IMG-20240328-WA0037Katibu Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bw. Patience Ntwina (kushoto) akibadilishana nyaraka na Mkurugenzi Mtendaji wa MISA TAN Bi. Elizabeth Riziki baada ya kutia saini mkataba wa ushirikiano baina ya taasisi hizo mbili.

IMG-20240328-WA0031
Mwenyekiti wa bodi na Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mhe. Amina Talib Ali akipongezana na Mkurugenzi Mtendaji wa MISA TAN Bi. Elizabeth Riziki (kushoto) baada ya kutia saini mkataba wa ushirikiano baina ya taasisi hizo mbili.
****

Taasisi ya vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika Tawi la Tanzania (MISA-TAN) na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora wamesaini mkataba wa miaka mitatu (2024- 2027) wa ushirikiano makubaliano ya kufanya kazi kwenye maeneo mbalimbali ya haki za binadamu na hasa haki za waandishi wa habari na wananchi kwa ujumla.


Hafla ya utiaji saini Mkataba huo imefanyika leo jijini Dodoma
na kuhudhuriwa na Mwenyekiti wa bodi na Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mhe. Amina Talib Ali, Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mhe. Mohamed Khamis Hamad, Katibu Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bw. Patience Ntwina, Makamishina, wakurugenzi wa tume na kwa Upande wa MISA TAN, Makamu Mwenyekiti wa MISA TAN Bw. James Marenga na Mkurugenzi Mtendaji wa MISA TAN bi. Elizabeth Riziki.
IMG-20240328-WA0034
IMG-20240328-WA0038
IMG-20240328-WA0032

 

Upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP),Lilian Liundi akizungumza wakati wa kufungua Kilinge salama kwa Wanawake, Wasichana na Viongozi kilichofanyika leo Machi 28, 2024 katika Ukumbi wa Mtandao huo Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP),Lilian Liundi akizungumza wakati wa kufungua Kilinge salama kwa Wanawake, Wasichana na Viongozi kilichofanyika leo Machi 28, 2024 katika Ukumbi wa Mtandao huo Jijini Dar es Salaam.
Diwani wa wilaya ya Mtwara, Farida Abdallah akizungumza wakati akitoa Kestoria yake ya kuwania nafasi ya uongozi katika Kilinge salama kwa Wanawake, Wasichana na Viongozi kilichofanyika leo Machi 28, 2024 katika Ukumbi wa Mtandao huo Jijini Dar es Salaam.
Diwani wa wilaya ya Mtwara, Farida Abdallah akizungumza wakati akitoa Kestoria yake ya kuwania nafasi ya uongozi katika Kilinge salama kwa Wanawake, Wasichana na Viongozi kilichofanyika leo Machi 28, 2024 katika Ukumbi wa Mtandao huo Jijini Dar es Salaam.

Diwani wa wilaya ya Mtwara, Farida Abdallah akizungumza wakati akitoa Kestoria yake ya kuwania nafasi ya uongozi katika Kilinge salama kwa Wanawake, Wasichana na Viongozi kilichofanyika leo Machi 28, 2024 katika Ukumbi wa Mtandao huo Jijini Dar es Salaam.
Diwani wa wilaya ya Mtwara, Farida Abdallah akizungumza wakati akitoa Kestoria yake ya kuwania nafasi ya uongozi katika Kilinge salama kwa Wanawake, Wasichana na Viongozi kilichofanyika leo Machi 28, 2024 katika Ukumbi wa Mtandao huo Jijini Dar es Salaam.
Wanawake na Wasichana ambao ni washiriki kutoka Dar es Salaam, Pwani na Mtwara wakimsikiliza Diwani wa wilaya ya Mtwara, Farida Abdallah wakati akitoa Kestoria yake ya kuwania nafasi ya uongozi katika Kilinge salama kwa Wanawake, Wasichana na Viongozi kilichofanyika leo Machi 28, 2024 katika Ukumbi wa Mtandao huo Jijini Dar es Salaam.

KILINGE Salama (Safe Space) kilichoandaliwa na Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP) Chamwibua Diwani, Farida Abdallah ambaye ni Diwani wa wilaya ya Mtwara ambapo ameeleza changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo wanawake viongozi ikiwemwo kukatishwa tamaa ili wasiweze kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

Akizungumza leo Machi 28, 2024 wakati wa kilinge salama kilichofanyika katika ukumbi wa TGNP jijini Dar es Salaam, Diwani huyo ambaye aliishia kidato cha pili na kupata ujauzito huku akimpote Mama yake mzazi amewaasa wanawake kutokukata tamaa pale yanapojitokeza maneno ya kukatisha tamaa pale yanapojitokeza wakati wa harakati za kutafuta nafasi za uongozi.

“Wakati nawania nafasi ya uongozi watu walikuja kunikatisha tamaa ili ni sigombee….. hata kwenda kumshawishi Mme wangu ili anikatishe tamaa lakini hawakufanikiwa….” Amesema Farida.

Kwa Upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Lilian Liundi akizungumza wakati wa kufungua Kilinge salama ambapo ni mazingira ambayo ni rasmi au yasiyo rasmi ambayo wanawake na wasichana wanapata nafasi ya kujadili kwa uhuru masuala yao, amesema kuwa Katika mwezi Machi wa wanawake, TGNP imekuwa ikiandaa vilinge hivyo ili kuhamasisha wanawake kuingia katika nafasi za uongozi. 

“Mategemeo yangu ni kwamba mwisho wa siku ya leo tutaungana kwa pamoja kuendelea kusimamia Agenda ya mwanamke na uongozi katika mkoa wetu wa Dar es Salaam.” 

Pia Mkurugenzi Mtendaji Lilian ameweka bayana takwimu za Wenyeviti wa vijiji kuwa ni asilimia 2.1, Wenyeviti vitongoji ni asilimia 6.7 na Wenyeviti mitaa ni asilimia 12.6. 

Kwa upande wa Wabunge wa kuchaguliwa, wanawake ni 25 ya Wabunge 264 ambayo ni sawa na asilimia 9.5 tu ya Wabunge wote, idadi ya Wabunge wanawake wa Viti Maalumu ni 113 ambayo ni sawa na asilimia 29 ya Wabunge wote.  Jumla ya Wabunge Wanawake ni 142 sawa na asilimia 37 ya idadi ya Wabunge wote ambao ni 393 ambapo ili kufikia 50 kwa 50 ya uongozi wa Wanawake Viongozi lazima ifikiwe kwa kutoa elimu kwa wanawake na wasichana waweze kuwania nafasi mbalimbali za uongozi.

Lilia pia ameeleza kuwa malengo ya Kilinge salama kwa Wasichana na Wanawake ni kukaa pamoja na viongozi wanawake wanaochipukia na viongozi wanawake wenye uzoefu, kuandika na kusambazi kestoria za safari za uongozi za wanawake viongozi mahiri ili kuonesha michango waliyonayo katika maendeleo ya nchi.

Pia kutoa hamasa kwa viongozi wanawake wanaochipukia au wanawake wanaotamani kuwa viongozi. 

Kilinge Salama kwa Wanawake na Wasichana pamoja na viongozi leo ni kutoka mkoa wa Dar es Salaam, halmashauri za Ilala, Kinondoni na Temeke, Mtwara, Lindi na Pwani.

 315a7363-b952-4ff8-a482-54a348ef350f


Na Ashrack Miraji


Mkuu wa Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro Kasilda Mgeni ameagiza Maafisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wilayani humo kutumia ubunifu, weledi pamoja na busara katika kudhibiti mianya ya ukwepaji kodi kwa baadhi ya wafanyabiashara ambao sio waadilifu.


Mkuu huyo wa wilaya amebainisha hayo katika kikao cha kamati ya ushauri wa kodi cha wilaya na kusisitiza kuwa mfanyabiashara yeyote atakaye bainika kuendelea kukiuka kulipa kodi taarifa iwasilishwe Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake.


Amesema suala la ulipaji kodi ni wajibu wa kila mwananchi kisheria ili kusaidia Serikali kupanga shughuli za kuwaletea wananchi wake maendeleo, akihimiza TRA kuwa wabunifu katika ukusanyaji mapato na kufanya operesheni za mara kwa mara kwa wafanyabiashara wote wilayani humo.


“TRA fanyeni operesheni za mara kwa mara kwa wafanyabiashara wote ambao wapo ndani ya wilaya ya Same na wanaostahili kutumia mashine za Kielektroniki (EFD) basi wanakuwa nazo na kwa wale ambao watakuwa wakaidi baada ya kuwafuatilia na kuwapa elimu basi sheria iweze kuchukua mkondo wake juu yao kwani hao ni wahujumu uchumi wa serikali”.


Kwa upande wake meneja wa TRA wilaya ya Same Eliapenda Mwanri amesema ufanisi  wa utendaji unatokana na ziara za mara kwa mara za mkuu wa wilaya na kamati yake ya usalama ya kuwatembelea wafanyabiashara katika biashara zao kusisitiza utoaji wa risiti za kielektroniki, ulipaji wa kodi kwa wakati pamoja na kusikiliza na kutatua kero na changamoto za  kibiashara, pia kupata maoni ya kuboresha biashara zao.


Kwa mwaka wa fedha 2023/24 TRA wilaya ya Same imekusudia kukusanya shilingi bilioni 4. 6 (4,637,450,937.77) sawa na ongezeko la asilimia 48% ikilinganishwa na makusanyo ya mwaka 2022/23 ambapo lengo lilikuwa ni shilingi bilioni 3.6 (3, 685, 320, 179.62).


Katika kipindi cha mwezi Julai 2023 hadi Februari 2024 imekusanya kiasi cha shilingi bilioni 2.2 (2, 240, 762, 028. 53) sawa na ufanisi wa asilimia 74.2% ya lengo la kukusanya shilingi bilioni 3.0 (3, 021, 651, 706. 79. na makusanyo haya sawa na ongezeko la asilimia 8.2 ikilinganishwa na kipindi kama hiko mwaka 2022/23 ambayo yalikuwa Shilingi Bilioni 2.0 (2, 070, 285, 159. 60).


0ad179c7-ea82-41df-a95e-0526cc6d9b41

33a45fc0-5a96-43e9-bad3-774b98079df3

cbf13f26-7929-4443-8e86-047e42333a5c

 


Kocha Mkuu wa Timu ya Tabora United Denis Laurence amesema kuwa katika kipindi cha siku saba tangu alipojiunga na Timu anaridhishwa na viwango vya wachezaji kutokana na kujituma kwao kwenye mazoezi uwanjani.


Kocha Laurence amesema kuwa ameshangwaza kuona wachezaji kwa kipindi kifupi tangu alipojiunga na Timu hiyo yenye Makazi yake Mkoani Tabora wanamuonesha ushirikiano wakutosha nakusikiliza kila anachowaelekeza kwenye uwanja wa mazoezi na kwamba hajapata changamoto yoyote hadi sasa.


Ameongeza kuwa ushirikiano ambao wachezaji wanampa unatoa  taswira njema kuelekea kwenye michezo tisa ya Ligi Kuu ya NBC Soka Tanzania Bara pamoja na michuano ya Kombe la Azam Sport Federation dhidi ya Singida Fountain Gate kufanya vizuri kwani ndio mkakati uliopo kwa sasa kama Timu.


“Nafurahi kuona wachezaji wananisikiliza vizuri, tunakwenda sawa ,tunazungumza Lugha moja , kwa huumuda mfupi ambao nimekuwa nao hapa kwangu ni maajabu, wanafuata ninachowaambia lakini pia wanafanyia kazi, hii kwangu ni kubwa sana kama kocha, muhimu nazidi kuwasisitiza kila mmoja ananafasi kwenye kikosi changu cha kwanza” amesema Kocha Laurence.


Ukiangalia kila mmoja anauwezo mkubwa, nahii ni kawaida kwa wachezaji wa  Afrika, muhimu ninachokifanya ni kuwaweka kwa pamoja wacheze kitimu ili tuweze kushinda, morali na hari zao zipo juu hivyo ninafurahia sana kuwepo na wachezaji wangu mazoezini na mazingira yote kwa ujumla.


Aidha katika hatua nyingine Kocha Laurence amesema kuwa hadi sasa tayari ameshapata kikosi chake cha kwanza lakini akasisitiza sio ndio kitadumu milele hapana kwani mfumo wake ni kuhitaji kila mmoja aweze kucheza kweye michezo hii iliyosalia kabla ya kumalizika kwa msimu wa 2023/2024.


Tabora United itakuwa ugenini siku ya Aprili Nne katika Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza ikiwakabili Singida Fountain Gate kwenye mchezo wa ASFC na badae Aprili 14 katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya JKT Tanzania utakaopigwa katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi hapa Mjini Tabora.


Imetolewa leo Machi 28


Na Christina Mwagala


Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano


Tabora United



Serikali kupitia Wizara ya Afya inaendelea kuimarisha ubora wa huduma za Afya ya mama na mtoto katika vituo 25 vinavyotoa huduma ya upasuaji wa dharura wa kumtoa mtoto tumboni (CEmONC) katika Mkoa wa Dar Es Salaam ili kupunguza vifo vitokanavyo na Uzazi. 

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amesema hayo leo Machi 28, 2024 wakati akifungua mafunzo elekezi kazini juu ya huduma za Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto katika Mkoa wa Dar Es Salaam ambapo mafunzo hayo ni endelevu yanayotolewa nchini nzima ili kupunguza vifo vya mama mjamzito na mtoto. 

“kuimarisha ubora wa huduma za Afya ya mama na mtoto katika vituo 25 vya Afya vinavyotoa huduma ya upasuaji wa dharura wa kumtoa mtoto tumboni yaani (CEmONC) tutakua tumetatua asialimia 84 ya changamoto za Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto kwa Mkoa wa Dar Es Salaam.” Amesema Waziri Ummy 

Amesema, mafunzo haya ni muhimu sana ambayo yamesaidia kupunguza vifo katika katika Mkoa wa Tabora ambapo kwa mwaka 2023 vifo vya watoto wachanga vimepungua kutoka vifo 50 hadi vifo Vinne kwa miezi Mitatu, lakini pia mafunzo hayo yanasaidia kupeana mbinu mbalimbali za kuwahudumia vizuri wagonjwa ili kuendelea kupunguza vifo vitokanavyo na Uzazi. 

“Mkoa wa Dar Es Salaam kwa Mwaka 2023 kulikua na vifo vya wajawazito 219, vifo vya watoto wachanga 1,701 hivyo tunaamini kupitia mafunzo haya tutapunguza takwimu hizi za vifo kwa zaidi ya asilimia 50, inawezekana.” Amesema Waziri Ummy 

Aidha, Waziri Ummy amezitaka Halmashauri kutenga fedha kwa ajili ya kuwawezesha watoa huduma waliopatiwa mafunzo hayo ili waweze kwenda kutoa mafunzo hayo kwenye vituo vyao vya Afya vinavyotoa huduma ya upasuaji wa dharura wa kumtoa mtoto tumboni (CEmONC) vilivyobakia pamoja na Zahanati. 

Pia, Waziri Ummy amezitaka kila Hospitali pamoja na Vituo vya Afya vinavyotoa huduma ya upasuaji wa dharura wa kumtoa mtoto tumboni (CEmONC) zianzishe wodi maalumu ya watoto wachanga inayofanya kazi kwa kuwa na vifaa tiba pamoja na watoa huduma waliojengewa uwezo.

“Jambo jingine nataka nisisitize, tutoe taarifa sahihi za vifo vya wajawazito, vifo vya watoto wenye umri chini ya miaka Mitano, vifo vya watoto wenye umri chini ya Mwaka Mmoja pamoja na takwimu sahihi za vifo vya watoto wachanga wenye siku 0-28.” Amesema Waziri Ummy 

Mwisho, Waziri Ummy amesema, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anataka hadi kufika Mwaka 2027 tuwe tumepunguza vifo vya watoto wachanga kutoka 24 katika kila vizazi hai 1,000 hadi kufikia 12 katika kila vizazi hai 1,000 “hii inawezekana kupitia mafunzo haya, hatutamuangusha Rais Dkt. Samia.”

 1000684209


Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga amesihi wawekezaji kutoka Mataifa mbalimbali (USA) kuwekeza katika sekta ya nishati nchini ikiwemo eneo la nishati safi ya kupikia, nishati jadidifu pamoja na gesi ili kuendelea kuchochea maendeleo katika nyanja tofauti tofauti.

Kauli hiyo imetolewa Machi 27, 2024 katika Ofisi Ndogo ya Wizara iliyopo jijini Dar es Salaam alipofanya kikao na Naibu Waziri mdogo wa Nishati wa Marekani, Mhe. Joshua Volz *kwa niaba ya Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Mashaka Biteko*

1000684208

Mhe. Kapinga amesema kuwa Tanzania ni sehemu salama ya kuwekeza hususan katika Sekta ya Nishati ambapo ameeleza kuwa Tanzania ipo tayari kupokea wawekezaji katika sekta ya nishati ili kuongeza tija kwenye maendeleo ya Nchi.

‘’Tanzania ina vyanzo vingi vya umeme ikiwemo nishati jadidifu kama vile Upepo, Jua na Jotoardhi, ndio maana nachukua nafasi hii kuwakaribisha wawekezaji kutoka nchi ya Marekani wajitokeze kuwekeza katika sekta ya nishati hapa nchini,” amesema Mhe. Kapinga.  

Amesema kuwa Serikali inaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya umeme inayotokana na Nishati Jadidifu kama vile Mradi wa umeme Jua Shinyanga ambao unatarajia kuzalisha megawati 150 baada ya kukamilika, Mradi wa kuzalisha umeme kwa kutumia Upepo uliopo Singida na Miradi ya Jotoardhi iliyopo katika Mikoa ya Songwe na Mbeya.

Mhe. Kapinga amesema Tanzania inaendelea na hatua za utekekelezaji wa mradi wa kuzalisha umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) ambao unategemea kuzalisha jumla ya megawati 2,115 na utekelezaji wake umefikia asilimia 96.

Pia, Viongozi hao wamejadiliana kuhusu utekeleza miradi ya kuzalisha, kusafirisha na kusambaza umeme inayotekelezwa nchini ili kuhakikisha umeme unafika maeneo mbalimbali nchini na kuvutia wawekezaji katika nyanja tofauti tofauti, pia wemezungumzia miradi kusafirisha umeme kati ya Tanzania na nchi nyingine.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Nishati wa Marekani, Mhe. Joshua Volz ameonesha nia ya kushirikiana na Tanzania katika kuwekeza kwenye sekta ya nishati nchini ikiwemo miradi ya umeme na gesi.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Watendaji kutoka Wizara ya Nishati, Wizara ya Mambo ya Nje,Viongozi waandamizi kutoka Wizara ya Nishati ya Marekani na viongozi waandamizi wa Ofisi ya Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania.
IMG-20240328-WA0118
IMG-20240328-WA0112
IMG-20240328-WA0115
IMG-20240328-WA0113
IMG-20240328-WA0116

 1000684092


Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameeleza kuwa tayari Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia kuongeza kiasi cha Shilingi Bilioni 4 kukamilisha upanuzi wa barabara ya njia nne Bukoba Mjini (Rwamishenye Round about - Stendi ya Bukoba Mjini) yenye urefu kilometa 1.6.

Bashungwa amesema hayo leo tarehe 28 Machi 2024 wakati alipowasili katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Kagera kuanza ziara ya kikazi ya kukagua ujenzi wa miundombinu ya barabara Mkoani humo.
1000684118


Bashungwa amesema kuwa awali Serikali ilitoa kiasi cha shilingi Bilioni 4.64 kuanza ujenzi wa wa barabara hiyo kwa kipande cha kilometa 1 ambacho kinaanzia Rwamishenye hadi eneo la Mitaga ambapo kwa sasa utekelezaji wake umefikia asilimia 25.

Amesema kuwa kiasi cha shilingi Bilioni 4 kitakachoongezwa kitawezesha ujenzi wa kipande cha mita 600 kuanzia eneo la Mitaga hadi stendi na ujenzi wa daraja kubwa katika mto Kanoni.

“Mheshimiwa Rais ameshatoa kibali kwa TANROADS kuendeleza ujenzi wa barabara ya njia nne hadi stendi ya Bukoba ambapo Mkandarasi M/s Abemulo ambaye ameshaanza kazi kwa kipande cha km 1 ataendelea na ujenzi kwa kipande cha mita 600 na daraja kubwa”, amesema Bashungwa.

Aidha, Bashungwa amemuagiza Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Kagera kumsimamia Mkandarasi anayeendelea na ukarabarati wa barabara ya Lusahunga - Rusumo (km 92) kwa kiwango cha lami ambapo barabara hiyo inauunganisha Mkoa wa Kagera na nchi jirani.

Naye, Mbunge wa jimbo la Bukoba Mjini, Stephen Byabato amesema kazi ya ujenzi wa njia nne wa barabara ya Bukoba Mjini unaendelea kwa kasi kubwa na ameiomba Serikali kushughulikia suala la fidia kwa wananchi waliopisha ujenzi wa barabara hiyo.
IMG-20240328-WA0096
IMG-20240328-WA0093
IMG-20240328-WA0098
IMG-20240328-WA0095
IMG-20240328-WA0097

 1000684072


 Na Carlos Claudio , Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kumbukizi ya miaka 40 ya Hayati Edward Moringe Sokoine aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 

Hayo yameelezwa na msemaji wa familia ya hayati Edward Sokoine, Bw. Lembris Kipuyo alipokutana na kuzungumza na waandishi wa habari leo Machi 28, 2024 jijini Dodoma, kwa lengo la kuwaalika watanzania wote kwenye ibada maalum ya kumbukizi ya miaka 40 ya Hayati Edward Moringe Sokoine.

 

Amesema ibada hiyo iliyoandaliwa na familia ikishirikiana na Taasisi ya Hayati Edward Moringe Sokoine itafanyika siku ya Ijumaa Aprili 12, 2024, saa 3:00 asubuhi katika Kijiji cha Enguik, Monduli Juu mkoani Arusha.

 

Ibada hiyo ya kumbukumbu ya Hayati Sokoine itawashirikisha viongozi mbalimbali wa serikali wakiongozwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan,” amesema Bw. Kipuyo.

 

Amesema lengo kubwa la kuanzishwa kwa Taasisi ya Hayati Edward Moringe Sokoine ni kuenzi mema aliyoyafanya kwani aliacha alama kubwa ambayo taifa linamkumbuka hadi leo na kueleza kuwa taasisi hiyo imejikita katika masuala ya elimu, kilimo, hifadhi ya mazingira, vyanzo vya maji pamoja na afya.

 

Bw. Kipuyo amesema,“Hayati Sokoine alikuwa mzalendo wa kweli, alipenda taifa lake na wananchi wake, alihakikisha kwamba rasilimali za nchi zinatumika na watanzania wote, aliwatumikia wananchi bila kubagua na alikuwa na hofu ya Mungu katika kufanya kazi zake.”

 

Hayati Sokoine alikuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika vipindi viwili wakati wa uongozi wa awamu ya kwanza.

 

Hayati Sokoine alizaliwa Agosti 01, 1934, kijijini Enguik, Monduli Juu wilayani Monduli, mkoani Arusha na kufariki Aprili 12, 1984 kwa ajari ya gari katika kata ya Dakawa wilayani Mvomero mkoani Morogoro akitokea bungeni jijini Dodoma.


4baf199d-8920-4e0a-85f3-a263545ab0f3

 

Na Mwandishi Wetu ,Manyara.

Chama cha Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilmo Mkoa wa Manyara (TCCIA Manyara) kimekanusha taarifa zilizosambaa mitandaoni zikimtaja mshauri wa biashara na mwajiriwa wa TCCIA Manyara Bw. Ramadhani Rashid Msangi kuhukumiwa kwenda jela miaka 3 au kulipa faini ya shilingi 900,000 kwa kosa la kughushi nyaraka za mafunzo kwa wajasiriamali mwaka 2018 hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Manyara tarehe 23 March 2024. Ambapo Chama hicho kimedai kuwa licha ya tuhuma zinazomkabili Bw.Ramadhani Rashid Msangi, kwa sasa sio mwajiriwa wa Chama hicho kwani aliondolewa kazini tangu April 2019 .

Taarifa kwa vyombo vya habari imetolewa na Uongozi wa Chama hicho ikieleza kuwa Mfanyakazi huyo aliondolewa miaka kadhaa iliyopita na tangu wakati huo hahusiki na shughuli zozote za Chama hicho. Chama Chetu TCCIA, kinaendelea kufanya kazi kwa uwazi na kwa kufuata sheria na taratibu zilizowekwa katika katiba yetu.

 Tunajitahidi kufuata miongozo na mifumo iliyoainishwa katika katiba yetu, pamoja na kuzingatia sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Tunathamini uwazi na uwajibikaji katika kazi zetu, na tunajitahidi kuhakikisha kwamba tunazingatia viwango vya juu vya maadili na utawala bora katika kila hatua tunayochukua.(Mwenyekiti TCCIA Manyara)

 


Mahakama ya Wilaya ya Mbulu imemhukumu Melkiadi Zakaria Tlehema aliyekuwa Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Hayloto kata ya Nambris, Wilaya ya Mbulu Mkoa wa Manyara.

Mshtakiwa ametiwa hatiani kwa makosa mawili ambayo ni Ubadhirifu na Matumizi Mabaya ya Madaraka, makosa hayo ni kinyume na kifungu cha 28 na kifungu cha 31cha Sheria Ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa sura ya 329 kama ilivyofanyiwa marejeo Mwaka 2022.

Hukumu hiyo dhidi ya Melkiadi Zakaria Tlehema, shauri la Uhujumu Uchumi Na 03/2023, imetolewa chini ya Mhe.Vitalis Eusebius Kapugi, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Mbulu – Machi 2, 2024.

Mshtakiwa ameamriwa kulipa faini ya shilingi 200,000/= au kwenda jela miezi mitano. Pia mshtakiwa ametakiwa kurejesha fedha alizofanyia ubadhirifu kiasi cha shilingi 1,869,500/=.

Mshatikiwa alifanya ubadhirifu kwenye fedha hizo kupitia makusanyo ya fedha za wananchi kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Msingi Hyloto.

Hata hivyo, Mshtakiwa amelipa faini na kurejesha kiasi cha fedha alichofanyia ubadhirifu hivyo ameachiwa huru.