MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) zimeingia makubaliano ya ushirikiano yatakayowezesha waraibu waliopona matumizi ya dawa za kulevya kupata mafunzo ya ufundi stadi, hatua inayolenga kuwajengea uwezo wa kujitegemea kiuchumi na kuzuia kurejea kwenye matumizi ya dawa hizo.
Nilikuwa na matumaini kwamba mambo yangekaa sawa baada ya muda na ningeweza kulipa kila kitu bila shida. Lakini hali haikuwa rahisi kama nilivyotarajia. Biashara ilianza kuyumba.
Mapato yalipungua huku gharama zikiongezeka. Ili kuendelea kuendesha shughuli zangu, nilijikuta nikikopa tena. Baadaye nikakopa sehemu nyingine ili kufidia deni la awali.
Polepole nilinaswa kwenye mzunguko wa madeni. Kwa kweli ilikuwa hali ngumu sana. Kilichoniumiza zaidi ni presha ya wadai. Kila siku kulikuwa na simu, ujumbe, na ahadi za malipo ambazo sikuweza kutimiza kwa wakati.
Wakati mwingine nilikosa usingizi nikifikiria jinsi ningetoka kwenye hali ile. Nilianza kupoteza matumaini. Kulikuwa na wakati nilihisi kama maisha yangu yalikuwa yamesimama. Kila fedha niliyopata ilikuwa inaishia kulipa sehemu ya deni, na bado madeni yalionekana kutopungua. SOMAZ AIDI.
Tulikuwa tumezungumza kuhusu ndoa, maisha ya baadaye, na hata majina ya watoto tuliotamani kuwa nao siku moja. Nilikuwa na uhakika kwamba ndiye mtu ningeishi naye maisha yangu yote. Lakini siku moja kila kitu kilibadilika.
Bila kutarajia, alianza kuwa mbali. Mawasiliano yakapungua, mipango ikaanza kusogezwa mbele, na hali ambayo zamani ilikuwa ya furaha ikaanza kujawa na sintofahamu.
Kisha nikapokea maneno ambayo sikuwahi kutarajia kuyasikia. Aliniambia hataki kuendelea na uhusiano wetu. Kwa kweli nilivunjika moyo. Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilikuwa tayari nimejenga maisha yangu ya baadaye nikimhusisha yeye.
Ghafla ndoto zote nilizokuwa nimejenga zilionekana kuporomoka mbele ya macho yangu. Kulikuwa na usiku nilikosa usingizi.
Wizi ulitokea ghafla. Nilijaribu kuitafuta mara moja, nikapiga simu kwenye namba yangu mara kadhaa, lakini haikupatikana. Kadri muda ulivyopita, matumaini ya kuipata yalianza kupungua. Kwa kweli niliumia sana.
Kilichoniumiza zaidi ni kupoteza taarifa muhimu zilizokuwa ndani yake. Watu wengi waliniambia nisipoteze muda kuitafuta kwa sababu uwezekano wa kuipata ulikuwa mdogo sana. Baada ya wiki kadhaa, nilianza kuamini kwamba simu ile ilikuwa imepotea milele.
Miezi ilipita. Polepole nilijaribu kuendelea na maisha yangu. Nilinunua simu nyingine na kuanza kujenga upya baadhi ya taarifa nilizokuwa nimezipoteza. Hata hivyo, kila nilipokumbuka simu yangu ya zamani, bado nilihisi huzuni. SOMA ZAIDI.
Mwanzoni niliamini hali ile ingepita. Lakini kadri miezi ilivyopita, migogoro ilizidi kuwa ya kawaida. Watu waliokuwa wakicheka pamoja zamani walikuwa wameanza kuepukana. Wakati mwingine hata kula pamoja mezani kulikuwa jambo gumu.
Kwa kweli iliniumiza sana. Kilichoniumiza zaidi ni kuwaona wazazi wetu wakihangaika kujaribu kuleta amani bila mafanikio. Kila mtu alikuwa na upande wake wa hadithi, na hakuna aliyeonekana tayari kusikiliza mwingine.
Nyumbani palikuwa na ukimya mzito. Kulikuwa na siku nilikuwa nikihofia kwamba familia yetu ingeweza kugawanyika kabisa. Nilijiuliza ni lini tulipoteza upendo na umoja tuliokuwa nao hapo awali. SOMA ZAIDI.
Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia. Jaribio langu la kwanza halikufanikiwa. Nilijikuta nimefanya makosa ambayo sikutarajia. Ingawa niliumia moyo, nilijiambia nitajitayarisha vizuri zaidi na kujaribu tena.
Cha kusikitisha ni kwamba hata jaribio la pili halikufaulu. Nilianza kuona aibu kila mtu aliponiuliza kuhusu leseni yangu. Watu wengine walikuwa wakinicheka na kuniambia kwamba labda kuendesha gari hakukuwa jambo langu.
Kwa kweli maneno yale yaliniumiza. Nilijaribu kwa mara ya tatu nikiwa na matumaini makubwa, lakini matokeo yalikuwa yale yale.
Na Anangisye Mwateba, Zanzibar
MRADI wa Mifumo ya Chakula, Matumizi ya Ardhi na Urejesho wa Mandhari ya Misitu nchini Tanzania (FOLUR), unatarajia kutoa mafunzo maalum kwa viongozi wa serikali za vijiji na shehia mbalimbali visiwani Zanzibar. Hatua hiyo inalenga kujenga uwezo wa kiutendaji na kuhakikisha jamii inatekeleza shughuli za mradi huo kwa kuzingatia viwango vya kimataifa.
Akifungua mafunzo hayo kwa maafisa ugani wa kilimo na misitu upande wa Zanzibar, Mratibu wa mradi huo, Bi. Miza Suleiman Khamis, alisema dhumuni kubwa ni kuwawezesha watendaji hao kubaini, kuepuka au kupunguza athari hasi zinazoweza kujitokeza kabla hazijaletea madhara wanajamii na mazingira yao.
Kwa upande wake, Msimamizi wa Kitengo cha Jinsia, Usalama wa Mazingira na Jamii wa mradi huo, Bw. Revocatus Kadoshi, alibainisha kuwa viongozi wa shehia na maafisa ugani watafundishwa miongozo minne mikuu.
Miongoni mwa miongozo hiyo ni Mpango wa Usimamizi wa Mazingira na Jamii (ESMP), unaohusu udhibiti wa matumizi ya rasilimali na kuzuia uhamishaji wa watu usio wa hiari.
Bw. Kadoshi alifafanua kuwa mwongozo huo unalenga kudhibiti na kupunguza athari za kimazingira na kijamii wakati wa utekelezaji wa mradi. Aliongeza kuwa hatua hiyo inaenda sambamba na matakwa ya Mwongozo wa Sera na Taratibu Jumuishi za Ulinzi wa Kijamii za Shirika la Uhifadhi wa Mazingira Duniani (WWF).
"Viongozi hawa pia watafundishwa kuhusu Usimamizi Shirikishi wa Visumbufu. Huu unalenga kulinda afya na usalama wa jamii kwa kudhibiti athari zitokanazo na matumizi ya viuatilifu na mbolea," alisema Bw. Kadoshi.
Aidha, mafunzo hayo yatahusisha mbinu za usimamizi wa mazingira zinazohakikisha ustawi wa jamii, usalama mahali pa kazi, pamoja na usafi wa mazingira wakati wote wa utekelezaji wa shughuli za mradi huo.
Vilevile Aliongeza kuwa, ili kuhakikisha usalama wa jamii, mradi umeweka utaratibu maalumu wa kupokea nakufanyia kazi malalamiko kutoka kwa mwanajamii au kikundi cha kijamii kuhusiana na shughuli zinazotekelezwa na mradi. Hii inalwnga kuhakikisha jamii inashiriki vema kwenye shighuli za mradi na wanakuwa na nafasi ya kutoa dukuduku au lalamiko wakati wowote.
![]() |
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk. Leonard Akwilapo, ameielekeza Bodi mpya ya Wakurugenzi ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kusimamia kwa ukaribu ukusanyaji wa mapato na madeni ya Shirika, akisisitiza kuwa hakuna mdaiwa anayepaswa kupewa upendeleo katika kulipa fedha zinazodaiwa na taasisi hiyo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa Bodi mpya ya Wakurugenzi ya NHC uliofanyika jijini Arusha tarehe 3 Juni 2026 , Dk. Akwilapo alisema mafanikio ambayo Shirika limeyafikia katika kujiendesha kibiashara na kuendelea kuwa imara kifedha yanapaswa kulindwa kwa kuimarisha nidhamu ya mapato na usimamizi wa rasilimali zake.
