Katika kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050 inayolenga kuhakikisha wananchi wanapata makazi bora na ya gharama nafuu, Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) umeendelea kutekeleza mpango wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu ili kuwawezesha wananchi, hususan vijana, kumudu kumiliki makazi.

Akizungumza katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika kitaifa katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Huduma Saidizi wa TBA, Bi. Amina Lumuli, amesema kuwa TBA tayari imeanza kutekeleza miradi ya nyumba za gharama nafuu katika mkoa wa Dar es Salaam.

Bi. Lumuli ametaja Mradi wa Temeke Kota kuwa ni miongoni mwa miradi hiyo, akibainisha kuwa utekelezaji wa mpango huo utaendelea katika maeneo mbalimbali nchini.

"Tunawakaribisha wawekezaji kuja kushirikiana nasi ili kwa pamoja tuweze kufanikisha lengo la Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050 la kuhakikisha wananchi wanapata makazi bora na ya gharama nafuu," amesema Bi. Lumuli.

Aidha, Bi. Lumuli amesema utekelezaji wa mradi huu unatokana na dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuhakikisha wananchi wanapata makazi bora na yenye gharama nafuu.

Amesema TBA itaendelea kuhakikisha makundi yote, yakiwemo makundi maalum, yanafikiwa na kunufaika na programu hii ya nyumba za gharama nafuu.
Nilipoamua kugombea nafasi ya uongozi, watu wengi hawakunichukulia kwa uzito. Wapinzani wangu walikuwa na majina makubwa, uzoefu wa muda mrefu, na ushawishi mkubwa katika jamii. 

Wengi waliniambia nilikuwa napoteza muda wangu kwa kuingia kwenye uchaguzi ambao tayari ulikuwa umeamuliwa.

Lakini sikukata tamaa. Nilijua nilikuwa na maono ya kuwaletea watu maendeleo na nilitaka kuwapa sababu ya kuamini kwamba mabadiliko yanawezekana. 

Hata hivyo, kadri kampeni zilivyoendelea, changamoto ziliongezeka. Kulikuwa na maneno mengi ya kunikatisha tamaa.

Baadhi ya watu walieneza uvumi kwamba sikuwa na uwezo wa kuongoza. Wengine walisema sina mtandao wa watu wenye ushawishi wa kunisaidia kushinda. 

Wakati mwingine nilirejea nyumbani nikiwa nimechoka na kujiuliza kama kweli nilikuwa nimefanya uamuzi sahihi. SOMA ZAIDI.
Kwa zaidi ya miaka mitano, nilikuwa nimejenga biashara yangu kwa juhudi kubwa. Nilijitahidi kuwahudumia wateja wangu vizuri na kuhakikisha biashara yangu inakua mwaka baada ya mwaka. Lakini ghafla mambo yalianza kubadilika kwa njia ambayo sikuweza kuielewa.

Kila nilipoanzisha ofa mpya au mpango wa biashara, washindani wangu walionekana kujua kila kitu kabla hata sijaanza kuutekeleza. Mwanzoni nilidhani ilikuwa bahati mbaya. Lakini kadri hali ilivyoendelea kujirudia, nilianza kupata mashaka.

Wakati mwingine nilikuwa nazungumza mipango yangu na wafanyakazi wachache tu wa ndani, lakini baada ya siku chache washindani walikuwa tayari wamechukua hatua zinazofanana na zangu. Biashara yangu ilianza kupata hasara.

Wateja waliokuwa wakinifuata kwa muda mrefu walikuwa wakivutiwa na washindani waliokuwa wakionekana kujua kila hatua niliyopanga kuchukua. Nilihisi kama kuna mtu alikuwa akivujisha siri muhimu za biashara yangu.

Nilijaribu kuchunguza mwenyewe.

Nilifuatilia mawasiliano mbalimbali na kuangalia mienendo ya wafanyakazi wangu, lakini sikuweza kupata ushahidi wa kutosha. SOMA ZAIDI.
Hakuna jambo linaloumiza mzazi kama kuwaona watoto wake wakiteseka. Kwa muda mrefu, watoto wangu walikuwa wakiugua mara kwa mara.

Mwezi mmoja hawakuwa sawa, na kabla hawajapona kabisa, tatizo jingine lilikuwa limeanza. Safari za hospitali zikawa sehemu ya maisha yetu ya kawaida. Nilikuwa na wasiwasi mkubwa.

