Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), Ndugu Rabia Abdalla Hamid akiwa kwenye kikao kazi na Kansela wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) wa Ubalozi wa China nchini Tanzania, Ndugu Xu Sujiang, leo Jumatatu tarehe 27 Aprili 2026, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kupokea ugeni wa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CPC na Waziri wa Mambo ya Nje wa China, Mhe. Liu Haixing, anayetarajiwa kufanya ziara rasmi nchini Tanzania, mwezi Mei 2026.
#KazinaUtuTunasongaMbele
Wananchi wametakiwa kupanda miti na kutunza Misitu nchini kwa maslahi mapana ya Taifa na mtu mmoja mmoja.
Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Antony Mtaka, Mkoani Njombe, kwenye zoezi la upandaji wa miti katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kama sehemu ya maadhimisho ya Mei Mosi 2026
Mhe. Mtaka amesema kuwa, Misitu ni nguzo muhimu kwa uchumi wa nchi hivyo nivyema ikalindwa kwa wivu mkubwa na kutoichoma moto.
Amesisitiza kuwa zoezi la upandaji miti liendane sambamba na upandaji wa miti ya matunda hususani Miparachichi ambayo inasoko kubwa ndani na nje ya nchi.
Zoezi hilo la upandaji miti linalojulikana kwa Jina la "27 ya KIJANI, MTI WA MAMA" pamoja na viongozi wengine limeudhuriwa na rais wa Shirikisho la vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Cde. Tumaini Nyamhokya, Mkurugenzi Msaidizi Utawala Bi. Violeth Mlinga kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii na watumimishi mbalimbali wa serikali.
Na OWM - TAMISEMI, Dar es Salaam
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amemshukuru Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba kwa kuadhimisha miaka 62 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kukagua ujenzi wa miradi ya maendeleo ya daraja jipya la Mkwajuni, daraja jipya la Kigogo ikiwa ni pamoja na kutatua kero za wananchi wa jiji la Dar es Salaam.
Prof. Shemdoe ametoa shukurani hizo leo Aprili 26, 2026 jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na wananchi wa jiji la Dar es Salaam katika Uwanja wa Shule ya Msingi Msimbazi mara baada ya Mhe. Waziri Mkuu kukagua miradi hiyo ya maendeleo, ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Miaka 62 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
“Mhe. Waziri Mkuu nakushukuru sana kwa uamuzi wako wa kuadhimisha miaka 62 ya Muungano kwa kukagua miradi ya maendeleo na kutatua kero za wananchi wa Dar es Salaam tena siku ya Jumapili,” Prof. Shemdoe amesisitiza.
Prof. Shemdoe amefafanua kuwa, uwanja umefurika idadi kubwa ya wananchi licha kuwa ni siku ya jumapili kwasababu wana Imani na wanafahamu kuwa Mhe. Waziri Mkuu utawasikiliza kero zao na kuzitatua hivyo watarejea kwenye makazi yao na tabasamu la kudumu.
Akizungumzia mwendelezo wa Serikali kutatua kero za wananchi, Prof. Shemdoe amesema siku chache zilizopita Mhe. Waziri Mkuu alimtuma kuja jijini Dar es Salaam kushuhudia utiaji wa saini wa Mradi wa Uendelezaji wa Bonde la Mto Msimbazi utakaogharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 190, fedha ambazo ziliidhinishwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na kuongeza kuwa mradi huo ni sehemu muhimu kwa uchumi na mazingira mkoani Dar es Salaam.
“Nichukue fursa hii kumshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia kuletwa kwa fedha za kutekeleza Mradi wa Uendelezaji wa Bonde la Mto Msimbazi, lakini pia nikushukuru wewe Mhe. Waziri Mkuu kwani nikiwa Katibu Mkuu TAMISEMI nakumbuka ulikuwa ukiongoza vikao vya Serikali na wadau wa Maendeleo vilivyowezesha kupatikana kwa fedha hizo ,” amesema Prof. Shemdoe.


Na Mwandishi Wetu
Kampuni ya Taifa Gas imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi sahihi na salama ya gesi, sambamba na kuhamasisha usalama mahali pa kazi katika maadhimisho ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi Duniani.
Akizungumza katika viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mwema, Njombe, Mtaalamu wa Masuala ya Afya, Mazingira, Usalama na Ulinzi Mahali pa Kazi kutoka Taifa Gas, Aurelius Marcus Mdemu, alisema kampuni hiyo imeshiriki maadhimisho hayo yanayoanza Aprili 24 hadi 29, 2026 kwa lengo la kutoa elimu kwa wateja na jamii kwa ujumla.
Alisema kupitia banda lao, wanaonesha vifaa mbalimbali vinavyotumika kazini ili kuimarisha usalama wa wafanyakazi, pamoja na kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya gesi na faida zake. Aidha, alieleza kuwa wanajitahidi kuondoa hofu na dhana potofu zilizopo miongoni mwa watumiaji wa gesi.
“Tunawaonesha wananchi namna Taifa Gas inavyoweka kipaumbele kwenye usalama wa wafanyakazi, ikiwa ni pamoja na matumizi ya vifaa kinga vinavyotakiwa kutumika muda wote wakiwa kazini,” alisema Mdemu.

Kwa upande wake, Afisa Masoko wa Chapa wa Taifa Gas, Santina Ngaponda, alisema maonyesho hayo yameandaliwa na OSHA, yalianza Aprili 24 na yanatarajiwa kufikia kilele chake Aprili 29 mwaka huu.
Ngaponda aliwahimiza wakazi wa Njombe na maeneo ya jirani kutembelea banda la Taifa Gas ili kupata elimu kutoka kwa wataalamu wa usalama, kujifunza matumizi sahihi ya gesi, pamoja na kuona vifaa vya usalama vinavyotumika kazini na umuhimu wake.

Aidha, aliongeza kuwa kampuni hiyo inatoa punguzo maalum la bei ya gesi na vifaa vyake, pamoja na zawadi mbalimbali kwa wateja watakaotembelea banda hilo.

Naye Meneja Mauzo wa Kanda ya Nyasa wa Taifa Gas, Arnold Salewa, alisema wanaendelea kutumia maonyesho hayo kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya nishati safi pamoja na kuuza bidhaa zao kwa bei ya promosheni.
Alisema kanda hiyo inajumuisha mikoa ya Njombe, Iringa na Ruvuma, na kwamba pia wanatoa fursa kwa wananchi wanaotaka kuwa mawakala wao, kwa kuwapatia elimu ya biashara na usimamizi salama wa mitungi ya gesi.

Salewa alisisitiza kuwa Taifa Gas ipo mstari wa mbele kuhakikisha kaya, migahawa na taasisi mbalimbali zinaanza kutumia nishati safi ya kupikia kwa gharama nafuu, ili kupunguza athari za matumizi ya mkaa na kuni kwa mazingira na afya za Watanzania.
Aliongeza kuwa mwitikio wa wananchi umekuwa mkubwa, huku Taifa Gas ikiendelea kuwa chaguo sahihi kwa watumiaji wengi nchini.
Timu ya Wachezaji wa Karat a upande wa Kike na kiume zimeshiriki Mashindano ya mchezo wa Karata leo Aprili 25, 2026 katika viwanja vya Sabasaba mkoani Njombe.
Upande wa kike mshiriki Godlove Kyangala alichuana vikali na Timu ya Maliasili na kujinyakulia pointi nne (4) baada ya kumfunga Maliasili mzunguko yote miwili.
Mzunguko wa pili TCDC ilicheza na Wizara ya Madini na kupata pointi mbili (2) kwa mzunguko wa kwanza na mzunguko wa pili Timu zote mbili zilitoa sare ya mbilimbili.
Mzunguko wa tatu TCDC ilicheza na Uchukuzi na matokeo kuwa sare,ambapo kwa mzunguko wa nne TCDC ilipoteza pointi nne kwa kufungwa na timu ya IRDT na mzunguko wa tano na mwisho TCDC ilipoteza pointi nne dhidi Uwekezaji.
Kwa upande wa timu ya Karata ya kiume mshiriki alikuwa ni Zawadi Joseph ambapo mzunguko wa kwanza alicheza na Uchukuzi na matokeo kuwa sare ya mbili kwa mbili, mzunguko wa pili matokea pia yalikuwa sare Kati ya TCDC na Uwekezaji, mzunguko wa tatu kati ya TCDC na mzunguko wa tatu TCDC ilitoka sare tena dhidi ya TAKUKURU.
Mzunguko wa nne, TCDC ilipoteza pointi tatu dhidi ya Wizara ya Maji na kupoteza tena pointi tatu kwenye mchezo wake dhidi ya Ulinzi katika mzunguko wa tano.Katika mzunguko wa sita na wa mwisho Dodoma Jiji ilijinyakulia pointi nne kwa sifuri kwa TCDC.
Kwa matokea hayo TCDC Sports Club upande wa Karata Timu zote mbili hazikufanikiwa kuvuka hatua za makundi 16 bora katika michezo hiyo ya Meimosi.
Hapo Kesho Aprili 26, 2026, Jackson Mkoloweko na Grace Mnare wanatarajia kushiriki mchezo wa Bao utakaochezwa saa 2:30 asubuhi katka viwanja vya Sabasaba mkoani humo.


