Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amelitaka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kumsimamia kikamilifu Mkandarasi anayetekeleza mradi wa ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi asilia kutoka eneo la ugunduzi la Ntorya hadi Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asilia cha Madimba ili kuhakikisha unakamilika ifikapo Septemba 2026
Amesema hayo, leo tarehe 27 Februari 2026 mkoani Mtwara mara baada ya kuweka jiwe la msingi la mradi wa bomba la gesi asilia Ntorya–Madimba ambao utekelezaji wake umefikia asilimia 35 akieleza kuwa mradi huo utachangia kuongeza matumizi ya gesi asilia na kuchochea ukuaji wa uchumi
“Tumeweka ‘taget’ ya mwezi wa tisa kuhakikisha visima hivi vinazalisha gesi na kuunga kwenye bomba kuu la Madimba, ikifika muda huo kusiwe na hadisi nyingine, ili haya yasitokee tunahitaji usimamizi wa hali ya juu kuhakikisha TPDC mnakuwa site muda wote, Watanzania wanataka wanataka kuona maendeleo,” amesisitiza Ndejembi
Aidha, Ndejembi amewataka wataalamu wa TPDC kuhakikisha shughuli zote zinafanyika kwa ubora na kwa kuzingatia muda uliokubaliwa kwenye mkataba huku akibainisha kuwa mradi huo utachochea ukuaji wa sekta ya gesi kwa kuongeza uzalishaji wa umeme kuvutia uwekezaji na kukuza viwanda vitakavyozalisha ajira kwa Watanzania
Ameihimiza TPDC kuongeza kasi ya utafutaji na uendelezaji wa visima vipya ili kuhakikisha upatikanaji wa gesi ya kutosha hususan ikizingatiwa kuwa miundombinu ya usafirishaji tayari ipo nchini pamoja na kutekeleza kikamilifu miradi ya uwajibikaji kwa jamii katika maeneo ya mradi kwa kushirikiana na wananchi kutatua changamoto kama ujenzi wa vyumba vya madarasa uchimbaji wa visima vya maji na miradi mingine kulingana na mahitaji ya eneo husika
Vilevile, Waziri Ndejembi amesema Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 imelenga kuongeza upatikanaji na matumizi ya gesi asilia hatua itakayowezesha kufikiwa kwa lengo la kuzalisha megawati 8000 za umeme ifikapo mwaka 2030
Awali, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi Dkt. James Mataragio amesema kitalu cha Ntorya kitaongeza upatikanaji wa gesi asilia huku akibainisha kuwa mahitaji ya gesi hiyo yanaongezeka kila siku na wawekezaji wa viwanda wamekuwa wakiwasilisha maombi ya gesi hiyo
Mradi wa bomba la kusafirisha gesi asilia ghafi kutoka kitalu cha Ntorya ulisainiwa tarehe 3 Julai 2025 kati ya TPDC na mkandarasi wa kampuni za China Petroleum Pipeline Engineering Co. Ltd. na China Petroleum Technology & Development Corporation kwa thamani ya Dola za Marekani Milioni 46.8 na unatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 30 Septemba 2026.
