Wapiga Kura 127,632 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki katika uchaguzi wa kuchagua Mbunge katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mkoa wa Ruvuma na Kata ya Shiwinga iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele ameyasema hayo leo Februari 25, 2026 mjini Songea Mkoani Ruvuma wakati akisoma risala maalum kuhusu uchaguzi katika jimbo na kata husika utakao fanyika kesho Februari 26, 2026 na kusema kuwa jumla ya vituo 373 vya Kupigia Kura vitatumika.
“Kati yao wapiga kura 120,780 ni wa Jimbo la Peramiho na wapiga kura 6,852 wapo katika kata ya shiwinga na jumla ya vituo 373 vya Kupigia Kura vitatumika, ambapo vituo 354 vipo Jimbo la Peramiho na vituo 19 vipo katika Kata ya Shiwinga Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi,”amesema Jaji Mwambegele.
Aidha, amesema kwa uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Peramiho vyama vya siasa 15 vimesimamisha wagombea na kwa upande wa uchaguzi mdogo wa udiwani katika Kata ya Shiwinga vyama vya siasa nane (08) vimesimamisha wagombea.
“Natumia fursa hii kuvikumbusha Vyama vya Siasa vinavyoshiriki uchaguzi kesho Februari 26, 2026 kuzingatia wajibu wao wa kuweka mawakala katika vituo vyote vya zoezi la kupiga, kuhesabu na kujumlishia kura. Wasimamizi wa uchaguzi katika Jimbo na Kata husika, wamekamilisha taratibu zinazoweka mazingira yanayowawezesha mawakala wa vyama vya siasa kufuatilia mchakato mzima wa uchaguzi,”alisema Jaji Mwambegele.
Amesema, mawakala hao, wanawajibika katika kulinda maslahi ya vyama na wagombea wao. Hivyo, wanapaswa kuzingatia Sheria, Kanuni, taratibu za Uchaguzi na maelekezo ya Tume katika utekelezaji wa majukumu yao vituoni.
Jaji Mwambegele amesema vituo vitafunguliwa saa 01:00 asubuhi na kufungwa saa 10:00 jioni na kwamba ifikapo muda wa kufunga kituo saa 10:00 kamili jioni, kama wapiga kura bado wapo kwenye mistari, mlinzi wa kituo atasimama nyuma ya mtu wa mwisho na zoezi la upigaji kura litaendelea hadi wapiga kura walio kwenye mstari watakapomalizika.
“Baada ya kumaliza kupiga kura, mpiga kura anatakiwa kuondoka eneo la kituo cha kupigia kura; na Mpiga kura awapo kituoni, anatakiwa kufuata maelekezo yote atakayopewa na karani mwongozaji wapiga kura,”amesema Jaji Mwambegele.
Kwa mpiga kura ambaye ameandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na taarifa zake zipo katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura lililopo katika kituo husika, lakini amepoteza kadi yake au kadi yake imeharibika, ataruhusiwa kupiga Kura kwa kutumia moja wapo ya vitambulisho cha Taifa NIDA, Leseni ya udereva au Pasi ya kusafiria (Passport).
WANANCHI wa Kata ya Mzenga na Mafizi wamepongeza hatua ya Mbunge wao, Dkt. Selemani Jafo, kusimamia binafsi ujenzi wa Daraja la Kitomondo hadi usiku, wakisema imeongeza kasi na uwajibikaji kwa mkandarasi.
Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Mafizi, mmoja wa wazee wa eneo hilo, Ramadhani Zungwe amesema si jambo la kawaida kwa kiongozi kubaki kijijini hadi usiku akihakikisha kazi inafanyika kama ilivyopangwa.
“Ameonyesha mfano wa kujitoa kwa ajili ya maendeleo yetu. Hii inatupa matumaini mapya,” amesisitiza Zungwe.
Msukumo huo umefuatia maelekezo aliyoyatoa Dkt. Jafo wiki iliyopita kwa mkandarasi, kampuni ya Neloyt Tanzania Limited, akitaka ifikapo tarehe 24 nguzo za daraja hilo ziwe tayari zimemwagwa.