Chama cha Wafanyakazi Serikali za Mitaa (TALGWU), tawi la RUWASA, kimefanya mkutano mkuu wa uchaguzi wa viongozi wapya ambapo Mwenyekiti aliyemaliza muda wake, Mhandisi Rashid Abdallah, amefanikiwa kutetea nafasi yake ya uenyekiti.
Uchaguzi huo ulifanyika Aprili 24, 2026 jijini Dodoma, katika mazingira ya uwazi na ushirikishwaji mpana wa wanachama, waliotekeleza haki yao ya kidemokrasia kwa kuchagua viongozi watakaoongoza tawi hilo kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Katika uchaguzi huo, viongozi waliochaguliwa ni pamoja na Mhandisi Rashid Abdallah (Mwenyekiti wa Tawi), Ibrahim Fungo (Katibu wa Tawi), Tumaini Gwatalile (Mwenyekiti wa Makundi Maalum – Wanawake), Ashura Nkunya (Katibu wa Makundi Maalum – Wanawake), Victoria Charles (Mjumbe wa Makundi Maalum – Vijana), na Adam Suleiman (Mjumbe wa Makundi Maalum – Watu wenye Ulemavu).
Uongozi huo mpya unatarajiwa kuimarisha mshikamano miongoni mwa wanachama, kulinda na kutetea maslahi yao, pamoja na kuendeleza maendeleo ya chama katika tawi la RUWASA.









NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM
SERIKALI imewahimiza wawekezaji wazawa kuchangamkia fursa zilizopo katika sekta ya viwanda, ikisisitiza kuwa imeendelea kuboresha na kurahisisha mazingira ya biashara ili kuongeza uwekezaji wa ndani.
Na Augusta Njoji
Timu ya wataalamu wa afya kutoka Hospitali ya Halmashauri ya Mji Handeni imeanza rasmi mpango wa utoaji elimu kwa jamii ili kuimarisha kinga dhidi ya magonjwa na kuboresha ustawi wa wananchi.
Utoaji wa elimu hiyo imejikita katika afua za kuzuia malaria, lishe bora, bima ya afya kwa wote pamoja na huduma za mama na mtoto, ikiwa ni sehemu ya jitihada za serikali kuhakikisha jamii inakuwa na afya bora.
Akizungumza kuhusu zoezi hilo, Ofisa Afya wa Halmashauri na Mratibu wa Elimu ya Afya kwa Umma, Jonas Mkondya, amesema wamejipanga kutembelea kila mtaa katika kata zote 12 za Halmashauri ya Mji Handeni ili kuwafikia wananchi wengi zaidi na kuwapatia elimu sahihi ya afya.
Ameeleza kuwa elimu hiyo itasaidia kuongeza uelewa kwa wananchi juu ya namna ya kujikinga na magonjwa, kuboresha lishe pamoja na umuhimu wa kujiunga na bima ya afya kwa wote ili kupata huduma kwa urahisi.
Kata zitakazofikiwa katika ziara hiyo ya wataalamu wa afya ni Konje, Mabanda, Kwenjugo, Malezi, Chanika, Mlimani, Mdoe, Vibaoni, Kwediyamba, Kideleko, Msasa na Kwamagome.

Timu ya Mpira wa miguu TCDC Sports Club imeonyeshana ubabe na Timu ya Mpira wa miguu ya Benki Kuu ya Tanzania (BOT) baada ya kutoka sare ya goli mbili kwa mbili katika mechi ya kirafiki iliyochezwa leo Aprili 24, 2026 katika viwanja vya Chai mkoani Njombe.
Hapo Aprili 22, 2026 TCDC Sports Club ilikubali kipigo cha bao moja bila 1- 0 kutoka Timu ya Mpira wa miguu ya TANWART katika mechi ya kirafiki iliyochezwa viwanja vya Kibena mkoani humo.
TCDC Sports Club inaendelea kushiriki Michezo ya kirafiki mkoani humo baada ya kushindwa kuvuka hatua za makundi kwenye Mashindando ya Michezo ya Meimosi inayoendelea mkoani humo.

Katika kuelekea Kilele cha Siku ya Wafanyakazi Duniani ( Meimosi) ambayo kitaifa inafanyika mkoani Njombe, Timu ya Pooltable ya TCDC Sports Club imeshiriki mashindando ya mchezo huo Aprili 23, 2026 ndani ya African Club mjini humo.
Mchezaji Mbasso John ameiwakilisha TCDC Sports Club katika mchezo huo huku akishinda mechi ya kwanza kati ya TCDC na Ulinzi na ,mechi ya pili akicheza na Arusha DC na kutoka moja moja na kupoteza mchezo wa mwisho baada ya kufungwa na timu ya Mahakama.
Kwa hatua hiyo TCDC Sports Club haijafanikiwa kuingia nusu fainali katika mchezo wa Pooltable katika Mashindando ya Michezo ya Meimosi.