Mbunge wa Jimbo la Kisarawe,Mhe.Dkt. Selemani Jafo, ameendelea kuonesha dhamira yake ya dhati katika kuboresha huduma za afya kupitia kampeni yake ya “Kila Mtu Atibiwe Kwao”, inayolenga kuhakikisha kila kijiji kinakuwa na zahanati ili kusogeza huduma karibu na wananchi.
Akiwa katika ziara ya kuwashukuru wananchi wa Kitongoji cha Kola, Jafo amechangia tofali 1,500 kwa ajili ya ujenzi wa zahanati mpya itakayohudumia wakazi wa eneo hilo.
"Mchango huo ni sehemu ya mkakati mpana wa kupunguza adha ya wananchi kusafiri umbali mrefu kufuata matibabu, hususan wajawazito, watoto na wazee ambao kwa muda mrefu wamekumbana na changamoto ya kukosa huduma za afya karibu na makazi yao."amesema Dkt.Jafo
Akizungumza na wananchi, Dkt.Jafo amesisitiza kuwa afya ni haki ya msingi kwa kila mwananchi na kwamba ni wajibu wa viongozi kuhakikisha huduma hizo zinapatikana kwa urahisi bila usumbufu.
Ameeleza kuwa kampeni ya “Kila Mtu Atibiwe Kwao” inalenga kukamilisha ujenzi wa zahanati katika kila kijiji ndani ya jimbo hilo, ili kuimarisha ustawi wa jamii na kupunguza vifo vinavyoweza kuzuilika.
Aidha amebainisha kuwa katika kipindi cha miaka mitano kuanzia 2020 hadi 2025, aliweza kuhamasisha ujenzi wa zahanati 27 kupitia ushirikiano wa Mfuko wa Jimbo, Halmashauri, Serikali Kuu pamoja na wadau wa maendeleo.
Amesema mafanikio hayo yanatoa msingi imara wa kuendeleza juhudi zaidi katika awamu ijayo.
Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Masaki, Pili Kondo Chamgui, amempongeza Dkt.Jafo kwa juhudi zake za kuwajali wananchi. Ameeleza kuwa kwa sasa vijiji vyote vya kata hiyo vina zahanati, huku Kituo cha Afya cha Masaki kikiwa kinatoa pia huduma za upasuaji, hatua iliyopunguza kwa kiasi kikubwa rufaa zisizo za lazima.
Ameongeza kuwa ujenzi wa zahanati katika Kitongoji cha Kola utakuwa mkombozi mkubwa kwa wakazi wa eneo hilo ambao hulazimika kusafiri zaidi ya kilometa sita kufuata huduma za afya katika kijiji mama cha Kisanga.
Nao,Wananchi wa Kitongoji cha Kola, wameeleza shukrani zao kwa mbunge huyo, wakisema amesikia kilio chao cha muda mrefu cha ukosefu wa huduma za afya karibu na makazi yao. Walisema changamoto hiyo ilikuwa ikiweka maisha yao hatarini hasa wakati wa dharura za kiafya.
Kwa ujumla, kampeni ya “Kila Mtu Atibiwe Kwao” inaendelea kuleta matumaini mapya kwa wananchi wa Kisarawe, huku ushirikiano kati ya viongozi na jamii ukiwa chachu muhimu ya kusogeza huduma bora za afya karibu zaidi na wananchi.

Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro jana tarehe 26 Februari 2026 limepokea ugeni mzito uliongozwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi wa Tanzania, Mhe. Patrobas Paschal Katambi na Waziri wa Mambo ya Ndani na Usalama wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Jacob Jack Mwiimbu pamoja na ujumbe wa wageni 70 wa majeshi ya ulinzi na usalama waliopo nchini kwa majukumu mbalimbali na kufanya utalii hifadhi ya Ngorongoro.
Waheshimiwa mawaziri na Ujumbe wao waliopata fursa ya kutembelea vivutio vilivyopo Ngorongoro na kushuhudia Wanyama wakubwa watano (Simba, Chui, Nyati, faru na Tembo), makundi ya Pofu, pundamilia, swala, Nyumbu, Ngiri, Viboko, ndege, mimea ya asili, kasoko ya Ngorongoro na kupata simulizi mbalimbali kuhusu utalii wa miamba na hadhi tatu za kitamaifa zilizopo Ngorongoro.
Mhe. Katambi ameipongeza Ngorongoro kwa uhifadhi unaozingatia usalama wa mazingira, kulinda fahari ya Ngorongoro kama kivutio bora cha utalii Afrika.
Mtendaji Mkuu Dkt. Maulid J. Maulid amefunga mafunzo ya uongozi na usimamizi wa shule yaliyoendeshwa kwa Wakuu wa Shule za Sekondari za Wilaya ya Arusha pamoja na viongozi wa elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Arusha.
Akifunga mafunzo hayo amewasisitiza viongozi hao wa elimu kwenda kuweka mkazo kwenye uongozi bunifu wa kimkakati unaoleta mabadiliko kama msingi wa maendeleo katika taasisi za elimu.
Pia amesisitiza juu ya uongozi jumuishi ambapo wanapaswa kushirikisha wadau, kusikiliza maoni ya jamii na kujenga mazingira ya uaminifu na uwajibikaji wa pamoja katika kufikia mafanikio ya usimamizi wa taasisi za elimu wanazozisimamia.
“Nawasihi mwende kuwa viongozi wenye maono, wenye uwezo wa kufanya maamuzi ya kimkakati, na ujuzi wa kusimamia mabadiliko ya taasisi mnazosimamia kwa ufanisi kwani ninyi ndio mtachochea mabadiliko hayo”. Ameeleza Dkt. Maulid.
Aidha, Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma, Tafiti na Ushauri Elekezi Dkt. Lucas Mzelela amesema, mafunzo ya ADEM yamelenga kuwawezesha viongozi wa elimu kwa ujuzi wa vitendo, fikra za kimkakati na uwezo wa kusimamia taasisi za elimu kwa ufanisi ili kuleta mabadiliko ya kweli katika sekta ya elimu.
Nae Mwenyekiti wa TAHOSSA Mkoa wa Arusha, Mwalimu Omari Nyangu ameipongeza ADEM kwa namna ilivyoendesha mafunzo hayo kwa umahiri na weledi mkubwa na kutanabaisha kuwa maendeleo ya sekta ya elimu hayawezi kupatikana bila uwekezaji katika kuwajengea uwezo viongozi na wasimamizi wa taasisi za elimu na mafunzo waliyopatiwa ni dira katika usimamizi wa taasisi za elimu wanazozisimamia.
Wakuu hao wa shule wamejengewa uwezo kuhusu utawala bora wa elimu, Mpango wa Jumla wa Maendeleo ya Shule, usimamizi wa utekelezaji wa Mtaala, ustawi na usalama wa wanafunzi shuleni, ushirikishwaji wa jamii katika kuleta maendeleo ya shule, usimamizi wa rasilimali za shule, kuzingatia itifaki na huduma kwa wateja pamoja na ufuatiliaji na tathmini wa shughuli za elimu shuleni.


















WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Hamad Yussuf Masauni, amewaasa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuelimisha wananchi kuhusu misingi, faida na wajibu wao katika kulinda na kuutetea Muungano,
Pia amewataka Kupinga na kusahihisha upotoshaji wa taarifa kuhusu Muungano, hususani kupitia mikutano ya hadhara na mitandao ya kijamii.
Amesema, kwa kufanya hivyo, Wawakilishi watakuwa mabalozi wa amani, umoja na mshikamano wa kitaifa, kusikiliza na kuwasilisha.
Waziri Masauni aliyasema hayo Februari 27,2026 wakati akifungua semina ya elimu ya Muungano kwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, ikiwa ni sehemu ya mpango unaoendelea wa kutoa elimu hiyo kwa makundi mbalimbali ya jamii.
Amesema, kwa ujumla Wawakilishi ni nguzo muhimu ya kulinda na kuimarisha Muungano wa Tanzania kwa kupitia kutunga sheria, kusimamia Serikali na kuelimisha wananchi.
“Wawakilishi mnabeba dhamana ya kihistoria ya kuhakikisha Muungano unaendelea kuwa chanzo cha amani, mshikamano wa pande mbili na maendeleo,” alisema
Amesema, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi ni nguzo muhimu katika kuendelea kuuelimisha na kuulinda Muungano wa Tanzania kwa kuwa wako karibu zaidi na wananchi.
Amesema, Wajumbe hao wana nafasi kubwa ya kuifikisha elimu ya Muungano kwa wananchi kwa sababu wanawakilisha na kukutana na wananchi mara kwa mara katika majimbo yao.
“Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi ni nguzo muhimu katika kuulinda Muungano wetu, wanawafikia wananchi wengi zaidi, hivyo wana wajibu wa kueneza elimu ya Muungano
katika maeneo yao,” amesema
Ameeleza kuwa kwa kiasi kikubwa mpango huo unawalenga vijana ili waweze kufahamu fursa zilizopo ndani ya Muungano na kuzitumia kwa maendeleo yao na taifa kwa ujumla.
Amesema, fursa za Muungano ni nyingi, lakini changamoto iliyopo ni kutokuzitangaza na kuzifafanua ipasavyo kwa wananchi.
Kupitia semina hiyo mada mbali mbali zimewasilishwa kama vile Chimbuko, Misingi,Umuhimu wa Muungano, na Upekee wa Muungano.
Amesema, kupitia mada hizo wawakilishi hao watakuza na kuongeza uelewa na kutoa taswira pana juu ya umuhimu wa uwepo wa Muungano na kuibua hamasa ya katika kujenga uzalendo wa dhati kwa nchi, kuudumisha na kuuenzi Muungano kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Dkt. Richard Muyungi, amesema ofisi hiyo itaendelea kutoa elimu kwa makundi mbalimbali ili kuhakikisha uelewa wa masuala ya Muungano unaongezeka na kuimarika.
Ripoti mpya ya kimataifa imeitaja Tanzania kushika nafasi ya tano duniani kwa kuwa kizazi cha vijana ambao hawajaathiriwa na changamoto ya afya ya akili, ikizipita nchi za Ulaya, Amerika, Asia na Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Kwa mujibu wa matokeo hayo yaliyotangazwa Washington DC kufuatia utafiti uliofanywa na taasisi ya Sapien Labs, vijana barani Afrika wameonyesha kuwa na uimara wa afya ya akili wakati dunia ikishuhudia ongezekoo kubwa la changamoto ya afya ya akili miongoni mwa vijana duniani.
Tanzania imetajwa kushika nafasi ya tano duniani huku Ghana ikishika nafasi ya kwanza kidunia, na kufuatiwa na Nigeria, Kenya, Zimbabwe, hivyo kufanya nchi zote tano za kwanza kutoka barani Afrika.
Ripoti ya Dunia ya Afya ya Akili 2025 (The Global Mind Health Report 2025) inaonesha nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara kuzipita nchi nyingi zenye kipato cha juu, huku ikionesha kuongezeka kwa tatizo la afya ya akili miongoni vijana duniani.
Utafiti huo uliotumia data zilizokusanywa kutoka watu zaidi ya milioni moja katika nchi 84 umeonyesha asilimiia 41 ya vijana walio katika umri wa utu uzima ambapo wamezama katika matumizi ya teknolojia za kidigitali, wakitegemea intaneti kwa mawasiliano, elimu, burudani na maingiliano ya kijamii (umri kati ya miaka 18-34) duniani wanakabiliwa na changamoto ya afya ya akili.
Ripoti hiyo inaonesha kuporomoka kwa uwezo wao wa ufahamu, kijamii, kushindwa kudhibiti mihemko na kupungua kwa uwezo wa kimwili ambavyo kwa kiasi kikubwa vimethiri uwezo wao wa kupambana na changamoto za maisha.
