Ripoti mpya ya kimataifa imeitaja Tanzania kushika nafasi ya tano duniani kwa kuwa kizazi cha vijana ambao hawajaathiriwa na changamoto ya afya ya akili, ikizipita nchi za Ulaya, Amerika, Asia na Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Kwa mujibu wa matokeo hayo yaliyotangazwa Washington DC kufuatia utafiti uliofanywa na taasisi ya Sapien Labs, vijana barani Afrika wameonyesha kuwa na uimara wa afya ya akili wakati dunia ikishuhudia ongezekoo kubwa la changamoto ya afya ya akili miongoni mwa vijana duniani.
Tanzania imetajwa kushika nafasi ya tano duniani huku Ghana ikishika nafasi ya kwanza kidunia, na kufuatiwa na Nigeria, Kenya, Zimbabwe, hivyo kufanya nchi zote tano za kwanza kutoka barani Afrika.
Ripoti ya Dunia ya Afya ya Akili 2025 (The Global Mind Health Report 2025) inaonesha nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara kuzipita nchi nyingi zenye kipato cha juu, huku ikionesha kuongezeka kwa tatizo la afya ya akili miongoni vijana duniani.
Utafiti huo uliotumia data zilizokusanywa kutoka watu zaidi ya milioni moja katika nchi 84 umeonyesha asilimiia 41 ya vijana walio katika umri wa utu uzima ambapo wamezama katika matumizi ya teknolojia za kidigitali, wakitegemea intaneti kwa mawasiliano, elimu, burudani na maingiliano ya kijamii (umri kati ya miaka 18-34) duniani wanakabiliwa na changamoto ya afya ya akili.
Ripoti hiyo inaonesha kuporomoka kwa uwezo wao wa ufahamu, kijamii, kushindwa kudhibiti mihemko na kupungua kwa uwezo wa kimwili ambavyo kwa kiasi kikubwa vimethiri uwezo wao wa kupambana na changamoto za maisha.
Kwa upande mwingine, ripoti hiyo inaonesha tofauti ya kikanda kwa tatizoz la afya ya akili(regional) huku baadhi ya nchi za Afrika zikiongoza kwa kupata alama za juu katika matokeo ya afya ya akili kwa vijana.
Kwa mfano, vijana waliofikia umri wa utu uzima katika eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara wameonesha kuwapita wenzao wanaoishi kwenye nchi zenye kipato cha juu zikiwemo za Amerika ya Kusini, Ulaya na sehemu za Asia.
Hadi kufikia mwanzoni mwa mwaka 2,000 kundi la umri wa vijana iliohusisha utafiti huo (miaka 18-34) lilifanya vizuri katika ustawi na hali nzuri ya afya ya akili likilinganishwa na makundi mengine ya umri.
“Leo hii hali imegeuka, vijana watu wazima wako katika hatari mara nne zaidi ya wale wenye umri wa zaidi ya miaka 55 kupata changamoto ya afya ya akili yenye kuhitaji matibabu, hali ambayo kwa kiasi kikubwa imeathiri uwezo wao kuzalisha katika maisha yao ya kila siku.” Inasema sehemu ya ripoti hiyo.
Ripoti ya Afya ya Akili Duniani 2025 imehusisha badiliko hilo na sababu kadhaa zikiwemo matumizi ya mapema ya simu za kiganjani wakati wa utoto, kuongezeka kwa matumizi ya vyakula na vinywaji vinavyotengenezwa viwandani kama vile soda, vyakula vilivyogansishwa na vinavyohifadhiwa kwenye vifunashio, kuporomoka kwa uhusiano wa karibu katika family na kutothamini mambo ya kiroho.