Mbali na matatizo ya afya, amani nyumbani pia ilikuwa imepotea. Watoto walikuwa wakigombana mara kwa mara, kulikuwa na hali ya huzuni ambayo sikuweza kuieleza, na kila mtu ndani ya nyumba alionekana kuwa na mawazo mengi. Nilijaribu kufanya kila nilichoweza kama mzazi.

Nilihakikisha watoto wanapata matibabu wanapohitaji, wanakula vizuri, na wanapata mapumziko ya kutosha. Hata hivyo, nilihisi kama bado kulikuwa na jambo lililokuwa likinisumbua moyoni. Kadri miezi ilivyopita, uchovu na wasiwasi vilianza kunizidi. SOMA ZAIDI.
Baada ya kuhitimu masomo yangu, nilikuwa na matumaini makubwa ya kupata kazi nzuri na kuanza kujitegemea.

Nilituma maombi kwa kampuni mbalimbali na kuhudhuria mahojiano mengi. Kila nilipoitwa kwenye interview, niliamini safari hii ningepata nafasi niliyokuwa nikiiota. Lakini mara nyingi majibu yalikuwa yale yale.

“Sikuchaguliwa.” Kadri miezi ilivyogeuka kuwa miaka, hali ilianza kuniumiza sana. Niliona marafiki zangu wakipata kazi na kuendelea na maisha huku mimi nikiendelea kutuma maombi kila wiki bila mafanikio. Wakati mwingine nilifika hatua ya kujiuliza kama kulikuwa na kitu nilichokuwa nikifanya vibaya.

Nilijitahidi kuboresha wasifu wangu, kujifunza ujuzi mpya, na kujiandaa vizuri kwa mahojiano. Hata hivyo, kila nilipokuwa karibu kupata matumaini, nilipokea ujumbe mwingine wa kukataliwa. Familia yangu ilinipa moyo, lakini ndani yangu nilikuwa nimeanza kukata tamaa. SOMA ZAIDI.
Ndoa yangu ilikuwa imejengwa juu ya upendo, heshima, na matumaini makubwa ya maisha ya pamoja. Kwa miaka kadhaa mambo yalikuwa mazuri. Mimi na mume wangu tulielewana na tulifanya kila kitu kwa ushirikiano. Lakini hali ilianza kubadilika taratibu.

Mume wangu alianza kurudi nyumbani akiwa amechelewa, akawa mbali kihisia, na muda aliokuwa akitumia na familia ukapungua.
Mwanzoni sikutaka kuamini kwamba kulikuwa na tatizo. Nilijaribu kuzungumza naye mara kadhaa, lakini kila nilipouliza kuhusu mabadiliko yake, alinipa majibu mafupi au kubadilisha mada.

Kadri miezi ilivyopita, niligundua kwamba kulikuwa na mwanamke mwingine katika maisha yake. Habari hiyo ilinivunja moyo. Nilihisi hasira, huzuni, na kuchanganyikiwa kwa wakati mmoja.

Wakati mwingine nilitaka kuondoka kabisa, lakini nilikuwa bado na matumaini kwamba familia yetu ingeweza kuokolewa. SOMA ZAIDI.


Na Mwandishi Wetu - Dar es Salaam


Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la International Media Support (IMS), umeahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano na vyombo vya habari pamoja na wadau mbalimbali wa sekta ya habari nchini ili kukuza uandishi wa habari zenye maslahi kwa umma.

Akizungumza wakati wa semina iliyowakutanisha wawakilishi wa vyombo mbalimbali vya habari nchini, Mkurugenzi wa UTPC, Kenneth Simbaya, alisema ushirikiano kati ya wadau wa sekta ya habari ni muhimu katika kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi na zenye manufaa kwa maendeleo yao.

Alisema kuna haja ya kuimarisha ushirikiano kati ya vyombo vya habari, mamlaka za usimamizi wa sekta hiyo na wadau wengine ili kuleta mabadiliko chanya yatakayochochea upatikanaji wa habari zinazolenga maslahi ya wananchi.

“Tunao wajibu wa kufanya kazi kwa pamoja kuhakikisha tunajenga jamii yenye taarifa sahihi. Kila mmoja anatakiwa kutimiza wajibu wake ili kufikia malengo ya kuimarisha sekta ya habari nchini,” alisema Simbaya.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Tanzania Media Foundation Dastan Kamanzi (TMF), alisema waandishi wa habari wanapaswa kuweka kipaumbele katika kuandaa na kuchapisha habari zinazogusa maisha ya wananchi, haki zao pamoja na uhuru wao.