Kwa upande mwingine, ripoti hiyo inaonesha tofauti ya kikanda kwa tatizoz la afya ya akili(regional) huku baadhi ya nchi za Afrika zikiongoza kwa kupata alama za juu katika matokeo ya afya ya akili kwa vijana.
Kwa mfano, vijana waliofikia umri wa utu uzima katika eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara wameonesha kuwapita wenzao wanaoishi kwenye nchi zenye kipato cha juu zikiwemo za Amerika ya Kusini, Ulaya na sehemu za Asia.
Hadi kufikia mwanzoni mwa mwaka 2,000 kundi la umri wa vijana iliohusisha utafiti huo (miaka 18-34) lilifanya vizuri katika ustawi na hali nzuri ya afya ya akili likilinganishwa na makundi mengine ya umri.
“Leo hii hali imegeuka, vijana watu wazima wako katika hatari mara nne zaidi ya wale wenye umri wa zaidi ya miaka 55 kupata changamoto ya afya ya akili yenye kuhitaji matibabu, hali ambayo kwa kiasi kikubwa imeathiri uwezo wao kuzalisha katika maisha yao ya kila siku.” Inasema sehemu ya ripoti hiyo.
Ripoti ya Afya ya Akili Duniani 2025 imehusisha badiliko hilo na sababu kadhaa zikiwemo matumizi ya mapema ya simu za kiganjani wakati wa utoto, kuongezeka kwa matumizi ya vyakula na vinywaji vinavyotengenezwa viwandani kama vile soda, vyakula vilivyogansishwa na vinavyohifadhiwa kwenye vifunashio, kuporomoka kwa uhusiano wa karibu katika family na kutothamini mambo ya kiroho.
Sapien Labs ni taasisi isiyo ya faida iliyojikita katika kuelewa athari mabadiliko ya kasi ya kijamii, kiteknolojia, na mazingira ya kemikali katika ubongo na akilil ya mwanadamu. Mradi wao wa Global Mind Project ndio mkubwa zaidi unaofuatilia vipengele 47 ya afya ya akili na sababu nyingine za kimaisha na kimazingira katika nchi zaidi ya 85 kwa lugha 25.
Taasisi hiyo inaongozwa na wataalamu wa sayansi ya neva na mishipa ya fahamu, saikolojia na wale wa sayansi ya kompyuta katika kuchambua na kutatua masuala magumu ya kisayansi walikusanya data kupitia utafiti wa kimtandao uliofanywa Asia, Africa, Ulaya na Amerika.
“Hatari ya tatizo ya afya ya akili inaonekana kuwa endelevu kutoka kizazi hadi kizazi na linakwenda mbali zaidi ya kuongeza viwango vya juu vya mfadhaiko na wasiwasi,” alisema Prof Tara Thiagarajan, kiongozi wa waandaaji wa ripoti hiyo na mwanzilishi na mwanasayansi mkuu wa Sapien Labs.
“Tumetathimini uwezo wa aina mbali mbali ambao mtu anapaswa kuwa nao ili kukabili chanamoto za maisha na kugundua kuwa vijana wengi walio katika umri wa utu uzima wanahangaika. Pamoja na mifadhaiko na wasiwasi, mara nyingi wanakumbana na changagmoto za kudhibiti mihemko, kushughulikainjdwa kumudu uhusiano na wengine, na kupoteza uwezo wao wa kuelekeza akili zao katika jambo bila kuvuruga mawazo,”
Kwa mujibu wa utafiti huo, kufanya vizuri kwa baadhi ya nchi za Afrika kunaweza kumaanisha kuwa mambo ya kijamii na kifamilia yanayokuza uimara na ustawi na kupunguza athari mbayakama vile msongo wa mawazo au sababu hatarishi vinaweza kuwa vinachangia vizuri kwenye matokeo hayo.
Matokeo ya utafiti huo yanaonesha pia kuwa vijana walio katika umri wa utu uzima Kusini mwa Jangwa la Sahara wameripotiwa kuwa na uimara wa kiroho, kuchelewa kuanza matumizi ya simu za kiganjani wakati wa utoto na kuwa na uhusiano wa karibu wa kifamilia ukilinganisha na wenzao katika nchi tajiri.
Tanzania, kwa mfano, imeshika nafasi ya juu kabisa kidunia katika kipimo cha mambo ya kiroho na ndio yenye wastani wa juu wa umri wa watu waliochelewa kuanza matumizi ya simu za kiganjani licha ya kushuka kutoka nafasi ya kwanza mwaka jana hadi ya tano mwaka huu. Kenya na Nigeria pia miongoni mwa nchi ilizoshika nafasi ya juu kidunia, huku Kenya ikionesha kufanya vizuri zaidi ikilinganishwa na miaka iliyopita.
Licha ya tofauti za kikanda, tofauti ya afya ya akili kati ya wazee na vijana imeendelea duniani kote, huku wazee wakionesha kuwa na afya imara zaidi ya akili kuliko idadi ya vijana.
Utafiti uliotangulia wa Sapien Labs ulionesha kuwa tofauti hiyo ilianza kukua kabla ya mwaka 2020 na kuongezeka kwa kiasi kikubwa wakati wa janga la UVIKO-19 2020 na 2021, wakati ambao afya ya akili ya vijana wenye umri wa utu uzima (miaka kati ya 18 na 34) ilishuka kwa kasi, huku vizazi vya umri mkubwa vikiathirika kwa kiasi kidogo tu.