Tangu wakati huo, kazi imekuwa ikiendelea kwa kasi kubwa, huku Dkt. Jafo mwenyewe akishuhudia hatua za ujenzi zinavyopiga hatua.
Naye, Diwani wa Kata ya Mafizi, Mhe. Bora Mayage, amekiri kuwa usimamizi wa karibu wa mbunge huyo umeleta matokeo chanya.
Amesema kasi ya awali ya mkandarasi haikuwa ya kuridhisha, lakini kwa sasa mabadiliko yanaonekana wazi na nguzo za zege tayari zimesimama.
Mbali na hayo, Dkt. Jafo amemtaka mkandarasi kuhakikisha ifikapo Machi 5 zoezi la umwagaji wa slab linakamilika, akiahidi kushiriki pamoja na viongozi wa kata hizo mbili katika hatua hiyo muhimu.
Ameweka bayana kuwa hatokuwa tayari kuona wananchi wake wanaendelea kuteseka wakati Rais, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshatoa pesa ya kukamilisha daraja hilo.
Daraja la Kitomondo linatajwa kuwa kiungo muhimu kwa wakazi wa Mzenga na Mafizi, likirahisisha shughuli za kijamii na kiuchumi zikiwemo usafiri wa wanafunzi, wafanyabiashara na wagonjwa.
Kukamilika kwake kunatarajiwa kufungua ukurasa mpya wa maendeleo kwa wananchi wa maeneo hayo.
Wakala wa Nishati Vijijini imeanza utekelezaji wa mpango mkakati wa kitaifa wa nishati safi ya kupikia ili kufikia lengo la zaidi ya asilimia themanini 80% ya watanzania ifikapo mwaka 2034 wawe wanatumia nishati safi ya kupikia nishati ambayo ni salama kwa mtumiaji na rafiki kwa mazingira.
Akizungumza wakati wa ugawaji wa majiko katika Kata na Tarafa ya Irongero katika Wilaya ya Singida leo tarehe 24 Februari 2026 Mhandisi wa miradi ya REA Mkoani Singida, Mha.Nathan Msanze amesema kuwa Wakala ya Nishati Vijijini-REA katika mkoa huo umeanza usambazaji wa majiko banifu 6,692.
Amesema kuwa majiko hayo yatagawiwa kwa wananchi kwa bei ya ruzuku katika wilaya zote na Halmashauri za mkoa huo ambazo ni Ikungi majiko 1,116, Iramba 1,116, Itigi 1,115, Manyoni 1,115, Mkalama 1,115 na Singida 1,115.
Mhandisi Nathan amesema kuwa mradi huo unahusisha usambazaji wa majiko banifu yanayotumia kuni na mkaa kidogo ili kupunguza matumizi ya vyanzo hivyo vya nishati pamoja na athari za moshi zitokanazo na matumizi katika majiko ya kawaida. Katika mkakati huo Wakala wa Nishati Vijijini umeandaa mpango wa uuzwaji wa majiko banifu 200,000 kwa bei ya ruzuku yenye ufanisi mkubwa katika utumiaji wake.
Amesema kuwa mikataba hiyo ilisainiwa tarehe 9 Mei , 2025 na itatekelezwa ndani ya miezi 15. Gharama ya mradi ni TZS 340,288,200 kwa mkoa wa Singida na ruzuku inayotolewa na Wakala wa Nishati Vijijini ni TZS 289,230,508.47 sawa na asilimia 85 ya gharama ya mradi. Wananchi wanachangia TZS 51,057,691.53 sawa na asilimia 15 ya gharama ya mradi.
Mtoa huduma ni Tango Energy Limited ambapo jumla ya majiko banifu 6,692 yatauzwa kwa wananchi kwa bei ya ruzuku. Gharama ya jiko moja ni TZS 50,847.46 lakini serikali imetoa ruzuku ya asilimia 85 hivyo mwananchi atanunua kwa gharama ya TZS 7,600
Kwa upande wao wananchi ambao wamenufaika na majiko hayo katika kata ya Ilongero wakiongozwa na Diwani wa Kata hiyo Mhe Issa Mwiru kwa kauli moja wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuamua kutoa majiko bunifu kwa bei ya ruzuku ambayo itawanufaisha wananchi wote.
