Katika siku ya tano ya Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa (SabaSaba), Julai 2, 2026, Maafisa kutoka Wakala wa Vipimo (WMA) wamewatembelea wajasiriamali mbalimbali na kuwapatia elimu ya vipimo.

Wakiongozwa na Meneja wa WMA Mkoa wa Ki-vipimo Ilala, Bw. Muhono Nashon, wataalamu hao wa vipimo wamewaelimisha wajasiariamali wadogo wadogo namna sahihi ya uandishi wa alama katika vifungashio vya bidhaa zao ili zikidhi vigezo vya soko la kimataifa, pamoja na masuala mengine muhimu kuhusu vipimo.

Akizungumzia hatua hiyo, Meneja Mawasiliano wa WMA, Bi Veronica Simba amesema ni mojawapo ya mbinu za kuwafikia wadau mbalimbali wa vipimo wanaoshiriki katika Maonesho hayo.

Aidha, ameongeza kuwa, hatua hiyo pia imelenga kutekeleza maelekezo ya Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga ambaye awali alipotembelea Banda la Wizara pamoja na Taasisi zake, aliwataka watumishi hao kuwafuata wadau mbalimbali na kuwapatia huduma badala ya kusubiri wale tu wanaofika bandani.

Utaratibu huo umepongezwa na wajasiriamali waliofikiwa wakisema kuwa umewawezesha kupata elimu ya vipimo pasipo kulazimika kuacha mabanda yao kwenda katika banda la WMA kufuata huduma hiyo.

Utoaji elimu ya vipimo kwa wadau mbalimbali ni utaratibu wa kawaida ambao hutekelezwa siku zote na WMA kama sehemu ya majukumu ya kazi.





Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, George Masaju, akiwasilisha hotuba yake ya ufunguzi wa mafunzo ya usalama na afya kazini ya siku mbili (Julai 2-3, 2026) yanayotolewa na OSHA kwa Majaji wa Mahakama ya Rufani na Viongozi Waandamiziwa Mahakama.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Ngwaru Jumanne Maghembe (Mb.), ameshiriki Mhadhara maalum wa kuadhimisha Miaka 51 ya Uhuru wa Muungano wa Visiwa vya Comoro uliofanyika katika Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim, jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Reuben Kwagilwa akizungumza na waandishi wa vyombo vya habari Julai 2, 2026 Jijini Tanga kuhusu tamko la serikali kuhusiana na maandalizi ya Mkutano wa wa 12 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Nairobi (COP 12) unaotarajia kufanyika nchini kuanzia tarehe 6-9 Oktoba, 2026.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata tani 22.6 za dawa za kulevya, lita 30.5 na kilogramu 19.94 za dawa tiba zenye asili ya kulevya katika operesheni zilizofanyika nchini kati ya Mei na Juni mwaka huu, huku watuhumiwa 188 wakitiwa mbaroni na mali mbalimbali zinazohusishwa na biashara hiyo zikikamatwa.

Maofisa Utumishi nchini wameagizwa kushirikiana kwa karibu na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kwa kuhakikisha taarifa za watumishi wanaokaribia kustaafu zinajazwa na kuwasilishwa kwa usahihi na kwa wakati, ili kuondoa malalamiko yanayotokana na ucheleweshaji wa mafao.

Agizo hilo limetolewa jijini Arusha na Katibu Tawala Wilaya ya Arusha, Dk. Jacob Rombo kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa huo, Dk,Toba Nguvila, wakati akifungua mafunzo kwa waajiri na maofisa wanaoshughulikia masuala ya wanachama wa PSSSF kutoka taasisi mbalimbali za umma mkoani Arusha.

Dk, Nguvila alisema changamoto nyingi za ucheleweshaji wa mafao na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wastaafu husababishwa na taarifa kutokamilika au kutowasilishwa kwa wakati na waajiri.

Alisema maofisa utumishi wanapaswa kuhakikisha taarifa za watumishi wanaokaribia kustaafu zinahakikiwa na kuwasilishwa mapema ili kuwawezesha kupata mafao yao bila usumbufu. 

