Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema ujenzi wa Kiwanda cha Kutengeneza Nguzo za Zege cha TCPM Tabora kinachomilikiwa na Shirika la Umeme Tanzania - TANESCO kupitia kampuni tanzu ya TCPM haukusudii kuathiri wala kudhoofisha uwekezaji wa sekta binafsi bali unaongeza uzalishaji wa nguzo za zege ili kukidhi mahitaji yaliyopo ambayo bado hayajatosheleza uhitaji wa nguzo hizo nchini.

Ameeleza hayo Februari 15, 2026 wakati akikagua mradi wa ujenzi wa Kiwanda cha Kutengeneza Nguzo za Zege cha TCPM Tabora, ambao umefikia asilimia 95 ya utekelezaji. Kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha wastani wa nguzo za zege 120 kwa siku.

“Kiwanda hiki si tishio kwa sekta binafsi; kinakuja kuongeza nguvu katika kazi ambazo tayari zilikuwa zinafanywa na sekta binafsi ya kuzalisha nguzo za zege,” amesema Ndejembi.

Ndejembi amefafanua kuwa TANESCO kwa mwaka 2025 ilikuwa na uhitaji wa nguzo za zege 80,000, lakini zilizopatikana kupitia sekta binafsi ni nguzo 40,000 jambo lililosababisha kutokufikiwa kwa malengo ya mahitaji hayo.

Ameeleza kuwa pamoja na Serikali kujenga kiwanda hicho, bado kuna fursa kwa sekta binafsi kuwekeza katika viwanda vya nguzo za umeme kutokana na mpango wa TANESCO wa kuendelea kufanya maboresho kwa kuondoa nguzo za miti na kutumia nguzo za zege katika usambazaji wa umeme nchini.

Aidha, Ndejembi ameitaka Bodi na Menejimenti ya TANESCO kusimamia kikamilifu ukamilishaji wa kiwanda hicho ili mitambo itakapowashwa iweze kufanya kazi kwa ufanisi na ubora kulingana na mpango na malengo ya Kiwanda hicho.

Kadhalika, amewataka wafanyakazi waliopata ajira na watakaoajiriwa kutunza miundombinu na mitambo ya kiwanda hicho pamoja na kuweka mpango madhubuti na endelevu wa uendeshaji ili kuepusha hasara zinazoweza kujitokeza.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Lazaro Twange amesema utekelezaji wa mradi wa kiwanda hicho cha nguzo za zege, kinachomilikiwa na Serikali kwa asilimia 100, hadi kukamilika kwake utagharimu Shilingi bilioni 7.9.

Twange ameeleza kuwa ujenzi wa kiwanda hicho upo katika hatua za mwisho za ukamilishaji, ambapo kufikia tarehe 20 Februari 2026 mkandarasi atakuwa amekamilisha kazi zote, tayari kwa kuanza uzalishaji.











 Kaimu Mkurugenzi Mkuu FCC Bi. Khadija Ngasongwa,akitoa maelezo namna FCC inavyoshirikiana na wafanyabiashara wa sekta ya usafirishaji wa mizigo (logistics) katika kuongeza thamani kwenye biashara, ushindani na uwekezaji nchini Tanzania wakati wa kongamano la kimataifa la biashara na sekta ya usafirishaji wa mizigo (Tanzania Trade & Logistics Forum) liliofanyika Februari 13 - 14, 2026 katika Hoteli ya Shangri-La, Dubai, UAE

📍 Dubai, UAE

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo, pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa, wameshiriki kimkakati katika Kongamano la Kimataifa la Biashara na Sekta ya Usafirishaji wa Mizigo (Logistics) lililofanyika jijini Dubai, Falme za Kiarabu.

Lengo la kongamano hilo ni kuimarisha ushirikiano wa kibiashara na kuongeza fursa za biashara kati ya Tanzania na Falme za Kiarabu, sambamba na kufungua masoko mapya kwa bidhaa na huduma za Tanzania.
Akizungumza katika kongamano hilo kama mgeni rasmi, Mhe. Dennis Londo alisisitiza umuhimu wa kuimarisha miundombinu ya usafirishaji  ili kuongeza ufanisi katika upanuzi wa masoko, kukuza mauzo ya nje, na kujenga ushirikiano wa kimataifa wenye tija kwa Taifa.
Kwa upande wake,Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC Bi. Khadija Ngasongwa, alisema kuwa Tume ya Ushindani inaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali za kukuza biashara kwa kasi na ufanisi. Alieleza kuwa sekta ya usafirishaji wa mizigo ni mhimili muhimu katika kuongeza thamani kwenye biashara na uwekezaji nchini.
“Tutaendelea kuimarisha mifumo ya usimamizi wa ushindani sokoni ili kuchochea ukuaji wa biashara na kuitangaza Tanzania kama kitovu cha biashara na huduma za usafirishaji katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati,” alisisitiza.
Kongamano hilo limejumuisha Taasisi za Serikali, wawekezaji na watoa huduma wa Tanzania ambapo washiriki wamepata fursa ya kujadiliana na kubadilishana uzoefu juu ya fursa za biashara na uwekezaji katika sekta ya usafirishaji. 
Waandaaji wa kongamano hilo ni TANFORD, jukwaa linalowaunganisha wamiliki wa kampuni za Kitanzania zinazojihusisha na mizigo na usafirishaji wanaofanya shughuli zao Dubai na katika masoko ya kimataifa.
Kongamano hilo limefanyika tarehe 13 - 14 Februari, 2026 katika Hoteli ya Shangri-La, Dubai, UAE ikiwa ni sehemu ya jitihada za pamoja za serikali na sekta binafsi katika kulinda na kukuza maslahi ya Taifa katika biashara Duniani.

 Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dennis Londo (Mb),akizungumza na wafanyabiashara na wadau wa sekta ya usafirishaji (logistics) wakati wa kongamano la kimataifa la biashara na sekta ya usafirishaji wa mizigo (Tanzania Trade & Logistics Forum) Februari 13, 2026 katika Hoteli ya Shangri-La, Dubai, UAE.

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu FCC Bi. Khadija Ngasongwa,akitoa maelezo namna FCC inavyoshirikiana na wafanyabiashara wa sekta ya usafirishaji wa mizigo (logistics) katika kuongeza thamani kwenye biashara, ushindani na uwekezaji nchini Tanzania wakati wa kongamano la kimataifa la biashara na sekta ya usafirishaji wa mizigo (Tanzania Trade & Logistics Forum) liliofanyika Februari 13 - 14, 2026 katika Hoteli ya Shangri-La, Dubai, UAE

Baadhi ya washiriki wakifuatilia kwa makini kongamano la kimataifa la biashara na sekta ya usafirishaji wa mizigo (Tanzania Trade & Logistics Forum) lililofanyila Februari 13 - 14, 2026 katika Hoteli ya Shangri-La, Dubai, UAE

Baadhi ya washiriki wakifuatilia kwa makini kongamano la kimataifa la biashara na sekta ya usafirishaji wa mizigo (Tanzania Trade & Logistics Forum) lililofanyila Februari 13 - 14, 2026 katika Hoteli ya Shangri-La, Dubai, UAE

Baadhi ya washiriki wakifuatilia kwa makini kongamano la kimataifa la biashara na sekta ya usafirishaji wa mizigo (Tanzania Trade & Logistics Forum) lililofanyila Februari 13 - 14, 2026 katika Hoteli ya Shangri-La, Dubai, UAE

Kaimu Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Barabara Mhandisi Rashid Kalimbaga akimuelekeza jambo Meneja wa TANROADS Iringa Mhandisi Yudas Msangi (alieshika karatasi), wakati wa ziara ya ukaguzi wa barabara ya Iringa-Mtera. Kulia kwa Msangi ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Barabara Mhandisi Mussa Natty na Kaimu Mkurugenzi Huduma za Matengenezo wa Bodi Mhandisi Jacob Mukasa.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Taasisi isiyo ya kiserikali, Kaya Foundation, imekabidhi msaada wa viti mwendo vitano vilivyotolewa na Ubalozi wa Ufaransa nchini Tanzania, pamoja na bima za afya kwa watoto wenye changamoto ya ulemavu, hatua inayolenga kupunguza vikwazo katika makuzi na elimu yao.

 


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema wilaya za Urambo na Kaliua mkoani Tabora zipo tayari kwa uwekezaji, hususan wa viwanda kwani umeme unaozalishwa katika Kituo cha Kupoza na Kusambaza Umeme Urambo unatosheleza na hata kuzidi mahitaji ya sasa.

Amesema hayo leo, tarehe 14 Februari 2026, wakati akikagua mradi wa njia ya kusafirisha umeme msongo wa Kilovoti 132 kutoka Tabora hadi Urambo na Kituo cha Kupoza na Kusambaza Umeme cha Uhuru - Urambo cha Megawati 24.

“Urambo ipo tayari kwa uwekezaji. Uwezo wa kituo cha Urambo ni megawati 24, lakini matumizi ya wilaya mbili za Kaliua na Urambo ni megawati 2.5 wakati wa mchana na wakati wa usiku ambacho ni kipindi watu wengi wanakuwa majumbani, kiwango cha juu cha matumizi ni megawati 7,” amesisitiza Ndejembi.

Ndejembi amesema lengo na dhamira ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha kunakuwa na nishati ya umeme ya uhakika ili kuendelea kuchochea uwekezaji katika maeneo yote nchini, kwani nishati ya umeme ni kichocheo cha sekta zote.

Amesema wilaya za Urambo na Kaliua zimejikita zaidi katika kilimo hususan zao la Tumbaku, zao ambalo linahitaji kuongezewa thamani kupitia viwanda vilivyokuwa vinahitaji umeme wa uhakika.

Aidha, Ndejembi amesisitiza kuwa Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, tayari ametoa zaidi ya trilioni 1.9 kwa Wizara ya Nishati kupitia TANESCO kwa ajili ya Mradi wa Gridi Imara kujenga vituo vya kupoza na njia za kusafirisha umeme wa kutosha na wa uhakika katika maeneo mbalimbali nchini.

Kadhalika, Mhe. Ndejembi amemshukuru Mbunge wa Jimbo la Urambo, Magreth Sitta ambaye alitoa eneo la hekari 20 lililotumika kujenga Kituo hicho cha Kupooza Umeme.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Lazaro Twange, amesema mradi wa ujenzi wa Kituo cha Kupoza na Kusambaza Umeme Urambo ulianza kutekelezwa Septemba 2021 kwa gharama ya shilingi bilioni 44. Kati ya hizo, bilioni 24 zilitumika kujenga njia ya kusafirisha umeme, bilioni 16 zimejenga kituo cha kupoza  na bilioni 4 ilitumika kufidia wananchi waliopitwa na mradi.

Twange amesema kituo hicho kilianza kufanya kazi mwezi Machi 2025, ambapo ujenzi wa njia ya umeme pamoja na kituo cha kupokea na kupooza umeme vyote vimekamalika kwa asilimia 100.












Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Barabara Mhandisi Mussa Natty, akimuelekeza jambo Mkurugenzi wa Matengenezo ya Barabara TANROADS Mhandisi Dkt. Christina Kayoza wakati wa ziara ya ukaguzi wa barabara ya Dodoma hadi Mtera km 140.6 uliofanywa na Bodi ya Mfuko wa Barabara. Kulia ni Neema Mhondo Mjumbe wa Bodi hiyo.

 0J4A0321.JPG

2_2.jpg
Mshikamano wa viongozi wa sekta ya afya umeelezwa kuwa nyenzo muhimu katika kuongeza ufanisi wa usimamizi na ufuatiliaji wa huduma za chanjo, hatua inayolenga kuhakikisha kila mtoto anayestahili anapata chanjo kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.

Kauli hiyo imetolewa   tarehe 13,Februari 2026 Mkoani Tabora wakati kufunga  Mafunzo ya Wasimamizi wa Ngazi ya Kati (MLM)  ambapo viongozi walisisitizwa kuimarisha uratibu, usimamizi na matumizi ya takwimu katika kufuatilia utekelezaji wa huduma za chanjo kuanzia ngazi ya Mkoa hadi Halmashauri.

Akizungumza   wakati wa kufunga mafunzo hayo, Mratibu wa Chanjo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Dkt. Florian Tinuga, amesisitiza kuwa uhamasishaji kupitia mikutano ya vijiji na mitaa pamoja na elimu inayotolewa na Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii (CHW) ni nyenzo muhimu ya kuongeza mwitikio wa jamii kuhusu chanjo.