“Msitishike linapokuja suala la kudai malipo yenu halali. Hakuna mdaiwa anayepaswa kuogopwa. Wote wapeni ankara zao za madeni kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo,” alisema Dk. Akwilapo.
Waziri huyo wa Ardhi alisema NHC ni miongoni mwa mashirika ya umma yaliyoendelea kuonesha uimara katika biashara zake, tofauti na baadhi ya taasisi ambazo zilishindwa kujiendesha kwa ufanisi na hatimaye kupoteza nafasi yake katika uchumi wa taifa.
Alieleza kuwa, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ina matarajio makubwa kwa NHC katika kuendeleza agenda ya makazi bora, miji endelevu na uwekezaji wa kimkakati unaochochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Dk. Akwilapo pia aliitaka Bodi mpya kusimamia kwa karibu maandalizi ya Mpango Mkakati mpya wa Shirika utakaokwenda sambamba na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Mpango wa Tatu wa Taifa wa Maendeleo pamoja na malengo ya kimataifa ya maendeleo endelevu yanayohusiana na makazi na maendeleo ya miji.
Awali, Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Hamad Abdallah, alisema Shirika limeendelea kuimarisha utendaji wake kupitia uwekezaji katika miradi ya makazi, biashara na matumizi ya mifumo ya kidijitali inayorahisisha utoaji wa huduma na usimamizi wa shughuli zake.
Alisema NHC imeendelea kuimarisha vyanzo vya mapato kupitia upangishaji wa majengo, mauzo ya nyumba na viwanja pamoja na miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo tofauti nchini.
Bw. Hamad alibainisha kuwa Menejimenti ya Shirika itaendelea kushirikiana kwa karibu na Bodi mpya ili kuhakikisha maelekezo ya Serikali yanatekelezwa kwa ufanisi na NHC inaendelea kuwa taasisi ya mfano katika sekta ya makazi.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya NHC, Dk. Sophia Kongela, alimshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiamini Bodi hiyo na kuwapa wajumbe dhamana ya kuiongoza taasisi hiyo katika kipindi kingine cha utekelezaji wa majukumu yake.
Dk. Kongela alisema Bodi imepokea kwa uzito maelekezo yaliyotolewa na Waziri na iko tayari kuyafanyia kazi kwa kushirikiana na Menejimenti ya Shirika.
Alisema moja ya vipaumbele vya Bodi ni kuimarisha usimamizi wa mali za Shirika, kuongeza tija ya uwekezaji, kuimarisha ukusanyaji wa mapato, kusimamia miradi ya makazi nafuu na kuhakikisha NHC inaendelea kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya makazi nchini.
“Tunatoa hakikisho la ushirikiano wa karibu na Serikali pamoja na Menejimenti ya Shirika ili kuhakikisha NHC inafikia malengo yake na kuendelea kuwa chachu ya maendeleo ya sekta ya makazi Tanzania,” alisema Dk. Kongela.
Uzinduzi wa Bodi mpya ya Wakurugenzi ya NHC umeashiria mwanzo wa awamu mpya ya uongozi unaotarajiwa kuimarisha zaidi ukuaji wa Shirika, kuongeza uwekezaji na kuharakisha utekelezaji wa miradi ya makazi bora kwa manufaa ya Watanzania.
Bodi hiyo mpya inaongozwa na Mwenyekiti, Dk. Sophia Kongela na wajumbe wake wakiwa ni Eliud Sanga, Profesa Wilbard Kombe, Ali Hussein Laay, Doroth Mwanyika, Ayoub Omari Kasui, Vupe Ligate na Elias Kisamo
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Denis Londo, ametembelea banda la Tume ya Ushindani Tanzania (FCC) katika Maonesho ya Kimataifa ya Mbeya City Expo 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Uhindini, jijini Mbeya, ambapo alipata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na taasisi hiyo katika kulinda maslahi ya walaji na kuimarisha ushindani wa biashara nchini.
Katika maonesho hayo, FCC imekuwa ikitoa elimu kwa wananchi kuhusu haki za mlaji, namna ya kutambua na kuepuka bidhaa bandia pamoja na umuhimu wa ushindani wa haki katika shughuli za biashara.
Elimu hiyo imevutia mamia ya wananchi waliojitokeza kutembelea banda hilo na kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali yanayohusu biashara, ushindani na ulinzi wa walaji.
Akizungumza wakati akifunga Maonesho hayo yaliyodumu kwa siku tisa Mei 30, 2026 jijini Mbeya, Naibu Waziri Londo alisisitiza umuhimu wa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu madhara ya bidhaa bandia, akieleza kuwa bidhaa hizo zinaathiri afya za watumiaji, kudhoofisha biashara halali na kupunguza mapato ya Serikali.
Kwa upande wake, Mkuu wa Kanda wa FCC - Nyanda za Juu Kusini Bw. Dickson Mbanga, amesema taasisi hiyo imejipanga kuendelea kuimarisha kampeni za utoaji elimu kwa wananchi ili kuwajengea uwezo wa kutambua bidhaa halisi na kuepuka kununua au kutumia bidhaa zisizo na viwango vinavyotakiwa.
Mbanga alisema Maonesho ya Mbeya City Expo yamekuwa jukwaa muhimu la kuifikia jamii kwa karibu na kutoa elimu inayolenga kuongeza uelewa kuhusu sheria za ushindani na hatua zinazochukuliwa dhidi ya wafanyabiashara wanaojihusisha na usambazaji wa bidhaa bandia.
“Tunatumia maonesho haya kuwafikia wananchi wengi zaidi na kuwaelimisha kuhusu hatari za bidhaa bandia na kumlinda mlaji. Lengo letu ni kuhakikisha watumiaji wanakuwa na taarifa sahihi zitakazowasaidia kufanya maamuzi bora wanaponunua bidhaa mbalimbali sokoni,” alisema Mbanga.
Aliongeza kuwa FCC itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa biashara na vyombo vya usalama katika kudhibiti bidhaa bandia zinazoingia sokoni, huku ikiendelea kuhamasisha wananchi kutoa taarifa wanapobaini uwepo wa bidhaa zinazotiliwa shaka.
Maonesho ya Mbeya City Expo 2026 yamewakutanisha wadau kutoka sekta mbalimbali za uchumi, biashara na uwekezaji, huku yakitoa fursa kwa taasisi za umma na binafsi kuonesha huduma, bidhaa na mafanikio yao kwa wananchi. Kupitia ushiriki wake, FCC imeendelea kuonesha dhamira ya Serikali ya kulinda walaji na kujenga mazingira ya biashara yenye ushindani wa haki kwa


Kulikuwa na matatizo ya kifamilia, presha za kifedha, na mambo mengine mengi yaliyokuwa yakinifanya nifikirie kupita kiasi kila siku. Mwanzoni nilijaribu kuvumilia.
Nilijiambia kwamba hali ile ingepita yenyewe. Lakini kadri muda ulivyopita, nilianza kugundua kwamba sikuwa yule mtu niliyemzoea zamani. Kwa kweli nilibadilika. Nilianza kupoteza hamu ya kufanya mambo niliyokuwa napenda.
Mara nyingi nilikuwa nataka kukaa peke yangu. Furaha yangu ilipungua, na hata kuzungumza na watu wa karibu kulianza kuwa jambo gumu. Kilichoniumiza zaidi ni kupoteza kujiamini. SOMA ZAIDI.
Nilipoanzisha biashara yangu, sikuwahi kufikiria kwamba siku moja ningepokea oda kutoka sehemu ambazo sijawahi hata kufika. Mwanzoni biashara yangu ilikuwa ndogo sana.
Nilikuwa na wateja wachache kutoka eneo nililoishi, na mauzo yalitosha tu kuendesha shughuli za kila siku. Ingawa nilikuwa na ndoto kubwa, ukweli ni kwamba biashara ilikuwa inakua polepole kuliko nilivyotarajia.
Kwa kweli kulikuwa na wakati nilikata tamaa. Nilikuwa nikijitahidi kutangaza bidhaa zangu, kuboresha huduma, na kuwahudumia wateja vizuri, lakini matokeo hayakuwa makubwa. Wakati mwingine nilijiuliza kama biashara yangu ingeweza kufika kiwango nilichokuwa nikiota.
Kilichoniumiza zaidi ni kuona biashara nyingine zikikua kwa kasi huku yangu ikibaki pale pale. SOMA ZAIDI.









