Yajipanga Kubeba Suluhu ya Uhaba wa Gesi hiyo Duniani
Helium One Global Yasema Akiba ya Songwe ina Thamani Kubwa Kijiolojia
Mradi Kuanza Kutekelezwa baada ya Miezi 18, Zaidi ya Dola Milioni 60 tayari Zimewekezwa
Serikali Kumiliki Asilimia 17 ya Hisa kupitia Kampuni ya Ubia ya Songwe Helium Limited
Tanzania imeanza rasmi Safari Mpya ya Kihistoria ikiingia kwenye ramani ya dunia kama Mzalishaji na Msambazaji wa kimkakati wa Gesi ya Helium. Hatua hiyo inafuatia baada ya kusainiwa kwa Mkataba wa Uchimbaji wa gesi hiyo baina ya Serikali na kampuni ya Helium One Global Limited kupitia Kampuni ya Ubia ya Songwe Helium Limited, katika hafla iliyofanyika Mei 2, 2026 Mkoani Songwe.
Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa wakati akizungumza katika hafla hiyo na kueleza kuwa, uzalishaji wa helium duniani kwa sasa unatawaliwa na nchi chache, hususan Marekani na Qatar, zinazochangia zaidi ya asilimia 75 ya uzalishaji wote, huku Urusi, Algeria, Canada, China na Poland zikichangia kwa kiwango kidogo. Ameongeza kuwa mahitaji ya gesi hiyo tayari yamevuka futi za ujazo bilioni 6 kwa mwaka na yanatarajiwa kuongezeka hadi zaidi ya bilioni 8.5 ifikapo mwaka 2030 ambapo kwa Tanzania kampuni za Helium One Global Limited na Noble Helium zimepiga hatua kubwa katika shughuli za utafiti wa gesi hiyo.
Ameeleza kuwa, mradi wa Southern Rukwa ni wa kimkakati unaoiwezesha Tanzania kuingia kwenye soko lenye thamani kubwa na ushindani mdogo na kuiweka katika nafasi ya kuathiri mwelekeo wa soko la helium duniani, huku ikitarajiwa kuwa sehemu ya suluhisho la uhaba wa gesi hiyo duniani na kueleza kwamba, uchimbaji wa helium utakwenda sambamba na gesi ambata kama hydrogen ambapo manufaa yake kimapato yatatenganishwa.
Aidha, Dkt. Kiruswa amefafanua kwamba kupitia mkataba huo, Serikali itamiliki asilimia 17 ya hisa katika kampuni ya ubia ya Songwe Helium Limited, hatua inayoiwezesha kushiriki moja kwa moja katika maamuzi ya kimkakati na kunufaika na mapato ya mradi kwa manufaa ya Taifa na wananchi.
‘’Huu ni utekelezaji halisi wa falsafa ya Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa rasilimali za nchi lazima ziwe chanzo cha ustawi wa taifa,’’ amesema Dkt. Kiruswa.
Akizungumzia manufaa mengine ya mradi huo amesema utachangia ajira kwa vijana wa eneo husika na taifa kwa ujumla, fursa za kibiashara kwa wazawa kupitia huduma za ugavi, uboreshaji wa miundombinu, mapato kwa Serikali na fedha za kigeni na uboreshaji wa miundombinu muhimu kama barabara na huduma za kijamii.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Helium One Global Limited, Lorna Blaisse amesema utiaji saini huo ni hatua muhimu kwa Tanzania na soko la helium duniani, akibainisha kuwa mradi una akiba yenye thamani kubwa na unaelekea kwenye uzalishaji wa kibiashara baada ya mafanikio ya uchimbaji kisima mwaka 2024 ambacho kilipelekea ugunduzi wa helium katika kisima cha Itambula West-1.
‘’Katika upimaji wa kisima uliopanuliwa robo ya tatu ya 2024, kisima cha ITW-1 kilirekodi helium yenye mkusanyiko wa asilimia 5.5 hadi juu ya ardhi, na hadi asilimia 7.6 kutoka miamba ya Karoo iliyovunjika na miamba ya Basement iliyopasuka,’’ amesema
Amesema baada ya utiaji saini wa leseni ya uchimbaji, kampuni ya Songwe Helium Ltd itaendelea na hatua za uendeshaji kuelekea uzalishaji wa kwanza wa kibiashara wa heliamu. Amezitaja hatua hizo kuwa ni pamoja na kukamilisha mipango ya maendeleo; mfumo wa usimamizi wa tathmini ya athari za mazingira na jamii; kubuni miundombinu, na kununua vifaa vya uchakataji na usafirishaji wa bidhaa.
Pia, ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano wake na kuridhia muundo wa ubia unaohakikisha nchi inanufaika na rasilimali zake, akibainisha dhamira ya kuzalisha helium ya Tanzania kwa uwajibikaji na ubora wa juu kwa soko la dunia.
Awali, akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Majadiliano ya Wizara ya Madini Prof. Sifuni Mchome amesema kupitia utaratibu wa Serikali kumiliki hisa huru zisizohafifishwa thamani, Serikali inashiriki moja kwa moja katika miradi ya madini, inapata faida kupitia gawio, mrabaha,kodi na tozo mbalimbali, inashiriki maamuzi ya kimkakati, kulinda mapato na maslahi ya wananchi kwa uwazi na uwajibikaji.
" Tulijadiliana kwa utaratibu mzuri bila kugombana na tumefika kwenye hatua ya kila mmoja apate, na leo tuko hapa kuweka wazi na kila mmoja ashuhudie," amesema Prof. Mchome.
Naye, Mkuu wa Mkoa wa Songwe Mhe. Jabiri Makame amesema Mkoa huo ni wa kimkakati ukiwa na utajiri wa Madini mbalimbali yakiwemo ya rare earth elements ambao utafiti wake unaendelea.
" Tunaipongeza Wizara ya Madini kwa kutafsiri kwa vitendo. Kwetu sisi suala la kuwasaidia wawekezaji kutekeleza mradi Kwa mafanikio ni kipaumbele cha kwanza," amesema Mhe. Makame.
Helium ni gesi ya kipekee sana duniani kwa sababu haina mbadala wake na matumizi yake ni ya kimkakati kwa maisha ya kisasa ya binadamu; inatumika katika vifaa vya tiba kama MRI, uzalishaji wa vifaa vya kielektroniki na teknolojia za kidigitali; sekta ya anga; ulinzi na tafiti za kisayansi, teknolojia za kisasa kama fibre optics na quantum computing.
Mradi huo unatekelezwa katika eneo la kilomita za mraba 480 ukiwa zaidi katika Mkoa wa Songwe Wilaya ya Momba na sehemu ndogo ikiingia Mkoa wa Rukwa.
Wafanyakazi wa EWURA wakishiriki maandamano ya Mei Mosi mbele ya Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.
...
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) leo, Mei 1, 2026, imeungana na wafanyakazi wengine duniani kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi), maadhimisho yaliyofanyika kitaifa mkoani Njombe.
Sherehe hizo zilihudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ambaye alikuwa mgeni rasmi. Katika hotuba yake, Rais Samia amewahimiza waajiri na waajiriwa kote nchini kuendeleza ushirikiano, kuaminiana, na kutanguliza maslahi ya taifa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.
Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuboresha mazingira na ustawi wa wafanyakazi, huku akiwataka kuongeza bidii na ufanisi kazini. Aidha, alibainisha wazi kuwa Serikali inathamini mchango wa wafanyakazi na itaendelea kuwaunga mkono katika juhudi za maendeleo ya nchi.
Katika maadhimisho hayo, EWURA imewakilishwa na wafanyakazi wake bora kutoka idara na vitengo mbalimbali. Wafanyakazi hao walichaguliwa kwa kura za wenzao kwa kuzingatia vigezo muhimu kama vile utendaji uliotukuka, nidhamu ya kazi, ubunifu pamoja na kujituma kazini.
Wawakilishi hao walishiriki katika maandamano rasmi yaliyopita mbele ya mgeni rasmi, wakibeba mabango yenye ujumbe wa kuhamasisha mshikamano na uwajibikaji kazini.
Ushiriki wao umeonesha dhamira ya EWURA kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi na kuchangia maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Wafanyakazi wa EWURA wakishiriki maandamano ya Mei Mosi mbele ya Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapungia mkono wafanyakazi wa EWURA, wakati wa maandamano ya Maadhimisho ya Sherehe za Meimosi leo.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM
Wahitimu 12 wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) wamehitimu mafunzo ya awali ya lugha ya Kijapani, hatua inayolenga kuongeza ujuzi na ushindani wao katika soko la ajira la ndani na kimataifa.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA) Alban Kihulla ametuma ujumbe wa shukrani na pongezi kwa wafanyakazi wa Wakala hiyo, siku ya maadhimisho ya siku ya Mei Mosi, 2026.
Katika Andiko hilo, Mtendaji Mkuu ameielezea siku ya Mei Mosi kuwa ni sehemu ya kutambua mchango mkubwa wa wafanyakazi hao katika kujenga uchumi imara kupitia matumizi sahihi ya Vipimo vilivyo katika usahihi unaokubalika kimataifa.
"Ninajivunia kujituma kwenu, uadilifu, na weledi mnaouonesha kila siku katika uhakiki na ukaguzi wa Vipimo pamoja na ukaguzi wa bidhaa zilizofungashwa.
Kazi yenu ina mchango mkubwa katika kuimarisha biashara yenye haki, kuongeza imani kwa walaji, na kukuza maendeleo ya taifa letu."
Aidha, ameongeza kuwa katika kipindi hiki cha mabadiliko ya teknolojia na ukuaji wa sekta mbalimbali, anawiwa zaidi kuwapongeza kwa kuendelea kujifunza, kuboresha ufanisi, na kuendana na mahitaji mapya ya kazi.
Amewasisitiza kuendelea kushikamana, kudumisha nidhamu ya kazi, na kuzingatia maadili ya utumishi wa umma.
Kiulla ameweka bayana kuwa Uongozi wa Wakala unatambua na kuthamini mchango wa wafanyakazi, na utaendelea kuboresha mazingira ya kazi ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.

Wakala wa Vipimo (WMA) imeungana na wafanyakazi kutoka katika taasisi na mashirika mbalimbali nchi nzima kuadhimisha siku ya Wafanyakazi Duniani.
Siku ya Wafanyakazi Duniani huadhimishwa kila Mwaka tarehe 1 Mei na kaulimbiu ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mwaka 2026 ni *"Kazi zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050".
Wakala imeshiriki katika maadhimisho hayo Kitaifa Mkoani Njombe ambapo watumishi wa Mkoa huo wameongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa WMA Bw. Alban Kihulla.
Pamoja na ushiriki wa Kitaifa kadharika, WMA imeshiriki kuadhimisha siku ya Wafanyakazi katika ngazi za Mikoa kupitia ofisi za Mikoa za Kivipimo.
Uongozi wa WMA unaendelea kuwahimiza watumishi wake kufanya kazi kwa weledi na kuhakikisha wanatoa huduma sahihi kwa wananchi kwa kusimamia matumizi sahihi ya Vipimo katika sekta mbalimbali.






Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akizungumza wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akizungumza wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akizungumza wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza wakati wa Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakisikiliza Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir (hayupo pichani) wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akiwa katika picha ya pamoja wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akiwa katika picha ya pamoja wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akiwa katika picha ya pamoja wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir,akiwa katika picha ya pamoja wakati akifunga Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.
......
