Waziri Mkuu Dkt Mwigulu Nchemba leo Januari 02, 2026 amekagua maendeleo ya ujenzi wa Bwawa la Maji Kidunda lililopo Mkoani Morogoro.
Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Dkt. Mwigulu amesema kuwa mradi huo unaakisi maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha nchi inakabiliana na changamoto ya upungufu wa maji hasa kutokana na mabadiliko ya tabia nchi.
Pia, ameiagiza Wizara ya Maji kuhakikisha mradi huo hausimami na unakamilika kwa wakati ili uanze kutoa huduma ya maji kwa wananchi.












Mbunge wa Jimbo la Lushoto Prof. Riziki Shemdoe ameishukuru Taasisi ya The Sunshine Muslims Volunteers (SMV) yenye makazi yake jijini Dar es Salaam kwa kufadhili matibabu ya macho kwa wananchi 811 wa Lushoto, mkoani Tanga, yaliyofanyika katika Hospitali ya Wilaya ya Lushoto kuanzia tarehe 29 hadi 31 Disemba, 2025.
Miongoni mwa wananchi hao 811 wa Jimbo la Lushoto waliopatiwa huduma ya uchuguzi wa macho, 104 walifanyiwa upasuaji wa macho, 312 walipatiwa miwani ya macho na 267 walipatiwa miwani ya kujikinga na mionzi ya jua.
Kutokana na huduma hiyo, Prof. Shemdoe ameishukuru taasisi hiyo leo Januari 01, 2026 jimboni Lushoto, wakati akizungumza na Mweka Hazina wa taasisi hiyo Dkt. Juma Mzimbiri ambaye ni Daktari katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili MOI.
Aidha, Mhe. Prof. Shemdoe ametoa shukrani zake za dhati kwa Daktari Bingwa wa macho na timu yake kwa kuendesha kambi hiyo ya matibabu kwa kushirikiana wa Mganga Mkuu wa Wilaya pamoja na madaktari na wauguzi wa hospitali hiyo ya wilaya ya Lushoto.
Akizungumzia diplomasia ya mashirikiano, Prof. Shemdoe amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutengeneza diplomasia ya mashirikiano na nchi mbalimbali, ambayo imewezesha wananchi wa majimbo ya Lushoto, Mlalo na Bumbuli kunufaika na huduma hiyo.
“Ninawaomba wadau hawa waendelee kutoa udhamini huu wa huduma ya matibabu ya macho, natamani uwe endelevu kila mwaka ili wananchi wengi zaidi wanufaike,” amesema Prof. Shemdoe.
Prof. Shemdoe ameongeza kuwa, ana imani kuwa wadau hao wataendelea kuona umuhimu wa kusaidia watu, kama ambavyo kauli mbiu yao inavyosema kuwa We Serve to Please Allah yaani wanasaidia ili kupata radhi ya Mwenyezi Mungu.
Naye, Mweka Hazina wa SMV Dkt. Juma Mzimbiri amesema kuwa, kambi ya matibabu imekuwa na manufaa makubwa kwa wananchi ambao wamejitokeza kwani wamepatiwa huduma ya uchuguzi wa macho, upasuaji wa macho, na kupatiwa miwani za macho pamoja na za kujikinga na mionzi ya jua.
Kuhusiana na jitihada za kutafuta wadau wengine, Dkt. Mzimbiri kumshukuru Prof. Shemdoe kwa kuendelea kushirikiana na taasisi yake ya SMV katika kutafuta wadau ambapo mdau YERYUZ DOKTORLARI alipatikana na kushiriki kutoa huduma katika kambi ya matibabu.
Nilianza kuamini kuwa labda mwili wangu hauwezi kuvumilia mabadiliko ya msimu au presha ya mwanzo wa mwaka. Kilichoniumiza zaidi ni kwamba hali hii ilinifanya nipoteze siku nyingi za kazi na kuvuruga mipango yangu.
Nilijaribu kila nilichojua. Nilikunywa dawa za kawaida, nikabadilisha mlo, na nikajaribu kupumzika zaidi. Kulikuwa na afueni ya muda mfupi, lakini Januari iliyofuata hali ilijirudia. Nilipoona hali hii inakuwa mzunguko, nilijua nilihitaji kufanya mabadiliko ya kweli, si ya kubahatisha.
Ndipo nilipopata ushauri wa kutafuta mwongozo tofauti. Soma Zaidi....https://kiwangadoctor.com/kiswahili/januari-kila-mwaka-nilikuwa-naumwa-sana-nilichobadilisha-kikaanza-kunilinda/
Nilipoteza amani, usingizi ukaanza kunikimbia, na hofu ya kesho ikatawala mawazo yangu.
Siku zilivyoendelea, nilijaribu kuonekana imara mbele ya watu, lakini moyoni nilikuwa nimechoka.
Kuomba kazi kuligeuka kuwa mzigo nikakataliwa mara kwa mara. Nilianza kujiuliza thamani yangu iko wapi, na kwa nini milango yote ilionekana kufungwa kwa wakati mmoja. Presha ilizidi, na nilihisi kama nimekwama mahali pamoja.
Ndipo nilipogundua kuwa nilihitaji si juhudi pekee, bali pia mwelekeo sahihi.Soma Zaidi...https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilipoteza-amani-baada-ya-kupoteza-kazi-nilichojifunza-kilinisaidia-kuendelea-bila-kukata-tamaa/
Niliamka kila asubuhi nikijiuliza nitapata wapi ya chakula, na nitashughulikaje kodi na gharama zingine zilizokuwa zinanifuata kwa kasi. Ilikuwa hali ya kuchosha kiakili na kihisia.
Nilijaribu kila nilichoweza kwa njia za kawaida. Niliomba kazi za vibarua, nikapiga simu kwa marafiki na jamaa, na hata nikajaribu kuuza vitu vidogo nyumbani. Kilichopatikana hakikutosha.
Kadri siku zilivyopita, hofu iliongezeka na kujiamini kulipungua. Nilihisi kama Januari ilikuwa inanimeza taratibu. Ndipo nilipoamua kutafuta ushauri tofauti.Soma Zaidi....https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilianza-januari-bila-pesa-ya-mahitaji-hatua-moja-ilinisaidia-kusimama-tena/
Awali nilidhani ni kazi nyingi au msongo wa mawazo wa kawaida wa maisha, lakini hali iliendelea kwa miezi. Kila nilipojaribu kupumzika zaidi, haikusaidia.
Nilianza kutumia dawa za kuongeza damu na nguvu nikiamini huenda ni upungufu wa lishe, lakini bado nilijikuta nikiwa dhaifu. Watu waliniona nikikaa kimya sana, nikiepuka mikusanyiko, na wengine wakaanza kudhani nina chuki au kiburi.
Ukweli ni kwamba mwili wangu haukuwa na nguvu, na akili yangu pia ilikuwa imechoka. Kilichoniumiza zaidi ni kwamba hata vipimo vya kawaida havikuonyesha tatizo kubwa.
Siku moja niliamua kutafuta ushauri tofauti. Soma Zaidi...https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilikuwa-nachoka-kila-siku-bila-sababu-nilipoelewa-chanzo-nguvu-zikarudi-polepole/
Kila mara nilipomuuliza kitu, alitabasamu tu bila kujibu kwa maneno, na kila hatua ndogo ya kujisimamia alikosa kufanya. Nilijawa na hofu kuwa kuna kitu kilikuwa kimekwama kwenye ukuaji wake.
Nilijaribu kumchochea kwa michezo na maneno, nikajitahidi kuzungumza naye kila siku na kumfundisha maneno mapya. Lakini maendeleo hayakuonekana kwa kasi niliyokuwa natarajia. Nilianza kuogopa kuwa huenda tatizo hili litaendelea kumzuia maisha yote yake ya awali, na hofu hiyo ilinifanya nikae usingizi mchana usiku.
