Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) kwa kushirikiana na wataalam wa jiosayansi kutoka Chuo Kikuu cha Goethe  cha nchini  Ujerumani wafanya utafiti wa jiosayansi katika Mlima Oldoinyo Lengai. 

Akielezea kuhusu utafiti huo, Mkurugenzi wa Huduma za Jiolojia GST, Dkt. Ronald Massawe amesema kuwa, Mlima Oldoinyo Lengai ni moja ya milima ya volkano ambayo ipo hai, lakini pia ni mlima pekee duniani ambao volkano yake inatoa lava ya aina ya “natrocarbonatite” ambapo lava hii inapokauka na kugeuka vumbi, huweza kuwa na madhara ya kiafya kwa binadamu na wanyama, hasa inapovutwa kupitia hewa. 

Akifafanua  kuhusu malengo  ya utafiti huo, Dkt. Massawe amesema kuwa, kulingana na mfumo wa kijiolojia ndani ya mlima, utafiti huo una malengo makubwa matatu ambayo ni: kuchunguza muundo wa ndani wa volkano, kubaini maeneo ya hifadhi ya magma na njia zake, pamoja na kutambua mabadiliko ya tabaka la miamba katika Ukanda wa Ziwa Natron.

Lengo lingine ni kuongeza uwezo wa wataalamu wa ndani hapa Tanzania, ambapo itachangia kukuza uwezo wa rasilimali watu katika kufanya tafiti za jiosayansi hususan kwenye majanga asili ya jiolojia, na lengo la tatu ni kuimarisha ushirikiano na taasisi mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi katika kufanya tafiti za jiosayansi.

Dkt. Massawe amefafanua kuwa, katika awamu hii, jumla ya vituo 32 vya kufuatilia mwenendo wa mitetemo ya ardhi vimesimikwa katika eneo la mlima ambapo vituo hivyo vimewekwa katika mpangilio wa mstari wenye uelekeo wa upande wa Kaskazini-Magharibi/Kusini-Mashariki kupitia kwenye kilele cha mlima huo wenye urefu wa takriban mita 2,962 kutoka usawa wa bahari.

Sambamba na uelekeo huo, vipo baadhi ya vifaa vilivyosimikwa katika maeneo ya pembezoni na kwenye ulalo wa mlima.

Dkt. Massawe amebainisha kuwa, mtandao huu wa vifaa utanakili mitetemo ya ardhi inayosababishwa na nguvu za asili za mabadiliko ya jiolojia katika Ukanda wa Bonde la Ufa, pamoja na mitetemo inayotokana na fukuto la volkano.

Kuhusu manufaa ya kufanya utafiti huu, Dkt. Massawe ameendelea kuelezea kuwa, moja ya faida katika utafiti huu ni kwamba taarifa zitakazokusanywa katika kazi hii zitaongeza maarifa mapya kuhusu mfumo wa ndani wa volkano ya Mlima Oldoinyo Lengai na hivyo kuongeza uelewa wa hatari za kijiolojia na kuimarisha uwezo wa Serikali katika kukabiliana na majanga katika ukanda wa Ziwa Natron.

Akielezea kuhusu hali ya mlipuko katika mlima huo, Dkt. Massawe amesema kuwa, kwa mara ya mwisho Mlima Oldoinyo Lengai ulilipuka kati ya Julai, 2007 hadi 2008 na ulirusha majivu yaliyosambaa hadi umbali wa kilomita kumi (10).

Madhara yaliyojitokeza wakati wa mlipuko huo ni pamoja na vifo kwa wanyama, uharibifu wa mazingira ikiwemo maeneo ya malisho ya mifugo, pamoja na watu kuwashwa macho hadi umbali wa kilomita sabini kutoka kwenye mlima huo, alifafanua Mtaalam huyo.

Kwa kipindi kirefu GST imekuwa ikifanya tafiti mbalimbali zinazohusiana na majanga asili ya jiolojia ikiwemo maporomoko ya ardhi, matetemeko ya ardhi, mipasuko na mididimio ya ardhi kwa kushirikiana na taasisi za ndani na nje ya nchi.

Utafiti huo ulihusisha  wataalamu  mbalimbali akiwemo  Dk. Ronald Massawe na Gabriel Mbogoni kutoka GST pamoja na Prof. Georg Rumpker, Dr. Ayoub Kaviani,  Christoph Locker na Ms. Kamila Diaz kutoka Chuo Kikuu cha Goethe.







 

Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Andilile (kulia), akizungumza na watumishi wa Mamlaka hiyo wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja uliofanyika leo Oktoba 6,2025  katika ofisi za EWURA jijini Dodoma.

Na.Mwandishi Wetu-DODOMA

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imerahisisha upatikanaji wa vibali, leseni na utatuzi wa malalamiko kupitia mifumo ya kidijitali, hatua inayowawezesha wananchi kupata huduma popote walipo na kwa wakati bila kulazimika kufika ofisini.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Andilile, wakati akizindua maadhimisho ya wiki ya Huduma kwa Wateja, katika ofisi za EWURA, Dodoma, leo 6.10.2025.

“Tumeendelea kuboresha mifumo yetu ya kidijiti ambayo imeimarisha utoaji wa huduma kwa kasi zaidi na kwa wakati, na kuondoa kabisa malalamiko ya ucheleweshwaji yaliyokuwepo awali” alisema Dkt.Andilile

EWURA inatumia mifumo kadhaa ya kidijiti ikiwamo E- LUC, ambao unasaidia kupokea mrejesho na maoni ya wateja juu ya namna wanavyopokea huduma zinazodhibitiwa kutoka kwa watoa huduma wanaosimamiwa na EWURA. Mfumo huu unapatikana katika aplikesheni ya simu ya kiganjani.

Pia upo mfumo wa LOIS unaorahisisha maombi ya leseni, vibali vya ujenzi wa miundombinu ya bidhaa zinazodhibitiwa pamoja na uwasilishaji wa malalamiko yanayohusu huduma za nishati na maji.

Dkt Andilile amewataka wafanyakazi wa EWURA kuendelea kutoa huduma kwa weledi na kwa wakati ili wateja wake wafurahie zaidi huduma za udhibiti.

 

Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Andilile (kulia), akizungumza na watumishi wa Mamlaka hiyo wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja uliofanyika leo Oktoba 6,2025  katika ofisi za EWURA jijini Dodoma.

Baadhi ya wafanyakazi wa EWURA wakisikiliza kwa makini hotuba ya Mkurugenzi Mkuu, Dkt. James Andilile, wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja leo  Oktoba 6,2025 .

 

MWANASHERIA  Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza Johari,akizungumza leo Oktoba 7, 2025, jijini Dodoma, wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa mawakili wa serikali kuhusu masuala ya ubia, yaliyoandaliwa na Kituo cha Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC).

MWANASHERIA  Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza Johari,akizungumza leo Oktoba 7, 2025, jijini Dodoma, wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa mawakili wa serikali kuhusu masuala ya ubia, yaliyoandaliwa na Kituo cha Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC).

MKURUGENZI  wa Huduma za Sheria kutoka PPPC, Bi. Flora Tenga,akizungumza wakati wa  mafunzo ya siku tatu kwa mawakili wa serikali kuhusu masuala ya ubia, yaliyoandaliwa na Kituo cha Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC).

MKURUGENZI  wa Huduma za Sheria kutoka PPPC, Bi. Flora Tenga,akizungumza wakati wa  mafunzo ya siku tatu kwa mawakili wa serikali kuhusu masuala ya ubia, yaliyoandaliwa na Kituo cha Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC).

SEHEMU ya washiriki wakimsikiliza Mwanasheria  Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza Johari (hayupo pichani),wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa mawakili wa serikali kuhusu masuala ya ubia, yaliyoandaliwa na Kituo cha Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC).

MWANASHERIA  Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza Johari,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua mafunzo ya siku tatu kwa mawakili wa serikali kuhusu masuala ya ubia, yaliyoandaliwa na Kituo cha Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC).

Na Alex Sonna-DODOMA

MWANASHERIA  Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza Johari, amewataka mawakili wa serikali kuhakikisha maslahi ya taifa yanapewa kipaumbele wakati wa majadiliano na usimamizi wa mikataba ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP), ili miradi hiyo iwe na manufaa kwa Watanzania.

Mhe. Johari ametoa wito huo leo Oktoba 7, 2025, jijini Dodoma, wakati wa kufungua mafunzo ya siku tatu kwa mawakili wa serikali kuhusu masuala ya ubia, yaliyoandaliwa na Kituo cha Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC).

Mafunzo hayo yamelenga kuwawezesha mawakili wa Serikali  kuelewa kwa kina dhana ya PPP, sheria na mwongozo wake, pamoja na namna bora ya kusimamia, kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa miradi ya ubia kati ya Serikali na sekta binafsi.

Amesema kuwa  mafunzo hayo yanatarajiwa kuwajengea uwezo mawakili wa serikali kuhusu misingi ya miradi ya ubia, mfumo wa kisheria unaosimamia PPPC nchini, usimamizi wa vihatarishi, majadiliano na usimamizi wa mikataba ya ubia, pamoja na mifumo ya kifedha inayotumika katika utekelezaji wa miradi hiyo.

“Naamini baada ya mafunzo haya, mawakili wa serikali wataimarika katika kushauri, kujadiliana na kusimamia masuala ya kisheria kuhusu mikataba ya PPPC kwa ufanisi, huku wakihakikisha maslahi ya taifa yanabaki kuwa kipaumbele,” amesema Mhe.Johari

Aidha ameongeza kuwa mikataba ya ubia ni nyenzo muhimu katika kufanikisha maendeleo ya taifa, hivyo ni lazima iandaliwe kwa umakini na kwa kuzingatia maslahi ya muda mrefu ya nchi.

“Hii itasaidia kufanikisha malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ikiwemo kuboresha maisha na kuongeza kipato kwa wananchi,” amesisitiza Mhe. Johari.

Hata hivyo amesema kuwa  serikali imeweka misingi madhubuti ya kisheria na kitaasisi kusimamia miradi ya ubia, ikiwa ni pamoja na kutungwa kwa sera na sheria husika, ili kuhakikisha ubia huo unaleta manufaa kwa pande zote mbili.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Huduma za Sheria kutoka PPPC, Bi. Flora Tenga, amesema kuwa mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo mawakili wa serikali ili waweze kusimamia mikataba ya ubia kwa ufanisi na kuliepusha taifa na hasara.

“Mwanasheria Mkuu ndiye mwenye jukumu la kutekeleza mikataba ya ubia kwa niaba ya serikali. Hivyo ni muhimu mawakili wake wakapata mafunzo haya ili kuepuka makosa ya kisheria yanayoweza kulisababishia taifa hasara,” amesema Bi. Tenga.