Aidha, ameeleza kuwa usimamizi madhubuti wa mnyororo baridi (cold chain) na matumizi sahihi ya takwimu katika kupanga na kufuatilia huduma ni hatua muhimu za kuboresha ubora na ufanisi wa chanjo.

Kwa upande wake, Simon Nzilibili kutoka Wizara ya Afya amehimiza viongozi kuendelea kuunganisha nguvu, kuimarisha uwajibikaji na kufanya ufuatiliaji wa karibu wa utekelezaji wa shughuli za chanjo katika maeneo yao.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora amepongeza mafunzo hayo, akisisitiza umuhimu wa kuweka kipaumbele katika bajeti za chanjo na kuimarisha rasilimali ili kuhakikisha usimamizi na ufuatiliaji wa huduma hizo unakuwa endelevu na wenye tija kwa jamii.

 "Uhamasishaji kupitia mikutano ya vijiji na mitaa pamoja na elimu kupitia redio za kijamii, Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii (CHW) ni nyenzo muhimu ya kuongeza mwitikio wa jamii kuhusu chanjo"amesema.

Aidha, ameeleza kuwa usimamizi madhubuti wa mnyororo baridi (cold chain) na matumizi sahihi ya takwimu katika kupanga na kufuatilia huduma ni hatua muhimu za kuboresha ubora na ufanisi wa chanjo.

Kwa upande wake, Simon Nzilibili kutoka Wizara ya Afya amehimiza viongozi kuendelea kuunganisha nguvu, kuimarisha uwajibikaji na kufanya ufuatiliaji wa karibu wa utekelezaji wa shughuli za chanjo katika maeneo yao.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Honoratha Rutanisibwa  amepongeza mafunzo hayo, akisisitiza umuhimu wa kuweka kipaumbele katika bajeti za chanjo na kuimarisha rasilimali ili kuhakikisha usimamizi na ufuatiliaji wa huduma hizo unakuwa endelevu na wenye tija kwa jamii.
2_7.jpg

KIGOMA

Baraza la Ushindani(FCT), moja ya taasisi zilizo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara, imeendesha kikao cha kuwajengea uwezo watumiaji wa huduma, wadau na wafanyabiashara wa Mkoa wa Kigoma kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu haki za ushindani na taratibu za rufaa.

Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa Lake Tanganyika Hotel na kuhudhuriwa na wadau kutoka sekta mbalimbali za biashara na huduma.

Akifungua kikao hicho, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma, Ndg. Deogratias Sangu, aliwataka wananchi kutumia elimu waliyoipata kuelewa haki zao katika ushindani na udhibiti wa soko. Alisema uelewa wa sheria na taratibu za ushindani utasaidia kupunguza migogoro isiyo ya lazima, kuimarisha uwajibikaji wa taasisi na kujenga mazingira ya Soko yenye usawa na haki.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa FCT, Mhe. Jaji Rose Ally Ebrahim, alisema Baraza lina jukumu la kusikiliza na kuamua rufaa zinazotokana na maamuzi ya Fair Competition Commission (FCC) pamoja na mamlaka za udhibiti wa sekta mbalimbali ikiwemo LATRA, EWURA, TCRA, TCAA na PURA.

Aliwahimiza wananchi wa Kigoma kulitumia Baraza hilo wanapokuwa hawajaridhishwa na maamuzi ya vyombo husika, akisisitiza kuwa mfumo wa rufaa umewekwa kisheria ili kuhakikisha haki inapatikana kwa wakati na kwa uwazi.

“Watu wakijua wapi pa kupata haki, wanapunguza gharama za kuhangaika kutoka sehemu moja ya huduma hadi nyingine,” alisema Mhe. Jaji Ebrahim, akisisitiza kuwa elimu ya sheria ni nyenzo muhimu ya kuwawezesha wananchi na wafanyabiashara kukua kiuchumi.

Wadau waliohudhuria kikao hicho waliishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuendelea kuimarisha taasisi zinazolinda na kusimamia haki za wafanyabiashara na watumiaji wa huduma.

Walisema juhudi hizo zinaonyesha dhamira ya Serikali ya kuwawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika uchumi kupitia mfumo wa ushindani ulio wazi, shindani na wa haki, unaochochea ukuaji wa biashara na ustawi wa taifa.