“Kwa miaka mitano iliyopita, tofauti hii kwa kiasi kikubwa haijabadilika,” alisema
Dr Thiagarajan, na kuongeza kuwa waandaaji wa sera wanapaswa kutazama kwa karibu athari pana za kiuchumi za kuongezeka kwa vijana wanaoingia katiika kundi la nguvukazi wakiwa na afya dhaifu ya akili,” alisema.
Huku ikigusia sababu nyinginje nyingi za kushuka kwa afya ya akili, ripoti hiyo inabainisha sababu nne za msingi zinazochangia changamoto ya afya ya akili kwa vijana duniani. Imezitaja sababu hizo kuwa ni pamoja na matumizi ya mapema ya simu wakati wa utoto, ongezeko la vyakula vya viwandani, kupunggua uhusiano wa kifamilia na kutojali mambo ya kiroho. Kila moja ya sababu hizi inahusishwa na ongezeko la hatari matatizo ya afya ya akili na kupungua kwa uwezo wa vijana kuyakabili mahitaji ya maisha.“
Nchini Marekani, matumizi ya fedha kwa ajili ya utafiti wa afya ya akili na uangalizi yameongezeka sana kwa mabilioni ya dola, kama ilivyo kwa nchi za mashariki.
Na wakati hilo ni muhimu, halileti mabadiliko ya kuonekana,” alisema. “tuhahitaji kuacha kupambana na dalili na badala yake kupambana na matatizo makubwa zaidi yanayoathiri uzalishaji na ustawi wa vijana duniani. Kwa mfano, hatua za kisera zinazodhibiti upatikanaji wa simu za kiganjani kwa watoto na matumizi ya vyakula vya viwandani vinasaidia kulinda afya ya akili ya kizazi cha vijana---bila hivyo, uchumi wa dunia utatapatapa kwa miongo kadhaa ijayo.”
Ripoti hiyo pia imabainisha hatua mahususi za kisera zinazoweza kupunguza madhara, hasa madhara yanayosababishwa na matumizi ya mapema ya simu za kianjani kuongezeka kwa matumiizi ya vyakula vitokavyo viwandani. Kwa masuala yanayohusishwa na simu za kiganjani, ripoti hiyo imeshauri utungwaji wa sera zinazozuia matumizi yake wakati wa muda wa masomo na kuanzishwa kwa sharti la kuweka umri maalumu wa kutumia mitandao ya kijamii.
Kuhusu vyakuka vinanvyoandaliwa viwandani, ripoti hiyo imetaka kuwepo kwa uwekezaji mpya katiika tafiti ambazo zinaweza kufichua hatari zinahusishwa na aina mbali mbali za rangi, vikolezo, dawa za kuzuia vyakula visioze na vitu vinavyotumika kugandisha vyakula pamoja na viungio vingine vinavyopatikana kwenye vyakula—na kuleta ushahidi utakaounga mkono uanzishwaji wa kanuni za kupunguza matumizi yake.
“Wakati ripoti hii si ya kwanza kuhusisha vitu hivi na changamoto za afya ya akili, upana na kina cha data ilizofanyiwa kazi na Global Minds zitasimama kuonesha ukubwaa wa matatizo vinayosababisha,” alisema Prof David Blachflower, profesa wa uchumi katika Chuo cha Dartouth. “Kwa sababu pale unapoona ushahidi kuwa karibu nusu ya vijana wote duniani---moyo wa nguvukazi---wanapambana na mlolongo wa chanamoto za afya ya akili, hii ina maana tunakabiliwa na hatari inayoweza kudhoofisha afya ya uchumi wote na jamii. Ni kiashiria cha wazi kuwa tunahitaji kuchukua hatua kushughulikia mzizi wa tatizo.”
KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi.Mwajabu Nyamkomora,akizungumza wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.
Na.Alex Sonna,Mzalendo blog -DODOMA
KATIBU Tawala Msaidizi Mkoa wa Dodoma, Mwajabu Nyamkomora, amesema uwajibikaji na uaminifu ni miongoni mwa misingi muhimu inayochochea biashara endelevu na kukuza uchumi wa wananchi.
Bi.Nyamkomora ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara kuhusu shughuli za Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.
Amesisitiza kuwa wadau wa biashara wanapaswa kuzingatia maadili hayo ili kujenga mazingira bora ya ushindani wa haki sokoni, hatua itakayoongeza imani kwa wawekezaji na kuimarisha ustawi wa uchumi.
“Biashara endelevu inahitaji uwajibikaji na uaminifu. Bila misingi hiyo, ni vigumu kujenga soko lenye ushindani wa haki na linalomnufaisha mlaji,” amesema Bi. Nyamkomora.
Aidha ameeleza kuwa mafunzo hayo yanalenga kuongeza uelewa wa wadau kuhusu majukumu ya Baraza hilo pamoja na namna ya kulifikia kwa urahisi wanapokumbana na changamoto za kibiashara.
