Na Munir Shemweta, WANMM MTWARA

 

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo leo tarehe 22 Desemba 2025 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala.

 

Mhe. Dkt Akwilapo ambaye yuko ziarani mkoani Mtwara amemueleza Kanali Sawala juhudi za wizara yake katika kushughulikia changamoto za sekta ya ardhi nchini.

 

"Sisi kama wizara tutazifanyia kazi changamoto zote za sekta ya ardhi na hapa Mtwara tayari tumeshaanza kuzifanyia kazi, lengo ni kutaka kuwaacha wananchi wetu wawe na furaha". Amesema

 

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Sawala amempongeza Mhe. Dkt Akwilapo kwa kuaminiwa na Rais Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kuteuliwa kuwa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi wizara aliyoieleza kuwa ni nyeti kutokana na kugusa maisha ya kila mtu.

 

"Nikuahidi Mhe. Waziri sisi kama mkoa tutajitahidi kukusemea kwa yale yote mazuri unayofanya katika mkoa wetu". Amesema Kanali Sawala

 



Na Munir Shemweta, WANMM MASASI

 

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amesema wizara yake haitaki watumishi wa sekta ya ardhi kuwa sehemu ya migogoro ya ardhi nchini.

 

Mhe. Dkt Akwilapo ametoa kauli hiyo leo tarehe 22 Desemba 2025 wilayani Masasi wakati alipowasili wilayani Masasi na kupokelewa kwa mara ya kwanza tangu ateuliwa kuwa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

 

"Kuanzia sasa hatutaki mtumishi wetu awe sehemu ya tatizo tukigundua wewe mtumishi wa sekta ya ardhi umekuwa sehemu ya tatizo basi wewe siyo mfanyakazi wetu na hilo tutalisimamia". Amesema

 

Amebainisha kuwa, matatizo ya ardhi yapo na yanatengenezwa na watumishi wa sekta ya ardhi pamoja na wananchi ambapo ameweka wazi kuwa, matatizo yaliyotengenezwa basi wizara yake itayatatua.

 

"Hatupendi kufukuza kazi watumishi maana tunajua kila mfanyakazi anategemewa na kumfukuza itakuwa kitu cha mwisho lakini kuna mahali inabidi sheria ifuate mkondo wake.

 

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo yupo wilayani Masasi mkoa wa Mtwara ambapo pamoja na mambo mengine atakutana na wananchi wa jimbo lake kwa lengo la kusikiliza na kizitafutia ufumbuzi changamoto mablimbali jimboni humo

Baada ya kunicheat, uhusiano wetu ulivunjika vibaya. Aliniambia waziwazi hatarudi tena, hata nikijaribu kiasi gani. Maneno yake yaliniumiza, sio tu kwa sababu ya kuachwa, bali kwa sababu nilijua nilikuwa nimekosea.

Nilijilaumu, nikajuta, na nikaanza safari ngumu ya kujijenga upya nikiwa peke yangu. Sikuanza kwa kumfuata. Nilianza kwa kujitazama. Nilijifunza kukaa kimya, kukubali makosa yangu, na kubadilisha mienendo yangu.

Nilijenga nidhamu, nikabadilisha marafiki, na nikaanza kujiheshimu tena. Mabadiliko hayo hayakuwa ya kuigiza; yalitoka moyoni. Hapo ndipo nilitambua kuwa hata asiporudi, nilihitaji kupona mimi kwanza. Soma Zaidi........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/ex-aliapa-peupe-hatanirudia-baada-ya-kucheati-njia-hii-ya-kipekee-ilimvuta-kurudi/
Kwa muda mrefu tuliishi kama watu wawili ndani ya nyumba moja. Hakukuwa na ugomvi mkubwa, ila pia hakukuwa na amani. Kila mmoja wetu alibeba kimya chake, hasira zisizosemwa, na maumivu ya zamani.