"Kila mtumishi anakuwa na kumbukumbu rasmi za utumishi wake kuanzia anapoajiriwa hadi anapostaafu. Ni muhimu nyaraka zote zihifadhiwe vizuri na zipatikane kwa urahisi pale zinapohitajika ili walipwe mafao yao kwa mkupuo," alisema.

Aliongeza kuwa maofisa utumishi wanapaswa kuwahudumia watumishi na wananchi kwa weledi, kutoa taarifa sahihi na kushughulikia changamoto zao kwa wakati ili kuondoa usumbufu usio wa lazima.

Kwa upande wake, Meneja wa PSSSF Kanda ya Kaskazini Magharibi, Yessaya Mwakifulefule, alisema mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo  maofisa hao kuhusu maboresho na huduma mpya zinazotolewa na mfuko, pamoja na kuimarisha ushirikiano katika kuharakisha uchakataji wa mafao.

Alisema mafanikio ya utaratibu wa kulipa mafao kwa wakati yanategemea ushirikiano wa waajiri, hususan maafisa rasilimali watu, kwa kuhakikisha taarifa za watumishi zinawasilishwa na kukamilishwa mapema.

"Mfuko wetu unaendelea na mpango wa kuhakikisha wastaafu wanalipwa mafao yao siku moja kabla ya kustaafu sisi PSSSF tunasema  'tunalipa jana' "

Alifafanua kuwa taarifa zote za michango zinapokamilishwa kwa wakati, mfuko huweza kukokotoa na kulipa mafao kwa asilimia 100 kabla ya mtumishi kustaafu rasmi na kutoa rai kwa maofisa rasilimali watu kuendelea kufuatilia na kuhakiki taarifa za watumishi wanaokaribia kustaafu ili kuhakikisha wanapata mafao yao kwa wakati na bila changamoto.













Na Mwandishi Wetu

IRINGA – Mbunge wa Jimbo la Ismani, Mhe. Emmanuela Mtatifikolo, amezindua rasmi maonesho na sherehe za Sabasaba zinazofanyika katika Kata ya Ilolo Mpya, Tarafa ya Pawaga, wilayani Ismani, huku akiwataka wananchi kutumia maonesho hayo kujifunza, kufanya biashara na kuimarisha mshikamano wa kijamii.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mhe. Mtatifikolo alisema maonesho ya Sabasaba ni fursa muhimu kwa wananchi kukutana, kubadilishana uzoefu, kuuza na kununua bidhaa mbalimbali pamoja na kujifunza fursa za maendeleo kutoka kwa washiriki na wageni wanaotoka maeneo mbalimbali nchini.

Aliwahamasisha wananchi wa Kata ya Ilolo Mpya na Jimbo la Ismani kwa ujumla kushiriki kikamilifu katika shughuli hizo, akieleza kuwa mbali na burudani, maonesho hayo yana mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa wananchi na kuimarisha mahusiano ya kijamii.

"Mnatakiwa kutumia maonesho haya kama jukwaa la kujifunza, kufanya biashara na kujenga mahusiano yatakayochochea maendeleo ya Ismani na wananchi wake," alisema Mtatifikolo.

Mbunge huyo pia aliwataka vijana kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kujiepusha na vitendo vinavyoweza kuhatarisha amani na utulivu wa nchi, akisisitiza kuwa maendeleo hayawezi kupatikana bila kuwepo kwa mazingira ya amani.
Aidha, aliwahimiza wazazi na walezi kuendelea kuwalea watoto katika misingi ya maadili, uzalendo na uwajibikaji ili kujenga kizazi kitakachochangia maendeleo ya taifa.

"Malezi bora ndiyo msingi wa kujenga taifa lenye vijana wenye nidhamu, uzalendo na uwezo wa kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya nchi," alisisitiza.

Maonesho hayo ya Sabasaba yanajumuisha shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi, zikiwemo maonesho ya bidhaa, michezo ya mpira wa miguu, ngoma za asili pamoja na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali.
Waandaaji wa maonesho hayo wamesema lengo ni kutoa fursa kwa wananchi kuonesha bidhaa na huduma zao, kuhamasisha biashara ndogondogo na kukuza vipaji vya vijana kupitia michezo na sanaa.

Sherehe hizo hufanyika kila mwaka baada ya wananchi kumaliza shughuli za uvunaji, zikiwa sehemu ya kuimarisha mshikamano wa jamii, kuchochea biashara na kutoa burudani kwa wakazi wa Ismani na maeneo jirani.

Wananchi waliohudhuria uzinduzi huo walieleza kufurahishwa na maandalizi ya maonesho hayo, wakisema yameendelea kuwa kichocheo cha maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika Jimbo la Ismani.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

WANANCHI wanaotembelea Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) mwaka huu watapata fursa ya kujionea kwa mara ya kwanza sampuli za aina mbalimbali za dawa za kulevya pamoja na kemikali zinazotumika kuzitengeneza kupitia mabanda ya Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kuongeza uelewa wa jamii kuhusu madhara ya matumizi na biashara haramu ya dawa hizo.

 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akizungumza na Viongozi na Watumishi wa Baraza la Taifala Hifadhi na Usimamizi Mazingira (NEMC) wakati alipofanya ziara MakaoMakuu ya NEMC, Mikocheni Jijini Dar es Salaam leo tarehe 02 Julai 2026.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewasihi watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi naUsimamizi wa Mazingira (NEMC), kufanya kazi kwa bidii, weledi, ushirikiano nakujiepusha na vitendo vya rushwa ili kuifanya Taasisi hiyo kuwa chachu yauhifadhi wa mazingira na maendeleo ya Taifa.

Makamu wa Rais ametoa wito huo, alipofanya ziara Baraza la Taifa la Hifadhina Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Makao Makuu, Mikocheni Jijini Dar es Salaam. Amewataka watumishi kufanya kazi kwa uadilifu na kutokuwakikwazo katika utekelezaji wa miradi mikubwa kwa kutanguliza maslahi yaTaifa mbele.

Makamu wa Rais ameipongeza NEMC kwa kutimiza miaka 40 tangukuanzishwa kwake na kuendelea kuwa chombo kinachohitajika nakutumainiwa nchini.

Aidha, Makamu wa Rais ameipongeza NEMC kwa Mpango Mkakati wa miakaMitano ambao umeanisha vitu mbalimbali vitakavyowezesha usimamizi nautunzanji wa mazingira kwa ufanisi.

Amesema uanzishwaji wa mashindano yauhifadhi wa mazingira ni muhimu kwa kuwa itakua hamasa ya upandaji mitina usafi kitaifa.

Vilevile, Makamu wa Rais amesema ili kudhibiti masuala ya uchafu ni vema pia kuwatambua wanaokuwa wamefanya vibaya katika mashindano ya usafi nakuwataja hadharani ikiwemo kupatiwa vyeti.

Ameiagiza Ofisi ya Makamu waRais, Muungano na Mazingira, kushirikiana na NEMC katika kufanikishamashindano ya usafi na utunzaji mazingira nchini.

Halikadhalika Makamu wa Rais, ameitaka NEMC kutilia mkazo suala la nishatisafi, matumizi ya teknolojia za kisasa katika kulinda mazingira pamoja nakusimamia vema suala la urejerezaji taka.

Makamu wa Rais, amewapongeza Viongozi wa NEMC kwa kuendelea namchakato wa kuifanya NEMC kuwa Mamlaka kamili. Amesema suala hilolinashughulikiwa na katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita limepewaumuhimu wa kipekee.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi naUsimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Emmaculate Sware amesema NEMC imeaandaa Mpango Mkakati wa miaka mitano yaani mwaka 2026/2027 – 2030/2031 ambao umelenga kuongeza ufanisi wa usimamizi wa mazingira, kuimarisha matumizi ya teknolojia za kidijitali, kuimarisha ukaguzi nautekelezaji wa sheria pamoja na kuchochea uchumi wa kijani na ustahimilivuwa mabadiliko ya tabianchi.

Ziara hiyo imehudhuriwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais(Muungano na Mazingira) Mhe. Hamad Masauni pamoja na Katibu Mkuu Ofisiya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akikabidhiwa zawadi na Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Dkt. Emmaculate Swaremara baada ya kuzungumza na Viongozi na Watumishi wa Baraza hilo,alipofanya ziara Makao Makuu ya NEMC, Mikocheni Jijini Dar es Salaam leotarehe 02 Julai 2026.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu waBaraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Dkt. EmmaculateSware pamoja na Watumishi waliofanya kazi pamoja na Makamu wa Raiswakati akifanya kazi Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira(NEMC). Picha hiyo imepigwa mara baada ya Makamu wa Rais kukamilishaziara aliyoifanya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Mikocheni Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 02 Julai 2026. 


WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda ameutaka uongozi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kufanya tathmini ya kina ya mchango wake katika kipindi cha miaka 40 iliyopita badala ya kujikita katika kusherehekea mafanikio.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akizungumza na Viongozi na Watumishi wa Baraza la Taifala Hifadhi na Usimamizi Mazingira (NEMC) wakati alipofanya ziara MakaoMakuu ya NEMC, Mikocheni Jijini Dar es Salaam leo tarehe 02 Julai 2026.

*************


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewasihi watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi naUsimamizi wa Mazingira (NEMC), kufanya kazi kwa bidii, weledi, ushirikiano nakujiepusha na vitendo vya rushwa ili kuifanya Taasisi hiyo kuwa chachu yauhifadhi wa mazingira na maendeleo ya Taifa.

Makamu wa Rais ametoa wito huo, alipofanya ziara Baraza la Taifa la Hifadhina Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Makao Makuu, Mikocheni Jijini Dar es Salaam. Amewataka watumishi kufanya kazi kwa uadilifu na kutokuwakikwazo katika utekelezaji wa miradi mikubwa kwa kutanguliza maslahi yaTaifa mbele.

Makamu wa Rais ameipongeza NEMC kwa kutimiza miaka 40 tangukuanzishwa kwake na kuendelea kuwa chombo kinachohitajika nakutumainiwa nchini.

Aidha, Makamu wa Rais ameipongeza NEMC kwa Mpango Mkakati wa miakaMitano ambao umeanisha vitu mbalimbali vitakavyowezesha usimamizi nautunzanji wa mazingira kwa ufanisi.

Amesema uanzishwaji wa mashindano yauhifadhi wa mazingira ni muhimu kwa kuwa itakua hamasa ya upandaji mitina usafi kitaifa.

Vilevile, Makamu wa Rais amesema ili kudhibiti masuala ya uchafu ni vema pia kuwatambua wanaokuwa wamefanya vibaya katika mashindano ya usafi nakuwataja hadharani ikiwemo kupatiwa vyeti.

Ameiagiza Ofisi ya Makamu waRais, Muungano na Mazingira, kushirikiana na NEMC katika kufanikishamashindano ya usafi na utunzaji mazingira nchini.

Halikadhalika Makamu wa Rais, ameitaka NEMC kutilia mkazo suala la nishatisafi, matumizi ya teknolojia za kisasa katika kulinda mazingira pamoja nakusimamia vema suala la urejerezaji taka.

Makamu wa Rais, amewapongeza Viongozi wa NEMC kwa kuendelea namchakato wa kuifanya NEMC kuwa Mamlaka kamili. Amesema suala hilolinashughulikiwa na katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita limepewaumuhimu wa kipekee.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi naUsimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Emmaculate Sware amesema NEMC imeaandaa Mpango Mkakati wa miaka mitano yaani mwaka 2026/2027 – 2030/2031 ambao umelenga kuongeza ufanisi wa usimamizi wa mazingira, kuimarisha matumizi ya teknolojia za kidijitali, kuimarisha ukaguzi nautekelezaji wa sheria pamoja na kuchochea uchumi wa kijani na ustahimilivuwa mabadiliko ya tabianchi.

Ziara hiyo imehudhuriwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais(Muungano na Mazingira) Mhe. Hamad Masauni pamoja na Katibu Mkuu Ofisiya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akikabidhiwa zawadi na Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Dkt. Emmaculate Swaremara baada ya kuzungumza na Viongozi na Watumishi wa Baraza hilo,alipofanya ziara Makao Makuu ya NEMC, Mikocheni Jijini Dar es Salaam leotarehe 02 Julai 2026.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu waBaraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Dkt. EmmaculateSware pamoja na Watumishi waliofanya kazi pamoja na Makamu wa Raiswakati akifanya kazi Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira(NEMC). Picha hiyo imepigwa mara baada ya Makamu wa Rais kukamilishaziara aliyoifanya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Mikocheni Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 02 Julai 2026. 