Na OWM - TAMISEMI, Colombia
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu -TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa wa nchi zinazoshughulika na masuala Kilimo, Ardhi na Maendeleo vijijini, ulioanza Februari 24, 2026 nchini Colombia kwenye jiji la Cartegina.
Prof. Shemdoe amemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mkutano huo, baada ya Mhe. Rais kupokea mwaliko wa kuudhuria mkutano huo kutoka kwa Rais Gustavo Petro Urrego wa Colombia.
Lengo kuu la mkutano huo uliohudhuriwa na nchi zaidi 100 duniani, ni kutoka na mwafaka wa namna gani matumizi bora ya ardhi katika kilimo yanaweza kupunguza migogoro ya ardhi na kuharakisha maendeleo vijijini.
Aidha nchi hizo zaidi ya 100 zilizoshiriki mkutano huo, ambazo zinashughulika na masuala ya Kilimo, Ardhi na Maendeleo ya Vijijini, zimepata fursa ya kubadilishana uzoefu katika masuala ya kilimo, Ardhi na Maendeleo Vijijini pamoja na matumizi ya teknolojia katika shughuli hizo, ambapo wananchi katika mataifa hayo watanufaika
Katika Mkutano huo wa siku tano unaotarajiwa kufikia tamati Februari 28, 2026 Prof. Shemdoe ameambatana na Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. David Silinde, wataalam kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI na Wizara ya Kilimo, lengo likiwa ni kutimiza ndoto za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuleta mapinduzi ya kilimo nchini ili kuwanufaisha watanzania na kuwapatia tabasamu la kudumu.
.
TUME ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyojitokeza Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, Leo Februari 24 imekutana na aliyewahi kuwa mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya.
Mahojiano hayo ya Tume na Sabaya yamefanyika katika Ofisi za Tume hiyo zilizopo Benki Kuu ya Tanzania (BoT) mkoani hapa, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Tume kukusanya taarifa, maoni na ushauri kutoka kwa watu mbalimbali wakiwemo viongozi wa sasa, wastaafu.
Katika mkutano huo wa Tume na Sabaya yamejadiliwa kwa kina namna matukio ya uvunjifu wa amani yalivyoanza, athari zake kwa wananchi, mali zao na miundombinu, pamoja na ushauri na mapendekezo ya namna ya kudhibiti na kuzuia matukio kama hayo yasijirudie siku zijazo.
Hivi karibuni Mamlaka ya Uteuzi imeiongezea Tume muda wa siku arobaini na mbili (42) kuanzia tarehe 20 Februari, 2026 ili Tume iweze kukamilisha uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani ya wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba, 2025 na kuitaka ikamilishe kazi na kuwasilisha Taarifa yake kabla au ifikapo tarehe 3 Aprili, 2026.
Kwa sasa Tume inaendelea na mahojiano na waathirika wa Matukio hayo kwa ajili ya hatua zaidi kama Taifa ili Matukio kama hayo yasijirudie tena.
Ikiwa ni majira ya Masika na kiubaridi, Bustani ya Eden ya Ngorongoro ikizungukwa na kingo zenye urefu wa Mita 610 huku wanyama na ndege wakichagiza kwa sauti murua zinazoashiria kuwa Ngorongoro ni mwamba wa miamba usiotikisika na kusheheni msingi imara wa vivutio vya asili, urithi wa utamanuni na maajabu saba katika eneo moja.
Miamba inayounda Bodi ya Wakurugenzi ikiongozwa na makamu mwenyekiti Dkt Harrieth Mtae inatembelea hifadhi ya Ngorongoro kuanzia ofisi za makao makuu hadi Kreta ya Ngorongoro na kujionea Eden hiyo ikiwa imesheheni kila aina ya ufahari unaoweza kuelezeka kidunia.
Bodi hii ni sawa na miamba ndani ya Mwamba kwani imejaa wabobezi katika masuala mengi ikiwemo ulinzi,uhifadhi, uchumi, ikolojia, maendeleo ya jamii, ukaguzi, sheria, utawala na diplomasia
Kubwa wanalilosisitiza kwa menejimenti “mnafanya kazi nzuri endeleeni kuchapa kazi na tangazeni kitaifa na kimataifa fahari ya Ngorongoro ambayo ni kivutio bora cha Utalii Afrika mwaka 2025.
Serikali kupitia Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) imetia saini mkataba wa uwekezaji katika sekta ya madini kwa ajili ya kuendeleza leseni ya uchimbaji wa dhahabu katika eneo la Kigosi, mkoani Geita.
Hatua hiyo inaelezwa kuwa chachu mpya ya kukuza uchumi wa eneo hilo na taifa kwa ujumla.
Hafla ya utiaji saini imefanyika Februari 24, wilayani Bukombe mbele ya Naibu Waziri wa Madini, Steven Kiruswa, aliyekuwa mgeni rasmi.
Mkataba huo umehusisha pande mbili ambazo ni STAMICO na kampuni ya Plantcor Mining and Plant Hire PTY Ltd ya Afrika Kusini, ambayo itawekeza katika uendelezaji wa mradi huo wa dhahabu.
Kiruswa ametoa maagizo kwa STAMICO pamoja na mwekezaji kuhakikisha kuwa uwekezaji huo unatekelezwa kwa vitendo na kuanza kazi mara moja bila kupoteza muda, ili uweze kuleta manufaa kwa wananchi wa Kigosi na maeneo jirani.
Aidha, amesisitiza kuwa mradi huo unapaswa kupanua wigo wa shughuli za uchimbaji katika eneo la Kigosi ili kuwapa nafasi wachimbaji kupata maeneo halali ya kuendelea na shughuli zao.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa STAMICO, Simon Sirro, amewaomba wananchi waliokuwa wakifanya shughuli katika pori la Kigosi kushirikiana na uwekezaji huo mpya na kuepuka kuwa chanzo cha vikwazo, hasa kutokana na mazoea yaliyokuwepo kabla ya mradi kuanza rasmi.
Sambamba na hilo, Naibu Waziri Kiruswa amesisitiza umuhimu wa kampuni mwekezaji kuzingatia masuala ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR), ili kuhakikisha kuwa jamii zinazozunguka eneo la Kigosi na wilaya ya Bukombe zinanufaika moja kwa moja kupitia miradi ya maendeleo kama vile elimu, afya na miundombinu.
Mkataba huo unatarajiwa kuleta manufaa makubwa kwa Watanzania, ikiwa ni pamoja na Kuongeza ajira kwa vijana, Kuongeza mapato ya serikali,Kuchochea ukuaji wa uchumi wa vijiji vinavyozunguka Kigosi pamoja na Kukuza sekta ya madini nchini
Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO Venance Mwasse, amesema kuwa mradi huo utaanza kwa kufanya utafiti wa kina wa kijiolojia, uchorongaji na uthibitishaji wa rasilimali.
Aidha, hatua zitakazofuata ni pamoja na upembuzi yakinifu wa kiuchumi, maendeleo ya mgodi, ujenzi wa miundombinu muhimu na usimikaji wa mtambo wa uchenjuaji wa dhahabu.
Uwekezaji huu wa dhahabu katika eneo la Kigosi unaonekana kuwa fursa muhimu kwa maendeleo ya mkoa wa Geita na taifa kwa ujumla. Ushirikiano kati ya serikali, mwekezaji na wananchi utakuwa nguzo kuu ya kuhakikisha mradi huu unaleta matokeo chanya na endelevu kwa kizazi cha sasa na kijacho.
Na OWM - TAMISEMI, Muheza
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu -TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amewaelekeza Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakurugenzi wa Halmashauri kutowahamisha au kuwaombea uhamisho watumishi wanaobainika kuwa na changamoto za kinidhamu katika Mamlaka za Mikoa na Serikali za Mitaa, na badala yake kuchukua hatua kwa kuwafungulia mashauri ya kinidhamu.
Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo hivi karibuni akiwa katika kikao kazi na watumishi wa Muheza kilicholenga kuhimiza uwajibikaji katika usimamizi na matumizi ya fedha za miradi ya maendeleo, ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba, ambaye wakati wa ziara yake wilayani Muheza alibaini ubadhirifu wa fedha katika Mradi wa Jengo la Utawala na kumuelekeza Prof. Shemdoe na Waziri wa Ofisi ya Rais UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete kuchukua hatua.
Aidha, Prof. Shemdoe amewaeleleza viongozi hao, kutotumia fedha au vifungu vya bajeti ya maendeleo kufanya malipo ya stahiki za watumishi, na kwamba fedha za mapato ya ndani zinazotengwa na Halmashauri kwa ajili ya miradi ya maendeleo zitumike kwenye shughuli zilizopangwa na si vinginevyo.
Sanjali na hayo, Prof. Shemdoe amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuendelea kusimamia kikamilifu upatikanaji wa rasilimali fedha na matumizi sahihi ya rasilimali hizo ili kuwaletea wananchi maendeleo endelevu na tabasamu la kudumu.
Vivile, amewataka Makatibu Tawala wa Mikoa kufanya uchambuzi wa matumizi wa fedha za miradi ya maendeleo, pamoja na zinazotoka Serikali kuu na za mapato ya ndani katika kipindi cha kuanzia mwaka wa fedha 2024/25 hadi sasa, “Kama ikibainika kuna Halmashauri yoyote ina ubadhilifu na kuna watuhumiwa wa ubadhirifu huo mimi na Mhe. Ridhiwani Kikwete tutachukua hatua,” amesisitiza Prof. Shemdoe.
Hatua hiyo ya Prof. Shemdoe ni sehemu ya jitihada za kuunga mkono kwa vitendo azma ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kutaka fedha za miradi ya maendeleo kutumika katika kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi kupitia ujenzi wa miundombinu bora afya, elimu na barabara.
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Mashariki imewakumbusha wafanyabiashara na wadau wa gesi ya kupikia (LPG) kuzingatia usalama, afya na utunzaji wa mazingira, wakati wa kusafirisha, kuhifadhi na kuuza bidhaa hizo kwa wateja.
Meneja wa EWURA Kanda ya Mashariki, Mhandisi Lorivii Long’idu, akizungumza wakati wa semina ya wadau hao iliyofanyika mkoani Pwani, 24 Februari 2026 aliwasisitiza wafanyabiashara wa jumla wa LPG kuwa na mikataba na wasambazaji wao na wauzaji wa rejareja wa bidhaa hiyo ili kukidhi matakwa ya kisheria na kiusalama.
Mhandisi Long’idu aliwahimiza pia wadau hao kuwaelimisha wasambazji na wauzaji wa rejareja wa LPG kuhusu usalama na umuhimu wa kutumka mizani iliyohakikiwa na Wakala wa Vipimo wakati wa kutoa huduma ili wananchi wapate huduma bora.


Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) ameipatia tuzo Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kwa kutambua mchango wake na unaotolewa na Mamlaka hiyo katika usimamizi wa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira nchini.
Tuzo hiyo iliyotolewa wakati wa Usiku wa Tuzo za Umahiri katika Sekta ya Maji, tarehe 23 Februari jijini Arusha, ilipokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Andilile.
Akizungumza baada ya kukabidhi tuzo hiyo, Mhe. Aweso alieleza kuwa, lengo ni kutambua utendaji bora wa mamlaka za maji, wasimamizi na watendaji katika maeneo waliofanya vizuri kwa kipindi cha miaka mitatu (2021/22, 2022/23 na 2023/24).
Akizungumza baada ya kupokea tuzo, Dkt. Andilile, alisema kuwa EWURA itaendelea kushirikiana na Wizara ya Maji pamoja na kuzisimamia kwa uthabiti ili ziendelee kufanya vizuri katika utoaji wa huduma.



















.jpeg)






.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)