Sapien Labs ni taasisi isiyo ya faida iliyojikita katika kuelewa athari mabadiliko ya kasi ya kijamii, kiteknolojia, na mazingira ya kemikali katika ubongo na akilil ya mwanadamu. Mradi wao wa Global Mind Project ndio mkubwa zaidi unaofuatilia vipengele 47 ya afya ya akili na sababu nyingine za kimaisha na kimazingira katika nchi zaidi ya 85 kwa lugha 25.
Taasisi hiyo inaongozwa na wataalamu wa sayansi ya neva na mishipa ya fahamu, saikolojia na wale wa sayansi ya kompyuta katika kuchambua na kutatua masuala magumu ya kisayansi walikusanya data kupitia utafiti wa kimtandao uliofanywa Asia, Africa, Ulaya na Amerika.
“Hatari ya tatizo ya afya ya akili inaonekana kuwa endelevu kutoka kizazi hadi kizazi na linakwenda mbali zaidi ya kuongeza viwango vya juu vya mfadhaiko na wasiwasi,” alisema Prof Tara Thiagarajan, kiongozi wa waandaaji wa ripoti hiyo na mwanzilishi na mwanasayansi mkuu wa Sapien Labs.
“Tumetathimini uwezo wa aina mbali mbali ambao mtu anapaswa kuwa nao ili kukabili chanamoto za maisha na kugundua kuwa vijana wengi walio katika umri wa utu uzima wanahangaika. Pamoja na mifadhaiko na wasiwasi, mara nyingi wanakumbana na changagmoto za kudhibiti mihemko, kushughulikainjdwa kumudu uhusiano na wengine, na kupoteza uwezo wao wa kuelekeza akili zao katika jambo bila kuvuruga mawazo,”
Kwa mujibu wa utafiti huo, kufanya vizuri kwa baadhi ya nchi za Afrika kunaweza kumaanisha kuwa mambo ya kijamii na kifamilia yanayokuza uimara na ustawi na kupunguza athari mbayakama vile msongo wa mawazo au sababu hatarishi vinaweza kuwa vinachangia vizuri kwenye matokeo hayo.
Matokeo ya utafiti huo yanaonesha pia kuwa vijana walio katika umri wa utu uzima Kusini mwa Jangwa la Sahara wameripotiwa kuwa na uimara wa kiroho, kuchelewa kuanza matumizi ya simu za kiganjani wakati wa utoto na kuwa na uhusiano wa karibu wa kifamilia ukilinganisha na wenzao katika nchi tajiri.
Tanzania, kwa mfano, imeshika nafasi ya juu kabisa kidunia katika kipimo cha mambo ya kiroho na ndio yenye wastani wa juu wa umri wa watu waliochelewa kuanza matumizi ya simu za kiganjani licha ya kushuka kutoka nafasi ya kwanza mwaka jana hadi ya tano mwaka huu. Kenya na Nigeria pia miongoni mwa nchi ilizoshika nafasi ya juu kidunia, huku Kenya ikionesha kufanya vizuri zaidi ikilinganishwa na miaka iliyopita.
Licha ya tofauti za kikanda, tofauti ya afya ya akili kati ya wazee na vijana imeendelea duniani kote, huku wazee wakionesha kuwa na afya imara zaidi ya akili kuliko idadi ya vijana.
Utafiti uliotangulia wa Sapien Labs ulionesha kuwa tofauti hiyo ilianza kukua kabla ya mwaka 2020 na kuongezeka kwa kiasi kikubwa wakati wa janga la UVIKO-19 2020 na 2021, wakati ambao afya ya akili ya vijana wenye umri wa utu uzima (miaka kati ya 18 na 34) ilishuka kwa kasi, huku vizazi vya umri mkubwa vikiathirika kwa kiasi kidogo tu.
“Kwa miaka mitano iliyopita, tofauti hii kwa kiasi kikubwa haijabadilika,” alisema