Serikali imewataka watumishi wa sekta ya elimu nchini kuimarisha mshikamano, uwajibikaji na ubunifu ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa elimu bora inayokidhi mahitaji ya karne ya 21.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir wakati akifunga Mkutano wa Pili wa Baraza la 37 la Wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 30,2026 jijini Dodoma.
Mhe.Ameir amesisitiza kuwa mafanikio ya sekta ya elimu yanategemea kwa kiasi kikubwa ushirikiano kati ya wafanyakazi, menejimenti pamoja na wadau wote wa elimu, akibainisha kuwa mshikamano huo ni chachu ya kuleta mageuzi chanya na endelevu.
Ametoa pongezi kwa uongozi wa Wizara, ukiongozwa na Waziri Adolf Mkenda, kwa kuendelea kusimamia mageuzi ya elimu ikiwemo maboresho ya sera na mitaala inayolenga kuendana na maendeleo ya sayansi na teknolojia duniani.
Aidha, amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa uongozi wake unaoendelea kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya elimu, hususan katika kukuza ubora wa elimu, ubunifu na tafiti.
" Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kuimarisha elimu, ikiwemo uzinduzi wa Mkakati wa Kisayansi wa Kuimarisha Stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) pamoja na mpango wa kuunganisha taasisi za elimu na waajiri."amesema Mhe.Ameir
Ameeleza kuwa mipango hiyo inalenga kuwajengea wanafunzi ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko la ajira na hivyo kuongeza ushindani wao kitaifa na kimataifa.
Hata hivyo amewataka wajumbe wa baraza hilo kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma, akisisitiza umuhimu wa kuwa na maadili, nidhamu na uwajibikaji kazini.
Amebainisha kuwa baraza la wafanyakazi limeendelea kuwa jukwaa muhimu la majadiliano, ushauri na maamuzi yanayochangia kuboresha utendaji kazi pamoja na ustawi wa watumishi.
Katika mkutano huo, mada mbalimbali zilijadiliwa ikiwemo bajeti ya wizara, usimamizi wa rasilimali watu, maadili ya utumishi wa umma na afya ya akili mahali pa kazi.
Ameir amesema mada hizo zina mchango mkubwa katika kuboresha mazingira ya kazi na kuongeza tija kwa watumishi, hivyo kuimarisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi.
Aidha Ameir ametoa wito kwa watumishi wote kuendelea kudumisha mshikamano, uzalendo na uadilifu, pamoja na kuwa mabalozi wa kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa elimu.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof.Carolyne Nombo, amesema kuwa utekelezaji wa kaulimbiu ya mkutano wa wafanyakazi ya “Ushirikishwaji na Mshikamano wa Wafanyakazi ni Chachu ya Kuimarisha Elimu Inayochochea Ubunifu” ni muhimu katika kufanikisha malengo ya sekta ya elimu nchini.
Prof. Nombo amesisitiza kuwa mshikamano na ushirikiano kazini ni msingi wa kuleta mabadiliko ya kweli katika sekta ya elimu.
Ameeleza kuwa kaulimbiu hiyo inalenga kuwajenga watumishi kuwa na utamaduni wa kufanya kazi kwa pamoja, kwa bidii na kwa uwajibikaji, hali ambayo itachochea mageuzi makubwa yanayohitajika katika kuboresha ubora wa elimu nchini.
“Tunaposhirikiana na kufanya kazi kwa bidii kama timu moja, tunaweka msingi imara wa kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya elimu, yanayoakisi dira ya maendeleo ya taifa ya mwaka 2050,” amesema Prof. Nombo.
Ameongeza kuwa juhudi hizo zinapaswa kuendana na utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 (toleo la 2023), pamoja na kuzingatia mabadiliko mbalimbali yaliyofanyika katika mitaala iliyoboreshwa.
Aidha, amesisitiza umuhimu wa watumishi kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo ya serikali katika kutekeleza majukumu yao, akibainisha kuwa nidhamu na uwajibikaji ni nguzo muhimu za kufanikisha malengo ya wizara.






