Aidha ameongeza kuwa mikataba yoyote lazima ipitie hatua stahiki, ikiwemo tathmini ya thamani ya fedha, maandiko ya kisheria na ukaguzi wa kina kabla ya kutiwa saini. Kukosekana kwa mojawapo ya hatua hizo kunaweza kuleta changamoto kubwa.

Naye Mshiriki Moja kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw.Stanslaus Silayo,ametoa shukrani kwa Kituo cha PPPC kuwapa mafunzo hayo ambayo  yatawasaidia kuingia mikataba yenye tija kati ya serikali na sekta binafsi na kupunguza hatari ya hasara kwenye miradi ya ubia.

 


 Jina langu ni Caroline Wanjiku kutoka Nyeri. Kwa muda mrefu nilikuwa nikiishi maisha ya mateso niliyoshindwa kuyaelewa. Kila jambo nililojaribu halikufanikiwa. Nilipoteza kazi zangu mara kadhaa bila sababu, marafiki walinitenga, na hata familia yangu ilianza kuniogopa kana kwamba mimi ndiye chanzo cha mikosi.

Nilijaribu kila njia maombi, kufunga, na ushauri wa watu wa kawaida lakini hali yangu ilizidi kuwa mbaya. Nilijua hapa kulikuwa na kitu kisicho cha kawaida, kitu cha kiroho ambacho kilihitaji msaada wa kipekee.

Siku moja nilianza kupata ndoto za ajabu usiku. Nilikuwa naona watu wananifukuza, wengine wakinifungia mikono na miguu. Nilipoamka asubuhi nilikuwa nimechoka sana kana kwamba nilikuwa nimepigana vita usiku.

Kila mara nilihisi kama kuna kitu kinanifuatilia, na hata biashara ndogo niliyokuwa nimeanzisha ilianza kudorora ghafla. Nilipoteza wateja, mali, na hata wapenzi wa karibu walionekana kunikimbia. Nilianza kuwa na wasiwasi, nikaamini nimerogwa. Soma zaidi hapa 

 


Aitaka ifuatilie kampuni zilizoshika maeneo bila kuyaendeleza

Aipongeza kampuni ya Huaer International kwa uwekezaji.

Asisitiza uwekezaji  huo ni utekelezaji wa Maono ya Rais Dkt. Samia


WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Madini kufanya ufuatiliaji wa makampuni ya madini ambayo yameshilikilia maeneo kwa muda mrefu lakini hawajayaendeleza mpaka sasa yakiwemo makampuni matatu wilayani Ruangwa

Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa makampuni ya Nachu, Uranex na Paco Gems Ltd yanapaswa kusema hatma ya maeneo waliyoyahodhi kwa muda mrefu vinginevyo ardhi hiyo itarudishwa kwa wananchi.

Ametoa agizo hilo leo Jumanne (Oktoba 07, 2025) alipotembelea kampuni ya uchimbaji wa madini Huaer International Limited katika kijiji cha Ng’au Ruangwa mkoani Lindi.

“Kampuni ya Paco Gems tangu 2009 mpaka leo hakuna maendeleo, tunatoka Utanex pale Chunyu, wameshalipa fidia tangu 2012 lakini mpaka leo hii hakuna maendeleo yoyote, ipo kampuni ya Nachu ambayo ilipata heshima ya kusaini mkataba mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mpaka leo hii wamepotea na hakuna taarifa.”

Mheshimiwa Majaliwa ameipongeza kampuni ya Huaer International Limited ambayo imefanikiwa kuanza mchakato wa uwekezaji ndani ya kipindi kifupi baada ya kupata vibali vyote muhimu.

“Kampuni yako ambayo imeanza ukaguzi mwaka 2024, ukapata matokeo mwaka huohuo na kuomba vibali mwaka huohuo, leo mmeanza utekelezaji wa ujenzi na mmefikia hatua hii, ninyi mnapaswa kupongezwa na mnapaswa kuwa mfano wa makampuni haya mengine tata.”

Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa ujenzi wa kampuni hiyo ni utekelezaji wa maono ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuzalisha ajira kwa Watanzania kupitia uwekezaji. “Kampuni hii ndiyo inaanza na inaendelea na ujenzi mtakapokamilisha mtatoa nafasi ya Watanzania na Wana-Ruangwa kupata ajira hapa.”

Pia, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa vijana wa Kitanzania waliopata nafasi ya kufanya kazi katika kampuni hiyo kufanya kazi kwa bidii, weledi, nidhamu na uaminifu “Tunahitaji kuwahakikishia hawa wawekezaji kwamba tunaajirika na tunaweza kufanya kazi hizi.

Kwa Upande wake Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Lindi ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala ameishukuru Serikali kwa kuendelea  kufungua fursa za uwekezaji kwa mkoa wa Lindi na Tanzania kwa ujumla ambazo kwa kiasi kikubwa zimekuwa kichocheo cha maendeleo kwa wakazi wa maeneo hayo.

Amesema kuwa uwekezaji wa kampuni ya Huaer utakuwa ni moja ya fursa kubwa sio tu kwa uchumi wa Wilaya ya Ruangwa au Mkoa wa Lindi bali Tanzania kwa ujumla 

“Sisi upande wa Mkoa tunaendelea kuahidi kutekeleza sera zote za uwekezaji ambazo Serikali inaziweka na kuendelea kushirikiana na wawekezaji kwa kuweka mazingira rafiki ili waendelee kuwa kwa wingi katika mkoa wetu”

Thamani ya mradi huo ni dola za marekani milioni 20.










Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba, amekutana na wataalam kutoka Tume ya Taifa ya Mipango wakiongozwa na Naibu Katibu Mtendaji – Menejimenti ya Utendaji na Tathmini, Dkt. Linda  Ezekiel kwa lengo la kujadili namna ambavyo Wizara na Taasisi zake zimejipanga kutekeleza miradi ya kimkakati ya nishati inayochangia katika kufanikisha malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Msingi wa kikao hicho umetokana na  Sekta ya Nishati kuainishwa katika Dira 2050 kuwa ni moja ya  vichocheo vitano vitakavyoongeza kasi ya kufikia malengo ya Dira hiyo, ikielezwa kuwa Nishati ya uhakika ni nyenzo muhimu katika kuchochea maendeleo ya viwanda na shughuli mbalimbali za kiuchumi ili kuboresha viwango vya maisha kwa kutoa fursa za ajira kwa maendeleo endelevu katika jamii.

Katika kikao hicho kilichofanyika jijini Dodoma na  kuhusisha Watendaji kutoka Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati, 
Mha. Mramba amesema pande hizo mbili zimejipanga kuimarisha uratibu wa utekelezaji wa miradi ya nishati ili kuhakikisha kuwa  inalingana na vipaumbele vya kitaifa vya maendeleo. 

“Wizara ya Nishati inaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya nishati ukiwemo mradi wa  kusafirisha umeme wa kV 400 wa Chalinze–Dodoma, ambao unatarajiwa kukamilika Juni 2026. Huu ni moja ya miradi  itakayoleta chachu ya kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika katika mikoa ya Katavi, Kigoma na maeneo mengine ambayo yamekuwa yakikabiliwa na changamoto za upatikanaji wa umeme thabiti." Amesema Mhandisi Mramba

Amesema kukamilika kwa miradi ya kimkakati ya umeme kutawezesha kutimiza moja ya shabaha katika Dira 2050 ambayo inaelekeza kuwa matumizi ya umeme yanapaswa kuongezeka na 
kufikia wastani wa Kwh 3,000 kwa kila mtu kwa mwaka.

“Tunataka kuwa Taifa lenye nishati ya uhakika, nafuu na safi kwa watanzania wote,  ili kutimiza lengo hili Serikali inawakaribisha wadau wa sekta binafsi kuwekeza katika miradi ya nishati  kwa kuwa mafanikio ya sekta hii yanategemea ushirikiano wa wadau wote. " Amesisitiza Mhandisi Mramba

Katika kikao hicho, Wizara pia iliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa miradi ya Gesi Asilia na Mafuta,  Nishati Safi ya Kupikia, Umeme na Nishati Mbadala.

Kwa upande wake, Dkt. Linda  Ezekiel kutoka Tume ya Taifa ya Mipango, amepongeza ushirikiano uliopo kati ya Wizara ya Nishati na Tume hiyo akisisitiza kuwa mwelekeo wa miradi iliyoainishwa katika kikao hicho inaendana na malengo ya Dira 2050.

Amesema Tume itaendelea kufuatilia utekelezaji wa miradi hiyo ili kuhakikisha inachangia moja kwa moja katika ukuaji wa uchumi wa Taifa, kuboresha ustawi wa wananchi, na kulinda mazingira.

“DIRA ya 2050 inalenga kuwa na Taifa lenye uchumi wa kisasa, shindani na jumuishi. Sekta ya Nishati ni mhimili wa kufanikisha hayo yote, tunapongeza jitihada za Wizara ya Nishati katika kuhakikisha nishati inakuwa injini ya maendeleo." Ameeleza Dkt. Ezekiel

Kupitia kikao hicho, Wizara ya Nishati na Tume ya Taifa ya Mipango zimekubaliana kuendelea kushirikiana kwa karibu katika kupanga, kutekeleza na kufuatilia miradi yote inayogusa Sekta ya Nishati ili kuhakikisha Tanzania inafikia malengo ya  DIRA ya Maendeleo 2050 kwa ufanisi.







 


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila amemtaka Mkandarasi anayejenga daraja la Mohoro (MAC CONTRACTORS COMPANY LTD) lenye urefu wa mita 100 wilayani Rufiji mkoani Pwani kukamilisha ujenzi wa daraja hilo kwa wakati.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa daraja hilo, Mhandisi Mativila amesema fedha za mradi huo zipo hivyo, amemsisitiza Mhandisi Mshauri anayesimamia mradi huo kumsimamia Mkandarasi akamilishe kazi hiyo kwa wakati ili kutatua changamoto ya usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa kata ya Mohoro.

"Mliomba fedha kutokana na kazi hii kuongezeka, Serikali imeongeza fedha 50% ili kazi hii ikamilike, zipo kazi ndogondogo zinaweza kuendelea kufanyika, hivyo nasisitiza kazi hii ikamilike kwa wakati", amesema.

Aidha, amewataka Wakandarasi wazawa wajitahidi kukamilisha miradi kwa wakati ili Serikali iendelee kufanya kazi nyingi na Wakandarasi wa Kitanzania badala ya kuwatumia Wakandarasi wa nje.

Naye, Meneja wa TARURA mkoa wa Pwani, Mhandisi Ibrahim Kibasa amesema ujenzi wa daraja la Mohoro wenye thamani ya Shilingi Bilioni 17 unatakiwa kukamilika tarehe 24 Machi, 2026 na amemsisitiza Mkandarasi kuongeza kasi ya ujenzi wa daraja hilo likamilike kwa wakati ili wananchi waendelee kupata huduma katika maeneo yao.

