Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Kenan Laban Kihongosi kenani kihongosi amekutana na viongozi wa Dini na viongozi wa mila wa mkoa huo kwa lengo kufahamiana na kupata baraka, dua na maombi kutoka kwa viongozi hao, ili anapoianza kazi yake iwe na ulinzi wa Mungu, kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Mkuu wa mkoa, mapema leo Julai 01, 2025.
Amebainisha kuwa, anaamini Mhe.Rais kumleta Arusha si kwa uwezo wake bali ni mpango wa Mungu, na kuwaomba viongozi hao, licha ya kumpa ushirikiano katika utendaji wake kazi, amewasisitiza kuombea amani ya nchi, kumuombea, kumlea, kumfundisha, kumshauri na kumuelekeza pale atakapopotoka ili aweze kuitenda kazi vizuri na kuendeleza mkoa wao wa Arusha.
"Binafsi ninamshukuru Mungu kwa kunipa kibali cha kuja kuwatumikia tena, lakini katika utumishi wa Umma kuna mambo ambayo yanahitaji msaada wa Mungu, hivyo ninaamini ushauri kutoka kwenu kutokana na umri wangu mdogo, niwaombe viongozi wangu msiache kuniombea, ninaombe mnilee mimi ni kajana wenu". Ameweka wazi Mhe. Kihongosi.
Aidha, amewaomba kuuombea amani ya mkoa na Taifa kwa ujumla na kuongeza kuwa, waendeleze ushirikiano wao kama walivyoshirikiana na viongozi waliotangulia kwa kuwa mkoa ni ule ule, kilichobadilika ni uongozi tu lakini malengo ya kuujenga mkoa wetu yako pale pale.
Hata hivyo amewasisitiza kendelea kuhubiri amani ya nchi yao, kwa kuangalia manufaa ya amani na utulivu, na kuepuka kujenga chuki na uadui kwa misingi ya dini na vyama vyetu kwa kuweke mbele utaifa hususani katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2025
"Viongozi wa dini mnalojukumu la kuiombea Tanzania na viongozi wa mila wanayo kazi ya kuhubiri maadili na amani ya nchi yetu hivyo viongozi wangu ninaomba tushirikiane kuilinda amani, sisi ni watumishi wa Umma, tumekuja kufanya kazi tu, lakini iko siku tutaondoka, hivyo tusikubali kuharibu nyumbani zaidi tuilinde ardhi yetu" Amesema
Tutambue kuwa, Mheshimiwa Rais anayo nia njema kwa nchi yake kwa kuangali mifano ya miradi mikubwa inayotekelezwa nchini katika seka zote hivyo saidieni kuilinda nchi yetu na kumsaidie Mhe Rais.

Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kuonesha uwezo wake wa kiteknolojia na uaminifu wa huduma zake katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam.
Kupitia kaulimbiu yao ya "TEHAMA SALAMA, TAIFA SALAMA", TTCL linajitambulisha kama mhimili wa maendeleo ya kidijitali nchini, likiwa na huduma mbalimbali bunifu zinazowawezesha wateja wa sekta zote kupata mawasiliano ya uhakika, salama na ya gharama nafuu.
Meneja wa Banda la TTCL, Bi. Janeth Maeda, amesema TTCL linashiriki maonesho hayo si kwa lengo la kibiashara pekee, bali pia kuelimisha jamii kuhusu nafasi muhimu ya Shirika hilo katika kusimamia miundombinu ya mawasiliano ya Taifa.
“Tuna dhamana ya kitaifa ya kusimamia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB) na Kituo cha Taifa cha Kuhifadhi Data Kimtandao (NIDC). Huduma hizi ni msingi wa usalama wa taarifa na miundombinu ya TEHAMA nchini,” alisema Maeda.
Bi. Maeda alifafanua kuwa shirika hilo linatoa huduma kwa taasisi nyeti kama wizara, hospitali, mashule, taasisi za fedha, mashirika ya umma na sekta binafsi, kwa kutumia teknolojia ya fiber optic yenye kasi, uthabiti na usalama wa hali ya juu.
“Mashirika yanayotumia huduma za TTCL yameshuhudia kupungua kwa gharama za uendeshaji, ufanisi mkubwa katika utoaji wa huduma, na uimarishaji wa usalama wa taarifa,” aliongeza.
Katika msimu huu wa Sabasaba, TTCL linatoa ofasikabambe kwa wateja wake, ikiwa ni pamoja na punguzo maalum kwa vifaa vya mawasiliano kama vile routers, USB modems, na MiFi devices—ikiwa ni mkakati wa kusaidia wananchi kumiliki vifaa bora kwa urahisi zaidi.