Dr Thiagarajan, na kuongeza kuwa waandaaji wa sera wanapaswa kutazama kwa karibu athari pana za kiuchumi za kuongezeka kwa vijana wanaoingia katiika kundi la nguvukazi wakiwa na afya dhaifu ya akili,” alisema.
Huku ikigusia sababu nyinginje nyingi za kushuka kwa afya ya akili, ripoti hiyo inabainisha sababu nne za msingi zinazochangia changamoto ya afya ya akili kwa vijana duniani. Imezitaja sababu hizo kuwa ni pamoja na matumizi ya mapema ya simu wakati wa utoto, ongezeko la vyakula vya viwandani, kupunggua uhusiano wa kifamilia na kutojali mambo ya kiroho. Kila moja ya sababu hizi inahusishwa na ongezeko la hatari matatizo ya afya ya akili na kupungua kwa uwezo wa vijana kuyakabili mahitaji ya maisha.“
Nchini Marekani, matumizi ya fedha kwa ajili ya utafiti wa afya ya akili na uangalizi yameongezeka sana kwa mabilioni ya dola, kama ilivyo kwa nchi za mashariki.
Na wakati hilo ni muhimu, halileti mabadiliko ya kuonekana,” alisema. “tuhahitaji kuacha kupambana na dalili na badala yake kupambana na matatizo makubwa zaidi yanayoathiri uzalishaji na ustawi wa vijana duniani. Kwa mfano, hatua za kisera zinazodhibiti upatikanaji wa simu za kiganjani kwa watoto na matumizi ya vyakula vya viwandani vinasaidia kulinda afya ya akili ya kizazi cha vijana---bila hivyo, uchumi wa dunia utatapatapa kwa miongo kadhaa ijayo.”
Ripoti hiyo pia imabainisha hatua mahususi za kisera zinazoweza kupunguza madhara, hasa madhara yanayosababishwa na matumizi ya mapema ya simu za kianjani kuongezeka kwa matumiizi ya vyakula vitokavyo viwandani. Kwa masuala yanayohusishwa na simu za kiganjani, ripoti hiyo imeshauri utungwaji wa sera zinazozuia matumizi yake wakati wa muda wa masomo na kuanzishwa kwa sharti la kuweka umri maalumu wa kutumia mitandao ya kijamii.
Kuhusu vyakuka vinanvyoandaliwa viwandani, ripoti hiyo imetaka kuwepo kwa uwekezaji mpya katiika tafiti ambazo zinaweza kufichua hatari zinahusishwa na aina mbali mbali za rangi, vikolezo, dawa za kuzuia vyakula visioze na vitu vinavyotumika kugandisha vyakula pamoja na viungio vingine vinavyopatikana kwenye vyakula—na kuleta ushahidi utakaounga mkono uanzishwaji wa kanuni za kupunguza matumizi yake.
“Wakati ripoti hii si ya kwanza kuhusisha vitu hivi na changamoto za afya ya akili, upana na kina cha data ilizofanyiwa kazi na Global Minds zitasimama kuonesha ukubwaa wa matatizo vinayosababisha,” alisema Prof David Blachflower, profesa wa uchumi katika Chuo cha Dartouth. “Kwa sababu pale unapoona ushahidi kuwa karibu nusu ya vijana wote duniani---moyo wa nguvukazi---wanapambana na mlolongo wa chanamoto za afya ya akili, hii ina maana tunakabiliwa na hatari inayoweza kudhoofisha afya ya uchumi wote na jamii. Ni kiashiria cha wazi kuwa tunahitaji kuchukua hatua kushughulikia mzizi wa tatizo.”
KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi.Mwajabu Nyamkomora,akizungumza wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.
