Na WMA – Dodoma

Watumishi wa Wakala wa Vipimo (WMA), wameitikia wito wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unaowataka watanzania kupitia makundi mbalimbali kupanda miti katika maeneo yao ili kuhifadhi mazingira.

Akiongoza zoezi la upandaji miti katika eneo ilipo Ofisi Kuu ya WMA Medeli jijini Dodoma, mapema leo Machi 20, 2026 Meneja Utawala na Rasilimali Watu, Charles Mavunde amewasisitiza watumishi wa Wakala hiyo nchi nzima kuzingatia maelekezo ya Serikali kwa kupanda miti na kuitunza ili kulinda mazingira.

Amesema kuwa, Mheshimiwa Rais Samia amekuwa akisisitiza mara kwa mara kuhusu upandaji miti katika maeneo mbalimbali na kwamba yeye mwenyewe ameonyesha mfano kwa kuwa kinara wa upandaji miti, hivyo WMA imeona ni vyema pia iitikie wito huo.

“Mtakumbuka kwamba, hata Mheshimiwa Dkt. Emmanuel Nchimbi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akimwakilisha Mhe. Rais katika maadhimisho ya siku ya upandaji miti duniani na maadhimisho ya upandaji miti kitaifa, jana Machi 19, 2026 kule Lindi aliagiza kuwa makundi mbalimbali ya watanzania waendeleze utamaduni wa kupanda miti,” ameeleza Mavunde na kuhitimisha kuwa WMA imeyachukulia kwa uzito maelekezo ya viongozi hao na itayatekeleza kikamilifu.

Viongozi na watumishi mbalimbali wa WMA Makao Makuu wameshiriki zoezi hilo la upandaji miti akiwemo Mkurugenzi wa Huduma za Biashara Phanuel Mtuki, Meneja Sehemu ya Fedha, CPA Ibrahim Mbinga, Meneja Mkoa wa Dodoma Said Ibrahim na Meneja Mawasiliano Veronica Simba.

Wengine walioshiriki ni watumishi kutoka Idara mbalimbali wakiwemo maafisa, maafisa usafirishaji na wasaidizi wa ofisi.

WMA ni wakala ya serikali iliyo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara yenye jukumu kuu la kumlinda mlaji kupitia usimamizi wa matumizi sahihi ya vipimo katika sekta mbalimbali.

 




Na Mwandishi wetu- DAR ES SALAAM


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu  ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI ambaye pia ni Mbunge wa

Arumeru Magharibi Mhe. Johannes Lukumay ameipongeza  Serikali kuendelea kusaidia kundi la Watu waishio na Maamubikizi Virusi vya 

UKIMWI kupitia shughuli mbalimbali za kiuchumi ili kujikwamua kiuchumi.

Mhe. Lukumay ameyasema  hayo tarehe 19 Machi 2026 mara baada ya ziara ya kutembelea Baraza la Watu waishio na maambukizi ya Virusi vya  UKIMWI akiwa ameambatana na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI katika ( Konga ya Jiji) iliyofanyika   katika Viwanja vya Pugu Mnadani Jijini Dar es Salaam.

 Amesema kuwa watu waishio na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI ni sawa na watu wengine hivyo yapaswa kuwapa kipaumbele katika fursa mbalimbali za kimaendeleo.

Pia Mwenyekiti huyo amelipongeza kundi hilo kwa namna

wanavyojituma katika kuhakikisha wanajikwamua kiuchumi na kuondokana na umasikini hivyo  kuziagiza  sekta husika kusaidia katika kuwatafutia masoko kwa ajili ya bidhaa zao.

Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga amesema kuwa Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan wataendelea kuunga mkono jitihada zao kwa kuongeza nguvu zaidi kwa Wanakonga ili waweze kujikwamua kiuchumi.

Mhe. Nderiananga amempongeza Mkurugenzi wa Jiji, Mkuu wa Wilaya pamoja na Katibu Tawala wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam na timu nzima kwa kuwawezesha Wanakonga katika fursa mbalimbali na kuwataka kuendelea na desturi hiyo ya kuwawezesha kwani mwaka huu wa fedha bado haujamalizika.

Aidha  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam Elihuruma Mabelya amesema kuwa moja ya eneo waliloliwekea nguvu ni Konga hiyo kwa kuunga mkono shughuli zao za  kiuchumi ili kuhakikisha

wanainuka na kufanikiwa katika nyanja mbalimbali za maendeleo.





Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi FCC Bi.Magdalena Hall,akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha mara baada ya kuwapatia elimu kuhusu masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

....

KATIKA harakati za kuimarisha uelewa wa haki za walaji nchini, Tume ya Ushindani (FCC) leo Machi 19, 2026 imetoa elimu kwa wanachuo wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha kuhusu masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Elimu hiyo ilitolewa na FCC kwa lengo la kuwajengea uelewa wanachuo kuhusu haki zao wanapokuwa wanatumia bidhaa na huduma mbalimbali. Wanachuo walipata nafasi ya kujifunza mambo muhimu ambayo mara nyingi huyapuuzia katika maisha yao ya kila siku.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo,Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi FCC Bi.Magdalena Hall,amewaeleza wanachuo kuwa wengi wao huingia katika mikataba bila kusoma masharti yake, hali inayoweza kusababisha hasara au kunyimwa haki zao bila wao kutambua.