Serikali imezitaka Wizara, Taasisi za Umma, Sekta Binafsi, Watafiti na Mashirika ya Kiraia kuchangamkia fursa ya Tanzania kuwa mwenyeji wa 12 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Nairobi (COP 12).

Hayo yamesemwa leo Julai 2, 2026 Jijini Tanga na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Reuben Kwagilwa wakati akitoa tamko la Serikali kuhusu maandalizi ya Tanzania kuelekea Mkutano huo unaotarajia kufanyika nchini kuanzia tarehe 6-9 Oktoba mwaka huu.


Naibu Waziri Kwagilwa amesema katika Mkutano wa 11 wa Nchi Wanachama uliofanyika nchini Madagasca mwaka 2024, Tanzania ilichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya Mkataba wa Nairobi kwa kipindi cha miaka miwili hadi Disemba Mwaka 2026 pamoja na kuteuliwa kuwa mwenyeji wa COP12.


“Mkutano wa COP12 utajadili utekelezaji wa Mpango Kazi wa Mkataba kwa kipindi cha mwaka 2024–2026 pamoja na kujadili masuala muhimu ikiwemo hifadhi na urejeshwaji wa mifumo ikolojia ya bahari kama mikoko, miamba ya matumbawe na nyasi bahari” amesema Mhe. Kwagilwa.

Ameongeza kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kuipa kipaumbele sekta ya mazingira na uhifadhi wa rasilimali za bahari ili kuimarisha uhifadhi wa rasilimali za bahari, mito, maziwa, maji chini ya ardhi na maeneo oevu.

Kwa mujibu wa Naibu Waziri Kwagilwa, amesema Dira 2050 imeitambua sekta ya uchumi wa Buluu kuwa miongoni mwa sekta za kimkakati zinazokusudia kuleta mageuzi ya maendeleo endelevu na kuchangia ukuaji wa kijamii, kiuchumi na kiikolojia.

Amesema kuwa Tanzania ni nchi ya pwani yenye fursa kubwa ya kunufaika na sekta ya uchumi wa buluu kupitia uvuvi, nishati, usafirishaji, utalii, madini, mazingira na viwanda, hivyo mkutano huo utaliwezesha taifa kuwa katika nafasi bora ya kufikia maendeleo endelevu.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian amesema matokeo ya utafiti uliofanyika mkoani humo yanaonyesha athari za mabadiliko ya tabianchi zimeanza kuathiri kwa kiwango kikubwa shughuli za uvuvi na ukuzaji wa viumbe maji, hususan kilimo cha mwani.

Amesema utafiti uliofanyika kati ya mwaka 2021 na 2025 umebaini kuwa joto la bahari limeongezeka kutoka nyuzi joto 25.6 mwaka 2021 hadi kufikia nyuzi joto 28.39 mwaka 2024, hali inayobadili mfumo wa ikolojia wa bahari na kuathiri uzalishaji katika sekta ya uvuvi.

"Tumeshuhudia ongezeko la karibu nyuzi joto tatu baharini, huku siku za wavuvi kwenda kuvua zikishuka kutoka siku 221 mwaka 2021 hadi siku 170 kutokana na upepo mkali na hatari ya usalama baharini. Pia mavuno ya samaki yamepungua kwa wastani wa asilimia 25 hadi 30," amesema Dkt. Burian.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Balozi Baraka Luvanda amesema mkutano wa COP 12 utahusisha washiriki takribani 500-600 ikiwemo viongozi wa nchi, wataalamu na wadau mbalimbali.

Ameongeza kuwa lengo la tamko hilo la Serikali ni kuweka msingi wa maandalizi ya kina, ikiwa ni pamoja na kubainisha vipaumbele vya Taifa, na kupanga mikakati ya ushiriki ili kuhakikisha maandalizi yanafanyika kwa ufanisi na kwa wakati.

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi mwanachama wa Mkataba wa Nairobi unaohusu Hifadhi, Usimamizi na Uendelezaji wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani wa Magharibi mwa Bahari ya Hindi.

Mkataba huu ulisainiwa tarehe 21 Juni 1985 na unatekelezwa chini ya usimamizi wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP).