyo.

Baada ya kipindi hicho, mwaka mmoja wa ziada uliongezwa ili kutoa fursa zaidi kwa wahusika kukamilisha masomo yao na sasa ni miaka mitatu zaidi ikifanya jumla ya miaka 9.

“Katika kipindi hicho, wapo waliotumia nafasi hiyo vizuri, kuna walioanzia ngazi ya cheti (Astashahada) wakaendelea hadi Stashahada, wengine wakaenda hadi Shahada na hata ngazi ya Shahada ya Uzamivu.
Hata hivyo, wapo ambao walibaki wakitazama wenzao wakijiendeleza na sasa utekelezaji wa sheria unapoanza rasmi, wameanza kulalamika na kuomba huruma. Ni wakati muafaka kwao kurudi vyuoni, kipaji pekee hakitoshi,” amesema Kipangula.

Furaha hii imeonekana pia miongoni mwa waandishi wenye Shahada za Uzamili (PhD), wakiwemo Dkt. Cosmas Mwaisobwa na Dkt. Ayubu Chacha Rioba, waliothibitisha kuwa vitambulisho hivyo vinatambua hadhi yao ya kitaaluma.

Dkt. Mwaisobwa alisema, "Hatukutarajia kama kuna siku vitambulisho vyetu vitasomeka 'Dkt', hii ni heshima kubwa kwetu kwa sababu safari ya kufikia ngazi ya Uzamivu haikuwa rahisi. Tumeisotea sana PhD, sasa kuona cheo hiki kikiwa sehemu ya utambulisho wetu rasmi ni faraja isiyo na kifani."

Bodi ya Ithibati ni nini na Majukumu yake ni yapi?

Bodi ya Ithibati ni chombo cha kitaaluma kilichoundwa kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229, kifungu cha 11, ili kukuza taaluma ya uandishi wa habari nchini.
Waziri mwenye dhamana ya habari ndiye aliyepewa mamlaka ya kuteua wajumbe wa bodi hii, na hadi sasa wajumbe sita kutoka taasisi za habari, vyama vya kihabari, taasisi za elimu na za serikali wameteuliwa.

Majukumu makuu ya Bodi ya Ithibati ni, kuthibitisha na kutoa vitambulisho kwa waandishi wa habari kwa mujibu wa Sheria hii, kusimamia uzingatiaji wa maadili ya taaluma ya Waandishi wa Habari, kuzingatia viwango vya kitaaluma na kukuza maadili mazuri na viwango miongoni mwa waandishi wa habari;

Majukumu mengine ni kuishauri Serikali katika masuala yanayohusu elimu na mafunzo kwa waandishi wa Habari, kwa kushauriana na taasisi nyingine zinazohusiana na masuala ya habari, kuweka viwango vya taaluma na mafunzo kwa waandishi wa Habari, kuanzisha ushirikiano na taasisi zingine za aina hiyo ndani na nje ya Jamhuri ya Muungano.

Pia, Bodi ina jukumu la kushauriana na Baraza na kuandaa mafunzo kwa waandishi wa Habari pamoja na kutunza orodha ya waandishi wa habari waliothibitishwa.
Hadi kufikia Oktoba 2025, Bodi imetekeleza jukumu moja la kuthibitisha na kutoa vitambulisho vya uandishi wa Habari maarufu Press Card kwa Waandishi zaidi ya 3,720 huku ikiendelea kuthibitisha wanaoendelea kujisajili.

Faida za ithibati kwa waandishi wa habari ni pamoja na;Kwanza ni kuwa na Utambulisho wa Kitaaluma, mwandishi anayetambulika kisheria ana uhalali wa kufanya kazi za kihabari kwa uhuru na kupewa heshima yake.

Pili, Ulinzi na Haki, kitambulisho kinampa mwandishi ruhusa ya kuingia katika maeneo maalum na kumwezesha kutekeleza majukumu yake bila kizuizi na kimtambulisha kwa mamlaka mbalimbali kumpa mwandishi msaada anapokutana na changamoto kazini.


Bodi haijaundwa kwa lengo la kuminya uhuru wa habari. Wakili Patrick Kipangula, Kaimu Mkuu wa Bodi, anasema:"

Bodi haijaundwa kuumiza uhuru wa habari, bali ni kusaidia sekta kuwa rasmi, kuipa heshima na kuongeza umuhimu wa kusimamia maadili na weledi. Uhuru wa waandishi wa habari unahakikishwa na Sheria ya Huduma za Habari."

Vitambulisho vya Uandishi wa Habari, vinatoa nafasi sawa kwa waandishi wenye ulemavu au waandishi chipukizi kuonekana na kuthaminiwa.