Amefafanua kuwa mikataba mingi hasa ya huduma za simu, mikopo na manunuzi ya mtandaoni huwa na vifungu vinavyohitaji umakini mkubwa kabla ya kukubaliwa. Hivyo aliwataka wanachuo kujenga utamaduni wa kusoma na kuelewa kila wanachosaini.

Aidha, amesema  kuwa mlaji ana haki ya kupata bidhaa bora, taarifa sahihi na huduma stahiki. Pale haki hizo zinapokiukwa, mlaji anatakiwa kuchukua hatua za kisheria au kuripoti kwa mamlaka husika.

"FCC imesisitiza kuwa elimu hii ni endelevu na inalenga kuwafikia makundi mbalimbali ya jamii ili kujenga taifa lenye walaji wenye uelewa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi."amesema Bi.Hall

Kwa ujumla, mafunzo hayo yamewajengea wanachuo uelewa mkubwa na kuwahamasisha kuwa mabalozi wa haki za walaji, huku yakichangia mafanikio ya maadhimisho ya Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi FCC Bi.Magdalena Hall,akitoa elimu kuhusu masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha ,ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi FCC Bi.Magdalena Hall,akitoa elimu kuhusu masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha ,ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi FCC Bi.Magdalena Hall,akitoa elimu kuhusu masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha ,ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Sehemu ya wanafunzi wa wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata elimu kuhusiana na  masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa  ,ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Sehemu ya wanafunzi wa wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata elimu kuhusiana na  masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa  ,ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Sehemu ya wanafunzi wa wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata elimu kuhusiana na  masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa  ,ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha wakiuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha mikataba halisi na feki  mara baada ya kupatiwa elimu na FCC  ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani. 

Afisa Mlinda Mlaji Mwandamizi FCC Bi.Magdalena Hall,akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi VETA Kibaha mara baada ya kuwapatia elimu kuhusu masuala ya kumlinda mlaji na mikataba ya walaji kwa ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Bukulu, Mwl. Joseph Paul, akieleza namna huduma ya mrandao inavyorahisisha ujifunzaji katika maabara ya kompyuta shuleni hapo.

....

Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), kwa kushirikiana na UNICEF Tanzania, kimeanza kufungua ukurasa mpya wa maendeleo ya kidijitali katika Wilaya ya Kondoa, mkoani Dodoma, kupitia mradi wa kusambaza huduma ya intaneti kwa shule na jamii.

Katika ziara ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo iliyofanyika leo Alhamisi, tarehe 19 Machi 2026, ikiongozwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko wa UDOM, Bi. Rose Mdami, imeelezwa kuwa hatua kubwa tayari imefikiwa.

Msimamizi wa mradi huo, Dkt. Jabhera Matogoro, amesema vituo 10 tayari vimeunganishwa na huduma ya intaneti ya kasi ya 20Mbps, ikijumuisha shule tano za sekondari na Msingi, na vituo vitano vya jamii, hatua inayotarajiwa kuleta mageuzi makubwa katika upatikanaji wa taarifa, ujinzaji na ufundishaji.

Ameeleza kuwa mradi huo unalenga kuwezesha walimu, wanafunzi na wananchi kwa ujumla kupata maarifa kwa urahisi kupitia mtandao, sambamba na kuchochea fursa za ajira, ubunifu wa kibiashara na maendeleo ya kijamii katika wilaya hiyo.

Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko wa UDOM, Bi. Rose Joseph, akibadilishana mawazo na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kondoa, Bi. Sekela Mwasubila, kuhusu utekelezaji wa mradi wa Huduma ya Mtandao inayotolewa kwa shule 5 na ofisi 5 za Kata.

Miundombinu ya teknolojia ya mawasiliano ya mawimbi ya microwave inayotolewa na kampuni ya Airtel, ikisambaza huduma ya intaneti yenye kasi ya Mbps 20, kupitia Mradi unaofadhiliwa na UNICEF.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Bukulu, Mwl. Joseph Paul, akieleza namna huduma ya mrandao inavyorahisisha ujifunzaji katika maabara ya kompyuta shuleni hapo.

Mkuu wa Shule ya Msingi Isabe, Mwl. Jackline Richard, akizungumza wakati wa ukaguzi wa maendeleo ya mradi wa kusambaza huduma ya mtandao kwa shule na jamii.

Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko wa UDOM, Bi. Rose Joseph, akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Amani Abeid Karume kuhusu fursa za kujifunza kidijitali, wakati wakikagua huduma ya mtandao imavyofanya kazi shuleni hapo na kusaidia wanafunzi kujifunza.

Msimamizi Mkuu wa Mradi, Dkt. Jabhera Matogoro, akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko wa UDOM, Bi. Rose Mdami, wakikagua matumizi ya huduma mtandao darasani kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Amani Abeid Karume iliyopo WIlayani Kondoa.

Msimamizi Mkuu wa Mradi, Dkt. Jabhera Matogoro, akitoa maelezo kuhusu utendaji wa teknolojia ya intaneti katika moja ya vituo vilivyonufaika na mradi huo, Chama cha Ushirika cha Mawasiliano.