Na.Alex Sonna,Mzalendo blog -DODOMA
KATIBU Tawala Msaidizi Mkoa wa Dodoma, Mwajabu Nyamkomora, amesema uwajibikaji na uaminifu ni miongoni mwa misingi muhimu inayochochea biashara endelevu na kukuza uchumi wa wananchi.
Bi.Nyamkomora ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara kuhusu shughuli za Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.
Amesisitiza kuwa wadau wa biashara wanapaswa kuzingatia maadili hayo ili kujenga mazingira bora ya ushindani wa haki sokoni, hatua itakayoongeza imani kwa wawekezaji na kuimarisha ustawi wa uchumi.
“Biashara endelevu inahitaji uwajibikaji na uaminifu. Bila misingi hiyo, ni vigumu kujenga soko lenye ushindani wa haki na linalomnufaisha mlaji,” amesema Bi. Nyamkomora.
Aidha ameeleza kuwa mafunzo hayo yanalenga kuongeza uelewa wa wadau kuhusu majukumu ya Baraza hilo pamoja na namna ya kulifikia kwa urahisi wanapokumbana na changamoto za kibiashara.
Kwa mujibu wake, elimu hiyo itawasaidia washiriki kutambua njia sahihi za kutatua migogoro inayohusiana na ushindani wa kibiashara na masuala ya udhibiti wa soko, jambo litakalosaidia kuimarisha biashara na kuongeza ufanisi katika shughuli za kiuchumi.
“Kupitia semina hii, kama sekta na wadau wetu muhimu tunaendelea kuimarisha mshikamano, kubadilishana uzoefu na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yetu,” ameongeza.
Hata hivyo amewataka wadau kujikita katika misingi ya uwajibikaji na uaminifu ili kuvutia uwekezaji unaoendana na kasi ya maendeleo ya Serikali chini ya uongozi wa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.
Bi.Nyamkomora amebainisha kuwa Ofisi ya Mkoa itaendelea kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Viwanda na Biashara kupitia Baraza la Ushindani kwa kutoa ushirikiano wa kutosha utakaowezesha utekelezaji wa majukumu ya taasisi hiyo, kwa lengo la kuboresha mazingira ya biashara na kukuza ustawi wa wananchi.
Kwa upande wake, Msajili wa Baraza la Ushindani, Mbegu Kaskasi, amesema kuwa mafunzo hayo ni sehemu ya mkakati wa Baraza kutoa elimu kwa wadau kufuatia maelekezo ya Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga, ya kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu majukumu ya taasisi hiyo.
Naye Mkuu wa Idara ya Uchumi wa FCT, Kulwa Msogoti, ameeleza kuwa Baraza hilo ni chombo cha kisheria kinachosikiliza rufaa za ushindani na kulinda maslahi ya wafanyabiashara pamoja na watumiaji wa bidhaa na huduma, kwa lengo la kujenga uchumi shindani na jumuishi nchini.
Nao Baadhi ya washiriki wa semina hiyo wamesema kuwa mafunzo hayo yamewapa mwanga kuhusu namna ya kufuata taratibu sahihi za kisheria wanapokumbana na changamoto za ushindani au wanaporidhika na maamuzi ya mamlaka za udhibiti.
Semina hiyo ni sehemu ya mkakati wa Baraza la Ushindani wa kuwafikia wadau katika mikoa mbalimbali nchini ili kuongeza uelewa wa sheria za ushindani na kuimarisha utatuzi wa migogoro kwa njia ya kisheria.