Alieleza kuwa kufanya hivyo kutasaidia kuitendea haki taaluma ya uandishi wa habari na kuongeza mchango wake katika maendeleo ya jamii.

Wakichangia mjadala huo, baadhi ya wawakilishi wa vyombo vya habari walieleza kuwa utekelezaji wa habari za maslahi kwa umma unahitaji uwezeshaji zaidi kupitia mafunzo na upatikanaji wa vitendea kazi vya kisasa.

Walisema baadhi ya vyombo vya habari bado vinakabiliwa na changamoto ya uhaba wa wataalamu wenye ujuzi wa kutumia mbinu za kisasa katika kuandaa na kuandika habari za maslahi kwa umma.


Semina hiyo iliyoandaliwa na UTPC ililenga kufanya tathmini ya pamoja kuhusu changamoto zinazoathiri upatikanaji wa habari za maslahi kwa umma na kujadili mikakati ya kuzitatua. Semina hiyo ilifanyika Juni 19, 2026 katika Hoteli ya Mbezi Garden, jijini Dar es Salaam.




Vyuo vikuu nchini vinapaswa kuifanya agenda ya umataifishaji kuwa sehemu ya mikakati yake ya msingi kwa kuijumuisha katika ufundishaji, utafiti, ubunifu na huduma kwa jamii ili kuongeza ushindani wa kimataifa, kupanua fursa za elimu na ajira kwa vijana pamoja na kuchochea maendeleo ya kiuchumi.

Hayo yamesemwa na Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Prof. Maulilio Kipanyula wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kitaifa wa Kuimarisha Mikakati ya Umataifishaji wa Elimu ya Juu Juni 19, 2026 katika kampasi ya NM-AIST jijini Arusha, ukiwakutanisha wataalamu wa sekta ya elimu kutoka ndani na nje ya Tanzania kujadili mustakabali wa elimu ya juu nchini.

Prof. Kipanyula ameeleza kuw umataifishaji wa elimu ya juu una mchango mkubwa katika kuongeza ubora wa elimu na tafiti, kuvutia wanafunzi na wataalamu kutoka mataifa mbalimbali, kuimarisha ushirikiano wa kimataifa na kuwaandaa wahitimu wenye uwezo wa kushindana katika soko la ajira la dunia.

Aidha, aliipongeza Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kwa kuandaa mkutano huo na kutambua mchango wa Mradi wa TANZIE katika kuimarisha uwezo wa taasisi za elimu ya juu kupitia ushirikiano kati ya vyuo vikuu vya Tanzania na Ulaya.

Kwa upande wake, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Prof. William Mwegoha, amesema mkutano huo unatoa jukwaa muhimu la kujadili masuala ya sera, rasilimali fedha na ushirikiano wa kimataifa, huku ukitarajiwa kutoa mapendekezo yatakayosaidia kuimarisha utekelezaji wa agenda ya umataifishaji nchini.

Mkutano huo umeandaliwa na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kupitia Mradi wa TANZIE unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa kimataifa na kuongeza uwezo wa taasisi za elimu ya juu nchini.

Na.Alex Sonna-DODOMA

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limepongezwa kwa mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 50 tangu kuanzishwa kwake, huku likitakiwa kuendelea kwenda sambamba na maendeleo ya teknolojia na mabadiliko ya soko la dunia ili kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania kimataifa.

Pongezi hizo zimetolewa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga,wakati wa maadhimisho ya kilele cha miaka 50 ya shirika hilo yaliyofanyika katika ofisi zake zilizopo Njedengwa jijini Dodoma, sambamba na uzinduzi wa kitabu kinachoelezea historia, mafanikio na mchango wa taasisi hiyo katika kukuza ubora wa bidhaa na huduma nchini.

Waziri Kapinga amesema TBS imekuwa nguzo muhimu katika kulinda afya na usalama wa wananchi kupitia usimamizi wa viwango vya bidhaa mbalimbali, huku ikichangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa sekta za uzalishaji, biashara na viwanda nchini.

Ameeleza kuwa katika kipindi hiki ambacho dunia inaendelea kubadilika kwa kasi kupitia teknolojia na ubunifu, TBS inapaswa kuwa na dhana ya kujitegemea zaidi kwa kuimarisha mifumo ya kisasa ya utoaji huduma na kuongeza uwezo wake wa kitaalamu ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi.

"Tunapoadhimisha miaka 50 ya TBS, tunashuhudia mchango mkubwa wa taasisi hii katika kujenga imani ya bidhaa za Tanzania. Hata hivyo, ni muhimu kuendelea kuwekeza katika teknolojia, ubunifu na ushirikiano na sekta binafsi ili kuhakikisha bidhaa zetu zinakidhi viwango vya kimataifa," amesema Kapinga.