Siku moja, nilipata ushauri kutoka Kiwanga Doctors. Nilipowaeleza hali yetu, walinisikiliza kwa makini na kuniuliza maswali ili kuelewa mtoto na mazingira yake vizuri.
Walinionyesha njia ya asili ya kusaidia mtoto kufikia maendeleo yake, ikijumuisha mazoezi rahisi ya kila siku, maneno ya kumtia moyo, na mbinu za kumsaidia kuimarisha misuli na mazoezi ya akili.
Nilifuata mwongozo wao kwa nidhamu na kwa usahihi. Ndani ya wiki chache, nilianza kuona tofauti. Mtoto wangu alianza kutembea hatua ndogo ndogo bila msaada, akaanza kusema maneno ya kwanza, na tabia yake ya kila siku ilibadilika.
Nilijisikia furaha isiyoelezeka kuona maendeleo yake yanapanuka hatua kwa hatua. Leo, nimefurahi kuona mtoto wangu akipata mwendo wake wa kawaida na kuonyesha vipaji vyake. Soma Zaidi..…https://kiwangadoctor.com/kiswahili/mtoto-wangu-alichelewa-kutembea-na-kuongea-hatua-moja-iliibua-maendeleo-yake/
WANANCHI Kijiji cha Laja katika Halmashauri ya Wilaya ya Karatu mkoani Arusha wameishukuru TASAF kukubali Mradi wa kupunguza Umaskini (OPEC) kutekelezwa katika Kiji hicho na kutoa fedha kutekelezwa mradi wa ujenzi wa mpya ya Shule ya Sekondari ambao umesaidia wanafunzi kuondokana na changamoto ya kutembea umbali wa kilometa nane kuisaka elimu.
Wakizungumza wakati wa ziara ya Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii(TASAF) Shedrack Mziray aliyekuwa akikagua utekelezaji wa mradi huo,wananchi wa Kijiji hicho wamesema kupitia Mfuko huo wamepata shule hiyo ambayo imeondoa changangamoto wanafunzi waliokuwa wanachaguliwa kujiunga Sekondari kutembea umbali mrefu.
Mkazi wa Kijiji cha Laja Christina Lucas amesema wakati shule haijajengwa katika maeneo hayo wanafunzi walikuwa wanateseka haswa watoto wa kike ambao ndio kundi lililokuwa linaathirika kwasababu wanakutana na adha nyingi.
“Uwepo wa shule hii imepunguza utoro usio wa lazima kwasababu kwa vyovyote vile mtoto akitoka nyumbani kilometa nane njiani anakutana na changamoto nyingi ,mara nyingine wanasindikizwa na bodaboda ambao baadhi yao ni hatari kwa usalama wa wanafunzi Wetu.
“Baada ya kupata mradi huu na shule kujengwa hivi sasa watoto wanakaa katika mabweni hivyo wanakuwa salama na ndio maana mpaka sasa hakuna mwanafunzi ambaye amepata ujauzito kwani wazazi tunafuatilia sana ,watoto wako salama.
Kuhusu TASAF amesema wananchi wa Kijiji cha Laja wanaipongeza na kuishukuru lakini wanatoa ombi la kujengewa majengo ya maabara pamoja na kuongezwa nyumba za walimu kwani zilizopo hazitoshi.
“Tunatamani kama itawezekana basi Rais wetu Dk.Samia Suluhu Hassan kupitia TASAF atuone tena kwa kutujengea Maktaba,mabweni na nyumba za walimu.Pia namshukuru Rais wangu kwa kuliona hili kwani hii shule hatukutegemea ingejengwa katika maeneo haya.
“Rais wetu ni msikivu ameangalia mpaka huku kwetu ambako tulisahaulika lakini sasa ametujengea shule ya kifahari ambayo pengine ilitakiwa ijengwe hata Karatu ila kwa sasa iko kijijini kwetu.”
Kwa upande wake Andrea Mtupa amesema wanafunzi wanaofaulu kwenda kidato cha kwanza walikuwa wanatembea umbali wa kilometa nane kwenda na kilometa nane wakati wa kurudi kila siku lakini hivi sasa TASAF kupitia mradi wa OPEC wamejengewa shule ya Sekondari ya kisasa.
Awali Ofisa Mtendaji Kijiji cha Laja Daniel Mpigachai amesema mradi wa ujenzi wa shule hiyo umegharimu Sh.774,946,675, ambapo TASAF kupitia OPEC awamu ya Nne walitoa fedha Sh. 659,505,275 na fedha Sh.115,441,400 ni mchango wa jamii ambao umejumuisha mchanga,Kokoto ,mawe,maji na nguvu kazi wakati wa ujenzi.
Kuhusu manufaa ya mradi amesema shule hiyo iliyosajiliwa Novemba 2023 ilianza rasmi mwaka 2024 kwa kupokea wanafunzi 26 wa Kidato cha kwanza, kwa sasa shule ina Jumla ya wanafunzi 63 ambao ni kidato cha kwanza na cha pili na wote wanakaa Bweni.
“Uwepo wa mradi huu umeondoa tatizo la utoro shuleni, wanafunzi kuongeza morali ya kusoma tofauti na awali walipokuwa wanasoma shule ya kata iliyo na umbali wa Zaidi ya kilometa 8 kutoka kijini kwetu, shule imepokea pia watoto wanaotoka viji vya jirani.
Aidha amesema kwa niaba ya Wananchi wa Kijiji cha Laja wanatoa ombi kwa TASAF kama fursa nyingine itajitokeza wanaomba mradi wa ujenzi Majengo mengine yaliyosalia kama Maabara, Maktaba, Nyumba nyingine za walimu na Madarasa.
Wakati huo huo Mkuu wa Shule ya Sekondari Laja Daniel Panga amesema shule hiyo iliyojengwa kisasa mbali kuondoa changamoto wanafunzi kutembea umbali mrefu imeleta hamasa kwa wanafunzi wanaosoma elimu ya msingi wanaamini ipo siku watajiunga na shule hiyo.








Nilihisi kama nyota yangu ilizimika, kila jambo nzuri nililokuwa nalo likiisha haraka. Hii haikuwa tu hisia; kwa kweli nilihisi nikiwa na mizigo ya kifedha, familia, na afya ambavyo viliniondoa mwelekeo.
Nilijaribu kila njia za kawaida za kuboresha mwaka: kuomba ushauri, kupanga bajeti, hata kufanya maombi ya haraka. Lakini kila kitu kilionekana kudumu kwa muda mfupi tu, na hatimaye hali yangu ikawa mbaya zaidi.
Usiku nililala na mawazo ya hofu, na kila asubuhi nikiamka, moyo wangu ulikuwa unitetemeka kwa kuogopa changamoto zilizokuwa zikisubiri.
Nilipofikia hatua ya kukata tamaa, niligundua kwamba nilihitaji msaada wa kipekee. Soma Zaidi...
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilihisi-nyota-yangu-inazimika-kila-januari-kilichonisaidia-kuilinda-mwaka-huu/
Mwenye nyumba alianza kunikumbusha kila wiki, na hofu ya kufungiwa nje ikawa sehemu ya mawazo yangu ya kila siku. Nilijaribu kila njia: niliomba marafiki, ndugu, nikatafuta kazi za muda, hata kuuza vitu vidogo, lakini pesa haikutosha.
Kila kitu kilionekana kunipinga. Nilihisi nimekwama, na muda ukienda mbio, nikawa na wasiwasi mkubwa kuhusu familia yangu na mustakabali wa watoto wangu.
