Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Na.Alex Sonna-KISARAWE

MBUNGE wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, amewaomba wananchi wa Kisarawe na watanzania kwa ujumla kumuombea Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa ana maono makubwa ya kuwatumikia Watanzania na kulisukuma Taifa mbele kimaendeleo.

Dkt. Jafo ametoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza katika kikao maalum cha Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe, kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

“Niwaombe wajumbe wa Halmashauri Kuu kuhakikisha tunamuombea Rais Dkt. Samia kwa kuwa ana kazi kubwa ya kuwaletea maendeleo Watanzania na kuhakikisha Taifa letu linaendelea kusonga mbele,” amesema Dkt.Jafo

Ameongeza kuwa amani na usalama ni nguzo muhimu za maendeleo ya kiuchumi, hivyo ni wajibu wa kila Mtanzania kumuombea Rais na Taifa kwa ujumla.

“Bila amani na usalama, nchi yetu haiwezi kupata mafanikio ya kiuchumi. Nawaomba wananchi wa Kisarawe na Watanzania kwa ujumla tuendelee kumuombea Rais wetu na Taifa letu, kwa sababu kiongozi wetu mwenye maono ni Rais Samia, na lazima tumuombee ili nchi yetu iendelee kusonga mbele,” amesema Dkt. Jafo

Awali, amesema baada ya ushindi huo, chama na serikali vimeanza rasmi awamu mpya ya kazi kwa kipindi cha miaka 5, huku akiendelea na utekelezaji wa majukumu ya maendeleo jimboni kupitia mkakati wao wa ‘Chaka kwa chaka’.

“Tumeanza kazi kwa mara nyingine katika msimu wa 2025–2030. Tumeendelea na kazi za jimboni, tukikutana na viongozi wa kada mbalimbali wakiwemo viongozi wa kisiasa, watendaji wa halmashauri, madiwani pamoja na wenyeviti wa vijiji na vitongoji vya Wilaya ya Kisarawe,” amesema Dkt. Jafo.

Ameeleza kuwa kikao hicho na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ni cha muhimu sana kwa kuwa ni timu inayobeba jukumu la kuimarisha uhai wa chama pamoja na kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.

Aidha, Dkt. Jafo ametumia mkutano huo kueleza mikakati ya maendeleo ndani ya Wilaya ya Kisarawe, ikiwemo kuboresha sekta za afya, elimu, barabara, maji, umeme pamoja na ujenzi wa viwanda vya kati na vikubwa kwa lengo la kuongeza thamani ya mazao na kutoa ajira kwa vijana.

“Wilaya ya Kisarawe ipo na mtazamo mpya wa maendeleo, kuhakikisha tunasonga mbele kwa kasi zaidi katika kuboresha maisha ya wananchi,” amesema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kisarawe, Khalfan Sika, amesema jukumu la wanachama wa CCM ni kuipa ushirikiano Serikali ili kuhakikisha Ilani ya Uchaguzi inatekelezwa kikamilifu.

“Ilani tuliyowapa Mhe. Rais, Mbunge na Madiwani ni Ilani ya CCM. Utekelezaji wake ndio mafanikio na suluhisho la kero za wananchi. Huu ni mkataba kati ya wananchi na CCM,” amesema.

Ameongeza kuwa Ilani hiyo ni maelekezo ya chama ambayo Serikali imepewa dhamana ya kuyatekeleza kwa vitendo, huku akimpongeza Rais Samia na Mbunge Jafo kwa maono makubwa waliyonayo ya kuwaletea maendeleo wananchi.

Kadhalika, Mwenyekiti huyo amempongeza Dkt. Jafo kwa uungwana wake wa kukutana na Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya mara baada ya kumalizika kwa shughuli za uchaguzi.

“Mara nyingi baada ya uchaguzi, watu waliobeba mzigo mkubwa wa kampeni hawakumbukwi kushukuriwa. Nimpongeze sana Mbunge Jafo kwa kuona umuhimu wa kukutana na wajumbe hawa na kuwashukuru,” amesema.

