Wadaia kugawa hongo kati ya Sh.5000 na Sh.50,000 ,Mbunge mwenyewe atoa majibu
Na Shomari Binda,Rorya
WAKATI joto la uchaguzi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), likianza kupanda kwa baadhi ya majimbo imeelezwa katika Jimbo la Rorya
mkoani Mara wajumbe waliokuwa wakipatiwa mafunzo ya utendaji ndani ya Chama hicho wamedaiwa kupewa fedha kati ya Sh.5000 hadi Sh.50,000 kama sehemu ya kuwashawishi wajumbe hao kuelekea uchaguzi mkuu.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopo zinaeleza kwamba juzi katika mafunzo ya watendaji ndani ya Chama Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Rorya, Ongujo Wakibara kwa kushirikiana na mbunge wa Jimbo hilo, Jafari Chege wanadaiwa kuyavuruga kwa kumwaga hongo kwa wajumbe wa mafunzo hayo.
Wakati wa mafunzo hayo inadaiwa Mbunge Chege na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Rorya, Ongujo Wakibara waliingilia katika semina ya makatibu wa matawi na kata iliyofanyika Februari 20, 2025 ambapo wanadaiwa kugawa posho kiasi cha Shilingi 50,000 kwa kila katibu aliyehudhuria mafunzo hayo.
Tuko hilo ambalo liliibua mjadala katika makundi sogozi ya ya WhatsApp ya CCM Mkoa wa Mara ambapo yameeleza utaratibu huo unakiuka maelekezo kutoka makao makuu ya CCM Taifa.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa mafunzo hayo ya watendaji yasiingiliwe na viongozi au wanasiasa kwa sababu ni mafunzo ya kiutendaji na chama kilisema kitagharamia kila kitu ikiwemo chakula na posho.
“Lengo la chama kufanya hivyo ilikuwa ni kuondoa urasimu wa wagombea kutumia nafasi hiyo kutoa rushwa kinyume chake Mwenyekiti wa chama na mgombea wake ambaye ndiye mbunge kwa sasa wamevamia ukumbi na kutoa posho hizo.
“Jambo hili halijawafurahisha hata wakufunzi haswa kauli za Mwenyekiti na Mbunge baada ya kuzuiwa na wakalazimisha kufanya kwa nguvu,” imesema sehemu ya taarifa katika makundi hayo sogezi ya WhatsApp
Hata kupitia Gazeti tando la George Marato Tv, imefatilia taarifa hiyo na kuzungumza na Mbunge wa Jimbo la Rorya, Jafar Chege kwa njia ya simu na kudai yupo msibani toka asubuhi na hajaudhuria kikao hicho na kushangazwa na taarifa hiyo.
Hata hivyo Chege alikiri kuiona taarifa hiyo kwenye makundi sogozi ya CCM lakini hajui lengo lake.”Nimeshangazwa na taarifa hiyo,nipo msibani na nimeambiwa kikao hicho kimeenda vizuri na kimalizika salama hizo taarifa ni za uongo,” amejibu Chege alipokuwa akielezea taarifa hiyo.
Alipotafutwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Rorya, Ongujo Wakibara hakupatikana kwenye simu yake ya mkono hivyo jitihada za kumtafuta kuzungumzia jambo hili zinaendelea ili kupata ukweli wa madai ya taarifa hizo.
Hata hivyo pamoja na hali Mwenyekiti huyo wa CCM anadaiwa kuwa amekuwa akiwasimamisha viongozi hovyo hovyo na hivi karibuni katika Kata za Mkoma, Kirogo, Kinyenche, Nyathorogo, Goribe na Tai aliwasimamisha vongozi wa matawi bila kuihusisha kamati ya siasa.
Wakati kwa Mbunge Chege amekuwa akizunguka katika baadhi ya kata na matawi na kukutana na wajumbe moja kwa moja na kugawa fedha kiasi cha Shilingi 5,000 hadi Sh.50,000 kulingana na uwezo na hadhi ya mjumbe.
Na. Farida Ramadhani na Joseph Mahumi, WF, Dodoma
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Dkt. Anthony Diallo, amezihimiza taasisi za kilimo nchini kubadili mbinu za utendaji kwa kuachana na mazoea na badala yake kuimarisha matumizi ya utaalamu katika kuwawezesha wakulima kuongeza tija na kuendesha kilimo cha biashara.
Dkt. Diallo alitoa wito huo tarehe 19 Februari 2025, katika siku ya pili ya ziara ya Bodi na Menejimenti ya TFRA walipotembelea taasisi mbalimbali za Wizara ya Kilimo, ikiwemo Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI – Maruku), Kituo cha Uhaulishaji Teknolojia za Kilimo (MATI – Maruku), na Taasisi ya Utafiti wa Kahawa (TaCRI). Ziara hiyo inalenga kuelewa majukumu ya taasisi hizo na kuimarisha ushirikiano katika kuhamasisha matumizi sahihi ya mbolea miongoni mwa wakulima.
Akizungumza katika ziara hiyo, Dkt. Diallo amesisitiza kuwa ili kufanikisha malengo ya serikali kupitia kauli mbiu ya Agenda 10/30: Kilimo ni Biashara, wataalamu wa kilimo wanapaswa kuongeza jitihada katika kutoa elimu na ushauri kwa wakulima ili kubadili mitazamo hasi kuhusu matumizi ya mbolea na kuchochea uzalishaji wenye tija kwa ajili ya soko la ndani na nje ya nchi.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TFRA, Bw. Joel Laurent, ameeleza kuwa, ziara hiyo imetoa fursa kwa TFRA kufahamu kwa undani zaidi shughuli za taasisi hizo na kutathmini maeneo ya ushirikiano ili kuongeza ufanisi katika uhamasishaji wa matumizi sahihi ya mbolea.
Amebainisha kuwa TFRA inajumuisha wakufunzi wa MATI katika programu zake za mafunzo kwa wakulima, ili kuwawezesha wakufunzi hao kuendeleza utoaji wa elimu kwa wakulima kwa ufanisi pindi mafunzo yanapohitajika.
Katika wasilisho lake, Meneja wa TARI – Maruku, Dkt. Mpoki Shimwela, ameeleza kuwa, matumizi duni ya mbolea katika kilimo cha migomba yamesababisha upungufu wa virutubisho kwenye udongo, hali inayochangia kuzalisha ndizi kilo chache na zisizo na ubora unaokidhi mahitaji ya masoko ya kimataifa
Alibainisha kuwa, TARI imeanzisha miradi mbalimbali ya kuhamasisha matumizi ya mbolea, ikiwa ni pamoja na vipimo vya afya ya udongo kwa wakulima ili kuwasaidia kuelewa mahitaji halisi ya udongo wao.
Shaban Mkulila, mkulima wa kahawa kutoka Kijiji cha Maruku, baada ya kutembelewa na Bodi na menejimenti ya TFRA shambani kwake Maruku ameeleza kuwa, tangu aanze kutumia mbolea katika kilimo cha kahawa mwaka 2019, ameshuhudia ongezeko kubwa la mavuno.
Ameishauri TFRA kuanzisha mashamba darasa ili wakulima wapate mafunzo kwa vitendo na kuwasaidia kuondokana na dhana potofu kwamba mbolea inaharibu udongo.
Naye, Bw. Siraji Amri, mkulima wa kahawa kutoka Kijiji cha Mulata, Kata ya Katerero, amethibitisha kuwa matumizi ya mbolea za viwandani yamemwezesha kuongeza uzalishaji hadi kufikia wastani wa kilo sita za kahawa kwa kila mti mmoja, hali inayothibitisha mchango wa mbolea katika kuimarisha tija ya kilimo.
Ziara hiyo imetoa mwangaza kuhusu umuhimu wa ushirikiano kati ya TFRA na taasisi za kilimo katika kuhakikisha wakulima wanapata elimu sahihi kuhusu matumizi ya mbolea kwa ajili ya kuongeza uzalishaji na kufanikisha azma ya kilimo biashara nchini.
Oparesheni maalumu ya kuwadhibiti wanyamapori wakali na waharibifu aina ya fisi waliokuwa wanaleta taharuki na madhara Kwa jamii inayoendelea Mkoani Simiyu imeonesha mafanikio makubwa baada ya fisi 16 kuvunwa ikiwa ni hatua muhimu iliyochukuliwa na Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii ya kuhakikisha usalama na utulivu Kwa wananchi vinarejea.
Hayo yamesemwa leo Februari 19, 2025 na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Kenani Kihongosi alipokuwa akiongea na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari.
Mhe. Kihongosi amesema kufuatia changamoto hiyo, Serikali ilichukua jukumu kubwa la kuhakikisha inalinda wananchi wake ikiwemo kuanzisha oparesheni maalumu inayohusisha Jeshi la Uhifadhi Kwa Taasisi za TAWA, TANAPA na TFS Kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi pamoja na wananchi, oparesheni inayotajwa kuanza Januari 25, 2025.
"Tarehe 20/12/2024 baada ya fisi kuvamia wananchi Serikali ilichukua hatua kubwa ya kushirikisha vyombo vyake (TAWA na Jeshi la Polisi) na kuanza Oparesheni, lakini ilipofika tarehe 25/01/2025 oparesheni ya mkoa mzima ilifanyika Kwa ukubwa kuhakikisha inakabiliana na fisi wote waliokuwa wanasumbua wananchi" amesema Mhe. Kihongosi
"Na Kwa taarifa njema ni kwamba tangu kuanza Kwa oparesheni hii vyombo vyetu vimeweza kudhibiti na kuua fisi 16 na ndio maana kwasasa mnaweza kuona hali imetulia" ameongeza Mkuu huyo wa mkoa wa Simiyu.
Aidha Mhe. Kihongosi ameendelea kuwatoa hofu wananchi wa mkoa huo akisisitiza kuwa hali ni shwari na kuwataka waendelee na shughuli zao kama kawaida huku akikemea vikali imani za kishirikina kuhusiana na mnyamapori aina ya fisi kwa baadhi ya wakazi wa Simiyu na kuwataka wote wanaofuga wanyamapori pori hao kuacha mara moja kwani ni kosa kisheria kumiliki nyara za Serikali bila Kibali.
Kwa upande wake Afisa Habari wa TAWA Beatus Maganja amewaomba wananchi wa Mkoa wa Simiyu hususani wilaya ya Itilima kuacha tabia ya kutembea nyakati za usiku na alfajiri kwani ni nyakati ambazo wanyama fisi huwa katika mawindo yao.
Vilevile amewasisitiza wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Maofisa wa Jeshi la Uhifadhi waliopo uwandani ili kuongeza ufanisi wa zoezi hilo huku akiwahakikishia kuwa Serikali imedhamiria kulinda wananchi wake na kwamba Askari wapo uwandani wanafanya Kazi usiku na mchana kuwahakikishia usalama wao.
Kwa upande wao wananchi wa Simiyu hususani wilaya ya Itilima wameshukuru Kwa juhudi zinazofanywa na Serikali katika kukabiliana na changamoto hiyo, wakisema kuwa hatua hiyo imeweza kuwarejeshea matumaini, utulivu na amani.
"Kwakweli tulikuwa tunasumbuliwa sana na haya mafisi ambayo yalikuwa yanauma watu, baada ya Serikali kusikia ikaweka ulinzi, kwakweli imetufanyia vizuri sana mpaka leo hatujawasikia tena tangu Askari waanze kuwashambulia hao fisi, mpaka leo hii tuna utulivu sana kwakweli tunashukuru sana" amesema Mozo Mabula mkazi wa Kijiji cha Mwamunhu kilichopo wilaya ya Itilima.
▪️Viwanda vya uongezaji thamani madini kupewa kipaumbele
▪️Waziri Mavunde asisitiza madini kuongezwa thamani ndani ya nchi
▪️Serikali yatenga eneo maalum Kahama-Shinyanga
📍 Dar es salaam
Waziri wa Uingereza anayeshughulikia masuala ya Afrika Mh.Lord Collins amevutiwa na mpango wa nchi ya Tanzania kuandaa mkakati maalum wa uongezaji thamani madini nchini Tanzania na kuahidi kwamba Uingereza itatoa ushirikiano katika kusaidia eneo la uongezaji thamani madini hayo ndani ya nchi.