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akizungumza wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akizungumza wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akizungumza wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akizungumza wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

MSAJILI wa Baraza la Ushindani (FCT), Mbegu Kaskasi,akizungumza wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

SEHEMU ya washiriki wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora (hayupo pichani) wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

SEHEMU ya washiriki wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora (hayupo pichani) wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.


SEHEMU ya washiriki wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora (hayupo pichani) wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

MKUU wa Idara ya Uchumi FC Bw.Kulwa Msogoti,akiwasilisha mada wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

MKUU wa Idara ya Uchumi FC Bw.Kulwa Msogoti,akiwasilisha mada wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

MKUU wa Idara ya Sheria FCT Bw.Kunda Mkenda,akiwasilisha mada kuhusu Sheria wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

AFISA TEHAMA FCT Athuman Kanyegezi,akiwasilisha mada kuhusu TEHAMA wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

WADAU mbalimbali wakichangia mada na kutoa ushauri wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akiwa katika picha ya pamoja na washiriki mara baada ya kufungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma .

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akiwa katika picha ya pamoja na washiriki mara baada ya kufungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma .

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akiwa katika picha ya pamoja na washiriki mara baada ya kufungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma .

Serikali imejipanga kupeleka fedha kwenye miradi mbalimbali ya kimkakati ili wananchi waendelee kufaidika, ikiwemo kupata ajira katika sekta binafsi na serikalini.
Akizungumza Februari 26, 2026 wakati alipotembelea mradi wa ujenzi wa barabara ya Ntendo – Kizungu wenye urefu wa kilomita 25 kwa kiwango cha lami mkoani Rukwa, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu, amesema kuwa fedha zinazotolewa na Serikali zinalenga kuwanufaisha wananchi moja kwa moja kupitia fursa za ajira na kukuza kipato.
Ziara hiyo ni sehemu ya mwendelezo wa ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Rukwa, ambapo Waziri Sangu alisisitiza kuwa dhamira ya Serikali ni kuhakikisha uwekezaji unaofanyika unaleta tija kwa wananchi wa maeneo husika.
Aidha, ametoa wito kwa mkandarasi wa mradi huo, China Geo Engineering Ltd, kuhakikisha kuwa ajira zinazohitaji wazawa zinatolewa kwa kipaumbele kwa wananchi wanaozunguka mradi huo ili waweze kunufaika moja kwa moja na utekelezaji wake.
Waziri Sangu amesema kuwa lengo la Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kujenga uchumi imara, shindani na jumuishi unaowagusa wananchi wote.
“Tunaposema uchumi jumuishi ni kwamba fedha zinazokuja kwa wananchi ziweze kuzalisha ajira kwa wananchi wazawa,” amesema Waziri Sangu.
Katika hatua nyingine, ameitaka kampuni hiyo kuzingatia Sheria za Kazi katika utoaji wa ajira, ikiwemo kuhakikisha wafanyakazi wanaostahili wanapelekewa michango yao katika Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) pamoja na michango ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) kwa mujibu wa sheria.
Kaimu Meneja Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Rukwa Mhandisi Joseph Gimonge, amesema kuwa utekelezaji wa mradi unaendelea vizuri ambapo hadi sasa ujenzi umefikia asilimia 53.37.
Akizungumza kuhusu maendeleo ya mradi huo, Mha. Gimonge alieleza kuwa kazi zinaendelea kulingana na mpango uliopangwa, ambapo kwa hatua zilizofikiwa zinaendelea vizuri kulingana na maendeleo ya mradi.
Kwa upande wao, wananchi wa Kata ya Muze, Kijiji cha Kizungu, wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kupeleka fedha za ujenzi wa barabara hiyo katika awamu ya kwanza. Wamesema mradi huo umekuwa na manufaa makubwa kwao kwani umechangia kupatikana kwa ajira kwa wakazi wa eneo hilo pamoja na kukuza kipato chao.
Wananchi hao wameeleza kuwa kukamilika kwa barabara hiyo kutarahisisha usafirishaji na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika eneo lao.
Na. Benny Mwaipaja, Dar es Salaam
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amesema kuwa Tanzania iko tayari kushirikiana na kubadilishana uzoefu na nchi ya Qatar kukuza sekta ya fedha pamoja na utafiti, uchimbaji na uendelezaji wa gesi asilia ili sekta hizo ziweze kuchangia zaidi ukuaji wa uchumi wa nchi.
Mhe. Balozi Omar amesema hayo katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, Jijini Dar es Salaam, baada ya kupokea ujumbe maalumu kutoka nchi hiyo na kufanya mazungumzo na Balozi wa Qatar nchini Tanzania, Mhe. Fahad Rashid Al-Marekhi.
Alisema kuwa Qatar ina uzoefu mkubwa katika sekta ya utafutaji, uchimbaji na uendelezaji wa gesi asilia eneo ambalo Tanzania inaweza kujengewa uwezo zaidi.
“Tunafahamu kuwa Tanzania tumegundua gesi asilia na tayari kuna maeneo ambayo tunaendelea kuichimba na kuitumia kwa hiyo tunaweza kubadilishana uzoefu katika eneo la utafutaji na namna walivyoweza kuiendeleza kwa sababu bado tunaamini kuna maeneo makubwa kwa upande wa Jamhuri yetu hatujafanya utafiti wa kutosha na ambayo yana fursa ya kufanya ugunduzi mkubwa zaidi” alisema Mhe. Balozi Omar
Kuhusu sekta ya fedha, Mhe. Balozi Omar alisema kuwa Qatar ni Kituo kikubwa cha Fedha (financial Center) katika nchi za Ghuba ya Uajemi, na kwamba Tanzania inaweza kufaidika na uwepo wa kituo kama hicho na kuwezesha kuyafikia masoko ya mitaji.
📌Yasema mradi umesimamiwa na kutekelezwa kwa ufanisi
📌Yasisitiza ni kichocheo muhimu katika za fursa za kiuchumi na kijamii
Kamati ya Uongozi wa Mradi wa Bwawa la Julius Nyerere (JNHPP), tarehe 26 Februari 2026, imekagua maendeleo ya uzalishaji wa umeme katika mradi huo na kueleza kuridhishwa na usimamizi pamoja na utekelezaji wake, uliokidhi viwango vya ubora vinavyoendana na thamani ya fedha iliyowekezwa na Serikali.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, ambaye pia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Dkt. Jim Yonazi , amesema kamati imefurahishwa na namna bwawa hilo linavyochochea ukuaji wa uchumi kwa kuongeza uzalishaji wa umeme unaosambazwa katika maeneo mbalimbali nchini, hatua inayochangia kuimarika kwa upatikanaji wa nishati ya umeme.
“Tumeridhishwa na jinsi mradi huu ulivyosimamiwa na kutekelezwa kwa ufanisi mkubwa.
Ukilinganisha na miradi mingine barani Afrika, mradi huu umejengwa kwa ubora wa hali ya juu na umeleta unafuu katika huduma ya umeme nchini. Haya ni mafanikio makubwa kwa Taifa,” alieleza Dkt. Yonazi.
Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Bw. Petro Lyatuu, amesema mradi huo umekamilika kwa asilimia 100 na mchango wake tayari umeanza kuonekana.
Amefafanua kuwa mwaka 2021, gridi ya taifa ilikuwa na jumla ya megawati 1,600, lakini kwa sasa uwezo wa uzalishaji umefikia zaidi ya megawati 4,000, zaidi ya mara mbili ya kiwango cha awali.
“Kwa sasa bwawa linazalisha umeme na tija yake imeonekana wazi. Kuongezeka kwa uzalishaji kumeimarisha gridi ya taifa na tunaendelea kuongeza nguvu katika sekta ya nishati kwa ajili ya maendeleo ya nchi na ustawi wa wananchi,” alisisitiza Bw. Lyatuu.
Aidha kwa hatua nyingine Kamati hiyo ilitembelea kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Chalinze, kinachopokea umeme kutoka Bwawa la Julius Nyerere na kusambaza katika maeneo mbalimbali ya nchi.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Naibu Mkurugenzi Mtendaji Uzalishaji, Mhandisi Antony Mbushi, amesema kituo hicho kimekamilika na tayari kinafanya kazi.