Amefafanua kuwa katika Wilaya ya Kisarawe, kampeni zilifanyika katika vijiji vyote 84 na mikutano 105 ilifanyika katika ngazi ya vijiji na vitongoji, kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanaielewa Ilani ya CCM na sababu za kuchagua chama hicho.

Amesema katika matokeo ya uchaguzi, Rais Samia alipata ushindi wa asilimia 98 huku Mbunge Jafo akipata asilimia 95, hali inayoonesha imani kubwa ya wananchi wa Kisarawe kwa viongozi wao na Chama Cha Mapinduzi.

“Jukumu letu sasa ni kusimamia utekelezaji wa Ilani, kwa sababu uchaguzi mwingine utafanyika mwaka 2030, na wananchi watataka kuona ni kwa kiasi gani tumetekeleza ahadi tulizotoa,” amesema.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwasili katika ukumbi  kwa ajili ya kuzungumza na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

 

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kisarawe Khalfan Sika,wakati ,akizungumza   na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Katibu  wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kisarawe Bi.Josephine Mwanga wakati akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kisarawe, Aidan Kitare wakati akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

 

Wajumbe wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo (hayupo pichani) wakati,akizungumza  na Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,kikao kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja  Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,mara baada ya kuzungumza nao kikao  kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja  Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,mara baada ya kuzungumza nao kikao  kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja  Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,mara baada ya kuzungumza nao kikao  kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja  Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,mara baada ya kuzungumza nao kikao  kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja  Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,mara baada ya kuzungumza nao kikao  kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja  Wajumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kisarawe,mara baada ya kuzungumza nao kikao  kilicholenga kuwashukuru wajumbe kwa mchango wao katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Na Mwandishi Wetu, Singida Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Dkt. James Mwainyekule, amewataka watumishi wa Ofisi hiyo kutekeleza majukumu yao kwa weledi na uadilifu wa hali ya juu ili kukidhi matarajio ya Watanzania kwa ufanisi na tija zaidi. Ametoa rai hiyo leo 17 Desemba 2025 wakati wa kikao cha baraza la Wafanyakazi wa EWURA kilichofanyika mkoani Singida. “ Tufanye kazi kwa ushirikiano, tutoe huduma kwa weledi na tuendelee kuwa waadilifu. Tukumbuke pia sisi ni timu moja, tuepuke majungu na manung’uniko mahali pa kazi kwani husababisha kutokuelewana na hivyo kuathiri utendaji,” alisema Dkt. Mwainyekule. Aliongeza kuwa wafanyakazi wote wana wajibu wa kutekeleza majukumu yao kwa uwazi, ufanisi na tija ili kuhakikisha ubora na upatikanaji endelevu wa huduma za umeme, mafuta, gesi asilia na maji na usafi wa mazingira. “Ifahamike kuwa, baraza la wafanyakazi ni chemchemi ya mawazo mapya. Tutafanya mabadiliko ya namna tunavyofanya kazi, ili tuendane na wakati wa sasa, hatuwezi kufanya kazi kama ambavyo tulifanya miaka iliyopita,” alisema. Naibu Katibu Mkuu TUGHE Taifa, Mha. Amani Msuya, aliipongeza EWURA kwa maandalizi mazuri ya kikao cha baraza la wafanyakazi na kwa kulipa umuhimu suala la ushirikishwaji wafanyakazi.
NA EMMANUEL MBATILO, DODOMA 

Umoja wa Kitaifa wa Asasi za Kiraia wa Shule Salama (NCSS), unaoratibiwa na shirika la HakiElimu, umetoa wito kwa wadau kuunga mkono jitihada za pamoja za kumlinda mtoto dhidi ya vitendo vya ukatili.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Na.Alex Sonna-,Kisarawe

MBUNGE wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, ametangaza kuanza kutolewa kwa Tuzo ya Jafo ya Ufanisi wa Juu kwa Mradi wa Maendeleo, ikiwa ni mpango wa kutambua na kuhamasisha utendaji bora, ubunifu na uwajibikaji miongoni mwa Wenyeviti wa Vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe.

Akizungumza na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wilayani humo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo, Dkt. Jafo amesema tuzo hiyo (JAFO’s High Perfomance Development Project Award), inalenga kukuza ufanisi wa juu katika usimamizi wa miradi ya maendeleo, kuongeza uwajibikaji na kuibua ushindani chanya miongoni mwa wenyeviti hao.

Amesema tuzo hiyo itatolewa kila mwaka ili kumtambua na kumzawadia Mwenyekiti au Mwakilishi wa Kijiji aliyeonesha utendaji wa hali ya juu, ubunifu na matokeo yanayopimika katika kusimamia mradi ndani ya Halmashauri hiyo

“Tuzo hii ni kwa Mwenyekiti wa Kijiji au mwakilishi wa kijiji atakayeng’ara kwa mafanikio ya kipekee katika kuibua, kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kasi, hususan ile yenye athari chanya katika sekta za afya, elimu, kilimo, biashara, michezo na miundombinu, ninalenga kuhamasisha viongozi wetu wa vijiji kufanya kazi kwa bidii, ubunifu na uwazi zaidi. Tunataka kuona matokeo halisi yanayogusa maisha ya wananchi,” amesema Dkt. Jafo.

Mbunge huyo ameongeza kuwa tathmini ya mshindi wa tuzo hiyo itazingatia vigezo mbalimbali, ikiwemo utekelezaji wa miradi yenye athari kubwa ndani ya muda uliopangwa, maboresho yanayopimika katika utoaji wa huduma, usimamizi bora wa rasilimali, ushiriki wa wananchi na wadau pamoja na uendelevu wa miradi iliyotekelezwa.

Amesema pia tuzo hiyo itahusishwa moja kwa moja na mradi au mpango mahsusi wa maendeleo, ambapo ushahidi wa matokeo kama ongezeko la ufanisi, ubora wa huduma na kuridhika kwa wananchi utatumika kama msingi wa tathmini.

Awali, Dkt. Jafo amepongeza mchango mkubwa wa Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji, akisema wao ni kiungo muhimu katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya serikali ngazi ya msingi.

Ameeleza kuwa mkutano huo ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wake wa uongozi wa miaka 2025–2030, akisisitiza dhamira ya kufanya kazi kwa kasi ya ‘chaka kwa chaka’ ili kuharakisha maendeleo vijijini.

Amebainisha kuwa kupitia usimamizi bora wa viongozi wa vijiji, azma ya kuhakikisha kila kijiji kinakuwa na zahanati ifikapo mwaka 2030, pamoja na kuimarisha sekta ya elimu na shughuli za kiuchumi, itawezekana kwa vitendo.

“Ndani ya miaka mitano ijayo tunahitaji kufanya kazi kwa mchakamchaka, kuanzia ukusanyaji wa mapato hadi matumizi yake, ili miradi ya maendeleo isimamiwe kwa ufanisi na kuleta matokeo yanayoonekana kwa wananchi,” amesisitiza.

Nao baadhi ya wenyeviti wa vijiji na vitongoji wamempongeza Dkt Jafo kwa ubunifu huo, wakisema kuwa utaongeza hamasa na ushindani chanya wa kimaendeleo katika Halmashauri ya Kisarawe.

Wamesema tayari wamejipanga kikamilifu kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao ili kuongeza ufanisi na hatimaye kuibuka washindi wa tuzo hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,aakiwasili katika ukumbi wa halmashauri wilaya ya Kisarawe kwa ajili ya kuzungumza na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri hiyo ya  ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, Nyahori Mahumbwe,wakati ,akizungumza  na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri hiyo  ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kisarawe, Aidan Kitare,,wakati ,akizungumza  na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri hiyo  ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo akimsikiliza Afisa Utumishi wa halmashauri ya wilaya ya Kisarawe Bi.Sabra Mwankenja wakati ,akizungumza  na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri hiyo  ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzungumza  na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzungumza  na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzungumza  na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzungumza  na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzungumza  na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo pamoja na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayoifanya.