Na Mwandishi Wetu, Muheza

Mkuu wa Wilaya ya Muheza mkoani Tanga, Ayoub Sebabili, amewahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi katika shughuli za mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2026, akisema ushiriki mkubwa wa wananchi utasaidia wilaya hiyo kufanya vizuri katika mashindano ya Kitaifa ya Mwenge wa Uhuru.

Sebabili ametoa wito huo wakati wa zoezi la Jogging lililoandaliwa kama sehemu ya maandalizi ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru, ambapo aliwashukuru wananchi kwa kujitokeza kwa wingi na kushiriki shughuli hiyo.

Alisema Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kuwasili wilayani Muheza Juni 23, 2026 ukitokea Wilaya ya Mkinga na kupokewa katika eneo la Kilapura, huku ukitarajiwa kulala katika Uwanja wa Jitegemee.

"Niwashukuru kwa namna mlivyojitokeza leo. Ushiriki wenu unaonyesha dhamira ya kuhakikisha Muheza inafanya vizuri katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru. Kila mmoja wetu awe balozi wa kuhamasisha wananchi wengine kujitokeza kwa wingi," alisema Sebabili..

Kwa upande wake, Mratibu wa Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Muheza alisema maandalizi yanaendelea vizuri na kuwa viongozi katika ngazi zote wamepewa jukumu la kuhamasisha wananchi wa makundi mbalimbali, wakiwemo vijana, wanawake, wazee na watu wenye ulemavu kushiriki kikamilifu katika shughuli hizo.

Alisema Mwenge wa Uhuru utapitia maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo kwa ajili ya kuzindua na kukagua miradi ya maendeleo pamoja na kutoa ujumbe wa umoja, uzalendo na mshikamano wa kitaifa.

Kwa mujibu wa ratiba iliyopangwa, Mwenge wa Uhuru utaanzia Kata ya Mlingano kabla ya kuelekea Machemba kwa uzinduzi wa mradi na ukaguzi wa banda la lishe litakaloonyesha juhudi za Halmashauri ya Muheza katika kupambana na utapiamlo, malaria na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi.

Baadaye utaelekea katika Shule ya Venance Mabeyo na Kata ya Mpapayu kwa ajili ya uzinduzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Katika Kata ya Genge, Mwenge wa Uhuru utazindua maabara katika Shule ya Sekondari Chief Mang'enya iliyojengwa kwa nguvu za wananchi na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa madarasa mapya kwa ajili ya maandalizi ya wanafunzi wa Kidato cha Kwanza mwaka 2027.

Mratibu huyo alisema pia kutakuwa na shughuli za Klabu ya Wapinga Rushwa pamoja na programu mbalimbali za elimu kwa jamii.

Katika Kata za Magila na Majengo, Mwenge wa Uhuru utatembelea kikundi kilichonufaika na mkopo wa asilimia 10 wa Halmashauri unaotolewa kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, ambapo kikundi hicho kimepata Sh25 milioni kwa ajili ya shughuli za maendeleo ya kiuchumi.

Aidha, katika eneo la Mikwamba kutakuwa na maonesho ya fursa za zabuni kupitia PPRA, yakilenga kuhamasisha vikundi maalumu kushiriki katika zabuni zinazotengwa kwa makundi hayo.

Ratiba hiyo itahitimishwa kwa shughuli mbalimbali katika Kata ya Tongwe na eneo la Mpaa, ikiwemo uzinduzi wa daraja la karavati, uzinduzi wa Jengo la Havest Inn na mkesha wa Mwenge wa Uhuru katika Uwanja wa Jitegemee.

Viongozi hao wamewataka wananchi kuzingatia amani, utulivu na usalama katika kipindi chote cha shughuli hizo, huku wakisisitiza kuwa vitendo vya uhalifu na uvunjifu wa amani havitavumiliwa.

Akizungumza katika hafla hiyo, Katibu Tawala wa Wilaya (DAS) wa Muheza, Mohamed Mfaki, aliwashukuru wananchi kwa ushirikiano wao katika maandalizi ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru na kuwataka kuendelea kushiriki kikamilifu.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza, Dk Juma Mhina, alisema wilaya hiyo imejipanga kufanya vizuri zaidi mwaka huu na inalenga kushika nafasi ya kwanza kitaifa katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru


Alisema maandalizi yaliyoanza mapema chini ya usimamizi wa Mkuu wa Wilaya yanalenga kuongeza ushiriki wa wananchi na kuhakikisha shughuli zote zinafanyika kwa mafanikio makubwa.

"Malengo yetu ni kuona wananchi wanajitokeza kwa wingi katika shughuli zote za Mwenge wa Uhuru. Tunataka Muheza iwe mfano wa mafanikio na ushirikiano katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2026," alisema Dk Mhina.


 


Na OWM - TAMISEMI, Dar es Salaam


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe ametaka Mkandarasi kampuni ya China Railways and Bridges Corporation (CRBC) inayojenga barabara tisa (9) za lami zenye urefu wa kilometa 5.42 kukamilisha ujenzi wa barabara saba (7) zilizosalia ifikapo Agosti 14, 2026, barabara hizo zinajengwa kupitia Mradi wa Uboreshaji wa Jiji la Dar es Salaam Awamu ya Pili (DMDP II) katika kata za Sinza, Mburahati, Mabibo na Makurumla wilayani Ubungo.

Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo Juni 13, 2026 Katika Manispaa ya Ubungo jijini Dar es Salaam wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua ujenzi wa barabara 23 zenye urefu wa kilometa 52.37 zinazojengwa wilayani Ubungo katika kata 11 kupitia utekelezaji wa Mradi wa Uboreshaji wa Jiji la Dar es Salaam Awamu ya Pili (DMDP II).

Prof. Shemdoe amesitiza kuwa, mkandarasi huyo anayesuasua katika ujenzi wa barabara hizo kwa kisingizio cha lami kuchelewa kufika kutokana na vita ya Mashariki ya Kati, hatopewa muda wa nyongeza wa kukamilisha ujenzi wa barabara hizo iwapo atashindwa kukamilisha ifikapo Agosti 14, 2026 kwa mujibu wa mkataba.

“TARURA hakuna kumuongezea muda mkandarasi huyu, atafute lami popote atakapoipata na afanye kazi usiku na mchana kukamilisha barabara hizi 7 zilizosalia ili kuwaondolea adha wananchi,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Katika kuhakikisha barabara zinakamilika kwa wakati, Prof. Shemdoe ameitaka TARURA na Mshauri Elekekezi (NIMETA Consult (T) kumshauri mkandarasi CRBC kwa kuangalia uwezekano wa kukabidhi baadhi ya barabara hizo kwa mkandarasi mwingine (sub contract) ili ujenzi ukamilike kwa wakati.

Aidha, Prof. Shemdoe amemuelekeza Mtendaji Mkuu wa TARURA Mhandisi Victor Seff kumuondoa Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu Bw. Evans Mgeusa anayesimamia Fedha za Miradi ya Benki ya Dunia kwa kitendo cha kuchelewesha malipo na kumleta mwingine ambaye atafanya kazi kwa weledi na wakati.

Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe amemuelekeza Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI Bw. Adolf Ndunguru kuwaondoa Wahasibu Bw. Julius Bashuta na Mbwana Mkembe wa kitengo hicho cha Fedha na Uhasibu kinachosimamia  fedha za miradi ya Benki ya Dunia, na kuwaleta wengine ambao watafanya kazi vizuri na kwa uaminifu. 

Akizungumzia jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita, Prof. Shemdoe amempongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha utiaji saini wa mikataba minne ya ujenzi wa barabara za wilaya ya Ubungo yenye thamani ya shilingi bilioni 77, 457,169,172.73 kupitia Mradi wa Uboreshaji wa Jiji la Dar es Salaam Awamu ya Pili (DMDP II).

Kwa upande wake Mkazi wa Sinza Bw. Jawa Waziri amemshukuru Prof. Shemdoe kwa kufanya ziara ya ukaguzi wa barabara ya mtaa wake wa Sinza Lion na kumpongeza kwa kumuelekeza mkandarasi CRBC kukamilisha kwa wakati barabara hiyo ambayo imekuwa ni kero kwa wakazi wa eneo hilo.

Na Abdu Madenge, WAF – Dar es Salaam

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe, ametoa wito kwa wadau wa maendeleo kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha afya ya uzazi kwa kutoa msaada wa kifedha, kiufundi na rasilimali nyingine muhimu, huku akisisitiza dhamira ya Serikali ya kutokomeza au kupunguza kwa kiwango kikubwa vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga vinavyoweza kuzuilika.
Nilipoanzisha biashara yangu, nilikuwa na matumaini makubwa. Nilikuwa nimewekeza akiba yangu, muda wangu, na nguvu zangu zote kwenye mradi huo. Niliamini kwamba kwa kufanya kazi kwa bidii, mafanikio yangekuja haraka. Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia.

Kuanzia mwezi wa kwanza hadi wa sita, biashara yangu ilihangaika kupata faida ya kutosha. Wateja walikuwa wachache na mauzo hayakufikia kiwango nilichokuwa nimekitarajia. 

Wakati huo huo, washindani wangu walionekana kufanya vizuri zaidi kila siku. Kwa kweli nilianza kuwa na wasiwasi.

Kila mwisho wa mwezi nilipokagua hesabu zangu, niliona faida ndogo sana au wakati mwingine kutokuwepo kabisa. 

Nilijiuliza kama nilikuwa nimefanya uamuzi sahihi wa kuanzisha biashara hiyo. Kilichoniumiza zaidi ni kuona watu wakiniambia kwamba biashara yangu isingeweza kushindana na zile ambazo tayari zilikuwa zimejijengea jina sokoni.

Kadri miezi ilivyopita, shinikizo liliongezeka.

Kulikuwa na nyakati nilifikiria kufunga biashara na kutafuta jambo lingine la kufanya. Nilihisi kama juhudi zangu zote zilikuwa zinaenda bure.

Lakini sikuwa tayari kukata tamaa. Badala ya kuacha, nilianza kutafuta njia za kuboresha huduma zangu.SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mingi, kulikuwa na mtu mmoja ambaye alikuwa amechukua nafasi ya pekee moyoni mwangu. Tulijuana vizuri na tulikuwa marafiki wa karibu. 

Tulizungumza mara kwa mara, tulicheka pamoja, na mara nyingi tulisaidiana katika mambo mbalimbali ya maisha. Kadri muda ulivyopita, hisia zangu kwake zilianza kukua.

Lakini kulikuwa na tatizo moja. Sikuwahi kumwambia ukweli. Niliogopa kwamba nikifungua moyo wangu, ningeharibu urafiki wetu. 

Nilihofia kukataliwa na kupoteza mtu ambaye tayari alikuwa muhimu sana maishani mwangu. Hivyo niliamua kunyamaza.

Miezi iligeuka miaka huku nikificha hisia zangu. Kila nilipomwona akiwa na watu wengine, nilihisi wivu kidogo, lakini sikuwa na ujasiri wa kusema chochote. 

Kwa kweli hali ile ilinichosha.
Kulikuwa na nyakati nilitaka kumweleza kila kitu, lakini kila nilipopata nafasi, hofu ilinishinda.

Nilianza kuamini kwamba labda hisia zile zingebaki siri yangu milele. Kadri muda ulivyopita, nilijaribu kuendelea na maisha. SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mingi, nilikulia nikiamini kwamba familia yetu ilikuwa kamili. Nilijua wazazi wangu, ndugu zangu, na historia ndogo niliyokuwa nimeelezwa tangu utotoni. Sikuwahi kufikiria kwamba kulikuwa na siri kubwa ambayo ilikuwa imefichwa kwa muda mrefu.

Mambo yalianza kubadilika baada ya kifo cha bibi yetu.

Wakati familia ilipokusanyika kwa ajili ya shughuli za mazishi, nilianza kusikia mazungumzo ambayo yalionekana kuwa ya ajabu. 

Kulikuwa na majina ambayo sikuwahi kuyasikia na watu waliokuwa wakizungumza kwa tahadhari kana kwamba hawakutaka kila mtu asikie. Mwanzoni sikutilia maanani.

Lakini kadri siku zilivyopita, udadisi ulianza kunisumbua. Nilihisi kwamba kulikuwa na jambo muhimu ambalo sikuwa najua kuhusu familia yetu. Kwa kweli sikutarajia kile nilichokuja kugundua. SOMA ZAIDI.

Kwa muda mrefu, nyumba yetu ilikuwa imepoteza amani. Kila siku kulikuwa na mabishano kati ya wazazi wangu.

Jambo dogo tu lingeweza kugeuka kuwa ugomvi mkubwa uliodumu kwa saa nyingi. Mimi na ndugu zangu tuliishi katika mazingira ya hofu na wasiwasi, tukijiuliza ni lini mambo yangerudi kuwa kawaida.

Mwanzoni niliamini kwamba migogoro hiyo ilikuwa ya muda mfupi. Lakini miezi iligeuka miaka. Badala ya hali kuwa bora, mambo yalizidi kuwa magumu. 

Wazazi wangu walikuwa hawakubaliani karibu katika kila jambo, na mara nyingi walitishia kutengana. Kwa kweli hali ile iliniumiza sana.

Kilichoniumiza zaidi ni kuona familia yetu ikivunjika taratibu mbele ya macho yangu. Sikujua nifanye nini, lakini sikutaka kuona wazazi wangu wakiachana baada ya miaka mingi ya maisha pamoja. Kadri muda ulivyopita, matumaini yangu yalianza kupungua.

Kulikuwa na nyakati nilihisi kwamba hakuna mtu angeweza kurekebisha hali ile. Kila mmoja alionekana kuchoshwa na migogoro iliyokuwa ikiendelea bila mwisho. Lakini bado nilitamani kuona familia yetu ikipata amani tena. SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mingi, nilikuwa na ndoto ya kusafiri nje ya nchi. Nilitaka kupata fursa mpya, kuona mazingira tofauti, na kujenga maisha bora kwa ajili yangu na familia yangu. 

Lakini ili kufanikisha ndoto hiyo, nilihitaji kitu kimoja muhimu sana. Visa. Mara ya kwanza nilipoomba visa, nilikuwa na matumaini makubwa.

Nilijaza nyaraka zote nilizoambiwa niwasilishe na nikasubiri majibu kwa hamu kubwa. Lakini majibu yalipokuja, nilikataliwa. Kwa kweli iliniumiza sana. 

Nilijaribu kujifariji kwamba huenda kulikuwa na jambo nililokuwa nimekosea kwenye maombi yangu. Hivyo nilijipanga upya na kujaribu tena baada ya muda.

Mara ya pili nilikuwa na matumaini zaidi.
Nilihakikisha kila kitu kiko sawa na nikawasilisha maombi yangu kwa kujiamini. Lakini kwa mshangao wangu, nilikataliwa tena.

Sikuamini kilichokuwa kimetokea. Baada ya kukataliwa mara mbili, nilianza kupoteza matumaini. Watu wengi waliniambia niache kujaribu kwa sababu huenda haikuwa bahati yangu. SOMA ZAIDI.
DAR ES SALAAM

Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limeendelea kuthibitisha ubora wake barani Afrika baada ya kutwaa tuzo mbili muhimu katika Tuzo za Kampuni Bora za Mwaka Afrika (Africa Company of the Year Awards - ACOYA).
Na: OWM-KAM, Mwanza

Serikali imeendelea kusisitiza umuhimu wa kuendeleza mshikamano, umoja na amani kwa kuwa ni nguzo muhimu zinazowezesha taifa kufikia maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii.
Kwa miaka mingi, kulikuwa na msichana mmoja ambaye sikuwahi kumuondoa moyoni mwangu.....................TAZAMA VIDEO.

Kila nilipomwona, nilihisi furaha ambayo sikuweza kuelezea kwa maneno. Alikuwa mchangamfu, mwenye heshima, na mtu ambaye nilifurahia kuwa karibu naye. Tatizo pekee lilikuwa kwamba hakujua nilivyokuwa najisikia.
Kwa kweli nilikuwa mwoga.

Mara nyingi nilitaka kumwambia ukweli, lakini kila nilipopata nafasi, nilikosa ujasiri. Niliogopa kukataliwa na kuharibu urafiki uliokuwepo kati yetu. Miezi iligeuka miaka.

 Niliendelea kumtazama kwa mbali huku nikificha hisia zangu. Wakati mwingine niliona watu wengine wakimkaribia na hilo liliniumiza, lakini bado sikuweza kupata nguvu za kusema kile kilichokuwa moyoni mwangu.

Kadri muda ulivyopita, nilianza kuamini kwamba huenda nafasi yangu ilikuwa imepita.
Nilijaribu kujisahaulisha na kuendelea na maisha, lakini kila nilipokutana naye, hisia zile zilikuwa zinarudi tena. SOMA ZAIDI.
Kwa muda mrefu, nilikuwa mtu ambaye alipenda kukaa kimya. Kila nilipojikuta kwenye mkutano, darasani, au sehemu yenye watu wengi, niliepuka kuzungumza....TAZAMA VIDEO.

Nilikuwa na mawazo mazuri kichwani, lakini nilikosa ujasiri wa kuyasema mbele ya wengine. Tatizo hilo lilianza kunisumbua tangu nikiwa mdogo.

Kila niliposimama kuzungumza mbele ya watu, moyo wangu ulianza kwenda mbio. Mikono ilitetemeka na wakati mwingine nilisahau hata kile nilichotaka kusema. 

Kwa kweli hali ile ilinifanya nijisikie duni. Niliona watu wengine wakizungumza kwa kujiamini, wakitoa maoni yao na kupata fursa mbalimbali maishani.

Mimi nilibaki nyuma kwa sababu ya hofu iliyokuwa ndani yangu. Kadri miaka ilivyopita, confidence yangu ilizidi kupungua. 

Nilianza kuamini kwamba labda sikuumbwa kuwa mtu wa kuonekana au kusikilizwa. Hata kwenye kazi na mahusiano yangu, nilikuwa na tabia ya kujishusha na kuhisi kwamba watu wengine walikuwa bora kuliko mimi.

Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilijua uwezo nilikuwa nao. Lakini uwezo ule ulikuwa umefichwa nyuma ya hofu na kutojiamini. SOMA ZAIDI.
Kwa zaidi ya mwaka mmoja, nilikuwa nikiishi kwa hasira na kuchanganyikiwa. Kila baada ya wiki chache, niligundua kuwa kuku wangu walikuwa wanapungua.....TAZAMA VIDEO.

Mwanzoni nilidhani ni wanyama wa porini au makosa ya kuhesabu, lakini kadri muda ulivyopita, ilibainika wazi kwamba kulikuwa na mtu aliyekuwa akiwaiba.

Tatizo lilikuwa moja.

Hakukuwa na ushahidi. Kila nilipoamka asubuhi na kukuta kuku wamepungua, nilianza kuwashuku watu tofauti. Lakini sikuwa na namna ya kuthibitisha tuhuma zangu. 

Mwizi alikuwa akifanya kazi yake kwa ustadi mkubwa na hakuacha alama yoyote nyuma. Kwa kweli hali ile ilinichosha sana.

Hasara ilikuwa inaongezeka, na kila nilipoongeza ulinzi, mwizi alionekana kupata njia nyingine ya kuendelea na wizi wake. 

Wakati mwingine nilikesha usiku nikisubiri, lakini hakutokea.
Watu wengi walianza kuniambia nikubali hasara na kuendelea na maisha. Lakini sikuwa tayari kufanya hivyo.

Kuku wale walikuwa sehemu ya chanzo changu cha kipato, na nilijua lazima siku moja ningepata ukweli.SOMA ZAIDI.
Nilipoanzisha biashara yangu, nilikuwa na ndoto kubwa sana. Nilitaka kuona biashara yangu ikikua na kuvutia wateja wengi, lakini ukweli ulikuwa tofauti.....TAZAMA VIDEO.

Eneo nililokuwa nafanyia biashara lilikuwa tayari na wafanyabiashara wakubwa waliokuwa wamejijengea jina kwa miaka mingi.

Kwa hiyo haikuwa rahisi. Kila siku nilifungua biashara yangu mapema na kusubiri wateja. Wakati mwingine nilikaa kwa saa nyingi bila kufanya mauzo ya kuridhisha

Wakati huo huo, nilikuwa nikiona maduka ya washindani wangu yakiwa yamejaa watu. Kwa kweli iliniumiza.

Kulikuwa na nyakati nilijiuliza kama nilifanya makosa kuanzisha biashara ile. Nilikuwa najituma kwa bidii, lakini matokeo hayakuwa yale niliyotarajia. 

Badala ya kukata tamaa, niliamua kuboresha huduma zangu. Nilihakikisha kila mteja anahudumiwa kwa heshima.

Nilisikiliza maoni yao na kujitahidi kufanya maboresho pale nilipoweza. Polepole baadhi ya watu walianza kugundua tofauti. Lakini bado ushindani ulikuwa mkubwa.SOMA ZAIDI.
Kwa miaka mingi, pumu ilikuwa sehemu ya maisha yangu ambayo sikuweza kuikwepa.

TAZAMA VIDEO.

Kila siku niliishi kwa tahadhari. Mabadiliko ya hali ya hewa, vumbi, moshi, au hata harufu kali zingeweza kunisababishia matatizo ya kupumua. 

Wakati mwingine nilihisi kama kifua changu kilikuwa kizito kiasi kwamba kuvuta pumzi ya kawaida ilikuwa kazi ngumu.

Usiku ndiyo ulikuwa wakati mgumu zaidi.
Mara nyingi nilishtuka usingizini nikihangaika kupata hewa ya kutosha. Wakati familia yangu ilikuwa imelala kwa amani, mimi nilikuwa nimekaa kitandani nikijaribu kutuliza pumzi zangu. Kwa kweli hali ile ilinichosha sana.

Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilianza kuogopa kufanya baadhi ya shughuli nilizozipenda. Nilihofia kwamba pumu ingeanza ghafla na kunifanya nishindwe kuendelea na nilichokuwa nikifanya. Miaka ilipita katika hali hiyo. Nilitafuta ushauri wa wataalamu wa afya na kujifunza namna ya kudhibiti hali yangu.

Ingawa kulikuwa na nyakati nilizopata nafuu, bado kulikuwa na vipindi ambavyo pumu ilinisumbua sana.SOMA ZAIDI

Wathibiti Ubora wa Shule nchini wametakiwa kusimamia kwa weledi matumizi ya Mfumo wa Kielektroniki wa Ununuzi wa Umma (NeST) ili kuhakikisha manunuzi yote ya Serikali yanafanyika kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa.

Rai hiyo imetolewa Juni 11, 2026 jijini Arusha na Mkurugenzi wa Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Fredrick Salukele, akimwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, katika ufunguzi wa mafunzo kuhusu matumizi ya Mfumo huo.

Dkt. Salukele amesema mafunzo hayo yatawawezesha washiriki kutumia mfumo huo kwa ufanisi katika usimamizi wa fedha za uchangiaji, ununuzi wa bidhaa na huduma mbalimbali pamoja na malipo ya shughuli za tathmini za shule.

Amewasisitiza washiriki kusimamia kwa ufanisi rasilimali zilizopo, ikiwemo rasilimali watu na miundombinu, sambamba na kuimarisha huduma bora za elimu.

Aidha, Dkt. Salukele amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri na Wathibiti Ubora wa Shule kuhakikisha taasisi za elimu zinazingatia taratibu zote za uendeshaji ikiwemo masuala ya malazi, chakula na usalama wa wanafunzi.

Naye, Miurugenzi wa Uthibiti Ubora wa Shule kutoka Wizara hiyo Dkt. Ephrahim Simbeye amesisitiza uzingatiaji wa miongozo ya elimu, akitaka kukomeshwa kwa adhabu zisizokubalika na kuhakikisha kuna mazingira bora ya ufundishaji na ujifunzaji kwa wanafunzi.

Wakizungumza kuhusu mafunzo hayo, Bi. Lilian Kasenga Mthibiti Ubora kutoka Manispaa ya Temeke pamoja na Emmanuel Hangaya kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema, wametaja mbinu wanazotumia kufikia malengo huku wakisema mafunzo hayo yatakwenda kuwaongezea ufanisi kazini.









Na: OWM (KAM) – Geneva, Uswisi

Ujumbe wa Tanzania umeunga mkono Mkataba mpya wa Kimataifa unaolenga kulinda haki, usalama na ustawi wa Wafanyakazi wa Mtandaoni ikiwa ni dhamira ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuhakikisha maendeleo ya teknolojia na majukwaa ya kidijitali yanakwenda sambamba na ulinzi wa utu wa mfanyakazi, usawa na haki za msingi za kazi.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Tume ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imezindua filamu ya “Kifurushi” itakayooneshwa katika mabasi yanayosafiri mikoa mbalimbali nchini kwa lengo la kuongeza uelewa wa jamii kuhusu mbinu zinazotumiwa kusafirisha dawa za kulevya na madhara yatokanayo na vitendo hivyo.

 

Na; Mwandishi Wetu - Chato

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Profesa Mohammed Ali Sheikh, Ametoa wito kwa wataalam kutoka katika Sekta zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu kuwa na mbinu bora za kiutendaji zitakazowezesha programu hiyo kutekelezeka kwa kasi zaidi.

Ameyasema hayo Wilayani Chato Mkoani Geita Tarehe 12 Juni 2026 alipozungumza na wataalam wa programu wanaofanya kazi ya utekelezaji ya mapitio ya programu mara baada ya ziara yake maalum ya kutembelea kituo cha kuendeleza Ukuzaji viumbemaji cha Rubambagwe kilichopo Wilayani chato.

“Niwapongeze sana kwa kuchukua hatua za haraka baada na maagizo ya kikao cha Mawaziri kukaa pamoja kama wataaalamu na kuyafanyia kazi maagizo yale. Hii ni hatua muhimu sana inayoonesha ni kwa namna gani mnaweza kuwajibika kiutaalamu, mnapewa maelekezo na mnayatekeleza” Alisema.

Naibu Katibu Mkuu Sheikh alibainisha kuwa, kukutana kwa wataalamu hao ni hatua muhimu sana ya kukaa pamoja na kujaribu kujitathmini kuona kila kinachofanyika kinakwenda sawa ama vinginevyo, ‘’Niipongeze sana timu ya Uratibu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu kuitisha kikao kazi hiki “Mnapoona kitu hakiendi hebu muitane muone namna ya kukifanyia kazi sisi kama watekelezaji wa Programu hii ni familia moja, Serikali ni moja na tunachotaka ni kufikia malengo na kumsaidia mtanzania katika kilimo na uvuvi kwa ukubwa wake” Alisisitiza

Alibainisha kuwa, kwa kufanya tathmini kunasaidia kujua wapi ulikwama na wapi pa kuboresha. Zaidi aliendelea alisema kuwa, kukua na kubadilika kwa teknolojia kufanya tathmini kunaweza kusaidia  kwenda mbele zaidi, “lazima tusaidianae tuje na mbinu bora za utekelezaji katika utendaji wa mradi msione aibu kushauri na kutoa mapendekezo ya kiutendaji kuhusiana na Programu.” Alisema


Akizungumza katika kikao kazi hicho, Mhandisi Enock Nyanda, Mkurugenzi msaidizi sehemu ya Sekta za Uchumi na Uzalishaji Idara ya Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) alisema lengo mahususi ya wataalam kukutana katika kikao kazi hicho ni kuongeza kasi ya utekelezaji wa Programu ili kufikia malengo.


Na; Mwandishi Wetu - Chato

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Profesa Mohammed Ali Sheikh, Ametoa wito kwa wataalam kutoka katika Sekta zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu kuwa na mbinu bora za kiutendaji zitakazowezesha programu hiyo kutekelezeka kwa kasi zaidi.