Seif Nindilo, mwandishi mwenye ulemavu wa macho, alipokabidhiwa kitambulisho chake alisema, "Ninachohitaji si huruma, bali ni kutambuliwa kama mwandishi wa habari mwenye ithibati, ninayeweza kutekeleza majukumu yangu sawasawa na wengine. Vitambulisho vya JAB vinafungua milango ya usawa na jumuishi."
Kwa upande wake Sista Paulina Mshana, mwandishi chipukizi mkoani Tanga, aliongeza, "Kadi ya JAB imenijengea kujiamini. Sasa naweza kusimama kwa ujasiri nikiwa na sauti inayosikika sawasawa na wengine. Hii inaonyesha uandishi wa habari ni wito unaoweza kushirikiana na miito mingine ya kijamii na kidini, mradi tu mwandishi awe na ithibati."


Ili kupata Kitambulisho kupitia Mfumo wa kidijitali Mwandishi wa Habari anatakiwa kujaza taarifa zake wakati wa kujisajili na kisha kupakia nakala ya vyeti vya kitaaluma, barua ya mwajiri au udhamini wa chombo cha habari, picha ndogo na nyaraka nyingine zinazohitajika.

Baada ya kukamilisha maombi Mwandishi atalipia malipo ya TSh 50,000 kwa kitambulisho kilicho na muda wa matumizi wa miaka miwili kwa wale wa Kitaaluma na 20,000 kwa wanafunzi wa mafunzo kwa vitendo kama ilivyoainishwa katika Sheria na Kanuni.

Kila mwandishi anayepata ithibati anathibitisha kuwa ana ujuzi, weledi, na sifa stahiki za taaluma, tofauti na wale wanaofanya kazi bila ithibati.Ithibati, Nguzo ya Heshima na Uaminifu.

  

Sikuwahi kufikiria siku moja jina langu lingesikika redioni kama mshindi wa jackpot. Ilikuwa Jumapili jioni nikiwa kwa duka langu dogo nikitazama mechi ya mwisho ya ligi ya England. Nilikuwa nimepiga bet kama kawaida, bila matumaini yoyote, maana mara nyingi nilikuwa napoteza hadi nimezoea. Nilikuwa nimeweka timu 13, na moyoni nilijua huu ungekuwa mpira mwingine wa kupoteza hela bure.

Ghafla simu yangu ikaanza kulia kwa nguvu. Nilipoipokea, sauti ya mwanamke ilisema kwa furaha, “Hongera, wewe ndiye mshindi wa jackpot ya wiki hii.” Nilidhani ni mzaha. Nilicheka nikasema, “Usinichezee akili dada, mimi kushinda milioni? Haiwezekani.” Lakini aliponisomea jina langu kamili na namba ya tiketi, nilihisi mwili mzima unatetemeka. Moyo wangu ulianza kudunda kwa kasi, macho yakajaa machozi, na midomo yangu ikakosa maneno.

Watu wa mtaa walikimbia hadi dukani kwangu. Nilihisi kama ndoto. Niliambiwa nimejinyakulia zaidi ya milioni 22, kitu ambacho nilikuwa nasikia tu kwenye redio au kuona kwa watu wengine. Nilipoitwa ofisini kuchukua hundi yangu, kamera zikapigwa, watu wakapiga makofi, lakini ndani yangu nilijua ushindi huu haukuwa wa kawaida. Kulikuwa na siri kubwa nyuma yake. Soma zaidi hapa 



Na.Ashura Mohamed-Karatu 

Naibu katibu Mkuu wizara ya Nishati bw.Dkt.James Mataragio  ameridhishwa na kasi ya  mradi  mradi wa utafutaji mafuta na gesi asilia kitalu cha EYAS WEMBERE kilichopo karatu mkoani  Arusha.

Ziara hiyo ya Naibu katibu mkuu inaeleza kuwa  mradi huo ambao ni mkakati maalum wa serikali ya Awamu ya sita na pia unatajwa iwapo utakamilika na mafuta kupatikana  utalisaidia taifa kuokoa fedha nyingi za kigeni na kuwezesha nchi kupata maendeleo badala ya fedha hizo kutumika kwenye kuagiza mafuta nje ya nchi.

Akizungumza na Vyombo vya habari mara baada ya kutembelea mradi huo  ambao unalenga kutafuta mafuta na gesi katika bonde la Ufa la Afrika Mashariki Dkt.Mataragio alisema kuwa mradi huo ulianza mwaka 2015 ulianza kwa kukusanya data mbali mbali ambazo zinahusiana na mafuta na gesi katika eneo hilo.

"Awamu ya kwanza mradi huu tulianza kukusanya data  kwa kutumia ndege yaani na baada ya hapo tulikusanya data zingine ambazo zilikuwa zinahusisha na  uchorongaji visima vitatu katika maeneo ya Singida ,Simiyu na Tabora zilibainisha miamba tabaka ambayo Ina mafuta  kwahiyo tukajiridhisha kuwa katika Eyas Wambele Kuna miamba ambayo inaweza kihifadhi Mafuta mbapo iligharimu kiasi Cha shilingi bilioni nane,kwa shughuli hizo na kazi hii ilifanywa na Shirika letu la Mafuta ambalo ni  (TPDC)."Alisema Dkt.Mataragio

Aidha alibainishi kuwa Awamu ya Pili ilihusisha ukusanyaji wa data Mtetemo kuangalia kina Cha miamba tabaka, kwa sababu asili ya mafuta ni lazima uwe na kina kiasi Fulani ili uweze kupata mafuta au lah ambapo shughuli hiyo unafanya na kampuni ya kitanzania ya African Geophysical  Services (AGS).

Pia amemtaka Mkandarasi wa Kampuni ya  Africa Geophysical Service (AGS),kuharakisha kasi ya mradi ikiwa ni pamoja kuongeza rasilimali watu ili mradi huo uweze kukamika  ndani ya wakati uliopangwa.

"Katika Zoezi hili  Awamu hii hili la kukusanya data Mtetemo lilifanyika kwa Awamu mbili Awamu ya kwanza tulichukua data za 2D za size na zilikuwa na urefu wa kilometa 260 kilometa na tulitumia kiasi Cha shilingi zaidi ya bilioni 10,ambapo baada ya kukamilika tulikuja katika Awamu  ya pili  ya uchukuaji wa data mitetemo ambayo ndio hii na tumeshaikamikisha kwa asilimia 47, na tumeshachukua kiasi Cha data kilometa 430,na itagharimu bilioni 45 kazi inaendelea na kama mnavyoona vifaa vipi imara kuhakikisha mradi huu utakamilika na kuleta matokeo chanya kwa nchi."Alisisitiza Dkt.Mataragio

Dkt.Mataragio alisema kuwa huo ni  mradi muhimu kwa serikali kwa kuwa kama mafuta yatagundulika basi nchi itaweza kuokoa fedha za kigeni ambazo hutumika kununua mafuta nje ya nchi na umeajiri watanzania zaidi ya 500.

Kwa Upande wake Mwenyekiti bw.Salim Ajib  Mwenyekiti wa kampuni  ya AGS alisema kuwa mradi huo ni muhimu kwa taifa na kampuni hiyo pia ambapo wameongezeka wataalamu kutoka ndani na nje ya nchi ili kuhakikisha kuwa kazi inafanyika kwa ufanisi ili kuweza kutoa data nzuri sana na kuweza kupata mafuta na kuhakikisha nchi inaendelea.

Pia alitumia fursa hiyo kusema kuwa kampuni hiyo Ina mchango katika eneo hilo kwa kuwa inawawezesha kupata ujuzi Vijana wa kitanzania pindi nmradi utakamilika.

Bwana Pastory  Maduka Mkazi wa Mwanza ambaye anafanya kazi katika eneo hilo alieleza kuwa uwepo wa mradi huo ni fursa kwao kama Vijana ambapo unawawezesha kupata ujuzi na kipato kinachowawezesha kujikimu wao na familia zao.

Mjiolojia Paschal Njiko ni kaimu  Mkurugenzi wa Utafutaji Uendelezaji na Uzalishaji kutoka  TPDC alisema kuwa Shirika hilo lina jukum la  kufanya Utafiti wa Mafuta na Gesi ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,na katika eneo hilo wanashirikiana na kampuni ya AGS,katika kutekeleza hilo ili kupata Taarifa za kina ili kuendelea na Zoezi linalofuata la uchimbaji Visima virefu vya Mafuta.

"Wenzetu nchi za jirani Kenya na Uganda walishafanya tafiti na kugundua mafuta katika maeneo yao ya bonde la Ufa sisi Tanzania ndio tulikuwa tumebakia nyuma na sasa  TPDC kama Shirika la Taifa  tumeamua katika  mabonde yetu ya Ufa haswa hili la Upande wa Mashariki  tuendele na utafiti wa kina na tuone kama tunaweza kuchimba mafuta au lah ila kwa kutumia data za kampuni hii ya AGS dalili ni kubwa na tunaweza kufanya maamuzi makubwa hapo baadae ndani ya miaka miwili ijayo."Alisema Njiko

Kwa upande wake, mmoja wa wanufaika wa  mradi wa Bonde la Eyasi Wembere, Biru Benjamini alisema kuwa kupitia mradi huo wameweza kunufaika na elimu,ujuzi na utaalamu ikiwa ni pamoja na kujiongezea kipato na kukua kiuchumi.

Mradi huo  unatarajiwa kumalizika April 2026 ambapo ambapo naibu katibu mkuu ametaka kasi ya utekelezaji wa shughuli za mradi unaharakishwa ili kumalizika ndani ya kipindi kilichopangwa.

Mradi huo wa utafiti wa uchimbaji wa mafuta na gesi unahusisha mikoa ya Arusha,Manyara,Tabora,Singida na Simiyu.