Hayo yamesemwa leo wakati wa kikao kati ya Mh. Lord Collins na Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde kilichofanyika leo Jijini Dar es salaam.
“Tanzania na Uingereza zina ushirikiano wa muda mrefu katika maeneo mengi ya kiuchumi ikiwemo sekta ya Madini.
Nimevutiwa na mkakati wa Tanzania wa kuongeza thamani ndani ya nchi, mkakati ambao Uingereza tunauunga mkono na tupo tayari kuwezesha utekelezaji wake kupitia Mradi wa “Manufacturing Africa“ ambapo ya pauni 2.1 bilioni zimetengwa kusaidia nchi 6 za Afrika,ikiwemo Tanzania,kutengeneza bidhaa za kati na za mwisho kupitia madini“ Alisema Lord Collins
Akizungumza katika Kikao hicho,Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde amesema Tanzania inayo mkakati wake maalum wa uongezwaji thamani madini ili kuongeza manufaa makubwa zaidi kwa nchi kupitia sekta ya madini,ambapo kwa sasa madini yanapaswa kuchakatwa na kuongezwa thamani nchini.
Serikali imetenga eneo maalum la ujenzi wa viwanda vyakuongeza thamani wilayani Kahama,Mkoani Shinyanga kwa lengo la kuvutia uwekezaji katika eneo hili.
“Mradi wa “Manufacturing Africa“ utasaidia kufanikisha azma ya Tanzania kwa kuwezesha uanzishwaji wa viwanda vya kuchakata,kusafisha na kutengeneza bidhaa zitokanazo na madini“ Alisema Mavunde
Kikao hicho pia kimehudhuriwa na Balozi wa Tanzania-Uingereza Mh. Mbelwa Kairuki na Balozi wa Uingereza-Tanzania Mh. Marianne Young






Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi,Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Ridhiwani Kikwete, ameitaka Tume ya Usuluhishi na Uamuzi kuwaTaasisi ya kimkakati katika utatuzi wa migogoro ya kikazi nchini ikiwa na lengo la kuchochea ukuaji wa kiuchumi na kuhakikisha mahala pa kazi panakuwa na amani ili kuwafanya wafanyakazi na waajiri watumie muda mwingi kufanya uzalishaji Wenye Tija.
Ameyasema hayo wakati akifungua kikao kazi cha Tathmini ya Utendaji Kazi na mafunzo kwa watumishi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi Tanzania bara, kilichofanyika Leo tarehe 19 Februari, 2025 Mkoani Morogoro.
Aidha, Mhe. Kikwete ameitaka Tume hiyo kushughulikia migogoro kwa haraka, ufanisi na weledi ili kuweza kutimiza matarajio ya wadaawa na wadau ambao wengi wao ni wawekezaji, hivyo kusaidia kukuza Uchumi wa nchi.
“Serikali iliongeza bajeti ya Tume kiasi cha zaidi ya Shilingi Milioni mia tisa (900,000,000+) bila shaka mmeona ongezeko hilo limeleta mabadiliko siyo tu kwenye maslahi ya wafanyakazi lakini pia kuiwezesha Tume kutekeleza majukumu yake ya msingi” amesema Mhe. Kikwete
Kwa upande wake, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi, Dkt. Yose Mlyambina amewakumbusha wasuluhishi na waamuzi kutilia mkazo suala la matumizi ya mfumo wa kielekroniki na hususani kuangalia namna bora ya kupokea vielelezo ili kuwasilisha jalada kamilifu pindi litakapoitishwa mahakamani.
Awali akiongea katika kikao hicho Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) Usekelege Mpulla amemhakikishia Waziri Kikwete kuwa Tume hiyo ya itaendelea kuwa Taasisi ya kimkakati katika kukuza uchumi nchini kwa kuimarisha utatuzi wa migogoro ya kikazi nchini ili kuweza kuhakikisha mahala pa kazi panakuwa na amani na kuwafanya wafanyakazi na waajiri watumie muda mwingi kufanya uzalishaji Wenye Tija.
Mama Samia legal Aid yafanya mafunzo ya kikao kazi cha usaidizi kwa wataalamu na watakao shiriki katika kutoa huduma ya msaada wa kisheria kutoka wilaya zote za Mkoa wa Lindi ambapo kesho ufunguzi rasmi wa kampeni katika Halmashauri ya wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi Na kufunguliwa na Waziri Mkuu wa jamuhuri ya Tanzania.
Tayari mikoa 17 ya Tanzania bara tayari imesha fanyaka uzinduzi wa kampeni na Leo tarehe 18 Februari usinduzi unafanyika katika Mkoa wa Mwanza n lengo Hadi kufikia mwisho wa mwezi huu iwetayari wamesha fikia mikoa 22.
Natalis Linuma kwa niaba ya katibu tawala wa Mkoa wa Lindi Amesema mafunzo hayo ya kikao kazi Amesema anamshukuru sana Rais Samia kwa kutoa kuweza kutoa malekezo kwa wizaran ya katiba na sheria kwakuhakikisha kunakua na program ya kutoa elimu kwa wanainchi kwa kuweza kupata msaada wa kisheria katika kutatua changamoto mbali mbali za kisheria.
Aitha Linuma ametoa wito kwa wataalamu hao waweze kuelewa namna ya kuweza kuwasaidia na kuwaelewesha wanainchi kwenye maeneo watakayo kwendaa.kwasababu wanainchi hao wanahitaji haki za binaadam na utawala Bora.
Pia Linuma amewataka wataalamu mufunzo hayo yakawe chachu na mwangaza Ili kwenda kupunguza migogoro kwenye maeneo mbali mbali ya Mkoa wa Lindi.
"Kwa hawa ambao wanapata mafunzo leo waweze kujifunza na kuelewa jinsi ya kuwaelewesha na kuwasaidia wanainchi kule wanakoenda Mkoa wetu wa Lindi ni miongoni mwa mikoa ambayo tunazo changamoto za kawaida na kisheria katika sehemu mbali mbali, kuhusu migogoro ya ardhi, Migogoro ya mirathi pamoja na maswala ya ndoa."
Nae Ester Msambazi Mkurugenzi huduma za msaada wa kisheria wizaran ya katiba na sheria Amesema kwa kushirikiana na wadau wanatekeleza kampeni yenyejina la mama Samia legal Aid kampeni ambayo inatekelezwa katka ngazi ya kijiji n jamii kwa lengo kuwafikia wanainchi walio maeneo ya pembezoni ambao hawapati huduma za kisheria.
Aitha Ester Msambazi Amesema kampeni imetokana na ombwe kubwa kwakua wanainchi wengi hawana uelewa juu ya msaada wa kisheria hata wanapokua wamepata changamoto wanakua hawajui wapi kwa kukimbilia na kutatua changamoto zao.
"Lengo la kwanza kabisaa tunataka wanainchi wapate uelewa kuhusuana na masuala ya kisheria na upatikanaji wa haki za kwa wanainchi kwa kupitia huduma za msaada wa kisheria mwanainchi yeyote ambae anahitaji msaada wa kisheria na anashindwa kwenda mahakamani kwasababutu hana muwakilishi Wala wakili basi atapata huduma hizo kwa kupitia msaada wa kisheria"Amesema Ester Msambazi
Andrew Munisi afisa aridhi mteule manispaa ya Lindi amesema kampeni hizo za msaada wa huduma za kisheria ya mama Samia itaenda kuondoa changamoto za kisheria pamoja na kutoa elimu kwa wananchi.
"Tunamatarajiao makubwa kama idara ya aridhi kunachangamoto nyingi sana kama migogoro ya wakulima na wafugaji,migogoro ya kifamilia kama watu wa aridhi tunamatarajiao ya kutoa msaada wa kisheria sekta ya aridhi"amesema Munisi
Munisi ameongeza kwakusema kwakiasi kikubwa wanaenda kutatua hizo changamoto watakapoenda kutoa msaada wakisheria.
"Kwakiasi kikubwa tunaenda kutatua hizo changamoto tutakapotoa msaada wakisheria wananchi wataelewa nini chakufanya lakini kama kunamtu anataka ushauri wakisheria hivyo itamsaidia kuondoa hizo changamoto.Hii kampeni itaenda kuleta usawa,utulivu,haki na maendeleo"amesema Munisi.
