Nilikuwa nimekata tamaa kabisa ya maisha. Kila asubuhi ilikuwa mzigo mwingine wa kuamka, na usiku nilijikuta nikilia kimya kimya bila sababu. Watu waliniona kama mtu mwenye huzuni ya kawaida au hata msongo wa mawazo, lakini ndani yangu nilihisi kitu tofauti kabisa. Sikuwa mimi yule niliyekuwa kabla mwenye matumaini, furaha na ndoto nyingi. Hali hii ilianza ghafla, bila tukio kubwa la maisha kuichochea. Nilidhani ni msimu tu wa huzuni, lakini kila siku iligeuka kuwa vita ya kiakili na kimwili.

Nilianza kujitenga na marafiki, nikakosa hamu ya kula, na mara nyingi nilitaka tu kulala au kutoweka. Nilipokwenda hospitali, madaktari walinitaja kuwa na ‘depression ya kiwango cha chini’. Nilijaribu dawa na ushauri nasaha, lakini hakuna kilichonisaidia kabisa. Ndipo nilianza kuhisi labda kuna kitu zaidi ya afya ya akili kitu kisichoonekana kwa macho.

Nilipoanza kuuliza na kuchunguza kwa kina, dada mmoja aliyekuwa rafiki wa karibu alinieleza jinsi hali kama yangu inaweza kuwa matokeo ya nguvu za kiroho hasa uchawi wa kunifanya nijinyime maisha.

Aliniambia pia jinsi watu huweza kuwekewa vitu ili washindwe kuendelea na maisha yao, wakate tamaa, na kujiua hata bila kuelewa kwa nini. Sikuchukua kwa uzito mwanzoni, hadi alinielekeza kwa Kiwanga Doctors ambao husaidia watu waliopitia hali kama yangu. Soma zaidi hapa 

  

Nilikuwa nimekaa mbele ya kioo, nikiangalia pua yangu, ngozi yangu yenye madoa na mdomo wangu uliokuwa mwembamba. Sikuwa najipenda. Kilichoniumiza zaidi ni maneno aliyoniambia mtu niliyempenda kwa moyo wangu wote: “Wewe si mrembo, na huwezi kuwa mrembo bila kufanya upasuaji.” Alikuwa mpenzi wangu wa miaka miwili, lakini siku hiyo alikatiza uhusiano wetu kwa kauli hiyo ya kikatili.

Toka utotoni nilikuwa na matatizo ya kujiamini. Nilichekwa sana shuleni, wenzangu waliniita majina kama “kiatu cha mguu mmoja” na “uso wa ndoo.” Nilijua sina ngozi laini kama ya wenzangu, nilikuwa na chunusi za mara kwa mara na nywele zangu hazikuwa laini wala zenye mvuto.

Nilipokuwa mtu mzima, nilijaribu bidhaa nyingi scrubs, serums, hata vipodozi vya bei ghali vilivyosemekana vinatoka Ulaya lakini hakuna kilichobadilika.

Kipindi nilipoingia kwenye uhusiano huo, nilidhani nimempata mtu wa kunikubali jinsi nilivyo. Kwa muda fulani alionyesha kunijali, lakini baadaye alianza kuniambia nivae makeup nene au nijifunge shungi kuficha uso. Mwisho wa yote, akaniambia ukweli wake: siwezi kuwa mrembo kwa hali yangu ya asili. Alinitaka nifanye upasuaji wa sura. Soma zaidi hapa 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Innocent Bashungwa amesema Chuo Cha Uhasibu Arusha (IAA) kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza kimeeleza mpango wa kuanzisha kituo cha umahiri cha utoaji wa mafunzo kwa wafungwa ili kuwapa maarifa, ujuzi na stadi za biashara zitakazowawezesha kujikimu kiuchumi pindi wanapomaliza vifungo vyao na kutoa wito wa kuhakikisha maandalizi ya kituo hicho yanafanyika.

Ameyasema hayo  Agosti 6, 2025 katika hafla ya kutunuku vyeti vya ujasiriamali na stadi za biashara kwa wafungwa, iliyofanyika katika viwanja vya Gereza Kuu Arusha.

Waziri Bashungwa pia amempongeza Mkuu wa Chuo Cha Uhasibu Arusha (IAA) Prof. Eliamani Sedoyeka kwa namna anavyosimamia chuo, ubunifu alionao, maono ya kutafsiri mahitaji ya jamii na taaluma zinazotolewa chuoni, na mafanikio makubwa aliyoleta katika upande wa michezo. Aidha, Waziri Bashungwa ameishukuru IAA kwa ushirikiano ambao imeutoa kwa Jeshi la Magereza katika programu ya mafunzo ya ujasiriamali na stadi za biashara yaliyotolewa kuanzia Mei 7, 2025 kwa wafungwa takribani 170 wakiwemo wanawake 41 na wanaume 129.

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza CGP Jeremiah Katungu amemshukuru Prof. Sedoyeka kwa maono ya ushirikiano katika utoaji wa mafunzo hayo, akisema kuwa tangu mashirikiano na IAA kumekuwa na matokeo chanya ikiwemo mahafali hayo ya kwanza ya wahitimu wa mafunzo ya ujasiriamali na stadi za biashara yaliyotolewa kwa wafungwa.

 Aidha, CGP Katungu amesema mafunzo yatawafanya wahitimu kuwa wema, wenye maarifa na kuwataka kutumia mafunzo kuanzisha shughuli mbalimbali za kuwaingizia kiptao watakapomaliza vifungo vyao.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo Cha Uhasibu Arusha (IAA) Prof. Eliamani Sedoyeka amesema mafunzo hayo yameanzishwa kwa kutumia uhalisia wa mazingira, mahitaji ya washiriki, ambayo yalihusisha vipindi vya nadharia na vitendo juu ya stadi za uanzishaji biashara kisheria, ujasiriamali, vyanzo vya mitaji, usimamizi wa fedha pamoja na utafutaji wa masoko na mazingira ya kufanyia biashara; eneo ambalo IAA ina uzoefu mkubwa kitaaluma na kiutendaji ili kuwawezesha wafungwa kupata ujuzi wa kujitegemea mara baada ya kumaliza vifungo vyao.

Aidha, Prof. Sedoyeka ameongeza kuwa IAA kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza nchini wamejipanga kupanua programu hii kwenye magereza mengine, kutoa vifaa vya kuanzisha biashara, kusaidia wahitimu kupata mitaji kupitia mamlaka za serikali za mitaa na kutoa mafunzo endelevu na msaada kwa wafungwa waliohitimu mafunzo. 

Pia, Prof. Sedoyeka ametoa rai kwa wahitimu kutendea haki fursa hii ya mafunzo waliyoyapata.












 


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Innocent Bashungwa amempongeza Mkuu wa Chuo-IAA, pamoja na menejimenti nzima kwa namna anavyosimamia chuo, umahiri na ubunifu wake katika sekta mbalimbali ikiwemo mashirikiano aliyoanzisha na Jeshi la Magereza katika kutoa mafunzo ya ujasiriamali na stadi za biashara kwa wafungwa.

“Kama Mkuu wa Chuo pamoja na timu yako naomba tuwapongeze na tuwashukuru kwa ushirikiano, ambao mnalipa Jeshi la Magereza Katika hii programu ambayo leo hii tunatunuku wahitimu 170” amesema

Waziri Bashungwa ameyasema hayo Agosti 6, 2025 katika hafla ya kutunuku vyeti vya ujasiriamali na stadi za biashara kwa wafungwa waliohitimu mafunzo ya ujasiriamali na stadi za biashara yaliyotolewa na Chuo Cha Uhasibu Arusha-IAA kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza, hafla iliyofanyika katika viwanja vya Gereza Kuu Arusha

Aidha, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza CGP Jeremiah Katungu amesema ana imani kubwa kuwa wahitimu wa mafunzo hayo wamepata elimu na maarifa muhimu, yatakayowawezesha kuwa wabunifu na wajasiriamali mahiri pindi watakapomaliza vifungo vyao na kwenda kwenye jamii.

“lengo la mafunzo ni kuwaandaa na kuwarejesha kwenye jamii wakiwa raia wema na wenye uwezo wa kuendesha shughuli za kiuchumi” amesema

Naye, Mkuu wa Chuo-IAA Prof. Eliaman Sedoyeka amemshukuru CGP Katungu kwa mashirikiano mazuri na IAA katika urekebishaji wafungwa, kupitia utoaji wa mafunzo ya ujasiriamali na stadi za biashara na kutoa rai kwa taasisi zingine za elimu, mashirika ya kiraia na taasisi binafsi kushirikiana na IAA katika kuhakikisha wafungwa wanapata ujuzi na maarifa.

Nao, baadhi ya wahitimu wa mafunzo hayo yaliyoanza Mei 7, 2025 wamepongeza  viongozi wote na walimu kutoka IAA kwa kuwapa elimu ya ujasiriamali na stadi za biashara, wakisema italeta tija kwao kiuchumi baada ya kumaliza vifungo vyao.




NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limekutana na kuwapa elimu wafanyabiashara wadogowadogo wanaofanya shughuli zao ndani ya mkuza wa bomba la gesi asilia katika eneo la Kinyerezi Mwisho, Mtaa wa Kanga na Kibaga ili kuweza kuondoka eneo hilo ambalo sio rasmi na salama kwa shughuli zozote za kibinadamu ikiwemo kufanya biashara.



Dodoma, Agosti 7, 2025


Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Dkt. Janet R. Lekashingo, ameongoza ujumbe wa Tume kutembelea Banda la Tume ya Madini katika Maonesho ya Kitaifa ya Wakulima (Nane Nane) yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma.

Dkt. Lekashingo ameambatana na Makamishna wa Tume, Mhandisi Theonestina Mwasha na Dkt. Theresia Numbi, pamoja na Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Ramadhani Lwamo. 

Wakiwa katika banda hilo, wamepata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na Tume, ikiwemo utoaji wa elimu kwa wananchi kuhusu fursa za uwekezaji katika Sekta ya Madini, taratibu za upatikanaji wa leseni, biashara ya madini, uongezaji thamani madini, pamoja na usimamizi wa mazingira katika shughuli za uchimbaji.

Akizungumza na maafisa wa Tume na wananchi waliotembelea banda hilo, Dkt. Lekashingo amewapongeza watumishi wa Tume kwa kazi nzuri ya kutoa elimu na huduma kwa umma. 


Amesisitiza umuhimu wa kutumia maonesho hayo kama jukwaa la kuelimisha na kuhamasisha Watanzania kushiriki kikamilifu katika Sekta ya Madini, hususan kupitia uongezaji thamani madini na kuzingatia sheria, kanuni na miongozo iliyopo.

“Ni muhimu wananchi wakapata uelewa mpana kuhusu namna wanavyoweza kunufaika na rasilimali za madini zilizopo nchini iwe ni kupitia uchimbaji, biashara, uongezaji thamani au utoaji wa huduma kwenye migodi. Sekta hii ina mchango mkubwa katika Pato la Taifa na ajira kwa Watanzania,” amesisitiza Dkt. Lekashingo.

Kwa upande wao, Makamishna wa Tume wameeleza kufurahishwa na mwitikio mkubwa wa wananchi kutembelea banda la Tume na kuonesha dhamira ya kujifunza zaidi kuhusu Sekta ya Madini, jambo linalodhihirisha hamasa na mwamko chanya wa Watanzania kushiriki kwenye sekta hiyo muhimu.

Naye Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Ramadhani Lwamo, amewataka maafisa wa Tume kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kulingana na mahitaji ya wadau waliopo katika maonesho mbalimbali nchini.

“Yapo madini yanayotumika kama mbolea, na pia zipo fursa nyingi za usambazaji wa bidhaa za kilimo kwenye migodi. Ni muhimu wananchi wakafahamu fursa hizi na kushiriki kikamilifu ili Sekta ya Madini iendelee kuwa kichocheo cha maendeleo ya kiuchumi na mchango wake katika Pato la Taifa uongezeke,” amesema Mhandisi Lwamo.

Tume ya Madini ni miongoni mwa Taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Madini zinazoshiriki kikamilifu katika Maonesho ya Nane Nane mwaka huu, ikiwa na lengo la kuelimisha umma kuhusu Sekta ya Madini, kuonesha mafanikio yaliyopatikana, pamoja na kuhamasisha uwekezaji zaidi katika sekta hiyo kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.

 

Kila mmoja anapenda kuona maisha yake yanapiga hatua kila siku, hakuna mtu ambaye hapendi kuona maendeleo yake binafsi ingawa vikwazo ni vingi hasa upande wa utafuta riziki.

Naitwa Uledi kutokea Bagamoyo, kwa sasa nimeajiriwa kwenye kampuni kubwa ya usambazaji vinywaji baridi, nimefanya kazi hii kwa miaka zaidi ya 12 sasa.

Miaka mitatu iliyopita nilifanikiwa kupandishwa cheo na kuongezewa mshahara baada ya kufanya kwa miaka tisa bila kupata fursa hiyo ambayo kila mfanyakazi huwa anaitamani.

Sababu ya kuikosa kwa muda mrefu sio kwamba sikuwa na vigezo au ofisi yangu haikuwa na uwezo, laah hasha!, bali ni fitna za kikazi ambazo baadhi ya wafanyakazi wenzangu walikuwa wanazifanya kwa kushirikiana na uongozi. Soma zaidi hapa 




Na Okuly Julius, OKULY BLOG, DODOMA


Wanafunzi wa Shule ya Msingi Brother Martin ya mkoani Dodoma wamepata elimu ya vipimo kutoka kwa Meneja Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa Wakala wa Vipimo (WMA), Veronica Simba, walipotembelea Banda la Wakala huo katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika kwenye Viwanja vya Nanenane, Nzuguni jijini Dodoma.

Moja ya mikakati ya Wakala wa Vipimo katika kupanua wigo wa utoaji elimu hiyo ni kuanzisha vilabu vya vipimo katika shule mbalimbali nchini ili kuwajengea wanafunzi uelewa wa masuala ya vipimo tangu wakiwa wadogo.









Ukweli ni kwamba kila mfanyabiashara ambaye unaona amefanikiwa, ana siri kuhusu mafanikio, kuna jambo la muhimu nyuma ya pazia katika yale mafanikio yake, na sio wote wapo tayari kuzungumzia hilo.

Nimekuja kuamini hilo baada ya kukutana na Kiwanga Doctors na kunieleza wafanyabiashara maarufu na wakubwa wengi wamepita kwao kutazamwa nyota zao kibiashara, na ndipo wakaenda kufanya kazi katika eneo la nyota zao na kufanikiwa. 

Jina langu ni Ally, mimi ni Mfanyabiashara ambaye najishughulisha na usafirishaji wa mizigo kutokea bandari ya Mombasa kuja Nairobi. 

Nashukuru sana kazi hii ambayo nimeifanya kwa miaka zaidi ya mitano sasa, imekuwa yenye faida sana kwenye maisha yangu na jamii yangu kwa ujumla, kipato kizuri napata sio haba, maisha yanasonga. 

Hata hivyo, kabla ya kazi hii niliangaika sana kwenye kazi nyingi na biashara mbalimbali bila mafanikio yoyote yale hadi kufikia hatua ya kukata tamaa na maisha naana nilikuwa naona kama ninapoteza tu muda wangu hapa duniani. Soma zaidi hapa 

 


Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Sendiga, amesema bunifu za kijasiriamali na teknolojia zinazofanywa na wanafunzi wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) zina mchango mkubwa kwa jamii kwa kuwa zinagusa moja kwa moja mahitaji halisi ya wananchi na kutoa suluhisho la changamoto mbalimbali za kijamii na kiuchumi

RC Sendiga amesema hayo alipotembelea banda la chuo cha Uhasibu Arusha IAA kwenye maonesho ya 31 ya nane nane kanda ya kaskazini yaliyofanyika katika viwanja vya Themi, Njiro -Arusha

Kwa upande wake, Meneja wa Kampasi ya Chuo cha Uhasibu Arusha Dkt. Joseph Daudi amesema chuo kimejipanga kikamilifu kuhakikisha kinatoa elimu bora, yenye kuendana na mahitaji ya soko la ajira kwa kuzingatia ubunifu, teknolojia na ujasiriamali kama nguzo kuu za maendeleo ya kitaaluma

Nae Sarah Adamson, ambaye ni Center Administration Coach wa kituo cha ubunifu na ujasiriamali cha IAA Business Start-Up Center, amesema kupitia mafunzo ya vitendo na  ushauri wa kibiashara, kituo hicho kimefanikiwa kulea miradi mbalimbali ya ubunifu ambayo sasa inatoa mchango wa moja kwa moja kwa jamii

“tunajivunia kuona baadhi ya wanafunzi wetu wakigeuza mawazo kuwa biashara halisi, zinazoweza kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla" amesema

Godfrey Chuse  mwanafunzi mjasiriamali na mmiliki wa kampuni ya Cabo Group of Companies, inayojishughulisha na Kilimo (shamba direct) pamoja na kutumia mabaki ya mbao kutengeneza mapambano ya nyumbani, amesema kuwa  IAA imempa maarifa, ujasiri na jukwaa la kubadilisha ndoto zake kuwa halisi

Chuo cha Uhasibu Arusha kinashiriki katika maonesho ya nane nane yanayofanyika katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Dodoma na Mbeya