Aidha, Bi. Maeda ametoa wito kwa washiriki wa maonesho, taasisi za ndani na nje ya nchi pamoja na wananchi kwa ujumla, kutembelea banda la TTCL namba 26 ili kujionea huduma za kisasa, kupata ushauri wa kitaalamu kuhusu TEHAMA, na kujifunza mbinu za kuongeza ufanisi wa kazi kwa njia za kidijitali.
“TTCL ni zaidi ya mtoa huduma; sisi ni sehemu ya maendeleo ya Taifa,” alisisitiza.
Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) amewavisha cheo manaibu kamishna wawili na kushuhudia uvishwaji vyeo kwa makamishna wasaidizi waandamizi watano waliovishwa vyeo na mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi NCAA Jenerali Venance Mabeyo (Mstaafu)
Waliovishwa Cheo na Mhe. Waziri ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Joas John Makwati aliyepandishwa cheo kuwa Naibu Kamishna wa Uhifadhi anayesimamia Uhifadhi, utalii na Maendeleo ya Jamii na Naibu Kamishna wa Uhifadhi Aidan Paul Makalla anayesimamia Huduma za Shirika NCAA.
Kwa upande wa makamishna waliovishwa vyeo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi NCAA Jenerali Venance Mabeyo (mstaafu) ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi anayesimamia idara ya Mipango na uwekezaji, Gasper Stanley Lyimo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Paul Geofrey Shaidi anayesimamia Kitengo cha huduma za Sheria, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Charles Marwa Wangwe anayesimamia Idara ya Uhasibu na fedha.
Wengine ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Godwin Felician Kashaga anayesimamia Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani, na Afisa Uhifadhi Mkuu Daraja la kwanza Mariam Kobelo anayesimamia idara ya Huduma za Utalii na masoko aliyepandishwa cheo kuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi.
Baada ya kuwavishwa vyeo hivyo waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) amewaelekeza maafisa hao kufanya kazi kwa bidiii na weledi mkubwa katika kutekeleza majukumu yao kwa kuwa cheo ni dhamana na kinakuja na majukumu.
“Nimatumaini yangu kuwa viongozi wote mliovaa vyeo leo mtakuwa chachu ya kufanya kazi kwa kujituma na kuonesha mfano wa kuigwa kwa Maafisa na Askari mnaowaongoza, juhudi zenu ndiyo zitakazochangia kulinda na kuhifadhi eneo la Ngorongoro na kuendelea kuwa kivutio kwa wageni wanaotembelea” ameongeza Balozi Chana.
Kamishna wa Uhifadhi NCAA Abdul-Razak Badru ameeleza kuwa kwa sasa watumishi wote wa NCAA wameshapatiwa mafunzo ya kijeshi kutoka mfumo wa awali wa kiraia na kuwa mamlaka hiyo itahakikisha inatumia rasilimali ya watumishi waliopo kuongeza nguvu ya kuhifadhi, kulinda, kuendeleza jamii na kuboresha miundombinu ya utalii.
Mwenyekiti wa bodi ya NCAA Jenerali, Venance Mabeyo (mstaafu) ameeleza kuwa mafanikio ya Ngorongoro yanategemea uadilifu na uwezo wa viongozi wake na kuwaasa viongozi waliovishwa vyeo kubeba matumaini mapya katika utekelezaji wa majukumu ya uhifadhi, utalii na maendeleo ya jamii.
-REA kuendela kuwajengea uwezo Magereza uendelezaji Miradi ya Nishati Safi
-Mhe. Balozi Radhia Msuya amewahamasisha Maafisa na Watumishi wa Magereza kuwa Mabalozi wa Nishati Safi
Serikali imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza (Gereza la Ukonga) mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko yake 464 ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kama njia ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia nchini ambapo msisitizo ni angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ifikapo Mwaka 2034.
Hafla ya ugawaji wa mitungi na majiko yake iliongozwa na Mhe. Balozi, Radhia Msuya, Mkurugenzi wa Bodi ya Nishati Vjijini (REB) katika gereza la ukonga, Jijini, Dar es Salaam, leo Juni 30, 2025 ambapo kwa upande wa Magereza uliwakilishwa na Msaidizi wa Mkuu wa Gereza hilo, Kamishna Msaidizi, (ACP); Athuman Recha.
Balozi, Radhia amesema kuwa, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA). Watumishi hao watasambaziwa mitungi ya gesi na majiko yapatayo 464 na kuongeza kuwa huo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Awamu ya Sita; Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhusu matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kama nyenzo ya kulinda afya za Watanzania, kulinda na kutunza mazingira
Amesema kuwa, Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeingia makubaliano na Jeshi la Magereza ili kuwawezesha, kuhama kutoka katika matumizi ya nishati isiyo salama kwenda katika matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia katika magereza yote nchini.
“Serikali kupitia REA, ilishaanza uwezeshaji kwa Jeshi la Magereza na wameshaanza kutumia Nishati Safi na kwa msisitizo huo, tuliona ni vyema, kuwawezesha Watumishi na Maafisa ili nao waachane na nishati chafu ili kulinda afya zao pamoja na kulinda mazingira yetu”. Amesema, Mhe. Balozi, Radhia.
Naye, Mkurugenzi wa Fedha na Uwezeshaji, CPA, Daniel Mungure ambaye alimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), amewataka watumishi wa jeshi la magereza kuibeba Ajenda ya Mhe. Rais Samia ya kuwa Mabalozi wa Nishati Safi ya kupikia kwa kuendelea kutumia gesi na siyo kuni na mkaa.
Akishukuru kwa uwezeshaji huo kwa Watumishi na Maafisa wa Jeshi la Magereza, Mrakibu Mwandamizi, (SSP); Moses Mumbi amesema, wanaishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuwajali na kuongeza kuwa teknolojia hizo za Nishati Safi ya Kupikia si tu zinalinda afya zao lakini zinaongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao wakati wa kuwahudumia Mahabusu na Wafungwa.







Aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum Kundi la Wenye Ulemavu Ummy Nderiananga Juni 30,2025 amechukua fomu ya kugombea Ubunge Viti Maalum kundi la Wanawake Wenye Ulemavu.
Nderiananga amekabidhiwa fomu hiyo katika Ofisi ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) na Katibu UWT Mkoa wa Kilimanjaro Ndug. Jane Chatanda.
WAHITIMU MAFUNZO YA MFUMO STAKABADHI GHALA WATAKIWA KUONGEZA UWAZI NA UBORA KATIKA UTENDAJI KAZI WAO






