Na Fredy Mgunda, Lindi.
Kampeni ya kitaifa ya msaada wa kisheria ya mama Samia imezinduliwa rasmi katika mkoa wa Lindi kwa kuhakikisha wananchi wananufaika kwa kupata haki zao ambazo awali walikuwa wamenyang'anywa.
Akizungumza kampeni hiyo waziri mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa majaliwa alisema kuwa kampeni hiyo imefanikiwa kutatua migogoro mingi iliyodumu kwa muda mrefu hadi hivi sasa.
Waziri mkuu alisema kuwa Kampeni hiyo imeongeza wigo wa utoaji haki kwa wananchi ambao walikuwa hawana uwezo wa kupata haki kwa kukosa fedha hivyo sasa kila mwananchi anapata haki bure.
Alisema kuwa huduma hiyo ya kampeni ya kitaifa ya msaada wa kisheria ya mama Samia inatolewa bure bila malipo yoyote yale kwa kuwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suhulu Hassan.
Majaliwa alisema kuwa zaidi ya wananchi milioni 1.3 hadi sasa wamefikiwa na huduma hiyo huku wanaume wakiongoza kufika kupata huduma hiyo kuliko wanawake.
Aliwasisitiza wananchi wa mkoa wa Lindi kujitokeza kwa wiki kupata huduma ya kisheria kwa siku 9 kwenye kila wilaya na kufanikisha wananchi kupata haki zao.
Na Josephine Maxime- Dar es Salaam
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mheshimiwa Dkt. Doto Biteko ameagiza Mwanafunzi Mirabelle Msukari na Wenzake wa Shule ya Msingi Sun Rise iliyopo Wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam kupelekwa katika Mradi wa kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) ili kujifunza zaidi kwa Vitendo namna mradi huo unavyozalisha Umeme.
Mheshimiwa Biteko amesema hayo leo Februari 18 kwa njia ya simu baada ya Naibu Waziri wa Nishati Mheshimiwa Judith Kapinga kutembelea shule hiyo kwa lengo la kumpongeza mwanafunzi huyo ambaye video yake ilijizolea umaarufu kupitia mitandao ya kijamii ambapo Mirabelle alielezea kwa ufanisi juu ya miradi mbalimbali ya umeme inayotekelezwa nchini ukiwemo mradi wa Julius Nyerere.
‘’Sisi tukupongeze na tumefurahi kwa umri wako unafuatilia masuala ya Nishati, sasa tutakupeleka kuliona Bwawa la Julius Nyerere uone Umeme unavyozalishwa ili uendelee kujifunza zaidi. Sisi tunatamani kukuona ukifanikiwa zaidi,” amesema Mhe. Biteko
Kwa Upande wake Naibu Waziri wa Nishati Mheshimiwa Judith Kapinga amesema Miradi hii ya kimkakati ambayo inatekelezwa nchini ni jitihada za Serikali chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dokta Samia Suluhu Hassan ambaye ameonesha dhamira ya dhati kuendeleza miradi ya umeme nchini ukiwemo mradi wa JNHPP ambao kwa sasa umefikia asilimia 99.8.
“Wakati Mheshimiwa Rais anaingia madarakani, Mradi wa Julius Nyerere ulikuwa asilimia 33, leo tunavyozungumza umefikia zaidi ya asilimia 99 na mashine nane tayari zimeingizwa kwenye gridi ya Taifa. Imebaki mashine moja pekee ambapo mradi uko mbioni kukamilika,” amesisitiza mheshimiwa Kapinga
Nae Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa wateja Bi. Irene Gowelle akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) , amesema wamepokea kwa vitendo agizo la Mheshimiwa Dkt. Biteko la kuhakikisha mwanafunzi huyo anafanya ziara katika Mradi wa Julius Nyerere ambapo pia amefafanua kuwa elimu na taarifa zinazotolewa na TANESCO zinawafikia walengwa kwa usahihi.
“Hatua hii inatupa nafasi ya kuona kwamba elimu na taarifa mbalimbali tunazozitoa zinawafikia moja kwa moja makundi mbalimbali i?wakiwemo watoto na ndio maana mmeweza kuona Mirabelle akizungumza kwa ufasaha.
Sisi kama Shirika la Umeme tutaendelea kufanya hivyo” amefafanua Bi. Gowele
Mwanafunzi huyo licha ya pongezi ,amepewa zawadi mbalimbali ikiwemo Komputa Mpakato (Laptop) pamoja na fedha kiasi cha Shilingi Milioni Mbili.
Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Mhe. Mrisho Gambo, Leo Jumatano Februari 19, 2025 wakati akizungumza na na Wazee wa Wilaya ya Arusha amehimiza wananchi wa Mkoa wa Arusha kumchagua kwa kishindo Rais Samia Suluhu Hassan kwenye uchaguzi Mkuu ujao, akisema Mkutano Mkuu wa CCM haukukosea kumpitisha kuwa Mgombea pekee kwenye uchaguzi huo.
Mradi huo ulio chini ya udhamini wa ubalozi wa Netherlands umezinduliwa Februari 18,2025 Mkoani Lindi ambapo utatekelezwa kwa kipindi cha mwaka mmoja ukijikita kuboresha ushirikiano baina ya vyombo vya ulinzi katika Mkoa wa Lindi hasa kwenye Wilaya ya Nachingwea na Ruvuma kwa Wilaya ya Nyasa.
Balozi wa Uholanzi nchini Tanzania Wiebe de Boer amesema inatia moyo kuona kila chombo kinafanya kazi na shirika hilo ili kuileta jamii karibu na kushiriki katika masuala ya ulinzi na usalama kwenye maeneo yao.
Mkurugenzi mtendaji wa shirika hilo la Global Peace Foundation Tanzania (GPF)Hussein Sengu (Wakili)amesema malengo makubwa ya mradi huo ni kuboresha masuala ya ulinzi na usalama kwa kushirikisha polisi jamaii na wanajamii wakiwemo wanawake na vijana ili waweze kushiriki katika masuala hayo kwenye jamii zinazowazunguka.
Aidha,ameeleza kwamba kupitia mradi huo wanakwenda kuboresha mbinu na ujuzi wa kiutendaji miongoni mwa maofisa wa polisi kuhusu ulinzi shirikishi kwa kutoa mafunzo maalum kwa maofisa hao.
Akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Lindi,Mkuu wa Wilaya ya Lindi Victoria Mwanziva amesema zipo dhana mbalimbali ikiwemo ya kufumbia macho matukio ya uhalifu na kuyamaliza nyumbani kimya kimya hali inayosababisha kuendelea kushamiri kwa matukio hayo na uwepo wa mradi huo wenye lengo la kuongeza ushirikiano kati ya polisi na wanajamii wanaenda kutatua hilo.
Nae,Naibu Kamisha wa Jeshi la Polisi na Mkuu wa dawati la ushirikishwaji Kamisheni ya Polisi jamii kutoka Makao Makuu ya jeshi hilo Dodoma Henry Mwaibambe,amesema wamepokea mradi huo ikiwa ni mwendelezo wa miradi walionao kwani unakwenda kufanya kazi kwenye kata ambayo tayari askari wao wapo hivyo amewahimiza wananchi kuendelea kushirikiana na jeshi la polisi kuibua changamoto mbalimbali kwenye jamii ambazo zimekuwa na sura ya uhalifu ili ziweze kutafutiwa ufumbuzi.
Kwa upande wa wakuu wa Wilaya ya Nchingwea Mohamed Moyo na Nyasa Peres Magiri ambazo mradi huo unakwenda kutekelezwa,wameshukuru serikali ya Uholanzi wakishirikiana na Shirika la Global Peace Foundation kwa kuwapelekea mradi huo wakiamini utakwenda kuongeza uelewa na uzalendo kwa jamii na hivyo kupunguza changamoto za uhalifu katika maeneo yao.
Moyo Amesema anamshukuru kupelekwa mradi huo wilaya Nachingwea na kuahikutoa ushirikiano na jeshi la polisi katika utekelezaji wa miradi huo.