"Mradi huu ukikamilika unaenda kuwasaidia wananchi wa Rufiji, shughuli nyingi za ukanda huu ni kilimo cha mazao mchanganyiko pamoja na viwanda hivyo kukamilika kwa daraja hili kutaongeza uzalishaji", amesema.

Kwa upande wake, Mhandisi Mkazi wa mradi huo, Emmanuel Mahimbo amesema ujenzi wa daraja hilo umefikia asilimia 50 ambapo wameshakamilisha ujenzi wa boksi kalavati mbili, nguzo nne na kuinua tuta la barabara ambapo ameeleza uchelewaji wa kazi umetokana na athari ya mafuriko ya mwaka jana pamoja na kupitia tena usanifu wa daraja hilo.

Nao, wakazi wa Mohoro, wameeleza furaha yao, wakisema daraja hilo litawasaidia wakazi wa vijiji vya Mohoro na Chumbi kusafirisha bidhaa zao,  litaepusha vifo vinavyosababishwa na mamba, litasaidia akina mama kujifungua hospitalini na kurahisisha usafiri wa watoto kwenda shule.

 


Wananchi waendelea kuitika kwa shauku kubwa kushiriki michezo na kupata elimu ya uhifadhi wa misitu.

Bonanza la michezo linaloendelea katika Shamba la Miti Sao Hill limeendelea kushika kasi na kuleta hamasa kubwa kwa wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Mufindi na maeneo ya jirani ambapo bonanza hili limekuwa ni jukwaa muhimu la kuelimisha, kuburudisha, na kuunganisha jamii katika kampeni endelevu ya kulinda na kuhifadhi misitu.

Michezo hii imeendelea Oktoba 6, 2025 katika Tarafa ya Nne ya Shamba Mgololo ambapo imeshirikisha timu kutoka vijiji mbalimbali ambazo ni Lugala, Misitu FC, Mabaoni, Magunguli, Kitasengwa, Mpanga na Luhunga.

Fainali ya mchezo huu imechezwa kati ya timu ya Misitu FC na timu ya Luhunga ambapo timu ya Misitu FC imefanikiwa kuibuka na ushindi wa penati 3 kwa 1 dhidi ya Luhunga baada ya mchezo huo kumalizika bila kufungana na hivyo kufanya timu ya Misitu FC kuwa mshindi wa jumla kwa upande wa tarafa ya Nne Mgololo.

Tangu kuanza kwake, michezo mbalimbali imekuwa ikiendelea kwa ushindani wa hali ya juu kwani timu kutoka vijiji vinavyopakana na msitu wa Shamba la Miti Sao Hill zimeonesha ari kubwa katika michezo kama mpira wa miguu, netiboli, kukimbia, kuvuta kamba, mashindano ya kula na kucheza draft ,na hivyo hali ya ushindani imekuwa ikichochea umoja na upendo baina ya washiriki huku furaha na shangwe zikitawala uwanjani.

Mbali na burudani, elimu kuhusu matumizi sahihi ya moto na njia bora za kulinda misitu imekuwa sehemu muhimu ya bonanza hili na  Wahifadhi Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kupitia Shamba la Miti Sao Hill wameendelea kutoa elimu hiyo kwa vitendo, wakisisitiza umuhimu wa kila mwananchi kuwa mlinzi wa mazingira. 

Hii imekuwa ni fursa adhimu ya kujenga uelewa wa pamoja kuhusu namna tunavyoweza kutokomeza  matukio ya moto misituni na washiriki na watazamaji wengi wameonesha kufurahishwa na ubunifu uliotumika katika kuandaa bonanza hili na  wengi wamesema kuwa michezo hii si tu burudani, bali pia ni shule ya maadili, ushirikiano, na uwajibikaji katika kulinda rasilimali za taifa. 

Bonanza limeendelea kuwa darasa la wazi linalounganisha michezo na elimu ya uhifadhi wa misitu na kadri siku zinavyosonga, idadi ya washiriki na watazamaji inaongezeka, jambo linaloonesha jinsi jamii inavyoitikia kwa moyo mmoja kwani watoto, vijana na watu wazima wamekuwa sehemu ya tukio hili, wakiendeleza ari ya ushiriki na kujifunza mambo mapya kuhusu utunzaji wa mazingira na uhifadhi wa misitu.

Bonanza hili linaendelea leo Oktoba 7, 2025 katika Tarafa ya Pili ya Shamba Ihefu kwa kukutanisha timu mbalimbali zinazolizunguka shamba katika tarafa hiyo

 


Katika mwendelezo wa kuchangia ukuaji wa  sekta nyingine  kwa maendeleo ya  Taifa na Jamii, shughuli za madini katika Mkoa wa Kimadini Chunya zimechangia ujenzi wa Uwanja wa Mpira wa Miguu wa Kisasa Wilayani humo kupitia michango ya wadau mbalimbali wa maendeleo wakiwemo wa Madini chini ya usimamizi ya Halmashauri husika.

Akizungumza katika mahojiano maalum na timu ya Madini Diary kutoka Wizara ya  Madini,  Mjumbe wa  Kamati ya maandalizi ya ujenzi wa uwanja  huo ambaye pia ni  Mkurugenzi  wa  KenGold Sports Club Keneth Mwakyusa amesema  kuwa, kujengwa kwa uwanja huo kunatokana na jitihada  zilizofanywa na  Halmashauri ya Chunya  kwa kushirikiana na wadau  mbalimbali wakiwemo wa  Sekta ya Madini zilizowezesha kujengwa kwa uwanja huo wa kisasa wa mpira wa miguu.