Tulizungumza kuhusu watoto, bili, na ratiba, si kuhusu hisia. Ndoa ikawa jukumu badala ya mahali pa kupumzika. Nilijaribu kujifanya niko sawa, nikijipa moyo kuwa mambo yatabadilika yenyewe.

Badala yake, umbali uliongezeka. Kila neno lilionekana kama lawama. Kila ukimya ulikuwa mzito. Nilianza kujiuliza kama tulipotezana kabisa au kama bado kulikuwa na kitu cha kuokoa.

Siku moja, nilichagua kuanza mazungumzo ya kweli. Sio ya kushindana, bali ya kusikiliza. Nilizungumza kwa hofu na unyenyekevu, nikakubali makosa yangu, nikasikiliza maumivu yake bila kujitetea.

Mazungumzo hayo hayakutatua kila kitu siku hiyo, ila yalifungua mlango tuliokuwa tumefunga kwa muda mrefu. Soma Zaidi..........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/tulikaa-ndoa-bila-amani-mazungumzo-moja-yalibadili-mwelekeo-wetu/
Siku ile maumivu yalipoanza, nilidhani maisha yangu yamefika mwisho. Yalikuwa ya ghafla, makali, na hayakufanana na chochote nilichowahi kuhisi. Nilishindwa kusimama wima, jasho likanitoka, na kila pumzi ilikuwa kazi.

Nilizungushwa hospitali, nikafanyiwa vipimo, ndipo nikaambiwa nina mawe kwenye figo. Niliogopa. Nilichokisikia kichwani mwangu ni upasuaji, gharama, na mateso yasiyoisha.

Nilianza kutumia dawa nilizopewa, nikafuata mashauri ya kula na kunywa maji mengi. Kulikuwa na nafuu kidogo, ila maumivu yalirudi mara kwa mara. Hofu ikaanza kunitawala.

Nilihisi kama mwili wangu umenigeuka, na sikuwa na uhakika nitapata lini ahueni ya kweli.
Mwelekeo ulibadilika nilipopata ushauri wa kujaribu matibabu ya asili. Soma Zaidi...
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/maumivu-ya-ghafla-yalinifanya-nidhani-ni-mwisho-baadaye-nikagundua-mawe-ya-figo-yanatibika-kwa-mitishamba/

 





Na Oscar Assenga, LUSHOTO.


MKUU wa wilaya ya Lushoto Mkoani Tanga Zephania Sumaye ameipongeza Hifadhi ya Mazingira Asili ya Magamba wilayani Lushoto kwa kuandaa matembezi y Magamba Walkathon ambayo yatasaidia kwa kiasi kikubwa kuendelea kutangaza vivutio vya Utalii vilivyopo wilayani Lushoto ikiwemo hifadhi hiyo.


Sumaye aliyasema hayo mara baada ya kushiriki mbio hizo ambazo zilikuwa za kilomite 20,10 na 5 huku akieleza matukio kama hayo yanasaidia kuwaweka pamoja na kusaidia kujenga afya na mahusiano kwa jamii mbalimbali zilizopo katika wilaya hiyo na maeneo mengine hapa nchini.


“Tunapoelekea kufunga mwaka matukio kama hayo yanatuleta pamoja na kutusahaulisha na matatizo yao na kujenga afya na kuwaimarisha leo hii nimesimama hapa Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Balozi Batilda Burian ametuma salamu nyingi na kupongeza matembezi haya ambayo yamekuwa na muendelezo kwa kipindi cha miaka mitatu”Alisema

 

SAME. Mbunge wa Jimbo la Same Mashariki kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Anne Kilango, amewasihi vijana wa jimbo hilo kujitokeza kwa wingi katika mkutano wa hadhara unaotarajiwa kufanyika Leo 22 Desemba 2025, katika viwanja vya Stendi ya Mabasi Ndungu, kufuatia ujio wa Waziri wa Maendeleo ya Vijana, Mhe. Joel Nanauka.