Kwa mujibu wake, elimu hiyo itawasaidia washiriki kutambua njia sahihi za kutatua migogoro inayohusiana na ushindani wa kibiashara na masuala ya udhibiti wa soko, jambo litakalosaidia kuimarisha biashara na kuongeza ufanisi katika shughuli za kiuchumi.
“Kupitia semina hii, kama sekta na wadau wetu muhimu tunaendelea kuimarisha mshikamano, kubadilishana uzoefu na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yetu,” ameongeza.
Hata hivyo amewataka wadau kujikita katika misingi ya uwajibikaji na uaminifu ili kuvutia uwekezaji unaoendana na kasi ya maendeleo ya Serikali chini ya uongozi wa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.
Bi.Nyamkomora amebainisha kuwa Ofisi ya Mkoa itaendelea kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Viwanda na Biashara kupitia Baraza la Ushindani kwa kutoa ushirikiano wa kutosha utakaowezesha utekelezaji wa majukumu ya taasisi hiyo, kwa lengo la kuboresha mazingira ya biashara na kukuza ustawi wa wananchi.
Kwa upande wake, Msajili wa Baraza la Ushindani, Mbegu Kaskasi, amesema kuwa mafunzo hayo ni sehemu ya mkakati wa Baraza kutoa elimu kwa wadau kufuatia maelekezo ya Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga, ya kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu majukumu ya taasisi hiyo.
Naye Mkuu wa Idara ya Uchumi wa FCT, Kulwa Msogoti, ameeleza kuwa Baraza hilo ni chombo cha kisheria kinachosikiliza rufaa za ushindani na kulinda maslahi ya wafanyabiashara pamoja na watumiaji wa bidhaa na huduma, kwa lengo la kujenga uchumi shindani na jumuishi nchini.
Nao Baadhi ya washiriki wa semina hiyo wamesema kuwa mafunzo hayo yamewapa mwanga kuhusu namna ya kufuata taratibu sahihi za kisheria wanapokumbana na changamoto za ushindani au wanaporidhika na maamuzi ya mamlaka za udhibiti.
Semina hiyo ni sehemu ya mkakati wa Baraza la Ushindani wa kuwafikia wadau katika mikoa mbalimbali nchini ili kuongeza uelewa wa sheria za ushindani na kuimarisha utatuzi wa migogoro kwa njia ya kisheria.

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akizungumza wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akizungumza wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akizungumza wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akizungumza wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

MSAJILI wa Baraza la Ushindani (FCT), Mbegu Kaskasi,akizungumza wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

SEHEMU ya washiriki wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora (hayupo pichani) wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

SEHEMU ya washiriki wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora (hayupo pichani) wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.


SEHEMU ya washiriki wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora (hayupo pichani) wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

MKUU wa Idara ya Uchumi FC Bw.Kulwa Msogoti,akiwasilisha mada wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

MKUU wa Idara ya Uchumi FC Bw.Kulwa Msogoti,akiwasilisha mada wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

MKUU wa Idara ya Sheria FCT Bw.Kunda Mkenda,akiwasilisha mada kuhusu Sheria wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

AFISA TEHAMA FCT Athuman Kanyegezi,akiwasilisha mada kuhusu TEHAMA wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

WADAU mbalimbali wakichangia mada na kutoa ushauri wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akiwa katika picha ya pamoja na washiriki mara baada ya kufungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma .

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akiwa katika picha ya pamoja na washiriki mara baada ya kufungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma .

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akiwa katika picha ya pamoja na washiriki mara baada ya kufungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma .




















.jpg)
.jpg)