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilianza-mwaka-mpya-nikiwa-na-kodi-imenifuata-hatua-nilizochukua-kuepuka-kufungiwa-nyumbani/
Nilijitahidi, nilijipanga, nilijaribu nidhamu kali, lakini kila nilichogusa kilionekana kukwama. Nilianza kujiuliza kama tatizo lilikuwa mimi au kuna kitu kingine kilikuwa kinanizuia.
Kadiri siku zilivyopita, nilipoteza morali. Kila nilipoangalia orodha ya malengo yangu, nilihisi mzigo moyoni. Niliona watu wakisonga, wakipata mafanikio mapema mwaka, nami nikabaki palepale.
Nilianza hata kuacha baadhi ya mipango niliyokuwa nimejipangia kwa sababu ya kuchoka moyo. Nilipotafakari kwa kina, niligundua kuwa nilikuwa nafanya kila kitu kwa nguvu nyingi lakini bila mwelekeo.
Nilihitaji msaada wa kunifanya nione kile ambacho macho yangu yalikuwa hayakioni. Soma Zaidi.........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilijiwekea-malengo-ya-mwaka-mpya-lakini-kila-kitu-kilikwama-nilipobadilisha-njia-mambo-yalisonga/
Kila siku niliamka mapema nikitafuta kazi mtandaoni na kutembea ofisi kwa ofisi, lakini milango ilikuwa imefungwa. Nilianza kujilaumu na kupoteza kujiamini. Nilihisi kama kuna kitu kinanizuia, hata pale nilipohitimu vizuri na kuwa na uzoefu.
Marafiki walinipita kimaisha, nami nikabaki pale pale. Wazo la kuanza mwaka mzima bila kazi lilinitisha sana.
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/mwaka-mpya-ulifika-bado-sina-kazi-uamuzi-nilioufanya-uliofungua-milango-ya-ajira/
Nilihofia siku ya kwanza ya muhula, walimu wakiuliza ada na watoto wangu wakirudishwa nyumbani kwa aibu.
Lakini kila nilipopata pesa kidogo, haikutosha. Muda ulikuwa unaenda mbio, na presha ilizidi. Usiku usingizi haukuja; nilikuwa nawaza mustakabali wa watoto wangu na kama wangepoteza masomo kwa sababu ya fedha.
Nilipofikia hatua ya kukata tamaa, nilibadilisha mbinu. Soma Zaidi.....
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/ada-ya-shule-ilinikaribisha-januari-bila-pesa-hatua-niliyopiga-kuokoa-watoto-wangu/
Na James Mwanamyoto - Lushoto
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amemuelekeza Mkandarasi Namis Cooperate Limited aliyepewa kandarasi ya Ujenzi wa Mahakama ya Wilaya ya Lushoto, kuwapatia vijana wazawa na akina mama kazi zote ambazo hazihitaji utaalam ili kutengeneza ajira zitakazowapatia kipato ambacho kitainua uchumi wao.
Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo leo Disemba 31, 2025 wilayani Lushoto, wakati wa hafla ya kupokea eneo la Ujenzi wa Mahakama ya Wilaya ya Lushoto iliyohudhuriwa na Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Prof. Elisante Ole Gabriel, viongozi wa mkoa na wilaya, watumishi wa Mahakama na wananchi wa Lushoto.
Prof. Shemdoe amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia kutoa kiasi cha Shilingi Bilioni 4.272 kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama hiyo ambapo ujenzi wake utawapatia kipato vijana watakaopewa kazi kwenye ujenzi wa jengo hilo.
“Mkandarasi ninakuomba huku nikikuelekeza kwamba, kazi zote ambazo hazihitaji expert wapewe vijana wetu wa hapa Lushoto ili tuweze kutengeneza ajira kwa vijana wetu wa hapa Lushoto,” Prof. Shemdoe amesisitiza.
Sanjari na hilo, Prof. amemtaka mkandarasi huyo kununua bidhaa za ujenzi zinazopatikana wilayani Lushoto ili kuongeza mzunguko wa fedha kwa wakazi wa wilaya hiyo ya Lushoto.
Pia, Prof. Shemdoe amemuelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto kuhakikisha anavikopesha fedha vikundi vya akina mama kupitia mikopo ya asilimia 10, ili vijishughulishe na biashara ya kuwauzia chakula vijana watakaoajiriwa kwenye mradi huo wa Ujenzi wa Jengo la Mahakama ya Wilaya ya Lushoto.
Aidha, Prof. Shemdoe ameushukuru ushirika wa kupanda kahawa Lushoto (coffee growers association) kwa uzalendo wao kwa kutoa bure eneo lenye ukubwa wa mita za mraba 6,269 kwa ajili ya Ujenzi wa jengo hilo la Mahakama.
Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Prof. Elisante Ole Gabriel amesema kuwa mkataba wa ujenzi wa Mahakama hiyo uliosaniwa leo hautakuwa na nyongeza ya muda wa mkataba wala nyongeza ya gharama, hivyo watasimamia ili kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa wakati kwani wananchi wanashauku ya kuhudumiwa katika jengo jipya la Mahakama ya Wilaya.
Mmoja wa wakazi wa Kata ya Magamba Wilayani Lushoto Bw. Salimu Omary amemshukuru Mbunge wa Jimbo la Lushoto ambaye ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe kwa kumuelekeza mkandarasi kuwapatia kazi vijana wazawa ili kupata kipato kitakachoendesha maisha yao.
Naye mkazi mwingine wa Wilaya ya Lushoto Bw. Shaban Adam Mbwana amesema yeye binafsi atachangamkia fursa hiyo ya ajira kwenye mradi huo wa ujenzi wa jengo la Mahakama kwani ana watoto ambao wanahitaji kulipiwa ada shuleni hivyo atakuwa mnufaika wa mradi huo.
Kiasi cha Shilingi Bilioni 4,271,942,834.98 kitatumika kukamilisha mradi huo wa Ujenzi wa Mahakama ya Wilaya ya Lushoto, ujenzi ambao unatarajiwa kutoa ajira kwa vijana, akina mama lishe na wafanyabiashara wa wilayani Lushoto.

Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari mkoani Dodoma (DPC) Bw.Musa Yusuf,akitoa neno la shukrani kwa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) mara baada ya waandishi wa klabu hiyo kupatiwa mafunzo kuhusu udhibiti wa huduma za nishati na maji yaliyofanyika leo Disemba 31,2025 jijini Dodoma.
Na.Mwandishi Wetu-Dodoma
Wanachama wa Klabu ya Waandishi wa Habari mkoani Dodoma, leo 31 Desemba 2025, wameishukuru Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kwa kuwapa mafunzo kuhusu udhibiti wa huduma za nishati na maji.
Mwenyekiti wa klabu hiyo, Musa Yusuf, ameipongeza EWURA kwa hatua ya kutoa mafunzo hayo, akibainisha umuhimu wa mkataba wa huduma kwa wateja, uvunaji wa maji ya mvua, na utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa matumizi ya nishati safi ya kupikia. Amesisitiza kuwa elimu waliyoipata wataitumia kwa kuelimisha umma.
“Asanteni sana EWURA kwa elimu hii, hakika imetufungua macho. Wenzangu wote ni mashahidi. Tunaomba mafunzo kama haya yaendelee,” amesema Bw. Yusuf.
Kwa upande wake Kaimu Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa EWURA, Wilfred Mwakalosi, amesisitiza umuhimu wa waandishi wa habari kuelewa masuala yanayodhibitiwa na EWURA, kwani yanagusa huduma ambazo kila mwananchi kwa namna moja au nyingine anazitumia.
“Ninyi waandishi wa habari ni daraja kati ya EWURA na wananchi, tuendelee kushirikiana katika kuelimisha umma ili kila mtumiaji wa huduma tunazodhibiti ajue haki na wajibu wake”. Amesisitiza Mwakalosi.