Ameongeza kuwa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Chalinze hadi Dodoma umefikia asilimia 71.58, huku mradi wa kusafirisha umeme kutoka Chalinze kupitia Kinyerezi hadi Mkuranga umefikia asilimia 59.76.
‘’Kamati imeridhishwa na maendeleo ya miradi hiyo na kusisitiza kuwa mpango uliopo ni kuendelea kuongeza uzalishaji ili kuhakikisha nishati ya umeme inakuwa ya uhakika na endelevu’,’Aliongeza Mha. Mbushi
Katika hitimisho la ziara hiyo, Kamati imeeleza kuwa utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya umeme unaifanya Tanzania kuwa kivutio cha uwekezaji na kitovu cha usambazaji wa umeme katika ukanda wa Afrika Mashariki, Kati na Kusini.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amesema Mashujaa wa Vita ya Majimaji wanapaswa kuenziwa kwa kuimarisha nidhamu ya utendaji kazi, kupinga masuala ya ukabila na kutambua wajibu wa pekee wa kulitetea na kulipigania Taifa.
Makamu wa Rais amesema hayo, wakati wa kilele cha Tamasha la 17 la Kumbukizi ya Miaka 120 ya Mashujaa wa Vita ya Majimaji, lililofanyika katika Viwanja vya Makumbusho ya Vita ya Majimaji, Songea mkoani Ruvuma. Amesema ni muhimu kuwaenzi mashujaa hao kwa kuendelea kusimamia umoja ili kuhakikisha makabila yote yanakuwa Taifa moja, kufanya kazi kwa bidii kuijenga Nchi, pamoja na kupinga vitendo vya rushwa na kutenda haki.
Ameongeza kwamba, Mashujaa wa Vita ya Majimaji waliweka pembeni ubinafsi kwa kuunganisha makabila zaidi ya 30 ili kuweza kupambana na wakoloni na hivyo kutengeneza mustkabali mzuri wa maisha ya sasa.
Makamu wa Rais, amesema kumbukizi ya Mashujaa wa Vita vya Majimaji ni muhimu katika kuwezesha kizazi cha sasa na kijacho, kuona na kujifunza jinsi ambavyo mashujaa hao walivyojitolea maisha yao katika kulinda heshima, utu na rasilimali za Taifa.
Aidha, Makamu wa Rais ametoa wito kwa jamii kushirikiana na Shirika la Makumbusho ya Taifa kuanzisha Makumbusho katika maeneo yao ili kuendelea kuhifadhi historia nzuri ya Taifa, pamoja na kutumia fursa mbalimbali zinazopatikana kwenye Malikale zilizopo nchini ikiwemo kuinua uchumi kupitia utalii wa utamaduni.
Amesema maboresho makubwa yaliyofanywa na Wizara ya Maliasili na Utalii katika Sheria ya Malikale, Sura 333 na Sheria ya Makumbusho ya Taifa, Sura 281, yametoa fursa kwa jamii kuanzisha Makumbusho.
Pia, ametoa wito kwa Taasisi binafsi na jamii kwa ujumla, kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii katika kuwekeza na kutumia kumbukumbu zilizopo nchini, kama chanzo cha ajira na majukwaa ya kutangaza bidhaa na vivutio vya uwekezaji na utalii.
Katika hatua nyingine, Makamu wa Rais amesema Serikali inatambua umuhimu wa barabara ya Songea – Makambako na inatarajia kuanza ujenzi wa awamu ya kwanza barabara hiyo hivi karibuni kwa kuwa tayari mkandarasi amepatikana.
Awali, Makamu wa Rais alishiriki tukio la uwekaji wa silaha za jadi katika mnara wa kumbukumbu ya Mashujaa wa Vita ya Majimaji pamoja na kuweka shada la maua katika makaburi waliozikwa mashujaa hao.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Makambusho ya Taifa Dkt. Noel Lwoga, amesema pamoja na kufanya kumbukizi ya kuwaenzi Mashujaa wa Vita ya Majimaji, lakini pia malengo mengine ni kurithisha urithi wa historia , mila na desturi kwa kizazi cha sasa na baadaye, kuibua na kuendeleza fursa za utalii na uchumi zinazotokana na historia na utamaduni pamoja na kuelimisha umma wa Watanzania umuhimu wa kutunza na kuhifadhi urithi wa Taifa.
Makumbusho ya Vita vya Majimaji yalianzishwa mwaka 1980 chini ya Ofisi ya Mkoa wa Ruvuma na Baraza la Makumbusho ya Majimaji, Mila na Desturi, na baadaye kupandishwa hadhi na kuwa Makumbusho ya Taifa ya Vita vya Majimaji mwaka 2009.
Tamasha la 17 la Kumbukizi ya Miaka 120 ya Vita vya Majimaji limebeba kaulimbiu isemayo “Utamaduni wetu ndiyo nguvu yetu kwa maendeleo ya utalii na uchumi” ambapo limewashirikisha Viongozi, Wananchi, wadau mbalimbali wa utalii na utamaduni na Viongozi wa Kimila kutoka Tanzania, Zambia, Msumbiji, Malawi, na Afrika Kusini.




.jpg)

