Akizungumza kuelekea siku hiyo, Kilango alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuona umuhimu wa kuunda Wizara ya Maendeleo ya Vijana, wizara ambayo amesema itakuwa na mchango mkubwa katika kushughulikia changamoto, mafanikio na kero zinazowakabili vijana nchini.

Kilango alisema kundi la vijana ndilo kubwa zaidi nchini likiwa na takribani asilimia 64 ya Watanzania wote, hali iliyomfanya aone umuhimu wa kuwakusanya vijana wa Jimbo la Same Mashariki ili wapate nafasi ya kumsikiliza Waziri wao na kushiriki moja kwa moja katika majadiliano yanayowahusu.

Aliongeza kuwa hotuba itakayowasilishwa na Waziri wa Maendeleo ya Vijana haitahusu tu vijana wa Same Mashariki bali itakuwa ni hotuba yenye mwelekeo wa kitaifa, itakayobeba sera, mipango na fursa mbalimbali zitakazolenga kuwawezesha vijana kiuchumi na kijamii.

Mbunge huyo aliwataka vijana kutumia fursa hiyo kueleza changamoto zao, kutoa maoni na mapendekezo yatakayosaidia serikali kuboresha sera na programu za maendeleo ya vijana, akisisitiza kuwa ushiriki wao ni msingi muhimu wa maendeleo endelevu ya taifa.



Na James K. Mwanamyoto

Waziri wa Nchi, Ofisi wa Waziri Mkuu - TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amewaelekeza Walimu Wakuu wa Shule za Sekondari na Msingi nchini kuhakikisha wanadhibiti changamoto ya utoro kwa wanafunzi na walimu katika shule wanazozisimamia.

Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo, wakati akifungua Mkutano wa 20 wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSSA), uliofanyika Jijini Arusha katika Ukumbi wa Tanzania Convention Center (Ngurudoto Mountain Lodge).

“Walimu Wakuu nendeni mkadhibiti utoro wa wanafunzi na walimu shuleni, wapo baadhi ya walimu wakiripoti kazini asubuhi baada ya muda mfupi wanaenda kufanya kazi ya bodaboda mtaani,” Prof. Shemdoe amesisitiza.

Prof. Shemdoe amefafanua kuwa, Walimu Wakuu wakidhibiti utoro shuleni watakuwa wamelihakikishia taifa kupata wanafunzi wenye ufaulu mzuri, nidhamu bora, ujuzi wa maisha na moyo wa kizalendo. 

Ameongeza kuwa, utoro unasababisha anguko la kitaaluma katika taifa, hivyo Walimu Wakuu wanapaswa kudhibiti utoro wa wanafunzi na walimu ili kutengeneza rafiki ya kuinua kiwango cha taaluma nchini, ikiwa ni pamoja na kuwawezesha vijana kufikia ndoto zao.

Akizungumzia suala la walimu kuwa na vyanzo mbadala vya kuongeza kipato, Prof. Shemdoe amesema kwamba Serikali haikatazi watumishi kuwa na shughuli mbadala za kuwaongezea kipato, iwapo shughuli hizo zitafanywa na watumishi mara baada ya muda wa kazi wa Serikali. 

Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe amewataka Wakuu wa Shule kuwa chachu ya kuwapatia watanzania tabasamu la kweli kwa kudhibiti utoro wa wanafunzi na walimu, ambao kitaaluma ni kikwazo cha wanafunzi kupata ufaulu mzuri.

Kwa maelekezo haya, Prof. Riziki Shemdoe ameunga mkono kwa vitendo jitihada za Serikali za kuendelea kuchukua hatua madhubuti ya kuimarisha nidhamu, uwajibikaji na ubora wa elimu nchini.

Na: OWM – KAM, Dar es Salaam

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mheshimiwa Deus Clement Sangu(Mb.), amekutana na kufanya mazungumzo na Viongozi wa Baraza la Maaskofu wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (CPCT) Disemba 20, 2025, Jijini Dar es Salaam.

Lengo la kukutana na viongozi hao ni kujitambulisha na kuelezea jukumu jipya la mahusiano ambalo Ofisi yake imepewa kuliratibu kufuatia Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kuunda Wizara inayohusu kujenga mahusiano baina ya Serikali na wadau wa makundi mbalimbali ya kijamii, kisiasa, kiuchumi, kikanda na Kimataifa.

Katika kikao hicho Waziri Sangu alisema mahusiano ni mchakato shirikishi, endelevu wa mawasiliano ya pande mbili au zaidi ambao unalenga kuwaleta pamoja na kuwawezesha wananchi na wadau kushiriki kikamilifu katika kutoa maoni, kushirikishwa katika maamuzi, kufuatilia utekelezaji wa Sera na Programu za Serikali ili kujenga uwajibikaji kwa ajili ya maendeleo ya Taifa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (CPCT), Askofu Vernon Fernandes amesema wataendelea kushirikiana na Serikali katika kusaidia jamii kiroho, kuimarisha mshikamano na kuunga mkono juhudi za maendeleo nchini.

Askofu Fernandes alishukuru kitendo cha Waziri Sangu kwenda kuwatembelea na kuzungumza nao ambapo aliongeza kusema ni hatua nzuri za Serikali kukuza mahusiano na Taasisi za dini pamoja na wananchi .

Katika kikao hicho, Waziri Sangu aliambatana na Wakurugenzi na Maafisa waandamizi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano. Mhe. Waziri alipata wasaa wa kusikiliza ushauri na maoni ya Viongozi wa Baraza la Maaskofu wa CPCT kwa lengo la kubainisha maeneo yanayohitaji kuimarishwa katika masuala ya mahusiano nchini.


Wanamichezo nchini wamehamasishwa kuwa mabalozi wa nishati safi ya kupikia ili kufikia lengo la Serikali la mwaka 2034 asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia.

Na John Mapepele – New Delhi

Serikali ya Tanzania na India zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) kuhusu ushirikiano kwenye Sekta ya Afya katika kuendeleza tiba asilia (Ayurveda), huku Tanzania ikiwakaribisha wawekezaji kutoka sehemu duniani kuja kuwekeza na kuwahakikishia kuwapatia mazingira mazuri ya uwekezaji.
Kulikuwa na kipindi maishani mwangu ambapo aibu ilikuwa rafiki yangu wa karibu. Nilikuwa nikikopa hata chakula cha jioni. Nilijua majina ya watu wanaoweza kunisaidia, na nilijua pia namna ya kujitetea kwa maneno ili nisijisikie mdogo sana.

Kila siku ilikuwa hesabu ya kuishi, si kuota. Nilijilaumu, nikajilinganisha, na nikaanza kuamini kuwa umaskini ulikuwa sehemu yangu ya kudumu.

Nilifanya kazi ndogo ndogo, nikajaribu biashara ambazo hazikudumu, na mara nyingi nilikata tamaa kabla hata ya kuanza upya. Kilichonivunja zaidi haikuwa kukosa pesa pekee, bali kukosa matumaini.

Nilijikuta nikihofia kuomba msaada tena, huku nikijua bila msaada ningeendelea kudidimia.
Mabadiliko hayakuja ghafla. Yalianza pale nilipokubali kuwa nilihitaji mwelekeo, si huruma.Soma Zaidi...........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilikuwa-nikikopa-hata-chakula-leo-nawasaidia-wengine-kuanzia-mwanzo/
Kwa muda mrefu nilihisi kama uzito wangu ulikuwa mzigo nilioubeba kila siku. Sio tu kimwili, hata kiakili. Nilijaribu njia nyingi kwa haraka kuacha kula ghafla, kufanya mazoezi bila mpangilio, na kujilinganisha na wengine.

Kila jaribio lilipoisha bila matokeo, nilizidi kuvunjika moyo. Nilianza kuamini kuwa labda mwili wangu hauwezi kubadilika. Kilichonikwamisha zaidi haikuwa chakula pekee, bali mawazo.

Kila niliposhindwa, nilijilaumu. Kila nilipoanza upya, hofu ya kushindwa ilinitangulia. Nilielewa baadaye kuwa mabadiliko ya kweli huanza akilini. Nilihitaji kuacha vita na mwili wangu na kuanza kushirikiana nao.

Hatua ya kwanza ilikuwa ndogo. Nilijifunza kula kwa uelewa, si kwa adhabu. Kutembea dakika chache kila siku kulinisaidia kujenga nidhamu. Badala ya kupima mafanikio kwa mizani pekee, nilianza kuyapima kwa nguvu niliyokuwa nayapata, usingizi mzuri, na hali ya kujiamini iliyokuwa inarudi taratibu. Soma Zaidi.......
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/uzito-ulionekana-kunizidi-nguvu-hatua-moja-baada-ya-nyingine-zilileta-mabadiliko/
Nilipojeruhiwa, haikuwa kwa kisu wala ngumi. Ilikuwa kwa maneno. Maneno kutoka kwa mtu niliyemwamini, niliyemheshimu, na niliyefungua moyo wangu kwake. Kila alichosema kilikaa akilini mwangu kama ukweli, na taratibu nikaanza kujiuliza kama nilikuwa wa thamani kweli.

Kujiamini kulipotea, sauti yangu ya ndani ikawa ya lawama. Kwa muda nilijifungia. Niliepuka mazungumzo, nikajifunza kunyamaza ili nisiongeze maumivu. Nilidhani ukimya ungeponya.

Badala yake, nilibeba mzigo mzito wa hasira na huzuni. Kila nilipokumbuka, nilihisi nimekwama kati ya kusamehe na kuondoka kabisa.
Hatua ya kwanza ya kupona ilianza nilipokubali kuwa kuumizwa hakumaanishi udhaifu.Soma Zaidi......
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilijeruhiwa-na-maneno-ya-niliyekuwa-ninamwamini-safari-ya-kujiponya-ilinisaidia-kuamua-hatua-ijayo/

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Mchemba leo Desemba 21, 2025 amekagua hali ya bandari ya Barazani mkoani Lindi na kuiagiza Mamlaka ya Bandari Tanzania kukamlisha kwa haraka michakato ya awali ya kitaalam ya ujenzi wa mradi wa Bandari ya Ngongo wilayani Lindi mkoani Lindi.

Amesema kukamilika kwa bandari ya Ngongo kutasaidia kuwaondolea adha watumiaji wa bandari inayotumika sasa ya Barazani ambayo hali yake haiendani na mahitaji ya sasa.

Dkt. Mwigulu ameongeza kuwa kukamilika kwa ujenzi wa bandari ya Ngongo kutaleta chachu ya maendeleo mkoani humo kwani bandari ya Lindi imeanza kuchangamkiwa na wafanyabiashara, wakiwemo wa nchi jirani.

 





Babati, Manyara Desemba 19, 2025: Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Cuthbert Sendiga, leo Desemba 19, 2025 amezindua rasmi na kuhamasisha utekelezaji wa Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote (NHIF) katika Mkoa wa Manyara, akisisitiza umuhimu wa kila mwananchi kuwa na bima ya afya ili kupata huduma za matibabu kwa urahisi na kwa gharama nafuu.


Uzinduzi huo umefanyika katika Ukumbi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) mjini Babati, na kuhudhuriwa na viongozi wa serikali, wataalamu wa afya, wawakilishi wa mpango wa kitaifa wa Bima ya Afya kwa Wote pamoja na wananchi mbalimbali.


Akizungumza katika uzinduzi huo, Mhe. Sendiga amesema mpango wa Bima ya Afya kwa Wote ni utekelezaji wa maelekezo ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kutimiza ahadi ya siku 100 za kuanzisha mfumo utakaohakikisha kila Mtanzania anakuwa na bima ya afya.




“Mfumo huu unalenga kumwondolea mwananchi mzigo wa gharama kubwa za matibabu na kuhakikisha kila mmoja, bila kujali kipato chake, anapata huduma bora za afya kwa wakati,” amesema Mhe. Sendiga.


Aidha, amewaelekeza Wasimamizi wa vituo vya kutolea huduma za afya mkoani Manyara kuhakikisha mpango wa Bima ya Afya kwa Wote unatekelezwa kwa kuzingatia miongozo, kanuni na taratibu zilizowekwa, ili kufikia malengo yaliyokusudiwa na Serikali.


Sambamba na hilo, Mhe. Sendiga amesisitiza kuwa ni wajibu wa viongozi na watendaji wote kwenda kutoa elimu na kuhamasisha wananchi kujiunga na mpango huo, ili waweze kunufaika na huduma za afya kwa uhakika.


Kwa upande wake, Bi. Janeth Kibambo, Mwakilishi wa Timu ya Kitaifa ya Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, amesema lengo kuu la mfumo huo ni kuhakikisha wananchi wote wanakuwa na uwezo wa kupata huduma za afya katika vituo vyote vya umma na binafsi vilivyosajiliwa, bila kikwazo cha kifedha.


Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Dkt. Andrew Method, ameeleza kuwa mkoa umejipanga kikamilifu kutekeleza mpango huo, akibainisha kuwa changamoto ya wananchi kushindwa kugharamia matibabu imekuwa kubwa, hivyo kuanzishwa kwa Bima ya Afya kwa Wote ni mwarobaini muhimu katika kuboresha sekta ya afya.


Dkt. Method ameongeza kuwa Mkoa wa Manyara uko tayari kuupokea na kuutekeleza mpango huo kikamilifu, kwa kushirikiana na vituo vyote vya afya na wadau mbalimbali, ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na endelevu.


Uzinduzi wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote mkoani Manyara unatarajiwa kuongeza wigo wa upatikanaji huduma za afya, kupunguza vifo vinavyotokana na ukosefu wa matibabu kwa wakati, na kuboresha ustawi wa jamii kwa ujumla.

   


Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Arusha, wametembelea vivutio vya utalii katika Hifadhi ya Ngorongoro na Serengeti sambamba na kupata mafunzo ya namna ya kukabiliana na msongo wa mawazo mahali pa kazi.

Akizungumza na watumishi, Meneja wa TARURA Mkoa wa Arusha Mhandisi Nicholas Francis amesema hiyo ni katika kutekeleza moja ya malengo ya Taasisi hiyo lengo (A) linalohusu jinsi ya kukabiliana na HIV/AIDS, magonjwa yasiyoambukiza, ikiwa ni hatua ya kuboresha ustawi wao na kuboresha ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao wawapo kazini.

Semina hiyo ililenga kuwaeleza hali halisi ilivyo ya maambukizi, njia ya kujikinga, umuhimu wa kupima kwa hiari na kwa usiri na kuondoa ile dhana za maambukizi zinazoathiri juhudi za kukabiliana na kudhibiti na kuenea kwa maambukizi ya VVU.

Aidha, washiriki walikumbushwa kuzingatia maadili, kujilinda na kuchukua tahadhari za kujikinga na maambukizi ya VVU katika maisha yao ya kila siku.

Vile vile Mhandisi Nicholas aliwataka washiriki hao kuchukua tahadhari na kujenga tabia ya kuchunguza afya zao mara kwa mara jambo ambalo litawasaidia kutambua afya zao, vile vile itawaepushia msongo wa mawazo.