Aidha, Waziri huyo amesisitiza umuhimu wa TBS kuendelea kufanya kazi kwa karibu na sekta binafsi ili kuongeza ubora wa bidhaa zinazozalishwa nchini na kusaidia kutafsiri kwa vitendo maono ya Tanzania ya kuwa taifa lenye uchumi wa viwanda unaozalisha bidhaa zenye ushindani mkubwa katika masoko ya kikanda na kimataifa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Ashura Katunzi,amesema  maadhimisho hayo  ni fursa ya kutathmini mafanikio yaliyofikiwa na kuweka mikakati mipya ya kuifanya taasisi hiyo kuwa ya kisasa zaidi na yenye uwezo mkubwa wa kukabiliana na changamoto za karne ya 21.

Dkt. Katunzi amesema TBS itaendelea kuimarisha maabara za kisasa, kuongeza matumizi ya teknolojia za kidijitali na kuwekeza katika rasilimali watu ili kuhakikisha huduma za viwango zinakuwa bora zaidi, za haraka na zenye kuaminika.

"TBS inatambua kuwa dunia inabadilika kwa kasi kubwa, huku teknolojia na mazingira ya biashara vikibadilika, hivyo shirika hilo linapaswa kuendelea kuwa imara, bunifu na lenye uwezo wa kujibu changamoto mpya zinazoibuka."aamesema Dkt. Katunzi

Amebainisha kuwa kwa kipindi cha nusu karne, TBS imekuwa mhimili muhimu wa maendeleo ya viwanda na biashara nchini kwa kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa na kuuzwa zinazingatia viwango vinavyotakiwa, jambo ambalo limeongeza imani ya walaji na kufungua fursa za biashara katika masoko mbalimbali duniani.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, Mariam Ditopile Mzuzuri, amesema TBS imekuwa mhimili muhimu katika kulinda maslahi ya walaji, kuimarisha ushindani wa bidhaa za Tanzania na kuchochea ukuaji wa sekta za uzalishaji nchini.

 Ditopile amesema ipo haja ya kufanyika kwa mapitio ya kina ya Sera ya Ubora wa Bidhaa ili iweze kuakisi mabadiliko makubwa yaliyotokea katika nyanja za sayansi, teknolojia, biashara na uzalishaji tangu sera hiyo ilipoanzishwa.

"Tunapoipongeza TBS kwa mafanikio ya miaka 50, ni muhimu pia kuangalia mbele na kufanya maboresho yatakayoiwezesha taasisi hii kuendelea kuwa nguzo ya maendeleo ya viwanda, biashara na kilimo katika mazingira ya sasa ya kiteknolojia," amesema Ditopile.

Ditopile amesema imejijengea rekodi ya kuwa taasisi muhimu katika kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa, kuuzwa na kutumiwa nchini zinakidhi viwango vinavyotakiwa kwa ajili ya kulinda afya, usalama na maslahi ya watumiaji.

Naye Katibu Mkuu wa Shirikisho la Viwango Afrika (ARSO), Dkt. Hermogene Nsengimana, amesema Julai 2026 Tanzania itakuwa nchi ya saba barani Afrika kupata Alama ya Ubora ya Afrika (Africa Quality Mark) kwenye bidhaa zake.

Amesema kwa hatua hiyo, Tanzania itaungana na Rwanda, Togo, Senegal, Ethiopia, Nigeria na Zimbabwe katika nchi zinazotumia alama hiyo ya ubora inayolenga kuimarisha viwango vya bidhaa barani Afrika.

Amesema Shirikisho la Viwango Afrika limekwisharatibu na kuoanisha takribani viwango 2,600 vinavyolenga sekta za kipaumbele ikiwemo usindikaji wa mazao ya kilimo, sekta ya magari, dawa na bidhaa za afya, usafirishaji na ugavi, pamoja na nguo na bidhaa za ngozi.

Ameeleza kuwa kwa sasa takribani bidhaa 500 katika ngazi ya Afrika zinapitiwa ili kupata Alama ya Ubora ya Afrika, hatua itakayosaidia kurahisisha biashara ndani ya Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA).

Amesema bidhaa za Tanzania ambazo kwa sasa zinabeba alama ya TBS, zitapata fursa ya kuwekewa alama ya ubora ya Afrika, jambo litakaloongeza ushindani na upatikanaji wa masoko katika nchi mbalimbali za bara hilo.