‘’ Tunaweza kusema mapato ya madini pia yamehusika katika ujenzi wa uwanja kwasababu wadau  waliochangia wapo pia wa madini  ambao  wametumia fedha zilizotokana na  na shughuli za madini lakini wapo na wadau wengine nje ya madini   na usimamizi  mkuu   umefanywa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chunya akisaidiana na kamati ya ujenzi,’’ amesema.

Ameongeza kwamba, mbali na uwanja huo kutegemewa kutumiwa na timu za Chunya ikiwemo KenGold unatazamiwa katika siku usoni   kutumiwa  kubwa kama Yanga,  Simba, Azam na nyingine  huku  uwepo wake  ukitarajiwa kuchochea ukuaji wa sekta nyingine  kama hoteli, usafiri, chakula na nyingine na kuongeza kwamba hatua iliyofikiwa hivi sasa ni uwekaji wa nyasi bandia.

Akizungumzia mwenendo wa timu ya Kengold amsema kwamba timu hiyo bado inaendelea na mazoezi  na  wana Imani  kwamba itapanda tena daraja na hivyo kutumia fursa hiyo kuwataka wadau wa michezo nchini wakiwemo wananchi wa Chunya kuendelea kuiunga mkono timu hiyo.

‘’Timu  yetu ipo inaendelea na mazoezi, kwa mfano hivi karibuni ilicheza mchezo wa kirafiki na Songwe na zote zilitoka suluhu ya  mabao mawili kwa  mawili 2-2 kwa hivyo bado tuna imani  ya kurejea ligi Kuu,’’ amesisistiza,’’.

Naye, Fundi wa uwanja huo Msafiri Napanja amesema kazi inayoendelea  hivi sasa ni uwekaji wa nyasi bandia iliyopangwa kufanyika ndani ya siku 30 huku maendeleo ya ujenzi wa uwanja yamefikia asilimia 85.

Awali, akizungumza na timu hiyo ya Madini Diary, Afisa Madini Mkoa wa Kimadini Chunya Mhandisi Laurent Mayalla amesema kwamba mchango wa Sekta ya madini wilayani chunya umeyagusa maeneo mengi ikiwemo ya michezo kutokana na ujenzi wa uwanja  huo.

  Vision 2030: Madini ni Maisha na Utajiri

  

Jina langu ni Mercy Naliaka kutoka Nakuru. Niliwahi kufika mahali nilihisi kama ndoa yangu inazama polepole. Mume wangu alikuwa amepoteza kabisa hamu ya kuwa karibu nami kimapenzi. Tulianza kulala kitanda kimoja lakini kila mtu akitazama upande wake.

Nilijua kitu hakiko sawa, na zaidi nilihisi kama kosa lilikuwa kwangu. Kila nilipojaribu kumvutia, alionekana kuchoka haraka au kupoteza hamu kabisa. Nilianza kuhisi aibu, nilikosa kujiamini, na hata marafiki waliona nimebadilika.

Kila usiku nilijaribu kufikiria ni nini nilichokuwa nikikosea. Nilinunua mafuta ya harufu nzuri, nguo za usiku za kuvutia, lakini bado hakukuwa na mabadiliko. Nilihisi kama nimekauka kabisa, na mwili wangu haukuwa na ule utelezi wa zamani.

Mume wangu alianza kutumia visingizio vya kazi nyingi, na hata nyakati tulipokuwa pamoja, hakuwa na ule moto wa zamani. Nilihisi kama mwanamke asiye na maana tena. Siku moja nikiwa nimechoka kabisa, nilimueleza rafiki yangu wa karibu kuhusu hali yangu. Aliniambia kwa utulivu kwamba tatizo hilo linaweza kutatuliwa. Soma zaidi hapa 

  

Jina langu ni Brian kutoka Eldoret, na hadi leo bado siamini kilichotokea. Nilikuwa nimepata mkopo mkubwa kupitia biashara yangu ya vifaa vya ujenzi, na nikafanya kosa kubwa zaidi maishani mwangu kumpa rafiki yangu deni kubwa bila maandishi.

Nilimwamini kwa moyo wote kwa sababu tulikua pamoja kama ndugu. Nilidhani urafiki wetu wa miaka mingi ungekuwa dhamana tosha. Lakini mambo yalibadilika haraka.

Nilipomkumbusha kuhusu deni, alianza kunikwepa. Kila mara nilimpigia simu, hakupokea. Nilimtumia ujumbe, hakujibu. Baada ya wiki chache, niliambiwa amehama kabisa mtaa wetu na hata kubadilisha namba. Nilihisi damu imenipanda kichwani.

Nilijua nimefilisika. Nilipoteza zaidi ya milioni moja, pesa ambazo zilikuwa mtaji wangu wa biashara. Nilianza kufungwa na madeni, nikashindwa kulipa kodi, na hatimaye nikafungwa biashara yangu. Soma zaidi hapa 

Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limezindua rasmi maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja kwa mwaka 2025, likiahidi kuendelea kuboresha huduma zake kwa ubunifu, kasi na ufanisi ili kukidhi mahitaji ya Watanzania na wateja wake wa kimataifa.


Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa wiki hiyo, Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa TTCL, Bi. Anita Moshi, amesema maadhimisho hayo ni sehemu ya kujitathmini na kuimarisha uhusiano kati ya shirika hilo na wateja wake.

“Wiki hii inatukumbusha wajibu wetu wa msingi wa kumweka mteja mbele kama kiini cha mafanikio ya TTCL. Tunajitathmini, tunasikiliza, na tunajifunza kutoka kwa wateja wetu,” amesema Bi. Moshi.

Maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja hufanyika duniani kote kila mwaka wiki ya kwanza ya Oktoba. Kwa mwaka huu, TTCL inasherehekea kuanzia Oktoba 6 hadi 10, 2025 chini ya kaulimbiu isemayo “Mission: Possible.”

Bi. Moshi amesema kaulimbiu hiyo imechaguliwa kuonyesha dhamira ya TTCL ya kuona kila changamoto kama fursa ya kuboresha huduma na kutafuta suluhisho la kudumu kwa manufaa ya wateja.

“Tutakuwa wabunifu, wenye bidii na maono. Kila mmoja wetu atakuwa sehemu ya suluhisho, na kwa pamoja tutahakikisha kila mteja anathaminiwa na kuhudumiwa kwa ubora wa hali ya juu,” amesisitiza.

Amesema TTCL imeendelea kutekeleza Mpango Mkakati wa kuboresha miundombinu ya mawasiliano nchini, ikiwa ni pamoja na kueneza Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano hadi kufikia wilaya zote za Tanzania, pamoja na ujenzi wa minara 1,400 vijijini ili kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma za mawasiliano bila vikwazo.

Aidha, amesema kupitia huduma ya “Faiba Mlangoni Kwako”, TTCL inaendelea kuwapatia Watanzania huduma ya intaneti ya kasi na uhakika inayokidhi viwango vya kimataifa.

Bi. Moshi ameongeza kuwa TTCL itaendelea kuwekeza katika teknolojia bunifu, kuboresha mifumo ya huduma kwa wateja na kuhakikisha Watanzania wote wanapata huduma bora popote walipo.

Amewahimiza wateja waendelee kutumia Kituo cha Huduma kwa Wateja kinachofanya kazi saa 24, pamoja na mitandao ya kijamii na maduka ya TTCL nchini kote, kupata ushauri na taarifa muhimu.

“Tutaendelea kuwa karibu na wateja wetu, kuwaheshimu, na kuhakikisha wanapata huduma bora zenye ufanisi na thamani,” amesema.

Bi. Moshi amewashukuru wateja wote walioliweka TTCL kama chaguo lao la mawasiliano kwa miaka mingi na kuwataka waendelee kushirikiana na shirika hilo katika safari ya maendeleo ya kidijitali.

“Wateja wetu ndiyo msingi wa mafanikio yetu. Tutaendelea kuwa bega kwa bega nao kufanikisha azma yetu ya pamoja — Mission: Possible,” alisisitiza kabla ya kutangaza rasmi uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja ya TTCL kwa mwaka 2025.






 

Mijadala kuhusu uhuru wa maamuzi na maadili barani Afrika inazidi kupamba moto, na Tanzania iko katikati ya mvutano wa kitamaduni wa kimataifa. Swali kuu linabaki: Nani anaamua jamii iishi vipi?

Kwa Umoja wa Ulaya (EU), jibu ni moja — haki za binadamu ni za wote, na usawa wa watu wenye mwelekeo wa jinsia au utambulisho wa kijinsia tofauti na ule wa kawaida wa kijamii unapaswa kulindwa kila mahali. Kwa Tanzania, viongozi na chama tawala CCM, jibu linapatikana katika misingi ya maadili, mila, na utamaduni wa kizazi kwa kizazi.

Mnamo Januari 2025, Huduma ya Utafiti ya Bunge la Ulaya ilisisitiza msimamo wa EU wa kuendeleza haki za jinsia na mwelekeo wa kijinsia duniani. Hata hivyo, ilikiri changamoto kwamba makubaliano na mataifa ya Afrika mara nyingi hayaelezi wazi masuala ya kundi hilo ili kuepuka mgongano wa kisiasa.

Wakosoaji nchini Tanzania wanaona hatua hiyo kama njama ya kifedha kupitia miradi ya mashirika yasiyo ya kiserikali, ikipuuza mahitaji muhimu kama afya, barabara na elimu.

Rais Samia Suluhu Hassan, alipowasilisha sera ya mambo ya nje mwezi Mei 2024, alionya wanaharakati wa kanda wasiingilie mambo ya ndani ya nchi. “Tusiruhusu Tanzania iwe shamba la bibi kwa kila anayepita kutoa tamko,” alisema.

Wakati huohuo, ripoti ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) ya 2024 ilionya kuhusu kupungua kwa uhuru wa kiraia na ongezeko la vitisho kwa wanaharakati na makundi yaliyotengwa, ikihimiza serikali kuoanisha sheria na viwango vya kimataifa. Serikali ilipinga ikisema ripoti hizo zinachochewa na ajenda za nje zinazotishia amani ya taifa.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dk. Dorothy Gwajima, alisisitiza kwamba kurejesha maadili ni jukumu la jamii nzima. “Kila taasisi inapaswa kushiriki katika kuimarisha maadili ya taifa,” alisema, akieleza kuwa wizara yake inaendeleza mwongozo wa malezi ya watoto unaolinda maadili ya Kitanzania.

Katika muktadha wa Kiafrika, familia ni zaidi ya wazazi na watoto; ni msingi wa utamaduni na nidhamu ya kijamii. Mpango wa Maendeleo wa Halmashauri ya Kilombero (2021–2026) unasema kuporomoka kwa familia kunaleta kuporomoka kwa maadili na milango kwa ushawishi wa nje.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza kwenye Maulid Kitaifa Tanga, alisema Tanzania imejengwa juu ya misingi ya amani, uzalendo na maadili mema. “Maisha ya Mtume yanatufundisha kuishi kwa maadili na kutegemea Mungu,” alisema, akisisitiza kulinda amani kama zawadi ya kiungu.

Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir bin Ali, aliwataka viongozi wa dini kuimarisha mahubiri dhidi ya vitendo vinavyohatarisha amani, akisema, “Amani si hiari, kila mmoja ana wajibu wa kuilinda.”

Kwa serikali, maadili si suala la kidini tu bali ni msingi wa usalama wa taifa. Ndiyo nguzo ya ibada, maisha ya kila siku, na maendeleo.

Mjadala huu umeingia pia katika siasa. Wagombea wa upinzani, kama Hassan Almas wa NRA na mgombea wa ADC, wameahidi sheria kali zaidi dhidi ya ushoga — ishara kuwa hoja hii imekita mizizi kwenye uwanja wa kisiasa.

Tanzania inaungana na mataifa mengine ya Afrika kama Ghana na Uganda, yanayopinga kile kinachoitwa “uenezi wa tamaduni za Magharibi.” Kwa CCM, kulinda amani na maadili ya ndani ni ushahidi wa ufanisi wa misingi ya taifa.

Kutoka falsafa ya Ujamaa ya Nyerere, misimamo ya Magufuli, hadi diplomasia ya Samia, msimamo unabaki uleule — Tanzania inaamua yenyewe jinsi jamii yake inavyoishi.

Na hivyo swali linaendelea kuzungumzwa kwenye ofisi, makanisa, misikiti na vijijini kote: Nani anaamua jamii iishi vipi?

  


Jina langu ni Carol kutoka Nakuru. Nilikuwa nimechoshwa na maumivu ya ndani moyoni na mwilini kwa sababu kila mara tendo la ndoa lilinifanya nihisi aibu badala ya raha. Mume wangu, George, alianza kubadilika. Alikuwa mtu wa furaha na upendo, lakini ghafla alianza kuepuka kunigusa.

Nilijua kitu hakiko sawa, ila sikutaka kukubali kuwa labda tatizo lilikuwa upande wangu. Nilihisi sipo sawa kama mwanamke aliye na afya. Kila jaribio la tendo la ndoa lilikuwa kama mateso.

Nilianza kutumia mafuta ya madukani na ushauri wa mitandaoni, lakini yote yalishindikana. Wakati mwingine nililia kimya kimya usiku nikimwona mume wangu amegeuka upande mwingine kitandani.

Nilihisi aibu na huzuni kubwa. Nilikuwa natamani kurudisha ule ukaribu tuliokuwa nao wakati wa uchumba, ule wakati hakulala bila kunishika mkono. Nilijua nikikaa kimya, ndoa yangu ingeyumba kabisa. Soma zadi hapa 

  


Jina langu ni Janet kutoka Arusha. Nilipendana sana na mpenzi wangu wa zamani, Kelvin. Tulikuwa tumedumu kwa zaidi ya miaka mitatu, na kila mtu aliyeniona naye alijua ni suala la muda tu kabla tuchumbiane rasmi. Lakini mambo yalibadilika ghafla.

Bila dalili yoyote, alianza kuniepuka, kupokea simu zangu kwa baridi, na hatimaye akaniambia hatuwezi kuendelea tena. Sikuamini. Nilijaribu kumuuliza nilikosea wapi, lakini aliondoka kimya kimya akaniacha nikiwa nimevunjika moyo.

Nililia kila usiku. Nilishindwa kula, nilishindwa kufanya kazi vizuri, na nilianza hata kupoteza hamu ya kuishi. Nilikuwa nikiingia Instagram na kuona picha zake na mwanamke mwingine.

Maumivu hayo yalikuwa makali sana. Watu waliniambia niusahau, lakini kila mara nilipofumba macho nilikuwa namuona. Nilijua bado nampenda, lakini sikujua nifanye nini ili anirudie. Soma zaidi hapa 

 

 

Dodoma

Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Dodoma, Bw. Pendolake Elinisafi, ameongoza watumishi wa mamlaka hiyo kushiriki katika bonanza maalum la michezo lililolenga kujenga na kuimarisha afya pamoja na kuongeza mshikamano miongoni mwao.

Bonanza hilo lililofanyika katika viwanja vya Kilimani Park jijini Dodoma, limehudhuriwa na watumishi kutoka vitengo mbalimbali vya TRA na lilipambwa na michezo ya kuvutia ikiwemo mpira wa miguu, kuvuta kamba, mbio za magunia, kukimbiza kuku, kutembea na yai kwenye kijiko, na mpira wa pete.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa bonanza hilo, Bw. Elinisafi alisisitiza umuhimu wa michezo katika kujenga afya bora na kuimarisha mahusiano kazini. “Michezo ni njia mojawapo ya kuimarisha afya ya mwili na akili, lakini pia huchangia katika kujenga mshikamano na ari ya kufanya kazi kwa pamoja kama timu,” alisema.

Watumishi walionekana kufurahia michezo hiyo ambayo iliibua ushindani wa kirafiki na kuongeza furaha, huku ikidhihirisha umuhimu wa matukio ya kijamii kazini. Washiriki walitunukiwa zawadi mbalimbali kama sehemu ya kutambua ushiriki wao na kuwahamasisha kuendelea na utamaduni wa kushiriki michezo kazini.

Bonanza hilo limeonesha kuwa, mbali na majukumu ya kikazi, TRA inatambua umuhimu wa shughuli za kijamii na kiafya kwa ustawi wa watumishi wake.